Monday, March 17, 2014


Top of the charts: Lionel Messi celebrates after scoring his record-breaking goal in the win
Leo Messi amefunga magoli matatu kwenye mechi kati ya Barcelona na Osasuna, magoli haya yamemfanya afikishe jumla ya magoli 371 akiwa na Barcelona na kumfanya awe mfungaji bora wa klabu hiyo. Kabla ya mechi ya leo Paulino Alcantara ndiye alikuwa mchezaji aliyefunga magoli mengi kuliko wote lakini magoli matatu ya Messi yamemfanya Muargentina huyu kuwa kinara wa kufunga magoli kwenye historia ya klabu ya Barcelona. Kwasasa Messi anaitafuta rekodi ya kuwa mchezaji mwenye magoli mengi kwenye ligi ya Hispania ambayo bado inashikiliwa na Telmo Zarra mwenye magoli 251 akiwa amemzidi Messi kwa magoli 18. Ikumbukwe magoli 371 ya Messi yanajumuisha mechi zote za Barcelona ikiwemo mechi za ligi, Uefa, Copa na mechi za kirafiki. Lakini magoli ya ligi pekee Messi ameshafunga 233 tu wakati mtani wake Cristiano Ronaldo ana magoli 171. 

Just another day: Messi walks away with the matchball at the final whistle
Messi akiondoka na mpira kama ukumbusho baada ya kufunga magoli matatu kati ya saba dhidi ya Osasuna.


Battle ready: Didier Drogba and his Galatasaray team-mates face a tough task at Stamford Bridge on Tuesday
Wachezaji wa Galatasaray wakiongozwa na  Didier Drogba wakiwasili nchini England tayari kukipiga na Chelsea siku ya jumanne kwenye michuano ya Uefa champions. Timu ya Galatasaray iliwasili mida ya kumi jioni jumapili kwenye uwanja wa ndege wa Heathrow na kupokelewa na kundi kubwa la mashabiki waliokuwa wamekusanyika kwenye uwanja. Mechi baina ya timu hizi mbili inategemewa kuwa na mvuto wa aina yake ikiwemo kurudi kwa Drogba ndani ya Stamford Bridge akiwa na timu pinzani. Uzuri wa mechi hii pia unakuja kutokana na matokeo ya awali ambapo timu hizi mbili zilitoka droo ya goli 1-1 jambo ambalo litazifanya timu zote kucheza mpira wa kushambulia. Timu ya Chelsea inapewa nafasi kubwa ya kushinda mchezo huu licha ya kuwa Galatasaray sio timu ya kubeza. 
Vocal support: Galatasaray fans sing loudly as they wait for their heroes to arrive at Heathrow
Mashabiki wa Galatasaray waliokusanyika kwenye uwanja wa ndege kuwapokea wachezaji 
Spotted: Fans have been warned that fake tickets are being sold for almost £500 for the match against Chelsea




ARSENAL imepata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Tottenham Hotspur Uwanja wa White Hart Lane mjini London jioni hii katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
Shukrani kwake Tomas Rosicky aliyefunga bao hilo dakika ya pili tu akimalizia pasi ya Alex Oxlade-Chamberlain na sasa The Gunners inatimiza pointi 62 baada ya mechi 29, sawa kabisa na Liverpool iliyo katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.
Hata hivyo, Arsenal inakaa nafasi ya tatu kwa kuzidiwa wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa na Liverpool, huku Chelsea ikibaki kileleni kwa pointi zake 66 za mechi 30 na Manchester City ni ya nne kwa pointi zake 60 kutokana na mechi 27.
Danger man: Podolski powers a low shot at Lloris' goal as Younes Kaboul chases him down
Lukas Podolski akifumua shuti 
Over the top: Former Arsenal striker Emmanuel Adebayor (right) attempts an acrobatic effort
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Emmanuel Adebayor kulia akibinuka 


Steven Gerard alifunga mikwaju miwili ya penalty na kukosa ya tatu Liverpool ikiendelea kuimarisha matokeo yake baada ya kuwacharaza mabingwa watetezi wa ligi ya uingereza Machester United tatu bila katika uga wao wa nyumbani Old Trafford.
Katika kile kilichoonekana kama harakati za kushinda taji lao la kwanza tangia mwaka 1990,Liverpool ilipita mtihani wao kwa kuonyesha mchezo mzuri dhidi ya timu ya Manchester United ambayo haikuweza kuwadhibiti wapinzani wao na hivyobasi kusogea hadi nafasi ya pili na pointi nne nyuma ya viongozi wa ligi hiyo Chelsea.
Nahodha wa Liverpool Gerard alionyesha uongozi wake huku wakifazawadiwa mikwaju ya penalty katika vipindi vyote viwili huku timu hiyo ya meneja Brenda Rodgers ikitawala dhidi ya timu ya Machester ambayo inahitaji marekebisho makubwa.
Kutokana na mechi hizo za leo Chelsea iko katika nafasi nzuri ya kushinda taji hilo kwa alama 66 ikiwa imecheza mechi 30 huku timu za liverpool na Arsenal zikiwa na pointi 62 kila mmoja, lakini liverpool inashikilia nafasi ya pili kwa wingi wa mabao.
Arsenal ni ya tatu huku Manchester City iliocheza mechi 27 ikiwa na pointi 60 na hivyobasi ikifunga udhia wa time nne bora

Wachezaji wa Liverpool wakipongezana baada ya kuwafunga United Old TraffordLiverpool leo imejichukulia pointi tatu baada ya kuwalaza Manchester United kwenye Uwanja wao Old Trafford. Liverpool wameanza kupata kupita mchezaji wake Kapteni Steven Gerrard kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 34 kipindi cha kwanza, Baada ya Rafael kuunawa mpira kwenye eneo hatari la penati. Liverpool 1-0 dhidi ya wenyeji United. Mapumziko Liverpool inaongoza bao 1-0.
Kipindi cha pili Dakika ya 46 Liverpool wanapata penati nyingine, Ni baada ya Jones kumfanyia rafu kwa kumwangusha Allen chini. Steven Gerrard anawapachika bao kwa mkwaju huo na kufanya bao 2-0 dhidi ya Manchester United kwenye uwanja wa Old Trafford.
Dakika ya 77 Nemanja Vidic aliondoshwa nje kwa kadi nyekundu baada ya kufanya rafu kwa Sturridge na mwamuzi kumtoa kwa kadi hiyo nyekundu huku Vidic akimlalamikia kwamba kajiangusha na
Dakika ya 78 Steven Gerrard alikosa penati hiyo iliyogonga mwamba na kurudi ndani na mchezaji wa Man United kuuondosha.
Dakika ya 84 Luis Suárez alipachikia bao la tatu Liverpool na kufanya 3-0 dhidi ya United baada ya mabeki wa United kupitiwa wakidhani ni faulu.
Ushindi huu wa Majogoo Liverpool unawapandisha hadi nafasi ya pili wakiwa na pointi 62, Nyuma ya pointi 4 ya vinara Chelsea wenye pointi 66 waliofungwa jana na Aston Villa.Steven Gerrard (kushoto) akishangilia bao lake 






Van Persie chupu chupu atupie bao hapa!!



waliotembelea blog