Saturday, June 14, 2014


Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameizawadi kwa kuifadhili timu ya taifa ya soka Harambe Stars ziara ya kwenda Brazil kutazama michuano ya kombe la dunia Hafla ya kuikabidhi rasmi ufadhili huo timu hiyo, ilifanyika katika ikulu ya Rais Ijumaa ambapo wachezaji kumi na moja wa timu hiyo walikabidhiwa tiketi za ndege kwenda Brazil. Kitendo cha Rais bila shaka ni jambo la kutaka kuwatia motisha wachezaji wa timu ya taifa ambao hivi karibuni waliicharaza Djibouti mabao mawili kwa moja katika duru ya kwanza ya michuano ya kuwania kombe la taifa bingwa Afrika baadaye mwakani.Rais Kenyatta akiongea na Wachezaji wa Timu hiyo.
Hapa Akigawa tiketi huku akishuhudiwa na mkewe Bi. Margaret Kenyatta na seneta wa Nairobi Mike Sonko (kushoto).
Picha ya Pamoja.


Mchezaji wa Chile Gary Medel akimwendesha mchezaji wa Australia Tim Cahill
Mfungaji wa bao la kwanza wa Chile Alexis Sanchez  akimfunga kipa wa Australia Maty Ryan

Sanchez akishangilia bao lake la kwanza kwa Chile

Sanchez akishangilia bao lake la kwanza dhidi ya Australia..

Mauricio Isla akiteleza kumpongeza  Sanchez kwenye kona

Mchezaji wa  Chile Jorge Valdivia ndie aliyeifungia bao la pili na kufanya 2-0

Valdivia akipongezwa na Wachezaji wa Akiba
Wachezaji wote timu mbili  Chile na  Australia walianza kuimba nyimbo za Taifa za Nchi zao
VIKOSI:
Chile:
Bravo, Diaz, Mena, Jara, Isla, Vidal, Valdivia, Vargas, Medel, Alexis, Aranguiz.
Subs: Toselli, Albornoz, Silva, Carmona, Pinilla, Rojas, Orellana, Beausejour, Gutierrez, Fuenzalida, Paredes, Herrera.
Goals: Sanchez 12, Valdivia 14 J. Beausejour 90'+



Australia: Ryan, Milligan, Cahill, Franjic, Davidson, Leckie, Wilkinson, Spiranovic, Jedinak, Oar, Bresciano.
Subs: Langerak, Wright, Taggart, Halloran, Bozanic, Troisi, Holland, McKay, McGowan, Vidosic, Luongo, Galekovic.
Referee: Noumandiez Doue (Ivory Coast)

Darly Janmaat  na Diego Costa wakiendana sambambaWasley Sneijder akifanya yakeSergio akiwekewa kigingi na NigelDiego Costa vipi...unasababisha penati...Mzee Mzima Alonso ndie aliyeipa bao kwa mkwaju wa penati SpainXabi Alonso akishangilia baoVan Persie akitupia kusawazisha...1-11-1....Van Persie akimpagawisha kipa wa Spain kwa bao la kiwangoVan Persie akishangilia bao lake Nipe tano bosi wangu!! Nilikwambia!! leo ni chinja chinja!!Robben akitupia..Kipa Cassilas leo hii kama mtoto !!Mpaka ndani ya nyavu!! bao la tatuStefan akipeta baada ya kufunga baoVan Persie tena...Chupuchupu!!5-1

Kipindi cha pili dakika za mwishoni dakika ya 80 Arjen Robben amewakaanga mabeki na kuwafunga pamoja na kipa wao Spain baada ya kuwazidi mbio na kuachia shuti kali lililofanya mabao kuwa 5-1 dhidi ya Spain ambao ni Mabingwa Watetezi wa Dunia wa Kombe hili.Historia hii...nimetupia 2!!!
Dakika ya 64 tena Stefan de Vrij ameoingozea bao la tatu timu ya Netherlands na kufanya matokeo kuwa 3-1 dhidi Spain. Wesley Sneijder ndie alietoa pande hilo lililozaa bao.
Stefan de Vrij aliyefunga bao la tatu huku van persie akimzonga kipa ili bao lifanikiwe...
De Vrij wa Holland akishangilia baada ya kuichakaza bao la tatu Spain kwa kufanya 3-1 akishangilia kwa raha zake...
Kipindi cha pili dakika ya 53 Arjen Robben alipewa pasi safi na Daley Blind na kufunga bao la pili kwa timu ya Netherlands na kufanya 2-1 dhidi ya Spain.Dakika ya 27 kipindi cha kwanza Xabi Alonso ndie aliyeifungia bao kwa mkwaju wa penati na kuitanguliza mbele Spain kwa bao 1-0 dhidi ya Netherlands. Dakika ya 44 mwishoni mwa kipindi cha kwanza cha dakika 45 mchezaji matata Van Persie amewatoka mabeki wa Spain na kuruka kwa kichwa maridadi na kuisawazishia bao kwa kufanya 1-1 timu ya Netherlands. Mpaka dakika za kipindi cha kwanza zinamalizika timu zote mbili zilikuwa kwenda kupumzika zikiwa nguvu sawa kwa bao 1-1. Van Persie akitupia.....
VIKOSI:
Spain:
Casillas, Azpilicueta, Sergio Ramos, Pique, Jordi Alba, Alonso, Xavi, Busquets, Silva, Diego Costa, Iniesta.
Subs: De Gea, Albiol, Javi Martinez, Juanfran, Villa, Torres, Fabregas, Pedro, Mata, Koke, Cazorla, Reina.

Holland: Cillessen, Janmaat, Vlaar, De Vrij, Martins Indi, Blind, De Guzman, Sneijder, De Jong, van Persie, Robben.

Subs: Vorm, Verhaegh, Veltman, Kongolo, Kuyt, Clasie, Lens, Fer, Huntelaar, Wijnaldum, Depay, Krul.
Referee: Nicola Rizzoli (Italy)

Mchezaji wa Netherlands  Stefan de Vrij  kamwangusha kwenye eneo la Hatari Diego Costa
Xabi Alonso akiifungia bao Spain kwa mkwaju wa penati...
Xabi Alonso wa Spain akishangilia bao lake
Asante baba!!!! Wachezaji wa Spain wakimpongeza Alonso.
Fowadi wa Spain Diego Costa akimwendesha difenda wa Holland Stefan de Vrij LIVE: Spain 1-0 NetherlandsNipishe!!!
Wachezaji wa Spain wakiimba wimbo wao wa Taifa

Wachezaji wa  Holland wakijifua wakiwa wao ni kundi  B kujiweka sawa na kipute na Spain
Wachezaji wa Holland wakijifua vikali
Wachezaji wa Spain nao wakijiweka sawa kuwakabili  Holland
Wachezaji wa Spain wakipasha
Costa kuanza kwenye kipute hiki....
Baada ya muda mfupi ni kipute kuanza...
Jezi za Wachezaji wa  timu ya  Holland

waliotembelea blog