Wednesday, June 3, 2015



Rafa Benitez atambulishwa kuwa Kocha mpya wa Klabu ya Real Madrid leo, Asaini Mkataba wa miaka 3.


Leo hii Manchester United imeripotiwa kutoa Ofa ya Pauni Milioni 110 kwa ajili ya Gareth Bale na Raphael Varane.
Wawili hao pia wanahusishwa na kuhamia Chelsea. 

Lakini kwa mujibu wa Magazeti ya Spain, Cuatro na El Mundo, Real Madrid imeikataa Ofa hiyo ya Man United ya kuwanunua Bale na Varane ingawa wao wenyewe wanataka kufanya dili kumchukua Kipa wa Man United David De Gea.huko Brazil Chombo cha Habari Sambafoot kimedai Man United wako mstari wa mbele kumnasa Staa mpya wa Timu ya Taifa ya Brazil Roberto Firmino anaechezea Klabu ya Bundesliga huko Germany, Hoffenheim, kwa Dau la Pauni Milioni 18.
Roberto Firmino nae njiani kutua Man United

Real Madrid wameweka dau nzito na kutaka ndani ya wiki mbili Raheem Sterling asaini mkataba na timu hiyo ya Spain. Kutokana na Raheem kukataa kusaini mkataba mpya na Liverpool, club nyingi zimeonyesha nia ya kumsaini.
Real inategemea kufungua mazungumzo na Liverpool na kuwalipa €60 million (£45m) ili Raheem Sterling ahamie Real ndani ya wiki mbili zijazo.

waliotembelea blog