Tuesday, January 12, 2016



Mtu wangu wa nguvu January 12 katika pitapita zangu mtandaoni nikakutana na list ya majina ya utani ya mastaa watano wa soka. Katika maisha kila mmoja anaweza akawa na jina la utani ambao huenda kapewa na familia yake au washikaji zake mtaani au kwa sababu ya umahiri wake uwanjani ndio anaweza kujkuta kapewa jina. January 12 naomba nikusogezee majina ya utani ya mastaa hawa wa soka Messi, Ribery, Torres, Robben na Kroos.
5- Toni Kroos huyu kutokana na umahiri wake uwanjani, kocha wa zamani wa klabu ya Real Madrid ya Hispania Carlo Ancelotti aliwahi kumtunga jina na kumuita “The professor” hii inatokana na uwezo na akili yake ya kuumiliki mpira uwanjani.
Kroos1
4- Mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania ambaye amewahi kuvichezea vilabu vya Liverpool na Chelsea vya Uingereza Fernando Torres alipewa jina la utani la “El Nino” ambalo lina maana ya kuwa mtoto, Torres ambaye ana umri wa miaka 31 amerudi kwenye klabu yake iliyomlea ya Atletico Madrid, lakini wakati ana umri wa miaka 16 akiwa Atletico alikuwa akicheza mpira kwa kiwango cha juu kutokana na wengi kutokuwa wamelishika jina lake na muonekano wake wa kitoto wakawa wanamuita “El Nino”
Torres4
3- Franck Ribery huyu jina lake la utani anaitwa “Scarface” jina ambalo alipewa kutokana na sura yake kuwa na makovu na mikunjo usoni. Makovu ya Ribery yalitokana na ajali aliyowahi kuipata wakati akiwa na umri wa miaka miwili, makovu ambayo yapo usoni kwake hadi leo.
Ribery1
2- Mshindi wa tuzo ya tano ya Ballon d’Or Lionel Messi yeye jina lake la utani anaitwa “La Pulga” ambalo limetokana na kimo chake ambacho kimekuwa kikiwasumbua  wapinzani, licha ya kuwa hana umbo kubwa sana.
Messi19
1- Winga wa kimataifa wa Uholanzi Arjen Robben yeye kutokana na uwezo na mbio zake uwanjani na uwezo wake wa kujirusha uwanjani pale anapokuwa kafanyiwa faulo uwanjani, alipewa jina la mdachi anayepaa “The Flying Dutchman” .
Robben5

Mchezaji Bora wa Mwaka 2015 kwa Wachezaji wa Ndani, mchezaji wa Taifa Stars na Klabu ya TP Mazembe ya DRC Congo, Mbwana Samatta.

BAADA ya kushinda Tuzo ya Afrika kama Mchezaji Bora wa Mwaka 2015 kwa Wachezaji wa Ndani, mchezaji wa Taifa Stars na Klabu ya TP Mazembe ya DRC Congo, Mbwana Samatta anatarajiwa kupongezwa na kuagwa rasmi na mashabiki wake leo ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem jijini Dar.  Akizungumza na Uwazi, Meneja wa Dar Live, Juma Mbizo alisema kuwa mapema kabla ya saa kumi na mbili jioni kutakuwa na matembezi sambamba na Samatta maeneo ya Temeke na baada ya hapo, saa kumi na mbili atatinga ndani ya Dar Live kuwaaga mashabiki wake. 


“Kutakuwa na red carpet ambapo mashabiki wote watapata fursa ya kupiga picha na Samatta sambamba na kuzungumza naye mawili matatu kisha burudani kabambe itafuatiwa kutoka kwa Khalid Chokoraa ambaye tayari amemtungia wimbo, Twanga Pepeta chini ya Ali Chocky pamoja na Msagasumu,” alisema Mbizo na kumalizia kuwa kiingilio kitakuwa ni 5,000 kwa wote.

 Naibu waziri  Wizara ya Kazi Vijana na Ajira Anthony Mavunde ( wa pili kushoto) akiwa na Mkurugenzi mkuu wa Airtel Bw, Sunil Colaso,akifatiwa na Mshauri wa Airtel Fursa, Eng George Mulamula kwa pamoja wakionyesha bango kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Airtel Fursa msimu wa pili. Akishuhudia (kushoto) ni Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel, Bi Beatrice Singano Mallya.
 Mkurugenzi mkuu wa Airtel Bw, Sunil Colaso akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mradi wa Airtel FURSA msimu wa 2. mradi unaowawezesha vijana kati ya miaka 18 hadi 24
kupata fursa za kuinua biashara zao, uliyozinduliwa Naibu waziri Wizara ya Kazi Vijana na Ajira Anthony Mavunde  katika ofisi ya Airtel makao makuu Jijini Dar es saalam
 Naibu waziri  Wizara ya Kazi Vijana na Ajira Anthony Mavunde akiongea wakati wa uzinduzi wa mradi wa Airtel FURSA msimu wa 2 mradi unaowawezesha vijana kati ya miaka 18 hadi 24  kupata fursa za kuinua
biashara zao. Uzinduzi huo ulifanyika katika ofisi ya Airtel makao makuu Jijini Dar es saalam
 Kijana aliyewezesha kupitia mradi wa Airtel FURSA msimu wa 1, Mohamed Kigumi akipongezwa na  Mkurugenzi mkuu wa Airtel Bw, Sunil Colaso kwa kufanya vizuri katika biashara yake wakati wa uzinduzi wa msimu wa pili wa mradi wa Airtel FURSA , mradi wenye lengo la kuwawezesha vijana kufikia malengo yao na kukuza biashara zao. Wakishuhudia (kushoto) ni Naibu waziri  Wizara ya Kazi Vijana na Ajira Anthony Mavunde  akifatiwa na Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel, Bi Beatrice Singano Mallya. (kulia) ni Mshauri wa Airtel Fursa, Eng George Mulamula
 Mshauri wa Airtel Fursa, Eng George Mulamula akiongea wakati wa uzinduzi wa mradi wa Airtel FURSA msimu wa pili
 Wageni waalikwa na waandishi wa habari wakifatilia uzinduzi wa mradi wa Airtel FURSA msimu wa pili uliofanyika katika ofisi za makao makuu ya Airtel Morocco jijini Dar es Saalam 

waliotembelea blog