Monday, January 4, 2016



Baada ya kuwepo na tetesi za muda mrefu kuhusu uongozi wa klabu ya Real Madrid kutoridhishwa na mwenendo wa timu yao January 4, umetangaza rasmi kumfuta kazi aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Rafael Benitez. Real Madrid walitangaza kumfuta kazi Benitez na Zidane kutajwa kurithi nafasi hiyo kwa muda hadi mwisho wa msimu.
Kufuatia kuteuliwa kwa Zidane kurithi mikoba hiyo, stori zilimfikia mchezaji mwenzake wa zamani David Beckham na kuonesha furaha yake kwa kupost picha yao ya zamani na ujembe wenye kuoneshwa kufurahishwa na nguli huyo wa kifaransa kuchukua mikoba hiyoo.
“Unaweza kumpata mtu bora zaidi yake? mtu ambaye alikuwa bora kiwanjani na watu wote tunampenda, anachukua nafasi ya kutumikia klabu ambayo mimi na watu wengine tunaipenda, mtu mwenye passion na siku zote huwa hakubali kushindwa kwa namna yoyote ile. Kiukweli ni mtu sahihi kwa hiyo kazi” >>> Beckham
1
David Beckham na Zinedine Zidane waliwahi kucheza pamoja kwa miaka mitatu katika timu ya Real Madrid, baada ya David Beckham kuhama Man United na kuhamia Real Madrid mwaka 2003. Hata hvyo Jose Mourinho anatajwa kuhusishwa na Madrid kutaka kurudi mwishoni mwa msimu.


Pamoja na mabingwa watetezi wa ligi kuu ya England Chelsea kupoteza matumaini ya kutwaa ubingwa kwa mara nyingine lakini kocha wao mpya Guus Hiddink ana mipango mingine ya ushindi.
Baada ya ushindi wa jana wa mabao 3-0 Hiddink amesema klabu yake hiyo inaweza kumaliza ligi hiyo ikiwa katika nafasi nne bora za juu mwishoni mwa msimu huu.
Klabu hiyo ya Stamford Bridge imeenda mechi nne bila kufungwa, kwa mara ya kwanza msimu huu, na kupanda hadi nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi.
Hata hivyo, bado wanapungukiwa na alama 13 kuweza kufuzu kcheza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Alisema ligi ni ngumu lakini pia ni rahisi kushinda hivyo watapambana kuhakikisha wanashika nafasi za juu.
Hiddink alichukua nafasi ya kuifundisha timu hiyo kwa muda baada ya kocha wa awali Jose Mourihno kuondolewa kutokana na mwenendo mbaya wa timu.
Paco Alcacer celebrates after  he scores a late equaliser for Valencia to earn a pointPaco Alcacer akishangilia baada ya kuisawazishia bao dakika za majeruhi na kufanya 2-2Real Madrid bao limefungwa na Karim Benzema dakika ya 16'
Valencia CF 1, Real Madrid 1. Daniel Parejo wa (Valencia CF) aliifanikishia bao kwa mkwaju wa penati na kwenda mapumziko kwa bao 1-1.

Alcacer akipongezwa na mwenzie Andre Gomes

Bao hilo liliwafanya wagawane pointi na Real Madrid

Wachezaji wa Valencia wakishangilia na kupongezana

Gareth Bale alifunga bao la kichwa na kufanya 2-1 dhidi ya Valencia

Patashika Bale akitupia

Valencia, Kikosi cha Mchezaji wa zamani wa Manchester United, Garry Neville, Jana kilimudu kutoka Sare ya 2-2 na Miamba ya Spain Real Madrid katika Mechi ya La Liga iliyochezwa Estadio Mestalla huku Atletico Madrid wakitwaa uongozi wa Ligi hiyo baada ya kuifunga Levante 1-0 Juzi Jumamosi.
Real walitangulia kufunga katika Dakika ya 10 kwa Bao la Karim Benzema na Valencia kusawazisha Dakika ya 45 kwa Penati ya Daniel Parejo.

Bale alizungukwa kupongezwa na Wana Real.
Katika Dakika ya 68 Real walibaki Mtu 10 pale Mateo Kovacic alipoewa Kadi Nyekundu lakini hilo halikuwazuia Real kufunga Bao la Pili katika ya 82 kupitia Gareth Bale, Bao lilidumu Dakika 1 tu kwani Paco Alcacer alifunga Bao la kusawazisha na kuwapa Valencia Sare ya 2-2.
Matokeo hayo yamewaacha Real wakiwa Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 2 nyuma ya Barcelona, ambao wamecheza Mechi 1 pungufu, huku Atletico Madrid wakiongoza wakiwa na Pointi 41 zikiwa ni Pointi 2 mbele ya Barcelona.



Espanyol's Hernan Perez (right) tugs Lionel Messi's shirt during the opening period against Barcelona on Saturday afternoon

Barcelona forward Neymar (left) drives towards Espanyol's goal in a bid to open the scoring in the first Catalan derby of the season

Andres Iniesta brings the ball down on his chest during Barcelona's visit to the Estadi Cornella-El Prat in their first game of 2016



Espanyol's Hernan Perez (right) tugs Lionel Messi's shirt during the opening period against Barcelona on Saturday afternoon

Barcelona forward Neymar (left) drives towards Espanyol's goal in a bid to open the scoring in the first Catalan derby of the season

Andres Iniesta brings the ball down on his chest during Barcelona's visit to the Estadi Cornella-El Prat in their first game of 2016


Wayne Rooney Leo ameipa mguu mwema wa kuanza Mwaka Mpya wa 2016 alipoipa Manchester United ushindi kwa kufunga Bao la ushindi walipoifunga Swansea City 2-1 katika Mechi ya Ligi Kuu England. Wayne Rooney akishangilia bao lake la ushindi la pili2-1Martial na Rooney wakipongezanaRooney
Ushindi huu, ambao ni wa kwanza katika Mechi 8, umeipandisha Man United hadi Nafasi ya 5.
Bao za Man United zilifungwa na Anthony Martial Dakika ya 47 na Swansea
kurudisha Dakika ya 70 kwa Bao la Gylfi Sigurdsson lakini Wayne Rooney, akipokea pasi safi ya Martial, alifunga Bao la ushindi kwa kisigino katika Dakika ya 77.
Bao hilo limemfikisha Rooney Nafasi ya Pili katika Ufungaji Bora kwenye Ligi Kuu England, akiwa nyuma ya Alan Shearer na pia Nafasi ya Pili katika Ufungaji Bora katika Historia ya Man United akiwa na Bao 238, Bao 11 nyuma ya Mshikilia Rekodi, Sir Bobby Charlton.


WAKATI Klabu ya Bournemouth ikiingia Sokoni kumchukua Kiungo wa AS Roma Juan Manuel Iturbe kwa Mkopo hadi mwishoni mwa Msimu, Meneja wa Man United Louis van Gaal anatafakari kununua Straika ili kunoa Fowadi yake butu huku ripoti zikidai Chelsea na Arsenal zina nia ya kuchukua Mastaa kutoka Uswisi na Italy. Juan Manuel Iturbe
Iturbe, mwenye Miaka 24 na ni Mchezaji kutoka Argentina, ilikuwa nusura aende Watford lakini Bournemouth wakatia mkono haraka na kumchota.
Stamford Bridge
Kutoka Stamford Bridge, zipo ripoti kuwa Chelsea inataka kumnunua Straika wa FC Basel Breel Embolo mwenye Miaka 18 ili kuziba pengo la Loic Remy na Radamel Falcao ambao wanatarajiwa kuondoka Mwezi huu Januari.
Inasemekana FC Basel wako tayari kumuuza Embolo ikiwa Chelsea watatoa Pauni Milioni 20.
Embolo huichezea Timu ya Taifa ya Switzerland na ameifungia FC Basel Bao 16 katika Mechi 47 za Ligi.
Emirates
Nao Arsenal wanadaiwa kuwa na nia ya kumsaini Straika wa Napoli Lorenzo Insigne mwenye Miaka 24.
Wakala wa Insigne, Antonio Ottaiano, ameiambia Radio Kiss Kiss Napoli kuwa Paris Saint-Germain na Arsenal zimeonyesha nia ya kumsaini Straika huyo.
Old Trafford
Huku wakitoka kwenye Mwezi mbovu kabisa katika Historia yao ya Miaka 138, Meneja wa Manchester United Louis van Gaal sasa anataka kununua Straika katika Dirisha la Uhamisho la Mwezi huu Januari.
Wakiwa wamefunga Bao 25 tu katika Mechi zao 25 zilizopita na pia kuambua Sare 7 za bila Magoli Msimu huu, 6 zikiwa Uwanjani Old Trafford, na pia kufungwa katika Mechi zao 4 zilizopita, 3 zikiwa za Ligi, Van Gaal ameona Straika mpya ndio Mwarobaini wa tatizo lao.
Hivi sasa tegemezi kubwa kwa ufungaji kwa Man United ni Kepteni wao Wayne Rooney na Anthony Martial ambao Msimu huu kila mmoja amefunga Bao 7.
Ijumaa, Van Gaal alifupisha Mkopo wa Chipukizi Will Keane, mwenye Miaka 22, kwa Preston na kumrudisha Old Trafford ili kuimarisha mashambulizi.
Van Gaal ametamka: “Kufunga Mabao ni kipaji. Tunacho hicho kipaji lakini Wachezaji hawajiamini hivi sasa na pengine itabidi tununue Straika mwingine!”
Akielezea matatizo yao, Van Gaal alisema: “Tatizo letu ni ufungaji. Ukitathmini Mechi zetu zote utaona tumeweza kucheza Staili yetu. Ukiondoa Mechi na Arsenal, na Kipindi cha Kwanza dhidi ya Stoke na Palace, hizo hatukucheza Mpira wetu.”
Man United walifungwa na Arsenal na Stoke na kutoka Sare na Palace.
Aliongeza: “Mechi zote zilizobaki tulicheza Mpira wetu na kutengeneza nafasi, kutawala lakini hatukufunga. Tunahitaji pia Straika awe na bahati. Wachezaji wengi hucheza nafasi hiyo na wanapata nafasi ya kufunga na hawafungi, huweza kueleza hilo.”
Mwanzoni mwa Msimu huu, Van Gaal aliruhusu Mastraika Wawili kuuzwa, Javier Hernández kwenda Bayer Leverkusen na Robin van Persie kwa Fenerbahce na kuruhusu Radamel Falcao kuondoka baada ya Mkopo wake kwisha na pia kumtoa Chipukizi James Wilson kwenda Mkopo huko Brighton & Hove Albion

Van Gaal amesema: “Tungeweza kuwabakisha Mastraika wote lakini tungekuwa na Mastraika wengi kwenye Benchi. Watakosa furaha na kutaka kuondoka. Hiyo ndio hadithi ya Chicharito. Anataka kucheza!”


Ligi Kuu England inaanza Mwaka Mpya 2016 kwa Mechi za Jumamosi Januari 2 na Mechi ya kwanza kabisa ni huko Upton Park kati ya West Ham na Liverpool.
Hadi sasa kila Timu kwenye Ligi hiyo imecheza Mechi 19 ambazo ni nusu ya Mechi zao zote na hivyo Mechi za sasa ni kuanza kwa Raundi ya Pili ya Ligi hiyo ambayo Msimu huu imekuwa haitabiriki.
Mbali ya Mechi hiyo ya West Ham ambao wako Nafasi ya 8 na Liverpool ambao ni wa 7 wakipishana kwa Pointi 1 tu, Saa 12 Jioni zitafuata Mechi 6 ambazo Vinara wa Ligi, Arsenal, wakiwa Nyumbani kucheza na Newcastle, Leicester City, wanaofungana kwa Pointi na Arsenal, kuwa Nyumbani kuivaa Bournemouth na pia Man United kuwa kwao Old Trafford kucheza na Swansea City, Timu ambayo imeifunga Man United ya Van Gaal Mechi 3 zilizopita za Ligi, zote kwa Bao 2-1.
Mechi nyingine za Saa 12 ni zile za Norwich v Southampton, Sunderland v Aston Villa na West Brom v Stoke.
Jumamosi Januari 2 itakwisha kwa Mechi ya Watford kuwakaribisha Man City.
Jumapili zipo Mechi mbili kati ya Crystal Palace na Chelsea na kisha Everton kucheza na Tottenham.
LIGI KUU ENGLANDRATIBA
Jumamosi Januari 2

15:45 West Ham v Liverpool
18:00 Arsenal v Newcastle
18:00 Leicester v Bournemouth
18:00 Man United v Swansea
18:00 Norwich v Southampton
18:00 Sunderland v Aston Villa
18:00 West Brom v Stoke
20:30 Watford v Man City

Jumapili Januari 3
16:30 Crystal Palace v Chelsea 

19:00 Everton v Tottenham 

MSIMAMO WAKE ULIVYO KWASASA BAADA YA KUFIKIA NUSU.
Barclays Premier League
PosLogo &TeamPWDLGDPts
1ArsenalArsenal1912341539
2Leicester CityLeicester City1911621239
3Manchester CityManchester City1911351736
4Tottenham HotspurTottenham Hotspur199821835
5Crystal PalaceCrystal Palace19946731
6Manchester UnitedManchester United19865630
7LiverpoolLiverpool19865030
8West Ham UnitedWest Ham United19784529
9WatfordWatford19856429
10Stoke CityStoke City19856129
11EvertonEverton19685726
12SouthamptonSouthampton19667324
13West Bromwich AlbionWest Bromwich Albion19658-623
14ChelseaChelsea19559-620
15Norwich CityNorwich City19559-1020
16BournemouthBournemouth19559-1220
17Swansea CitySwansea City19478-819
18Newcastle UnitedNewcastle United194510-1517
19SunderlandSunderland193313-1912
20Aston VillaAston Villa191513-198


WAFUNGAJI WANAOONGOZA MPAKA SASA 'TOP 5' 
Rank Name Club Goals
1 Jamie Vardy Leicester 15
1 Romelu Lukaku Everton 15
3 Odion Ighalo Watford 14
4 Riyad Mahrez Leicester 13
5 Harry Kane Spurs 11

waliotembelea blog