Wednesday, June 3, 2015


Leo hii Manchester United imeripotiwa kutoa Ofa ya Pauni Milioni 110 kwa ajili ya Gareth Bale na Raphael Varane.
Wawili hao pia wanahusishwa na kuhamia Chelsea. 

Lakini kwa mujibu wa Magazeti ya Spain, Cuatro na El Mundo, Real Madrid imeikataa Ofa hiyo ya Man United ya kuwanunua Bale na Varane ingawa wao wenyewe wanataka kufanya dili kumchukua Kipa wa Man United David De Gea.huko Brazil Chombo cha Habari Sambafoot kimedai Man United wako mstari wa mbele kumnasa Staa mpya wa Timu ya Taifa ya Brazil Roberto Firmino anaechezea Klabu ya Bundesliga huko Germany, Hoffenheim, kwa Dau la Pauni Milioni 18.
Roberto Firmino nae njiani kutua Man United

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog