Sunday, July 17, 2016



July 17 2016 headline kutoka Ikulu Dar es salaam ni pamoja na hii Rais John Pombe Magufuli kumteua Profesa Longinus Rutasitara kuwa makamu mwenyekiti wa bodi ya mamlaka ya usafiri wa anga (TCAA), Rutasitara anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Nyamajeje Weggoro ambaye muda wake umemalizika.
Pia Rais Magufuli amempandisha cheo kamishna msaidizi wa Polisi (ACP) Kedmon Mnubi kuwa kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi (SACP)
WhatsApp-Image-20160717
JK Comedian ni mchekeshaji ambaye amebarikiwa kipaji cha kuweza kuigiza sauti za watu mbalimbali wakiwemo mastaa wa Tanzania, leo katuonyesha ubora wake kwa kuziigiza sauti za wachekeshaji wa kundi la original comedy linaloundwa na mastaa kama vile Masanja, Joti, Mpoki, Wakuvanga na Makregani.
Unaweza kumtazama kwenye hii video hapa chini kisha niachie comment yako ukiniambia ni sauti ya nani katisha nayo zaidi…

Friday, July 8, 2016


Nyota wa soka aliyefanya vizuri michezo ya Shule za Sekondari (UMISETTA) Mussa Bakari akiwasili ndani ya uwanja cha ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kutokea katika kambi ya Kimataifa ya Copa Coca-Cola iliyofanyika jijini Paris nchini Ufaransa. 
Meneja Msaidizi wa Chapa ya Coca – Cola, Mariam Sezinga (kushoto) akimpokea kwa shangwe nyota wa soka aliyefanya vizuri michezo ya Shule za Sekondari (UMISETTA) Mussa Bakari (katikati) mara baada ya kuwasili ndani ya uwanja cha ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kutokea katika kambi ya Kimataifa ya Copa Coca-Cola iliyofanyika jijini Paris nchini Ufaransa. Pembeni ni Pamela Lugenge (kulia) mmoja wa Afisa Masoko. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog. 
Meneja Msaidizi wa Chapa ya Coca – Cola, Mariam Sezinga (kushoto) akimkabidhi taji la maua nyota wa soka aliyefanya vizuri michezo ya Shule za Sekondari (UMISETTA) Mussa Bakari mara baada ya kuwasili ndani ya uwanja cha ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kutokea katika kambi ya Kimataifa ya Copa Coca-Cola iliyofanyika jijini Paris nchini Ufaransa. Pembeni ni Pamela Lugenge (kulia) mmoja wa Afisa Masoko. 
 Meneja Msaidizi wa Chapa ya Coca – Cola, Mariam Sezinga (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na nyota wa soka aliyefanya vizuri michezo ya Shule za Sekondari (UMISETTA) Mussa Bakari (katikati) pamoja na Pamela Lugenge (kulia) mmoja wa Afisa Masoko.



Waziri wa Habari, sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnaye akizungumza katika uzinduzi wa mashindano ya magari jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Habari, sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnaye akiwa amenyanyua bendera ya Taifa juu kuashiria uzinduzi wa Mashindano ya Mbio za Magari ya 2016 jijini Dar es Salaam leo .Kulia kwa Nape ni Katibu wa Balaza la Michezo Tanzania(BMT), Mohamed Kiganja. 

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye amezindua mashindano ya magari ya hapa nchini  ya 2016 na kuwataka watazania kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye mchezo huo ambapo amewataka kuacha kujiweka nyuma na kuitwa kichwa cha mwendawazimu kila siku. Hayo ameyasema wakati akizindua mashindano hayo ya magari yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho wilaya ya Bagamoyo ikihusisha magari 25.

Nape amesema kuwa wanachotaka kuona ni kuwa Tanzania inafanya vizuri kwenye mashindano hayo na zaidi wanataka kuona wanazidi kuwavutia wageni kwenye mashindano hayo ili kuongeza utalii wandani na kuongeza pato kwa serikali pale watakapoamua kutembelea mbuga za wanyama. 

“Nawataka watanzania kuzidi kufanya vizuri kwenye mashindano na zaidi wawavutie wageni kwani watakapokuja kwa wingi wataongeza pato la taifa pale watakapotembelea hifadhi za taifa,”amesema. 

Naye  Rais wa chama cha Magari Tanzania (AAT), Bwana Nizar Jivani amesema kuwa mwaka jana waliweza kuondoa kauli ya kichwa cha mwendawazimu na walilitekeleza kama walivyomuahidi Raisi mstaafu wa awamu ya Pili Ally Hassan Mwinyi na mwaka huu watazidi kufanya vizuri na watabakisha ushindi nyumbani. Mashindano hayo yamezingatia viwango vyote ambapo jumla ya magari 25 yatashiriki ambapo kati  ya magari hayo, Magari 4 yatatoka Uganda, 2- Zambia, Kenya (1), Falme za Kiarabu (1). Na kwa magari ya kutoka Tanzannia ni  17.

Magari hayo  17  ya Tanzania ambapo  Dar es Salaam  magari 10, Arusha (3), Moshi (3), na Tanga (1). Aidha, magari hayo yanatarajiwa kushindana katika umbali wa kilometa 246 kwa siku ya kwanza na yatakuwa kwa muda wa siku mbili.


Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp ameweka kandarasi mpya ya miaka sita na mmiliki wa klabu hiyo akisema ingekuwa makosa kutompatia kandarasi ndefu.
Klopp alijiunga na Liverpool mnamo mwezi Oktoba ,baada ya kukubali mkataba wa pauni milioni 15 ambao umeongezwa hadi mwaka 2022.
''Uongozi wake utakuwa muhimu katika kufanikisha malengo yetu'',  alisema mmiliki wa Liverpool.

Klopp aliifikisha Liverpool katika fainali ya League Cup pamoja na fainali ya Europa League msimu uliopita.

Raia huyo wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 49 aliisaidia Borussia Dortmund kushinda mataji mawili ya Bundesliga pamoja na kucheza fainali ya vilabu bingwa Ulaya 2013.


Pep Guardiola held his first news conference since taking over as Manchester City manager, on FridayPepMkufunzi mpya wa Manchester City Pep Guardiola anasema kuwa alienda nchini Uingereza kuthibitisha kuwa inawezekana kucheza mchezo mzuri katika ligi ya Uingereza.
Gurdiola mwenye umri wa miaka 45 ambaye ametia kandarasi ya miaka mitatu ,amesema kuwa alipendelea kusalia kuifunza Bayern Munich,lakini alitaka mtihani mwengine katika ukufunzi wake.

Raia huyo wa Uhispania amekiri kwamba alikuwa na kila alichohitaji wakati alipokuwa Barcelona ,lakini akakana kuwa huenda anakabiliwa na kibarua kigumu katika klabu ya Manchester City.
''Niko hapa kuthibitisha kuwa ninaweza kuchezesha soka nzuri vilevile nimekuwa nikicheza'',alisema.

Alipoulizwa iwapo anaweza kuanzisha mtindo mzuri wa tiki-taka kama ule wa Barcelona, alisema Guardiola:''Hiyo ndio sababu niko hapa''.
Aliongezea:''Sijawahi kucheza wakati wa siku kuu ya Boxing Dei.Sijawahi kuwa katika uwanja wakati ambapo kuna upepo mkali na baridi na uwanja sio mzuri.Ni lengo langu. Nataka kuwathibitishia'


Baada ya tetesi za muda mrefu, hatimaye Mecky Maxime ametua Kagera Sugar. Maxime ambaye alikuwa akiinoa Mtibwa Sugar, sasa amesaini mkataba wa kuinoa Kagera Sugar. Meneja wa Kagera Sugar, Mohammed Hussein amesema Maxime ndiye kocha mkuu akichukua nafasi ya Adolf Rishard.
Awali, kulikuwa na taarifa za kuondoka kwa Maxime kwenda Kagera, lakini uongozi wa Mtibwa Sugar ulilikataa hilo. Kuna tarifa Mtibwa Sugar inatarajia kumrejesha Salum Mayanga ambaye sasa anainoa Prisons.

Tuesday, July 5, 2016



Oleksandr Zinchenko Kutoka FC Ufa kwenye Ligi ya premia ya Russian ambaye kwa sasa ana miaka 19.




Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande akizungumza kuhusu msaada ambao wameutoa kwa kituo cha Al--Madina.

Zikiwa zimesalia siku kadhaa kabla ya kusherekea sikukuu ya Eid El Fitri, Kampuni ya Multichoice Tanzania ambao ndiyo wasambazaji wa ving'amuzi vya DSTV nchini imetoa msaada wa vitu mbalimbali kwa watoto yatima ambao wanaishi katika kituo cha Al-Madina kilichopo Tandale kwa Tumbo, misaada ambayo kwa namna moja au nyingine inaweza kusaidia kubadilisha maisha ya watoto hao.
Misaada ambayo imetolewa kwa watoto hao ni Cherehani 4, kapeti 12, vikombe 60, sahani 40, magodoro 11, shuka 40, tenga za nguo 3, jagi 6, beseni kubwa 3, sufuria 9, chupa za chai 4 na mikeka 6.
Akizungumzia misaada hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande alisema msaada huo ni mwendelezo wa misaada ambayo Multichoice imekuwa ikitoa kwa kituo hicho kwa lengo la kuwasaidia kuishi maisha bora lakini pia kuwapatia msaada ambao unaweza kuwasaidia kuwa na uwezo wa kuingiza kipato.
"Multichoice tumekuwa tukitoa misaada yetu kwa kituo hiki tangu 2009 na leo tumewaletea mwingine ikiwa ni kila mwaka tunafanya hivyi lakini kwa mwaka huu tumeleta pia Cherehani ambazo zitawasaidia kupata kipato,
"Pamoja na hayo pia tumewafungia king'amuzi ambacho watoto watakuwa wakiangalia vipindi balimbali baada ya kurejea nyumbani na tuna chaneli mbalimbali za vipindi vya watoto na burudani kwahiyo tunaamini kuwa watoto watafurahi," alisema Chande.
Nae mlezi wa kituo hicho, Bi. Kuruthum Yusuf aliwataja Multichoice kama kampuni ambayo imekuwa mstari wa mbele kuwapatia misaada na kuyaomba makampuni mengine kuwa na utaratibu kama wa Multichoice wa kuwasaidia misaada kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watoto ambao wanahitaji misaada ili kuboresha maisha yao.

Mlezi wa kituo cha watoto yatima cha Al-Madina akizungumza kuhusu msaada ambao wamepokea na jinsi ambavyo Multichoice Tanzania imekuwa ikiwapatia misaada. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Mharage Chande.

"Tangu walipotufahamu wamekuwa wakitupatia misaada kila mwaka, niwashukuru sana kwa moyo wao na kutoa sio utajiri ila tu wana moyo wa kutoa na hata wenngine wanatakiwa kuwa na moyo kama wao (Multichoice) wa kusaidia," alisema Bi. Kuruthum.
Pamoja na hayo pia, Bi. Kuruthum alieleza kuwa kwa sasa bado wanakabiliwa na changamoto ya vifaa vya shuleni kwa watoto ambao wanasoma.
Kutokana na msaada ambao umetolewa na Multichoice kwa watoto wa kituo cha Al-Madina ambacho kina watoto 57, wasichana wakiwa ni 23 na wavulana ni 34 basi ni wazi kuwa kama wakitumia msaada huo vyema basi kwa namna moja au nyingine wanaweza kubadilisha maisha yao kwa hatua fulani ambayo awali hawakuwa nayo kama vile kutumia cherehani kwa kushona nguo na kujiongezea kipato.

Meneja Uhusiano na Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Sumalu akitoa neno la ufunguzi kuhusu misaada ambayo imekuwa ikitolewa na Multichoice Tanzania pamoja na historia fupi ya kituo hicho.

Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Mharage Chande akimkabidhi Cherehani, mlezi wa kituo cha Al-Madina, Kuruthum Yusuf. Wa tatu kushoto ni Meneja Uhusiano na Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu wakiwa na wafanyakazi wengine wa Multichoice Tanzania.

Meneja Uhusiano na Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu akimpongeza mlezi wa kituo cha Al-Madina, Kuruthum Yusuf baada ya kukabidhiwa misaada na Multichoice Tanzania.

Wafanyakazi wa Multichoice Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima wanaoishi katika kituo cha Al-Madina.

Meneja Uhusiano na Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu akiwaelekeza jambo watoto wanaoishi katika kituo cha Al-Madina.

Watoto yatima wanaoishi katika kituo cha Al-Madina wakiwa katika picha ya pamoja.

Mwonekano wa vitu vilivyotolewa na Multichoice Tanzania kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Al-Madina.

DIRISHA la Uhamisho la Ligi Kuu England limefunguliwa rasmi Julai 1 na litafungwa Agosti 31.
Klabu kadhaa zimeshavamia Soko na kununua na pia kuuza Wachezaji.

PATA DILI ZILIZOKAMILIKA HADI SASA:
AFC Bournemouth
MPYA

Emerson Hyndman (Fulham) Bure
Nathan Ake (Chelsea) Mkopo
Lys Mousset (Le Havre) ADA HAIKUTAJWA

NJE
Sylvain Distin (Ameachwa)
Tommy Elphick (Aston Villa) ADA HAIKUTAJWA
Matt Ritchie (Newcastle United) ADA HAIKUTAJWA

Arsenal
MPYA

Granit Xhaka (Borussia Monchengladbach) ADA HAIKUTAJWA

NJE

Mikel Arteta (Ameachwa)
Tomas Rosicky (Ameachwa)
Mathieu Falmini (Ameachwa)
Daniel Crowley (Oxford United) Mkopo

Burnley
MPYA

Robbie Leitch (Motherwell) Bure
Jamie Thomas (Bolton Wanderers) Bure

Chelsea
MPYA
Meneja:
Antonio Conte

NJE
Lewis Baker (Vitesse Arnhem) Mkopo
Nathan Ake (Bournemouth) 


Crystal Palace
MPYA
Andros Townsend (Newcastle United) Pauni Milioni 13

NJE
Dwight Gayle (Newcastle United) Pauni Milioni 10

Everton (evertonfc.com)
MPYA
Meneja:
Ronald Koeman
Bassala Sambou (Coventry City)
Chris Renshaw (Oldham Athletic) ADA HAIKUTAJWA
Maarten Stekelenburg (Fulham) ADA HAIKUTAJWA

NJE

Steven Pienaar (Ameachwa)
Leon Osman (Ameachwa)
Tony Hibbert (Ameachwa)

Leicester City
MPYA

Ron-Robert Zieler (Hannover 96) ADA HAIKUTAJWA
Luis Hernandez (Sporting Gijon) Bure
Raul Uche Rubio (Valencia) ADA HAIKUTAJWA
NJE
Andrej Kramaric (Hoffenheim) ADA HAIKUTAJWA


Zlatan Ibrahimovic of Manchester United poses after signing for the club at Aon Training Complex on July 1, 2016 in Manchester, England.
Zlatan Ibrahimovic

Taarifa za awali ambazo zimeripotiwa hivi punde ni kuhusu ajali iliyohusisha mabasi mawili, Kamanda polisi mkoa wa Singida, Thobias Sedoyeka amesema ajali ya basi namba T 531 BCE likitokea Dar es salaam kwenda Kahama na T 247 lililokuwa linatoka kahama kwenda Dar es salaam yote ya kampuni moja ya City Boys yamegongana uso kwa uso na kusababisha vifo vya watu 24 papo hapo na wengine kadhaa kujeruhiwa.
IMG-20160704-WA0027
.
IMG-20160704-WA0026 IMG-20160704-WA0028 IMG-20160704-WA0029 IMG-20160704-WA0031 IMG-20160704-WA0033 IMG-20160704-WA0036 IMG-20160704-WA0038

Sunday, July 3, 2016


Wanafunzi wa chuo Cha Uhasibu (TIA), jijini Dar es Salaam, wakipatiwa maelezo ya huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko wa Pensheni wa PSPF walipotembelea banda la Mfuko huo lililoko jingo la Wizara ya fedha kwenye maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, 2016 viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam Julai 2, 2016.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama, (kulia), akizungumza jambo wakati alipotembelea banda la Mfuko wa Pensheni wa PSPF kwenye jingo la wizara ya fedha viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam Julai 2, 2016 ambako yanafanyika maonyesho ya 40 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam. Hapa waziri akipatiwa maelezo na Afisa Uendeshaji wa PSPF, Hadji Hamisi Jamadari


Afisa Kumbukumbu wa Mfuko Pensheni wa PSPF, Lupakisyo J. Mwaipungu (kushoto), akimsikiliza Mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo na kuamua kujiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari PSS Julai 2, 2016



Afisa Msaidizi wa Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Mohamed Siaga akifurahia huku kionyesha tuzo walizokabidhiwa.
Baadhi ya wafanyakazi wa PPF wakiwa na furaha baada ya kukabidhiwa kikombe chao
Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio, akihojiwa na Waandhi wa habari baada ya Mfuko wake kukabidhiwa Kikombe cha ushindi wa kwanza wa Kundi la Mifuko ya Hifadhi ya jamii na Makampuni ya Bima katika Maonesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba.
Picha ya pamoja.
Meneja Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni w PPF, Lulu Mengele, akimuongoza Mkurugenzi Mkuu wa PPF William Erio (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof. Godious Kahyarara (katikati) walipokuwa wakitembelea Banda la Mfuko huo kwenye maonesho ya Biashara ya Kimataifa viwanja vya Sabsaba.

Maafisa wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Saluna Aziz Ally (kulia) na Glory Maboya, wakiendelea kutoa huduma kwa wateja wao waliofika katika Banda la maonesho Sabasaba la mfuko huo.

Sehemu ya Wananchi wakiwa ndani ya Banda la PPF wakipata huduma na maelezo kuhusu namna ya kujiunga na mfuko huo na jinsi wanachama wanavyoweza kufaidika kupitia michango yao.
.

Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Sostenes Lyimo, akitoa maelezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof. Godious Kahyarara, na wasaidizi wake wakati walipotembelea katika Banda la Maonesho la Mfuko huo kwenye Viwanja vya Sabasaba jana

waliotembelea blog