Wachezaji
wa Galatasaray wakiongozwa na Didier Drogba wakiwasili nchini England
tayari kukipiga na Chelsea siku ya jumanne kwenye michuano ya Uefa
champions. Timu ya Galatasaray iliwasili mida ya kumi jioni jumapili
kwenye uwanja wa ndege wa Heathrow na kupokelewa na kundi kubwa la
mashabiki waliokuwa wamekusanyika kwenye uwanja. Mechi baina ya timu
hizi mbili inategemewa kuwa na mvuto wa aina yake ikiwemo kurudi kwa
Drogba ndani ya Stamford Bridge akiwa na timu pinzani. Uzuri wa mechi
hii pia unakuja kutokana na matokeo ya awali ambapo timu hizi mbili
zilitoka droo ya goli 1-1 jambo ambalo litazifanya timu zote kucheza
mpira wa kushambulia. Timu ya Chelsea inapewa nafasi kubwa ya kushinda
mchezo huu licha ya kuwa Galatasaray sio timu ya kubeza.
Mashabiki wa Galatasaray waliokusanyika kwenye uwanja wa ndege kuwapokea wachezaji
0 maoni:
Post a Comment