Wednesday, December 7, 2016


Serikali imefuta hatimiliki ya viwanja 15 vilivyokuwa vinavyomilikiwa na Raia wa Uingereza, mfanyabiashara maarufu jijini Mwanza, Hermant Patel, Mwenye Uraia wa Tanzania na Kenya kitendo ambacho ni kinyume cha taratibu na sheria za nchi zinazozuia raia wa kigeni kumiliki ardhi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi William Lukuvi amesema anayeruhusiwa kumiliki ardhi nchini ni raia wa Tanzania pekee na kuongeza kwamba kwa watanzania waishio nje ya nchi na kuukana uraia wao nao hawataruhusiwa kumiliki ardhi bali watapewa ardhi kama ilivyo kwa wawekezaji kutoka mataifa mengine.
William Lukuvi amesema mtu akishaukana uraia wa Tanzania hana haki tena kama raia wa Tanzania, hivyo ataruhusiwa kumiliki ardhi kama mwekezaji tu na siyo kama raia wa Tanzania. Lukuvi amesisitiza kuwa ardhi itabaki kuwa ya Watanzania tu na ameagiza mamlaka zota kuwasaka wale wote ambao wanamiliki ardhi kinyume na sheria za nchi. Bonyeza Play kutazama video hii hapa chini
Staa wa timu ya taifa ya Ureno anayeichezea timu ya Real Madrid ya Hispania Cristiano Ronaldo leo December 7 2016 ameingia kwenye headlines baada ya kutoka kwa interview yake aliyofanya na FourFourTwo.
Ronaldo ameongea mambo katika interview yake ya FourFourTwo lakini moja kati ya vitu alivyoongea ni kitu gani angependa kufanya baada ya kustaafu soka “Maisha yangu mimi ni soka baada ya kustaafu ningependa kufanya movies”
czenqxzwqaa2hpl-759x1024
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Cristiano Ronaldo hivi karibuni alisaini mkataba mpya wa kuendelea kusalia Santiago Bernabeu hadi mwaka 2021, hata hivyo Ronaldo amesema huo sio ndio utakuwa mkataba wake wa mwisho katika soka


Category: 
Team: 
Azam FC
UJIO wa makocha kutoka Hispania ndani ya Azam FC, umeanza kuitangaza timu hiyo kutokana na watu wengi wa nchi hiyo kuanza kuwafuatilia mabingwa hao wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati.
Uongozi wa Azam FC kabla ya kuanza msimu huu, iliwaajiri makocha kutoka nchini hiyo inayosifika kuwa na Ligi Kuu bora duniani ‘La Liga Santander’ ikijitambulisha kwa soka lake la pasi na mchezo wa kasi.
Joto hilo la makocha linaundwa na Kocha Mkuu, Zeben Hernandez, Msaidizi wake, Yeray Romero, Kocha wa Viungo, Pablo Borges, Kocha wa Makipa, Jose Garcia na Mtaalamu wa Tiba za Viungo, Sergio Perez Soto.
Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz Kocha Mkuu Hernandez, alisema kuwa vyombo vingi vya habari katika eneo la Tenerife wanaloishi vimekuwa vikiifuatilia timu hiyo na kuripoti habari mbalimbali za Azam FC.
“Tuliporejea Hispania tulikutana na magazeti mbalimbali yakiielezea Azam FC na kazi yetu tunayofanya hapa, makala nyingi zimekuwa zikielezea kuwa kazi yetu itakuwa na umuhimu mkubwa kwa hapo baadaye ndani ya soka la Afrika na klabu hii,” alisema.
Alisema kuwa jambo jingine la umuhimu litakuwa pia ni kwa soka la Hispania, kwani falsafa yetu itakuwa ikisambaa sehemu mbalimbali duniani kutokana na makocha wa huko kuanza kusambaa duniani.
“La kufurahisha nililokutana nalo huko, ni Wahispania wengi kuanza kuijua Azam FC na kuifutilia pia, hili ni jambo zuri kwa Azam FC, duniani kuna nchi nyingi zinatamani kuwa na makocha kutoka Hispania, lakini zinashindwa kuwapata na Azam FC imebahatika kwa ujio wetu hapa na ndani muda mchache ujao itaanza kunufaika na ujio wetu hapa, ni suala la muda tu,” alisema.
Licha ya Azam FC kutopata matokeo mazuri kwenye baadhi ya mechi za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), mwanga mzuri wa makocha hao umeanza kuonekana baada ya kuiongoza timu hiyo kuandika rekodi mbalimbali ambazo huko nyuma zilishindikana kuwekwa.
Baada ya kusota miaka mitatu mfululizo bila kutwaa ubingwa na Ngao Jamii, hatimaye mwaka huu Azam FC chini ya makocha hao imeweza kuandika rekodi ya kubeba taji hilo kwa kuichapa Yanga kwa mikwaju ya penalti 4-1 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90 za mchezo huo.
Ikiwa ina rekodi mbaya huko nyuma ya kutoweza kuichapa Tanzania Prisons nyumbani kwao ndani ya Uwanja Sokoine (Mbeya), msimu huu imeweza kuichapa kwa mara ya kwanza (1-0) tokea ipande daraja mwaka 2008 na kuwa timu pekee iliyozoa pointi zote sita ndani ya dimba hilo msimu huu kufuatia kuichapa pia Mbeya City mabao 2-1.
Azam FC inayodhaminiwa na kinywaji safi cha Azam Cola kinachosisimua mwili na kuburudisha koo pamoja na Benki bora kabisa nchini kwa usalama wa fedha zako ya NMB, pia imeweza kuvuna jumla ya pointi tisa kati ya 12 kwenye mechi za ugenini za Kanda ya Ziwa.
Kati ya pointi hizo tisa, tatu ilivuna kwa kuibutua Toto African bao 1-0 ndani ya Uwanja wa CCM Kirumba (Mwanza) na kuandika rekodi ya kushinda kwa mara ya kwanza ndani ya dimba hilo dhidi ya Wakishamapanda hao, mechi nyingine za huko ikiichakaza Kagera Sugar 3-2 na Mwadui (4-1) huku ikifungwa na Mbao (2-1).
Hadi inamaliza raundi ya kwanza ya ligi, Azam FC imefanikiwa kumaliza katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 25 ikizidiwa 10 na kinara Simba aliyejikusanyia 35 na Yanga ikiwa nafasi ya pili kwa pointi zake 33, ambapo itaanza raundi ya pili kwa kumenyana na African Lyon Desemba 18 mwaka huu kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.




WATANZANIA watakiwa kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano katika Kukuza Uchumi kwa kujiunga pamoja na kuanzisha Viwanda vidogo vidogo na vya kati.

Rai hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Pangani Bi. Zainab Abdallah alipokuwa akifanya mahojiano maalum na mwandishi wa habari hii kuhusu maadhimisho ya miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania.

Akizungumzia kauli mbiu ya maadhimisho hayo amesema kuwa inasadifu kile ambacho Serikali imedhamiria kukifanya matharani suala zima la kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda kitu ambacho kimeanza kutekelezwa.

“Watanzania wanapaswa kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kutekeleza uanzishwaji wa Viwanda vidogo vidogo na vya kati kwani kufanya hivyo kutapunguza ama kuondoa kabisa tatizo la ajira kwa vijana,” alisema Bi. Zainab.

Aliongeza watanzania wanapaswa kushirikiana kwa pamoja katika kuijenga Tanzania ya Viwanda ili kuongeza uzalishaji wa bidhaa za ndani na kuongeza fursa ya ajira kwani viwanda ni eneo linalotoa ajira nyingi kwa wakati mmoja.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amempongeza Rais Magufuli kwa hatua kadha alizokwishachukua katika kuhakikisha anaweka mazingira rafiki kwa wawekezaji katika sekta ya viwanda akitolea mfano wa hatua ya Kampuni ya Bakhresa kupewa eneo la ekari elfu kumi kwa ajili ya kujenga kiwanda cha kusindika matunda.

Desemba 9 kila mwaka Tanzania imekuwa ikiadhimisha siku ya Uhuru wa Tanzania Bara ambapo kwa mwaka huu kitaifa yatafanyika Dar es salaam na kauli ya mwaka huu ni “Tuunge Mkono Jitihada za Kupinga Rushwa na Ufisadi na Kuhimarisha Uchumi wa Viwanda kwa Maendeleo ya Nchi Yetu.”


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika leo tarehe 07 Desemba Ikulu jijini Dar es Salaam. Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. PICHA NA IKULU

waliotembelea blog