Sunday, November 1, 2015


Pongezi!
Mabingwa Watetezi Chelsea leo hii wamefungwa Bao 3-1 wakiwa kwao Stamford Bridge na Liverpool na kuzidisha presha kwa Meneja wao Jose Mourinho.
Nascimento Ramires aliipa Chelsea Bao la Kwanza katika Dakika ya 4 baada ya kuunganisha Krosi ya Cesar Azpilicueta.
Dakika ya 48 Liverpool walisawazisha kwa Bao la Philippe Coutinho aliepokea pasi ya Roberto Firmino na kuachia kigongo cha Mguu wa Kushoto toka Mita 18.
Haftaimu Chelsea 1 Liverpool 1.
Kipindi cha Pili Liverpool waliongezi Bao 2 kupitia Coutinho na Christian Benteke na kumpa Meneja wao mpya Jurgen Klopp ushindi mtamu huku hali ikizidi kuwa tete kwa Jose Mourinho

Jose akibaki mdomo wazi hii leo baada ya kuchapwa bao 3-1 na LiverpoolPhilippe Coutinho akiifungia bao la pili Liverpool na kufanya 2-1, Bao la Chelsea lilifungwa mapema dakika ya 4 na Ramires nao Liverpool walifunguka na kuongeza mashambulizi na kupata bao mbili kupitia kwa Coutinho dakika ya 45 kipindi cha kwanza na lile la dakika ya 74. Bao la tatu lilifungwa na Christian Benteke aliyeingia kipindi cha pili na kuipa bao la tatu na kufanya 3-1 dhidi ya Wenyeji Chelsea na kwenye Uwanja wao Stamford Bridge.2-11-1
VIKOSI:
Chelsea:
Begovic, Zouma, Cahill, Terry, Azpilicueta, Mikel, Ramires, Willian, Oscar, Hazard, Diego Costa.
Akiba: Amelia, Baba, Matic, Fabregas, Kenedy, Falcao, Remy.

Liverpool: Mignolet, Clyne, Skrtel, Sakho, Moreno, Lucas, Can, Milner, Lallana, Coutinho, Firmino.
Akiba: Bogdan, Lovren, Benteke, Allen, Ibe, Teixeira, Randall.
Refa: Mark Clattenburg


Kwa sasa kocha wa klabu ya Chelsea ya Uingereza Jose Mourinho anahusishwa na kutaka kufutwa kazi endapo tu atapoteza mchezo dhidi ya Liverpool licha ya kuwa taarifa hizo sio rasmi. October 30 mtandao wa mirror.co.uk uliripoti kuwa klabu ya Real Madrid ya Hispania inamuhitaji Jose Mourinho arudi kuifundisha timu yao sambamba na kuombwa hamshawishi Eden Hazard kwenda Real Madrid.
October 31 Rais wa zamani wa Real Madrid ya Hispania Ramon Calderon amesema kuwa Jose Mourinho anakaribishwa tena Santiago Bernabeu kauli ambayo inaongeza nguvu tetesi za kuwa Jose Mourinho huenda akarudi Hispania kuifundisha timu hiyo.
jose-mourinho-chelsea-lam-437576 (1)
Ramon Calderon alifika mbali zaidi kwa kusema kuwa kocha wa sasa wa klabu hiyo Rafael Benitez alikuwa chaguo la nne baada ya Jose Mourinho, Joachim Low na Jurgen Klopp  kuhusishwa kutaka kuingia mkataba wa kutaka kuifundisha timu hiyo katika msimu wa 2015/2016.
Real Madrid's new President Ramon Calderon unveils Fabio Capello as the new manager of Spanish football club Real Madrid at the Santiago Bernabeu in Madrid, 06 July 2006. Capello signed a three year contract with Real and is expected to try and strengthen Madrid's midfield by targeting Lyon's Malian Mahamadou Diarra and Brazil's Emerson of Juventus in an attempt to end their three trophyless seasons. AFP PHOTO/PIERRE-PHILIPPE MARCOU
Ramon Calderon 
“Kiukweli Rafael Benitez alikuwa chaguo la nne kwa Real Madrid, nafikiri Perez bado anajaribu kutaka kumrudisha Mourinho Real Madrid, kiukweli anampenda, mimi sio shabiki wa Mourinho ila kwa rekodi aliyoiweka klabuni hapa kwa kipindi cha miaka mitatu sio vibaya akirudi” >>>Ramon Calderon

waliotembelea blog