Tuesday, September 30, 2014


Paris St-Germain watatinga Mechi hii ya Nyumbani kwao ya Kundi F dhidi ya FC Barcelona bila ya Straika wao mahiri Zlatan Ibrahimovic ambae ameumia kifundo cha Mguu.
Katika Mechi za kwanza za Kundi lao, PSG ilitoka Sare na Ajax na Barcelona kuichapa Apoel Nicosia Bao 1-0.

Wakati PSG hawajafungwa hata Mechi moja katika Mechi 9 Msimu huu, ingawa 6 kati yake ni suluhu, Barcelona wamekuwa hatari mno huku Mastraika wao Messi na Neymar wakicheka na nyavu kila mara na Juzi waliibamiza Granada 6-0 huku Neymar akipiga Hetitriki na Messi Bao 2.

Mechi hii inawakutanisha Mameneja wa Timu hizi mbili, Laurent Blanc wa PSG na Luis Enrique wa Barca, ambao waliwahi kucheza pamoja wakiwa Barcelona katika Msimu wa 1996/97 na kuiwezesha kutwaa Kombe la Washindi wa Ulaya, Copa del Rey na Spanish Super Cup.



RATIBA MECHI ZA LEO JUMANNE
Mechi zote kuanza Saa 21:45

Jumanne Septemba 30
KUNDI E
19:00 CSKA Moscow vs Bayern Munich
Manchester City vs Roma

KUNDI F
APOEL Nicosia vs Ajax
Paris St-Germain vs Barcelona

KUNDI G
FC Schalke 04 vs NK Maribor
Sporting Lisbon vs Chelsea

KUNDI H
BATE Borisovs vs Athletic Bilbao
Shakhtar Donetsk vs FC Porto


Dakika ya 15 Peter Crouch aliifungia bao la kwanza la kichwa na kuifanya Stoke City kuwa mbele ya bao 1-0 dhidi ya Newcastle baada ya Victor Moses kutoa krosi safi kwa Crouch ambaye ameunga kwa kichwa hadi langoni mwa Newcastle.Kibarua mashakani kwa kocha Pardew! 
Mpaka mapumziko Stoke ndio ilikuwa mbele ya bao 1-0 dhidi ya Newcastle United.Ushindi wa kwanza wa Nyumbani kwa Stoke City msimu huu wakimtungua Newcastle, bao likifunhgwa na Peter Crouch kipindi cha kwanza dakika ya 15 kwa kichwa.
Kocha wa Newcastle Pardew akiwa kwenye Mawazo mazito kipindi cha pili na hapa akiwa nyuma ya bao 1-0 kwenye Uwanja wa Stoke City Britannia.VIKOSI:
Newcastle XI: Krul, Janmaat, Coloccini, Williamson, Dummett, Tiote, Colback, Sissoko, Cabella, Gouffran, Riviere
Stoke XI: Begovic, Bardsley, Shawcross, Wilson, Muniesa, Whelan, Nzonzi, Diouf, Adam, Moses, Crouch



Wafanyakazi wa kampuni ya Airtel Tanzania (kutoka kushoto), Kema Mabango, Abdallah Gunda na Jackson Mmbando wakishiriki katika shindano la kukuna nazi wakati wa Siku ya Wanafamilia ya Airtel, iliyofanyika katika viunga vya Fun City Kigamboni jijini Dar es salaam jana.

Washindi wa shindano la kukuna nazi wakishow love. Kutoka
(kushoto), Mshindi wa Kwanza, Abdallah Gunda, Mshindi wa Pili, Jackson
Mmbando na Mshindi wa Tatu, Kema Mabango.

Watoto wa wafanyakazi wa kampuni ya Airtel Tanzania wakiogelea wakati wa Siku ya Wanafamilia ya Airtel, iliyofanyika katika viunga vya Fun City Kigamboni jijini Dar es salaam jana.

Watoto wa wafanyakazi wa kampuni ya Airtel Tanzania wakishiriki katika michezo wakati wa Siku ya Wanafamilia ya Airtel, iliyofanyika katika viunga vya Fun City Kigamboni jijini Dar es salaam jana.

Wafanyakazi wa Airtel na familia zao wakijisevia maakuli.

Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (kulia) akiwahudumia chakula wafanyakazi wa Airtel na familia zao.
Airtel Family day yalenga kuongeza hamasa kwa wafanyakazi kujituma katika kazi zao Imeelezwa kuwa ufanisi wa watumishi katika ngazi mbali mbali za kiutendaji unaweza ukaongezeka pindi wafanyakazi wanapokutana pamoja na kubadilishana mawazo na viongozi wao katika hali ya kiurafiki.

waliotembelea blog