Thursday, March 20, 2014

SAM_2237  
Hawa jamaa wanapokuja na njiwa au kuku uwanjani wanamaanisha nini?, au ndio mikwara kwa wapinzani?. Lakini njiwa hawa huwa hawaonekani pale timu inapofungwa.SAM_2239 SAM_2240Unaanzaje kumwambia shabiki kama huyu, mwenye mapenzi makubwa na klabu yake ahamie timu nyingine. Lakini wapo watu wanaendesha klabu watakavyo, wanasahau kuwa kuna uwepo wa watu wenye hisia kali kama huyu jamaa. 
Unamtesa sana unapoleta longolongo nyingi kwenye mambo ya msingi yahusuyo timu. Usishangae kumuona kazimia au kazirai kwasababu ya mtu mmoja kuharibu mambo.


KINYANG`ANYIRO cha ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014, bado kinabaki kuwa kitendawili kwa timu zilizopo juu katika msimamo.
Sare ya bao 1-1 jana uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam baina ya vinara Azam fc dhidi ya Yanga imezidi kuweka mazingira magumu kwa mabingwa watetezi, Young African.
Katika mchezo huo  uliovuta hisia za mashabiki, Yanga walikuwa wa kwanza kufunga bao kipindi cha kwanza kupitia kwa Didier Kavumbagu, lakini Azam fc walisawazisha dakika za lala salama kupitia kwa kinda, Kevin Friday.
Hiyo ilikuwa mechi ya 19 kwa Yanga, wakati kwa Azam fc ilikuwa ya  20, huku wakijikusanyia pointi 44, wakati Wanajangwani wakivuna pointi 40 katika nafasi ya pili.
Yanga SC wamebakiza mechi 7, wakati Azam fc wamebakiza mitanange  6.
PICHA YA PG.24 
Mtatwaa Ubingwa? : Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao la Didier Kavumbagu jana uwanja wa Taifa
Wikiendi hii timu zote zitashuka dimbani. Yanga watasafiri mpaka mkoani Tabora kuwafuata maafande wa Rhino Rangers, wakati jumapili machi 23, Azam fc watawakaribisha JKT Oljoro,  uwanja wa Azam Complex Chamazi.
Rhino Rangers ndio wanaoburuza mkia katika msimamo wakiwa wameshacheza mechi 21 na kujikusanyia pointi 13 tu kibindoni.
Kwa asilimia kubwa, maafande hawa wa Tabora, wameshachungulia kushuka daraja na inawezekana hakuna muujiza wa kubaki ligi kuu msimu huu kwasababu ya mazingira yao.
_DSC0044 
Mchezo dhidi ya Yanga utakuwa mkali endapo bado Rhino wanahitaji ushindi.
Lakini imani yao imeshuka na wanacheza bora liende na wameshapoteza matumanini ya kuendelea kucheza ligi kuu.
Pointi 13 kwa mechi 21 ni chache sana, zinahitajika nguvu za ziada kushinda mechi zote 5 walizobakiza, hapo sasa tunaweza kuzungumza mengine.
Yanga wataingia uwanjani wakiwa ma matokeo ya sare ya jana na suluhu ya Mtibwa Sugar wiki iliyopita uwanja wa Jamhuri.

Nokia-X-Dual-SIMNokia_X_familyNAIROBI, KENYA – 20th March, 2014 – Bharti Airtel (“Airtel”), a leading telecommunications services provider with operations in 20 countries across Asia and Africa and Nokia have announced that the new Nokia X smartphone will be available to purchase across 17countries in Africa from mid April 2014.
Designed for consumers in high-growth markets, the affordable Nokia X offers stunning design, a seamless user experience and access to the world of Android™ apps. Out of the box, they can enjoy signature Nokia experiences including free* HERE Maps, with true offline maps and integrated turn-by-turn navigation. The Nokia X family is also an affordable introduction to the most popular Microsoft services, including free cloud storage using OneDrive and Outlook.com.
An affordable introduction to the Nokia X family
The first offering, the flagship Nokia X, is beautifully crafted with Nokia’s signature design approach. The handset boasts a 4” capacitive display and exchangeable back covers that come in a variety of bold colours. Inside, the device runs on the Nokia X Software Platform and is powered by a1Ghz dual core Qualcomm® Snapdragon™ processor. Tile-based icons give the Nokia X’s user interface a fresh look, while by the upgraded Fastlane feature makes switching between favourite apps and content even smoother. 
Commenting on the partnership, Airtel Africa Chief Marketing Officer, Andre Beyers said: “This is yet another first from Airtel and Nokia. As Africa’s largest Internet provider, we are excited that Airtel customers in 17 countries will be amongst the first in the world to enjoy a unique combination of Nokia’s stunning design and user experience integrated with a wide range of services. In addition, Nokia X will come with data bundles for our customers to access their favorite social sites and chat applications.”
“We are delighted to partner with Airtel to offer the Nokia X smartphone” said Timo Toikkanen, executive vice president, Mobile Phones, Nokia. “Consumers can enjoy their favourite apps, the best of signature Nokia experiences and the most popular Microsoft Internet and cloud services, wrapped-up on a smartphone that holds-on the Nokia promise.”

SMART_d54ac.jpg
Dar es Salaam. Kampuni ya Microsoft, inayojishughulisha na utengenezaji wa kompyuta pamoja na programu, imebuni mbinu mpya ya kukabiliana na wizi wa mitandaoni ambao umezisababishia hasara benki, kampuni na watu binafsi katika maeneo mengi duniani

Mkakati huo umekuja wakati benki nyingi nchini zikiathiriwa na wizi huo kupitia mashine za kutolea fedha maarufu kama ATM pamoja na miamala inayofanyika kupitia mifumo ya mawasiliano ya kompyuta.
Takwimu zinaonyesha katika kipindi cha Oktoba 2012 hadi Februari 2013, Tanzania inakadiriwa kuwa Sh700 milioni ziliibwa katika benki kwa nyakati tofauti.
Kutokana na hali hiyo Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Benno Ndulu aliziagiza taasisi za fedha kuchukua hatua ili kukabilina na hali hiyo.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Microsoft, David Finn imeeleza kuwa wamebuni kompyuta mpya pamoja na programu ambazo zinaziba mianya ya wizi. Imeweka wazi kuwa uuzaji holela wa programu za kompyuta duniani umekuwa chanzo cha wezi hao kutumia ujanja katika kufahamu taarifa za siri zilizohifadhiwa kwenye kompyuta za taasisi na hata watu binafsi zilizounganishwa kwenye mtandao.
"Kampuni na taasisi na Serikali zinashauriwa kununua kompyuta mpya kwa mawakala maalumu zitakazowekewa 'software' (programu) zilizo halali," alisema Finn na kuongeza:
"Utafiti uliotolewa mwaka huu na kampuni ya kimataifa ya teknolojia ya mawasiliano ya kompyuta ikishirikiana na Chuo Kikuu cha Singapore unaonyesha, wizi wa kwenye mtandao unagharimu kampuni zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 315 kwa mwaka sawa na Sh504 trilioni,".
Sehemu ya ripoti hiyo imeeleza kuwa maeneo mengi ya Afrika yanakua kwa kasi katika matumizi ya mitandao kutokana na vitendo vya kiharamia na wengi wamejikuta wakipata hasara kwa kuibiwa fedha zao.
"Wizi wa njia ya mtandao unahamasishwa na tamaa ya pesa bila jasho kwa kutumia werevu wa teknolojia kuingilia na kuchukua taarifa muhimu za mtu, kitambulisho, namba za siri au hata pesa, hivyo Microsoft imedhamiria kudhibiti vitendo hivyo ili kuongeza usalama wa taarifa za wateja," alisema Finn.
Anasema utafiti umebaini kuwa kompyuta 203 zilizo nunuliwa katika maduka 11 tofauti, zilibainika kuwa asilimia 61 ziliathiriwa na programu za kiwizi maarufu kama virusi vinavyoitwa trojans, worms, viruses, hacktools, rootkits na adware




Msanii wa filamu nchini Yusuph Mlela kushoto akikabidhi vifaa mbalimbali kwa kocha wa klab ya Msisiri Daudi Muhunzi ikiwa ni uboreshwaji wa klabhiyo iliyopo CCM Msisiri Kinondoni Dasr es salaam katikati ni mdau wa mchezo huo Ally 

Msanii wa filamu nchini Yusuph Mlela kushoto akikabidhi vifaa mbalimbali vya mchezo wa ngumi kwa kocha wa klab ya Msisiri Daudi Muhunzi ikiwa ni uboreshwaji wa klab hiyo iliyopo CCM Msisiri Kinondoni Dar es salaam  

Msanii wa filamu nchini Yusuph Mlela kushoto akikabidhi vifaa mbalimbali vya mchezo wa ngumi kwa kocha wa klab ya Msisiri Daudi Muhunzi ikiwa ni uboreshwaji wa klab hiyo iliyopo CCM Msisiri Kinondoni Dar es salaam 
Na Mwandishi Wetu
Msanii wa filamu za bongo Yusuph Mlela ameibukia katika mchezo wa masumbwi nchini kwa kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya mchezo wa ngumi kama vile Glove,Clip bandeji,Proctecta,GumShit kwa klabu ya msisili iliyopo kinondoni Dar es salaam akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada wa vifaa hivyo Mlela alisema nimevutiwa na vijana wenzangu jinsi wanavyojituma kufanya mazoezi hivyo nikaamua kujitolea kidogo nilicho nacho kwa ajili ya kuendereza mchezo huu wa masumbwi katika kata yangu ambapo mimi naishi karibu na maeneo haya hivyowalivyo niomba nichangie nikawa sina jinsi kwa kuwa na mimi mwenyewe siku moja moja nitakuwa nakuja kufanya mazoezi hapa hapa nawaomba wadau wengine wenye uwezo zaidi yangu ata ambao wapo kama mimi wasaidie vijana kwa ajili ya kujiendeleza na mchezo huu waupendao
Nae kocha wa mchezo wa ngumi katika Klabu ya Msisiri Daudi Muhunzi alitoa shuklani zake kwa Mlela kuwakumbuka vijana wenzie ambao walikuwa na huaba wa vifaa vya ngumi kwani yeye amekuwa kama mkombozi katika kata hiyo aliongeza kwa kusema tunaomba wadau wengine waje watusaidie vifaa mbalimbali kama punch bag,pad na maswala ya hudhamini wa  muda mrefu   kwa ajili ya kuendereza gym hii ambayo tunaitumia kwa kuchangia kidogo
Meneja wa kinywaji cha Redd's Original Victoria kimaro akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam juu ya kuzinduliwa kwa mashindano ya Redd,s Miss Tanzania 2014kulia ni   mkurugenzi wa kamÃ¥uni ya LINO International Hashi Lundenga ambao ni waandaaji wa mashindano hayo na kushoto ni  Meneja Masoko wa kinywaji cha Redd's Original Vimal Vaghmaria.

Mkurugenzi wa kampuni ya LINO International Hashi Lundenga akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam juu ya kuzinduliwa kwa mashindano ya Redd's Miss Tanzania 2014 katikakati ni meneja wa kinywaji cha Redd's Original Victoria Kimaro na mwisho ni Meneja Masoko wa kinywaji cha Redd's Original Vimal Vaghmaria.
Baadhi ya waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari waliohudhuria kwenye uzinduzi jijini Dar Es Salaam.

waliotembelea blog