Thursday, November 5, 2015

DSC_0168

Mwanamuiki nyota nchini Tanzania, Nassib Abdul ama Diamond Platnumz akiongea na waandishi wa habari
KAMPUNI ya MultiChoice Tanzania mapema jana imezindua ofa kabambe za msimu wa siku kuu huku ikimtambulisha rasmi Mwanamuziki Diamond Platnumz kuwa balozi maalum wa bidhaa za kampuni hiyo ikiwemo kifurushi cha DSTV BOMBA chenye chaneli zaidi ya 65 ikiwemo huduma ya vituo kadhaa vya televisheni za hapa nchini.

Akimtambulusha rasmi Meneja Masoko wa kampuni hiyo, Furaha Samalu, amemtambulisha Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuwa balozi wa king’amuzi hicho na kutaja gharama zake kuwa ni shilingi 23,500/= kwa malipo ya mwezi na king’amuzi chenyewe kinapatikana kwa shilingi 79,000/= na kuwataka wananchi kuchangamkia huduma hiyo muhimu katika msimu huu wa ofa za sikukuu.

Meneja masoko huyo ameongeza kuwa, kifurushi hicho kimesambaa nchini mbalimbali barani Afrika hivyo wasanii wa filamu, muziki na wengineo ambao watang’aa kwenye vipindi hivyo watakuwa wakionekana pande mbalimbali barani Afrika na hivyo kuwapatia umaarufu na kuwaongezea soko la kazi zao.
DSC_0151
Mwanamuziki Diamond Platinumz akisoma kipeperushi chenye maelezo juu ya ofa mbalimbali za DStv wakati wa utambulisho wa ofa za sikukuu pamoja na kutangazwa kwa balozi huyo wa bidhaa za DSTV. Katikati Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu na kushoto ni Meneja Mwendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.
DSC_0233
Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu akifafanua jambo katika mkutano huo na kushoto ni Meneja Mwendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo na upande wa kulia ni msanii Diamond Platnumz balozi wa bidhaa za DSTV.
DSC_0159
Meneja mauzo wa DSTV, Bw. Salum Salum akifafanua jambo juu ya ofa hiyo mpya na mahaala wanapopatikana nchini kwa mawakala wote ambapo amewaomba watanzania kuchangamkia ofa ya kuunganishwa haraka huduma bora zaidi za chaneli za kisasa kupitia DSTV.
DSC_0174
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia mkutano huo wa DSTV..

DSC_0176
Mwandishi wa gazeti la Raia Tanzania akiuliza swali juu ya bidhaa za DSTV..
DSC_0171
Mpiga picha wa Magazeti ya Habari leo, Fadhili Akida akiuliza swali katika mkutano huo wa DSTV..
DSC_0185
Ilifika wakati wa zawadi.. Diamond akisoma jina la mwandishi wa habari aliyeshinda zawadi hiyo..
DSC_0190
Diamond Platnumz akimkabidhi mwandishi wa habari, Sangu Joseph king'amuzi alichojishindia katika droo iliyochezeshwa wakati wa mkutano huo.
DSC_0196
Diamond akikabidhi zawadi ya King'amuzi cha DSTV kwa mwandishi wa habari Rajab Musa baada ya kushinda..
DSC_0204
Diamond akikabidhi zawadi ya king'amuzi kwa mwandishi wa habari, Joseph Mchekadone baada ya kushinda..
DSC_0205
Diamond Platnumz akimkabidhi king'amuzi mwanahabari wa ITV, Ester Sangai baada ya kuibuka mshindi..
DSC_0165
Meneja mauzo wa DSTV, Bw. Salum akisisitiza juu ya ofa hiyo ambapo ameeleza kuwa wateja watapa kujionea chaneli mbalimbali zenye mvuto na picha za kuvutia huku bidhaa zake zikiwa ni tofauti kabisa na zingine.

jeff
Mwanamuziki aliyewahi ishi nchini Tanzania na pia mwenye asili ya Congo, Jeff Maximum ambaye anaishi Ughaibuni katika shughuli zake za Muziki katika pozi ambapo kwa sasa ameachia video ya wimbo wake mpya wa "Mama Afrika" ambao wimbo huo unatangaza Utalii wa Tanzania.


Mwanamuziki anayefanya kazi zake nchini Marekani na Dubai, Jeff Maximum tayari ameshaachia video ya wimbo wake mpya uitwao “Mama Afrika” ambao umetayarishwa Bagamoyo Nchini Tanzania hivi karibuni.

Kwa mujibu wa Jeff anaweka wazi kuwa, kuwa video hiyo iliyoachiwa Novemba 2 mwaka huu, tayari imeshaanza kuonekana katika vituo mbalimbali vya televisheni Bara la Afrika ikiwemo nchini, pia katika nchi za Nigeria, Afrika Kusini, Kongo, Ghana, Kenya na kwingineko.

Pia video hiyo inaonekana katika vituo vya televisheni vya nchini Uingereza, Dubai, Amerika na kwingineko huku ikitangaza utalii wa Tanzania kwa asilimia kubwa.Jeff anaweka wazi kuwa, aliamua kuitayarishia video hiyo nchini Tanzania kwa kuwa ni kati ya nchi nyingi anazozipenda zaidi Barani Afrika.

Na kuongeza kuwa, video hiyo imetengenezwa na mwongozaji anayechipukia kutoka Tanzania Hanscana (Wanene Films), huku audio yake ikiwa imetayarishwa katika studio yake iliyopo nchini Dubai



Ushirikina ni jambo ambalo limekuwa likihusishwa kwa kiasi kikubwa katika soka hususani barani Afrika, hata katika timu zetu za Ligi Kuu Tanzania bara zimekuwa zikifanya baadhi ya vitu ambavyo vinahusishwa na imani za kishirikina, millardayo.com ilipata bahati ya kufanya exclusive interview na Gaudence Mwaikimba kuhusu ishu za ushirikina katika soka.
DSC_0008
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Gaudence Mwaikimba ni mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Dar Es Salaam Young Afrika, Azam FC na timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, Mwaikimba kwa sasa anachezea klabu ya JKT Ruvu ila ni kweli anaamini ushirikina katika soka yeye kama mchezaji mkongwe?
Mwaikimba amekiri katika soka kuwa na imani za kishirikina ila yeye haamini kama inaweza msaidia mtu kucheza vizuri au kufunga magoli katika mechi, ila amewahi kushuhudia mtu akianguka uwanjani baada ya kuingia na irizi ila baadae alianguka na kuanza kutoa mapovu mdomoni.
m_Atlabara-Azam-Fc-share-spoils
“Ndio maana hadi leo mimi siamini ushirikina katika soka kwani nimewahi kushuhudia mtu akianguka uwanjani sababu ya hivyo vitu ila ilikuwa Ligi daraja la tatu, ilikuwa ni mtu kaweka irizi mguuni, mwisho wa siku akapigana kibuyu na mchezaji wa timu yetu akaanguka na kuanza kutoa povu kumvua soksi akakutwa na irizi” >>> Mwaikimba



Usiku wa November 4 kulichezwa michezo kadhaa ya mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya na tuliona baadhi ya vilabu vikiondoka na point tatu kwa furaha na timu nyingine zikiondoka vichwa chini baada ya kupoteza michezo hiyo, Usiku wa November 5 mechi za UEFA ndogo zilipigwa kama kawaida.
2198682_heroa
Klabu ya Liverpool ya Uingereza ililazimika kusafiri hadi Urusi kucheza na Rubin Kazan katika muendelezo wa mechi za Kundi B, Liverpool wakiwa ugenini wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 1-0, licha ya kuwa walikuwa ugenini Liverpool walifanikiwa kuibuka na point tatu mbele ya Rubin Kazan.
3000
Hadi dakika 45 za kwanza zinamalizika hakuna timu iliyokuwa imefanikiwa kuona lango la mpinzani wake, kipindi cha pili kilianza kwa kila timu kucheza kwa tahadhari, kabla ya dakika ya 52 Liverpool walifanikiwa kupata goli la kwanza kupitia kwa Jordon Ibe, goli ambalo lilidumu kwa dakika zote 90.
3000 (1)
Baadhi ya Matokeo ya mechi nyingine za UEFA EUROPA LEAGU November 5
  • Ajax 0 – 0 Fenerbahce
  • Celtic 1 – 2 Molde
  • Sion 1 – 1 Bordeaux
  • Borussia Dortmund 4 – 0 FK Qabala
  • FC Krasnodar 2 – 1 PAOK Thessaloniki FC
  • Club Brugge 1 – 0 Legia Warszawa
  • SSC Napoli 5 – 0 FC Midtjylland
  • Dinamo Minsk 1 – 2 Villarreal
  • Viktoria Plzen 1 – 2 Rapid Wien
Magoli ya Rubin Kazan Vs Liverpool


Mshambuliaji wa kimataifa wa Ureno anayekipiga katika klabu ya Real Madrid ya Hispania Cristiano Ronaldo kauli yake imeingia katika headlines usiku wa November 5 baada ya kuanza kuizungumzia klabu yake ya zamani ya Manchester United ya Uingereza.
Staa huyo wa Real Madrid amekiri kuwa Man United ina kazi nzito ya kufanya ili irejee katika kiwango chake cha juu kilichozoeleka, Ronaldo ambaye amekiri kuumia akiona Man United haifanyi vizuri kama zamani aliwahi kucheza Man United katika kipindi cha mwaka 2003 hadi 2009 na alishinda mataji matatu ya Ligi Kuu Uingereza na moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya.
2ADB00CB00000578-0-image-m-11_1437931908574
“Kiukweli nataka kuona Man United ikiwa katika kiwango cha juu kama ilivyokuwa zamani, kwa mfano Sporting Lisbon ilikuwa ni klabu yangu ya kwanza na napenda kuona ikiwa katika viwango vya juu, kuhusu kurudi Man United nipo vizuri hapa hakuna anayejua kitu cha mbele katika maisha kama nilivyosema awali mimi bado na mkataba na Real Madrid najisikia furaha hapa”>>> Cristiano Ronaldo
Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars inayojiandaa kwa ajili ya mchezo wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2018 dhidi ya Algeria, imeendelea na mazoezi ya kujiweka sawa kuelekea mchezo huo utakaopigwa November 14 uwanja wa Taifa Dar Es Salaam na November 17 kurudiana Algeria.
IMG_0029
Kabla ya kucheza mchezo huo Taifa Stars itacheza mchezo mmoja wa kirafiki Jumapili ya November 8 dhidi ya timu ya chuo kikuu cha Pretoria  Tucks FC jijini Johannesuburg Afrika Kusini, kocha wa Taifa Stars Charles Mkwasa ameomba kucheza mchezo huo ili kupata nafasi ya kuangalia kikosi chake kabla ya mchezo na Algeria.
IMG_0058
Taifa Stars wapo Johannesuburg Afrika Kusini kwa kambi ya siku 10 kabla ya kurejea Dar Es Salaam kucheza mechi dhidi ya Algeria, Stars inafanya mazoezi asubuhi na jioni kwa ajili ya kujiweka sawa na inatumia viwanja vya St. Peters College na kituo cha michezo cha Edenvale.
IMG_0043 (1)
IMG_0066
IMG_0039
IMG_0072
IMG_0086
IMG_0126
IMG_0131
IMG_0124
IMG_0107


Mwigizaji wa Hollywood, Marekani, Lupita Nyong’o aliweka headlines kubwa sana Africa na dunia nzima baada ya staa huyo kucheza movie iliyoingiza mamilioni ya faida kwenye movie Industry ya Hollywood, 12 Years A Slave, movie ambayo pia ilimuwezesha Lupita kupata tuzo ya Oscars mwaka 2014 kama Best Supporting Actress.
Nimekutana na interview moja aliyofanya Lupita Nyong’o na ndani yake amezungumzia vitu vingi ikiwemo, ilikuwaje akapata nafasi ya kucheza script ya movie hiyo na kama ana mipango ya kuja kucheza movie itakayopita kiwango chake kwenye 12 Years A Slave?
LUPITA
Kuhusu kupata nafasi ya kucheza script ya movie ya 12 Years A Slave, Lupita Nyong’o alisema…
>>> nilisikia kuhusu auditions za movie hiyo sema sikuwa New York so nikaipotezea, lakini manager wangu D.D Ray alifanikiwa kuipata ile script kwa ajili ya mteja wake mwengine ndipo alipo kutana na “Patsey” character ambaye alihisi nitaweza kumcheza… nikarekodi mkanda ya kwanza ya role hiyo na ikatumwa kwa manager wangu wa New York, baada ya wiki moja nikaitwa New York kwenye auditions za mwisho na baada ya kukaa kwa saa nzima kwenye foleni nikafanikiwa kupita, na wiki mbili baadae nikapigiwa simu kwenda kukutana na producer wa movie ili kuanza rasmi…<<< Lupita Nyong’o.
attends the 14th annual AFI Awards Luncheon at the Four Seasons Hotel Beverly Hills on January 10, 2014 in Beverly Hills, California.
Badaae Lupita akaulizwa kama atakuja kucheza movie itakayovuka kiwago chake kwenye movie ya 12 Years A Slave movie iliyomuwezesha apate tuzo kubwa ya Oscars, msanii huyo kutoka Kenya alikuwa na haya ya kusema…
>>> ” Sijui kama kuna movie nitakayokuja kucheza ikavuka levo ya 12 Years A Slave, sidhani! Movie ya 12 Years A Slave ipo kwenye levo ya juu sana, stori yake iligusa wengi duniani na imenifungulia milango mingi… lakini kuja kucheza movie ya kuzidi kiwango kile haitokuja kutokea kwa sababu experience niliyoipata ni ya kipekee sana, japo nataka kucheza role tofauti za movie na pia kujaribu character tofauti, na ninashukuru kwa sababu sasa hivi nimepata fursa ya kufanya hivyo na kutanaua kipaji changu...” <<< Lupita Nyong’o.
LUPITA2
Ukiacha 12 Years A Slave, movie nyingine zilizochezwa na Lupita Nyong’o ni pamoja na; Star Wars Episode VII – The Force Awakens inayotegemea kuwa sokoni tarehe 15 December 2015 na The Jungle Book inayotegemea kutoka tarehe 07 April 2016.

USIKU WA EUROPA LEO – TIMU KUTAFUTA POINTI MUHIMU, NANI KUFUZU, NANI KUFELI?

Borussia Dortmund, Napoli, Rapid Wien na Braga ni miongoni mwa Timu zinazoweza kufuzu Usiku huu huku wakibakisha Mechi 2 mkononi za Makundi yao.
Leo zinachezwa Mechi za 4 za Makundi na Timu 9 kati ya 48 zinaweza kufuzu hii Leo wakati Timu 5 zinaweza kutupwa nje ya Mashindano hayo hii Leo.

IFUATAYO NI TATHMINI TOKA KILA KUNDI:
Kwenye Mabango ni Pointi za Timu.

KUNDI A:
Celtic (2) v Molde (7)
Ajax (2) v Fenerbahçe (4)


-Ikiwa Molde watashinda na Ajax hawashindi, Molde watafuzu.

KUNDI B:
Rubin (2) v Liverpool (3)
Sion (7) v Bordeaux (2)
 

-Sion wakishinda wamefuzu.
KUNDI C:
Krasnodar (4) v PAOK (3)
Borussia Dortmund (7) v Qäbälä (1)
-Ikiwa Dortmund na Krasnodar watashinda, basi Dortmund watafuzu.

KUNDI D:
Club Brugge (1) v Legia Warszawa (1)
Napoli (9) v Midtjylland (6)
-Ikiwa Napoli watashinda, wamefuzu.
-Ikiwa Brugge v Legia ni Sare, Napoli wamepita.
-Ikiwa Midtjylland watashinda na Gemu nyingine Sare, wote Napoli na Midtjylland watafuzu

-Ikiwa Midtjylland watashinda, basi kipigo kwa Brugge au Legia kitamtupa nje aliefungwa.

KUNDI E:
Dinamo Minsk (0) v Villarreal (6)
Viktoria Plzeň (3) v Rapid Wien (9)
-Ikiwa Rapid watashinda, watafuzu.
-Ikiwa Dinamo watafungwa, watatupwa nje.

KUNDI F:
Marseille (3) v Braga (9)
Groningen (1) v Slovan Liberec (4)
-Ikiwa Braga watashinda, watafuzu.

KUNDI G:
Rosenborg (1) v Lazio (7)
Saint-Étienne (4) v Dnipro Dnipropetrovsk (4)
Kundi lipo wazi.

KUNDI H:
BeÅŸiktaÅŸ (5) v Lokomotiv Moskva (7)
Skënderbeu (0) v Sporting CP (4)

-Ikiwa Lokomotiv watashinda na Sporting hawashindi, basi Lokomotiv watafuzu.
-Ikiwa Skënderbeu wtafungwa basi wako nje.

KUNDI I:
Belenenses (4) v Basel (6),
Lech Poznań (4) v Fiorentina (3)
-Kundi lipo wazi.

KUNDI J:
QarabaÄŸ (3) v Monaco (5),
Tottenham Hotspur (4) v Anderlecht (4)
-Kundi lipo wazi.

KUNDI K:
Sparta Praha (5) v Schalke (7)
Asteras Tripolis (1) v APOEL (3)
-Ikiwa Schalke watashinda, watafuzu.
 

KUNDI L:
Augsburg (3) v AZ Alkmaar (3)
Athletic Club (6) v Partizan (6)
-Kundi lipo wazi.

waliotembelea blog