Saturday, August 23, 2014

 

 

Angel di María na Sami Khedira ni wazi sasa wako mguu mmoja nje ya Real Madrid baada ya kutupwa nje ya Kikosi kilichoteuliwa kuivaa Atletico Madrid Ijumaa Usiku huko Estadio Vicente Calderon kwenye Mechi ya Marudiano ya Supercopa de Espana ambayo Real walichapwa 1-0.
Awali wote wawili walitajwa kwenye Kikosi cha Wachezaji 22 kwa ajili ya Mechi hiyo na Atletico Madrid kwa mujibu wa Jarida la Marca wakimnukuu Kocha wa Real Carlo Ancelotti.

Lakini walipofika huko Valdebebas, Kituo cha Mazoezi cha Real, Di Maria na Khedira walijulishwa kuwa hawamo kwenye Kikosi cha kwenda kwenye Mechi na Atletico na hilo liliwakera sana Wachezaji hao kwa mujibu wa Marca.
Wakati Di Maria akiamua kurudi Nyumbani kwake, Khedira aliamua, bila ya ruhusa ya kusafiri ya Real, kupanda Ndege kwenda kwao Germany, Mji wa Leipzig kumshuhudia Ndugu yake akicheza Mechi.

Hadi sasa haijajulikana wazi Wachezaji hao wanakwenda wapi mbali ya Kocha Ancelotti kutoboa kuwa wote wamekataa Mikataba mipya na Di Maria ameomba kuhama.
Hadi sasa Di Maria anahusishwa sana na kuhamia Manchester United na Leo zimeibuka ripoti kuwa Khedira yeye atakwenda Bayern Munich kuchukua nafasi ya Majeruhi wa muda mrefu Javi Martinez.Jarida la Marca, ambalo lipo karibu mno na Klabu ya Real Madrid, limethibitisha Wachezaji hao wawili watahama rasmi Wiki ijayo.
Rojo tayari alishajiunga na Man United.


Aston Villa na Newcastle zimetoka Sare ya 0-0 kwenye Mechi ya kwanza ya Ligi Kuu England iliyochezwa Villa Park hii Leo.
Newcastle walimaliza Mechi hii wakiwa Mtu 10 baada ya Mike Williamson kupewa Kadi ya Njano katika Dakika ya 86 na Dakika 4 baadae kupewa Kadi ya Njano ya pili na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Mashabiki wa Newcastle United wakipamba Mechi yao.Kocha wa England Roy nae alikuwa kwenye mtanange huo..Mashabiki  wakiwapamba Mashujaa wao..Michael Williamson kwenye patashika!Kocha wa Aston Villa Paul Lambert akishuhudia Vijana wake wakimenyana vilivyo na Newcastle United.Mike Dean akiwapanga kwa kumimina Spray kupigwa Frii kiki.



Kocha mkuu wa Yanga sc (katikati), Mbrazil Marcio Maximo amewasili kisiwani Unguja kuendelea kuiwinda ligi kuu Tanzania bara

Na Baraka Mpenja
BAADA ya kukamilisha programu ya mazoezi ya siku tano kisiwani Pemba, kikosi cha Yanga kimewasili kisiwani Unguja (Zanzibar) tayari kwa kumalizia siku nyingine tano zilizosalia.
Yanga imeweka kambi ya siku 10 Zanzibar na tayari imekata tano ikiwa pemba ambapo ilicheza mechi moja ya kirafiki dhidi ya Chipukizi FC katika uwanja wa Gombani na kushinda bao 1-0.
Bao hilo pekee lilifungwa na mshambuliaji Mbrazil Geilson Santos Santos Santana ‘Jaja’ katika dakika ya 6 ya mchezo.
Katika mechi hiyo iliyokuwa ya kwanza kwa kocha mkuu, Mbrazil Marcio Maximo, Yanga ilitumia vikosi viwili tofauti kwa kila kipindi.
Ikiwa kisiwani Unguja, kesho Yanga inatarajia kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Shangani FC majira ya saa 10:00 jioni uwanja wa Aman mjini Zanzibar.
Hii itakuwa mechi nyingine muhimu kwa Maximo kuona kama wachezaji wake wamefuta makosa ya mechi ya Gombani au hapana, ili ajue nini cha kufanya zaidi kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi septemba 20 mwaka huu.
Wakati huo huo Mahasimu wao, Simba chini ya kocha Patrick Phiri wapo mjini Unguja wakiendelea na mazoezi yao.
Leo Simba walifanya mazoezi kidogo ili kuiandaa miili ya wachezaji kwa ajili ya mechi ya kwanza ya kirafiki kesho uwanja wa Aman dhidi ya Kilimani FC.
Kocha mkuu wa Simba akiongea na wachezaji wake
Mechi hii itapigwa majira ya 2:00 usiku saa chache tu  kupita baada ya kuishuhudia  Yanga ikicheze katika uwanja huo huo.
Mechi hizo zitatoa burudani kwa mashabiki wa Yanga na Simba visiwani Zanzibar kwasababu watazishuhudia timu zao zikicheza uwanja mmoja kwa kupishana saa chache.
Kocha wa Simba kwa muda mrefu sasa amekuwa akiwafundisha vijana wake jinsi ya kumiliki mpira, kukaba kwa mipango na kushambulia kwa kasi.
Lengo la Phiri ni kuifanya Simba kuwa bora katika maeneo hayo matatu kabla ya kuanza ligi kuu.
Simba wataanza kucheza mechi nyingi nyumbani ambapo mechi ya ufunguzi Septemba 21 uwanja wa Taifa watachuana na Wagosi wa Kaya, Coastal Union ambao nao wako Pemba kujifua.

Yanga wao wataanza kampeni ya kusaka ubingwa septemba 20 katika dimba la Jamhuri mkoani Morogoro dhidi ya wakata miwa wa Mtibwa Sugar.


Nightmare: Wolfsburg midfielder Junior Malanda produced a horror miss against Bayern Munich on Friday night
Maajabu:Kiungo wa Wolfsburg, Junior Malanda alikosa bao la wazi  dhidi ya  Bayern Munich jana usiku.

NYOTA wa Wolfsburg, Junior Malanda ameingia kwenye rekodi ya kukosa bao la wazi zaidi na kusababisha timu yake kufungwa.
Wakikabiliana na mabingwa watetezi, Bayern Munich katika mchezo wa ufunguzi wa Bundesliga, kiungo huyo wa ulinzi mwenye miaka 19 alishindwa kumfunga Manuel Neuer baada ya kufanikiwa kumuacha na kubaki yeye na goli, lakini alichofanya ni ajabu.Tazama picha. 
Easy does it: Malanda was stood almost on the goal line and looked destined to equalised against Bayern
Rahisi tu!: Malanda alikuwa kwenye karibu na mstari wa goli na kutakiwa kusawazisha kiulaini, lakini alikosa. 
How did he miss? The Wolfsburg midfielder was first to the rebound but managed to shoot wide
Alikosaje? Kiungo wa Wolfsburg alikosa  bao akiwa yeye na kipa.
Horror miss: Malanda can't believe his miss with Wolfsburg trailing 2-1 to Bayern Munich in the season opener
Majanga:  Malanda haamini kilichotokea 
Head in hand moment: Malanda reacts after missing the target when virtually stood on the goal line
Mikono kichwani: Malanda akijilaumu baada ya kukosa goli la wazi.
Laying low: The Belgian lays on the floor in shock in a game in which Bayern Munich held on for the win


Simba itarudia rekodi ya 1993 barani Afrika?: Rais wa Simba sc, Evans Elieza Aveva anaaminiwa kurudisha heshima ya klabu hiyo.

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
0712461976
MZAMBIA Patrick Phiri huwezi kuthubutu kumdharau hata kwa dakika moja, hakika ni miongoni mwa makocha wa kigeni waliopata mafanikio makubwa wakifundisha klabu za ligi kuu soka Tanzania.
Phiri ni kocha mwenye heshima kubwa ndani ya klabu ya Simba na sasa amekabidhiwa majukumu ya kuinoa timu kuelekea msimu ujao wa ligi kuu unaotarajia kuanza septemba 20 kufuatia aliyekuwa kocha wa klabu hiyo, Mcroatia, Zdravko Logarusic kuachishwa kazi.
Kilichomuondoa Loga sio uwezo mdogo wa kitaaluma. Huyu ni kocha wa kiwango cha juu, lakini sababu ilikuwa ndogo tu, tabia, matendo na mitazamo yake ambayo haikuonekana kuijenga Simba sc.
Siwezi kumkosoa Loga moja kwa moja kwa ukali wake kwa wachezaji na misimamo yake kwa viongozi au tabia ya nje ya uwanja kwasababu nafahamu kuwa kocha yeyote lazima awe na falsafa yake ya kufanya mambo yake.
Falsafa ya mwalimu huwa haibadiliki. Kama anaamini ukali kwa wachezaji ni suala zuri kwake, basi atasimama hapo hapo. Kama anaamini kuwatumia vijana zaidi kuliko ‘Mafaza’ basi inabidi aachwe afanye kazi yake.
Kuipinga falsafa ya mwalimu ni kuingilia taaluma yake. Kinachotakiwa ni kuangalia kama falsafa yake inaisaidia timu, kama ni hapana, lazima aondolewe mara moja, kama ni ndiyo apewe muda na kuaminiwa.
Najua Loga yupo sahihi kwa mitazamo yake kwasababu kuna sehemu inaweza kufaa, lakini kwa utamaduni wa Simba na soka la Tanzania na maeneo mengine Duniani yawezekana haifai.
Nimekuwa nikimkubali Loga kwa wakati wote linapofika suala la nidhamu kwa wachezaji. Anawasimamia na kuwafanya wajielewe na kujituma, lakini tatizo langu lipo kwenye namna anavyowasimamia.
Loga hakuwa rafiki kwa wachezaji. Alikuwa mkali mno na hili lipo wazi. Tatizo la msingi lilianzia hapo, sidhani kama Simba walikuwa na tatizo kwa yeye kukazania nidhamu, lakini tatizo lilikuja pale alipoanza kuwatukana watu wazima kama ‘Baba wawili’ Amri Kiemba na Shaaban Kisiga na wengineo.
Utanyanyua tena msimu ujao?: Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' Perez akionesha moja ya kombe la Ubingwa wa klabu hiyo

Unaweza kuwa sahihi katika jambo fulani, lakini namna ya kulitenda ikawa tatizo. Hii ni sawa na haki ya msingi ya  kila mtu kutoa maoni na kukosoa kitu au jambo fulani.
Ni vizuri kukosoa au kukosolewa, hakuna tatizo juu ya hili, lakini namna ya kukosoa ndio inafanya mtu asikuelewe na kuona una chuki binafsi, umetumwa au kwa lugha nyepesi una lako jambo.
Ukosoaji ninaopenda mimi ni kutoa hoja mbadala. Sipendelei kauli kama hapo umekosa sana, huna lolote, hii ndio Bongo, hawa ndio viongozi wa soka letu, huwa napenda kusikia mtu anaanika kosa na kutoa suluhisho.
Kama viongozi wa Simba na Yanga wanakosea, waambie, kisha wape njia mbadala ya kufanikiwa. Wakisikiliza, wasiposikiliza sawa, maoni sio sheria na ndio maana yakaitwa maoni na sio agizo.
Kwa bahati mbaya sana, wengi wetu si wazuri wa kutoa hoja mbadala. Unaweza kumsikia mtu anasema Loga hafai kabisa kuiongoza Simba, lakini ukimuuliza kwanini, anakwambia wewe si unaona tu?
Hawezi kujenga hoja kabisa. Kwa mtu wa aina hii huwa sipotezi muda kumsikiliza kwasababu anaongea “Mipasho tu” na natumia nguvu kubwa kufikiria anamaanisha nini.
Lakini mtu akikosoa kwa hoja, napima uzito wa hoja zake, kama zinazidi zangu, basi nampa kura ya ushindi na kuchukua zake na kuacha zangu. Lakini kwa waliowengi, ni kuponda tu na kupandikiza chuki.
Leo hii Simba wanafundishwa na Patrick Phiri baada ya Loga kuondoka. Wapo wengi walimpenda Loga na wamesikitishwa sana na kuondoka kwake, lakini wapo waliofurahi kuondoka kwasababu hawakumpenda.
Usajili umeridhisha?: Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba sc, Zacharia Hans Poppe

Pande mbili lazima ziheshimiane vizuri. Kama upande mmoja una hoja, wewe unayepinga weka zako mezani, tuone nani anashinda. Siamini kama kila mtu anaweza kuwa mchambuzi mzuri wa hoja, lakini hutakiwi kushambulia kama huwezi kujenga hoja yako.
Ya Loga yameshapita, yanayoendelea ni ya Patrick Phiri. Kinachosubiriwa kwa sasa ni kuona nini Mzambia huyu ataifanyia Simba.
Afanikiwe asifanikiwe, ndio mpira. Ndio maana Jose Mourinho aliyefanya makubwa na Chelsea miaka ya 2006 na kuendelea alishindwa kubeba kombe la Ligi kuu msimu uliopita. Tena alimaliza mikono mitupu.
Phiri kubeba ubingwa bila kufungwa mwaka 2009 sio kigezo cha kumpa asilimia 100 za kuwapa ubingwa msimu ujao. Mambo yanaweza kuwa mazuri au mabaya. Soka huwa liko hivyo.
Kinachotakiwa ni maandalizi ya kupokea matokeo yoyote. Najua zipo jitihada zinazofanywa ili Phiri afanikiwe, lakini kama atashindwa kufikia malengo, kuna mambo ya msingi yatatakiwa kufanyika.
Moja wapo ni kubaini makosa yalikuwa wapi na kuyafanyia kazi ili ajipange upya kwa msimu mwingine.
Atabebwa tena?: Patrick Phiri aliwapa ubingwa Simba mwaka 2009 bila kufungwa mechi yoyote

Ligi ya 2009 sio hii ya 2014/2015. Miaka ya nyuma kuwa kocha wa Simba au Yanga tu, ni kura tosha ya kutwaa ubingwa. Lakini sahizi kuna Azam fc, Mbeya City, Kagera Sugar ambao wanatoa ushindani mkubwa mno.
Kwahiyo Phiri ana kazi ngumu zaidi ya 2009 na ndio maana nasema kuna haja ya kujiandaa kwa matokeo yoyote yale. Utamaduni ni mmoja duniani kote, timu kubwa ina presha sana, suala la kupewa muda halivumiliki, na ndio maana Manchester United walifanya maamuzi ya kumtoa David Moyes haraka, pia Tata Martino kwa Barca na wengine wengi.
Lakini Man United na Barca haziwezi kuwa Simba. Pale unawakuta wachezaji wazuri (vijana kwa ‘mafaza’) na hela za kusajili unayemtaka zipo, lakini simba haijawa na uwezo huo. Hata mfumo wake wa kupata wachezaji una matatizo. Kwasababu hiyo nashauri Phiri kuaminiwa na kupewa muda mrefu.
Kuna kitu cha ziada nimekiona kwa Patrick Phiri katika kambi yake ya mazoezi uwanja wa Chuoni Chukwani mjini Zanzibar.
Kila baada ya mazoezi, waandishi hupenda kumuuliza Phiri, na kwa bahati mbaya maswali ni yale yale, unazungumziaje msimu ujao? Nini wana Simba watarajie?
Mkali sana kwa wachezaji: Zdravko Logarusic alitumuliwa Simba na nafasi yake kutua mikononi mwa Phiri

Phiri amekuwa akijibu swali hilo kwa namna moja akisema anajipanga kuwapa ubingwa Simba na kurudisha heshima iliyopotea. Kocha huyu anawapa matumaini makubwa wana Simba kutokana na historia yake.
Lakini kuna swali la msingi napenda sana kuona watu wanauliza, unatarajia kuijenga vipi Simba A na B ili kuwa na mwendelezo wa uchezaji mmoja katika klabu ya Simba?
Naamini kama Simba watakaa na Phiri na kuandaa programu nzuri ya soka la vijana watafika mbali. Tatizo la msingi la klabu ya Simba au Yanga sio kukosa wachezaji wazuri, bali ni kukosa muendelezo wa soka la vijana.
Hivi inawezekanaje mchezaji akawa na miaka 16,17, 19 katika kikosi cha Simba B, halafu akapandishwa kikosi A na ndani ya msimu mmoja humuoni tena? Naamini kuna tatizo linalotakiwa kutatuliwa.
Lazima utengenezwe mfumo sahihi wa kutunza na kuendeleza soka la vijana, kama kijana amevurunda akiwa na kikosi A basi anatakiwa kurudi tena kikosi B na sio kumuacha aondoke zake kwasababu umesajili wengine.
Jambo nililolifurahia kwa Phiri ni namna alivyoweza kuunganisha nguvu ya pamoja kwa wachezaji. Anaonekana ni mlezi na kocha. Wachezaji wamekuwa watulivu wakati wa mazoezi, wanamiliki mipira, wanakaba vizuri na kushambulia.
Utulivu umerejea?. Ndiyo, Kwanini? Sababu rahisi tu, wachezaji wamepata kocha mwenye kujua utamaduni wa soka la Simba na Afrika kwa ujumla.
Kinachowafanya makocha wa kizungu washindwe kufanikiwa Tanzania ni pamoja na kuleta ‘U-ulaya’ Afrika. Soka la Afrika lina matatizo mengi hasa mfumo wa uendeshaji na aina ya wachezaji waliopo.
Wengine hawataonekana msimu ujao: Moja ya kikosi cha Simba msimu uliopita

Aina ya wachezaji wanaopatikana sio kama Ulaya. Kuna akademi ngapi za kisasa Tanzania? Ni chache sana tena ambazo sio za kisasa. Ukisema nahitaji wachezaji kutoka akademi za soka tu, utawapata wapi?
Ndio maana ukiangalia wachezaji wengi ni walewale, kwasababu hakuna muendelezo wa kuwapata. Leo hii mchezaji hana misingi ya mpira kabisa.
Kocha anafanya kazi ya kumfundisha mambo ambayo alitakiwa kujifunza akiwa akademi wakati ana miaka 13,14, 15 au 16.
Lakini kwa wenzetu, mchezaji wa timu kubwa anafundishwa mbinu na ufundi wa kupata matokeo na kuujenga mwili kimazoezi na sio namna ya kupiga pasi au kupokea mpira.
 Wanajua tangu wakiwa wadogo, mazoezi ya koni wanayajua toka wakiwa wadogo, lakini kuna wachezaji wa Bongo hata ukiwaambia wazunguke koni wanachemsha, hawajui wafanyeje mpaka upate muda wa kuwaelekeza.
Akija kocha mzungu aliyetoka Ulaya, anawaona kama ‘wendawazimu’ lakini ndio ukweli. Ndio maana nasema kuna haja ya kujadili kutengeneza mfumo, lakini sio kila siku kulumbana juu ya makocha na viongozi wa soka.
Simba kuna mambo matatu nawashauri ili Phiri afanikiwe. Moja ni kumpa muda na kumuamini. Mwacheni afanye kazi yake, wekeni mipaka ya utawala na benchi la ufundi.
Simba na Yanga nani ataibuka mbabe msimu ujao?

Fanyeni kutekeleza mahitaji yake na msisajili kwa kushindana na upande wa pili. Kama Phiri ataachwa huru asimilia 100, nina uhakika atafanikiwa kwasababu ana faida ya kulijulia Simba na soka la Afrika.
Pili, utawala lazima utambue malengo na ndoto za wana Simba. Rais Aveva lazima uwe na jukumu la kuwa na mpango mkatati wa kuendeleza timu na kuutekeleza kama timu na sio kama Rais.
Kuna vitu huwa naamini. Wapo watu wanaingia katika soka kutafuta umaarufu na sio kuendeleza soka. Inawezekanaje kiongozi kila siku unasikika kwenye vyombo vya habari ukiongea mipasho kwa wenzako na kuendeleza “Mabifu”?
Watu wa mipango sio wazungumzaji sana. Kama unatekeleza mambo ya msingi na kufanikisha, kitakachojadiliwa ni mafanikio yake na hatimaye utapata umaarufu.
Kuna faida gani kubishana na kiongozi mwenzako kwenye gazeti? Leo hii ukifanikiwa kujenga uwanja wa Simba na kujengewe sanamu uwanjani hapo, huoni kama ina maana kuliko kukaa kupashana na mtu kwenye vyombo vya habari? Utawala wa Simba, fanyeni mambo ya kiutawala kwa weledi, mtaibadilisha timu.
Tatu, wachezaji lazima waachwe wafanye kazi yao. Ni faida kubwa kumuacha mchezaji acheze mpira vile anavyofikiria.
Sio unakwenda uwanjani na kuona Joseph Owino anapiga chenga eneo la goli la Simba na kumrudishia kipa Ivo Mapunda, halafu unalipuka kwa kelele, kocha toa huyooooo! Atatufungisha, piga mpira mbele bwana wewe! Unadhani Owino hajui kama kuna kupiga mpira mbele ua kufungisha?
Hiyo ni sehemu ya mpira. Kama haoni mtu wa kuanza naye kwanini asipige chenga wakati wenzake wanafungua?, wachezaji wanajua wanachokifanya, lakini kwa vile wengi wanajua mpira wa mdomoni, wanaishia kuzomea tu na kushinikiza mchezaji fulani aachwe.
Cha msingi ni kuwaamini wachezaji wenu na kuwapa nafasi ya kuonesha uwezo wao na sio kuwapa presha kwa kutaka wacheze mtakavyo ninyi.
Kama wanakosea unawaacha wajisahihishe. Mbona Iker Casillas alivurunda kombe la dunia, lakini Carlo Anacelotti ameendelea kumtumia.
Makipa wangapi wanafungisha?, mabeki wangapi wanakosea?, washambuliaji wangapi wanakosa magoli duniani? Au Tanzania tu ndio hakuna makosa ya kimpira, basi ni ajabu.
Kwanini akifungisha mtu asemwe kuuza mechi? Simba waacheni wachezaji wafanye kazi yao kwa misingi ya mtaalamu Patrick Phiri.
Sina masilahi na mtu yeyote, nina masilahi na kubadili mfumo wa soka letu.
Kila la kheri Simba na kocha mpya mwenye heshima ndani ya klabu yenu, Mzambia, ‘Chief’ Patrick Phiri.



Free agent Georgios Samaras took his two-footed talent to West Brom, signing a two-year contract with them. I don’t know why Celtic failed to offer him new terms at the end of his contract. He was very helpful to the team.
Nonetheless, welcome to the Premiere League. Can’t wait to show you around town.

waliotembelea blog