Friday, August 21, 2015


Ikiwa imebakia siku moja kabla ya mchezo unaosubiri kwa hamu na mashabiki wa soka Tanzania kuuona, mchezo wa ngao ya Hisani kati ya Yanga na Azam FC, klabu ya Azam FC imethibitisha kuwakosa nyota wake kadhaa akiwemo Allan Wanga aliyekwenda Kenya wiki moja iliyopita kwa ajili ya msiba wa mama yake.
pacha
Lakini pia itamkosa mshambuliaji kutoka Ivory Coast Kipre Bolou ambaye pia ni majeruhi lakini taarifa zilizotoka siku ya Ijumaa August 21 ni kuwa klabu ya Azam FC imeamua kumpeleka nyota huo Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi, kupitia afisa habari wa klabu hiyo Jaffar Iddi Maganga, Bolou atakaa Afrika Kusini kwa wiki mbili.
6Ikumbukwe kuwa Kipre Bolou ni ndugu wa damu na Kipre Tchetche ambao wote wanaitumikia klabu ya Azam FC ambayo ni makamu bingwa wa msimu uliopita na alikuwa bingwa wa msimu uliomalizika.


Meneja wa Chelsea Jose Mourinho amesema haikuwa nia ya Chelsea kuipiku Manchester United ili kumsaini Pedro kutoka Barcelona.
Man United walikuwa tayari wameshakubaliana na Barcelona kuhusu Uhamisho wa Pedro ambae nae alishaafika maslahi binafsi na Man United lakini Dakika za mwisho Chelsea ikaingia na kumsaini.
Habari toka Old Trafford zilitoboa kuwa Meneja Louis van Gaal ndie alieamua kutomsaini Pedro baada kubainika uhusiano wake wa karibu na Mchezaji mwingine wa zamani wa Barcelona, Kipa Victor Valdes, ambae yuko Man United lakini sasa ana bifu kubwa na Van Gaal kiasi cha kutimuliwa toka Timu ya Kwanza na sasa kuwekwa kwenye Listi ya Wachezaji wanaouzwa.
RATIBA:
Jumamosi Agosti 22

1445 Man United v Newcastle
1700 Crystal Palace v Aston Villa
1700 Leicester v Tottenham
1700 Norwich v Stoke
1700 Sunderland v Swansea
1700 West Ham v Bournemouth

Jumapili Agosti 23

1530 West Brom v Chelsea
1800 Everton v Man City
1800 Watford v Southampton

Jumatatu Agosti 24

2200 Arsenal v Liverpool



Klabu ya Manchester United ambayo msimu huu imedhamiria kupata saini za wachezaji mahiri watakaoweza kurejesha heshima ya kikosi chao kwani toka aondoke Sir Alex Ferguson, klabu hiyo imekuwa na wakati mgumu wa kurudisha makali yake ya awali.
manchester_united_logo_1280x1024
Njia pekee Man United walioamua kuitumia kukijenga upya kikosi chake ni kufanya usajili pekee ndio utakaoweza kuirudisha Man United katika ubora wake, kwa hivi siku za karibuni klabu ya Man United ilikuwa ikihitaji kuipata saini ya beki wa Real Madrid Sergio Ramos na kutumia kigezo cha Real Madrid kumtaka De Gea ili iweze kuwashawishi Real Madrid kumuachia beki huyo.
1420198841_extras_noticia_foton_7_2
Baada ya klabu ya Real Madrid kuweka ngumu na kugoma kumuuza beki huyo kwenda Man United na kumpa mkataba mpya, Man United waliamishia mawazo kwa beki kutokea Ureno anayeitumikia Real Madrid ya Hispania Pepe wakiwa na matumaini ya kumpata, August 21 Real Madrid wametangaza kumsainisha mkataba mpya beki huyo.
Jose Mourinho ni miongoni mwa makocha wanaopenda wachezaji wenye asili ya Afrika August 19 2015 habari za kumsajili beki wa kimataifa wa Ghana aliyekuwa anaichezea klabu ya FC Augsburg ya Ujerumani Baba Rahman na kujiunga na klabu ya Chelsea kwa ada ya uhamisho ya pound milioni 21.7.
2B78503700000578-3202562-image-a-28_1439923425179
Beki huyo wa Ghana mwenye umri wa miaka 21 huenda atapangwa kucheza beki ya kushoto namba ambayo ilikuwa ikichezwa na beki wa kihispania Cesar Azpiliceuta ambaye baada ya ujio wa Baba, Stamford Bridge Cesar Azpiliceuta ataenda kucheza upande wa  kulia.
Baba-Rahman-wanted-by-Chelsea
Klabu ya Chelsea ambayo imefanikiwa kumnasa Baba bado haijakata tamaa ya kusaka saini ya beki wa kiingereza anayeichezea klabu ya Everton John Stones licha ya ofa ya pound milioni 30 kukataliwa hivyo inajiandaa kutuma ofa nyingine ya pound milioni 40 ndani ya masaa 48.

waliotembelea blog