Monday, October 20, 2014

John Terry played his 500th game as captain of Chelsea against Crystal Palace on SaturdayJumamosi John Terry alicheza Mechi yake ya 500 kama Nahodha wa Chelsea na kusema anasikia fahari kuongoza Timu hiyo.
Terry, alivishwa Unahodha na kucheza Mechi yake kama Kepteni wa Chelsea Desemba 5, Mwaka 2001 walipofungwa kwao Stamford Bridge Bao 1-0 na Charlton Athletica na Jumamosi, akicheza Mechi yake ya 500 tangu Siku hiyo, aliiongoza Chelsea kuichapa Crystal Palace Bao 2-1 kwenye Mechi ya Ligi Kuu England na kendelea kutamba kileleni.
Mchezaji ambae alikuwa anashikilia Rekodi ya kuwa Nahodha kwa Mechi nyingi hapo Chelsea ni Lejendari Ron 'Chopper' Harris alieiongoza kwa Mechi 324.

Akielezea hali hiyo, Terry, mwenye Miaka 33, alisema: “Ukweli ni kuwa nafurahia Ukepteni. Napenda. Lakini ipo Siku nitakabidhi utepe na kutungika Buti. Kwa sasa niko safi, nacheza vizuri katika Kikosi kizuri na lengo letu ni kutwaa Mataji.”
Terry alitoa shukrani kubwa kwa Makepteni waliopita wa Chelsea, Marcel Desailly na Dennis Wise, ambao walimpa fursa na kumsaidia sana.
Alieleza: “Nakumbuka nilipopata Unahodha, Marcel alikuwa ndie Kepteni na akaitisha Mkutano na Menejimenti na Dennis. Walisema wakati wangu umefika. Nilikuwa bado Kijana lakini walinipa utepe na kuniongoza. Sitasahau hilo. Bila yao nisingeweza kufanya haya!”


UEFA CHAMPIONS, Kesho Jumanne Usiku inaanza Mechi zake za Tatu za Makundi ambapo safari hii Timu zitakazocheza zitakuwa zinacheza nje ndani, yaani kukutana Wiki hii na kurudiana Timu hizo hizo katika Ratiba inayofuata.Wachezaji wa City wakipasha
Wachezaji wa Man City wakipasha kujiandaa na kipute cha kesho kwenye UEFA champions dhidi ya
CSKA Moscow.
CSKA MOSCOW vs MANCHESTER CITY
Mabingwa wa England, Man City wanaenda huko Moscow, Urusi kucheza na CSKA Moscow huku Timu zote hizi zikisaka ushindi wa kwanza katika Kundi lao.

Fresh from scoring four against Tottenham, Sergio Aguero also trained with City team-matesTimu zote zinaingia kwenye Mechi hii wakitokea kwenye ushindi wa kishindo kwenye Ligi zao Siku ya Jumamosi kwa City kuibamiza Tottenham Bao 4-1 huku Bao zote zikifungwa na Sergio Aguero na CSKA ikiichapa Kuban Krasnodar 6-0.
Lakini Mechi hii ya UCL ndani ya Arena Khimki itachezwa bila ya Watazamaji baada ya UEFA kuiadhibu CSKA kwa vurugu Mwezi uliopita walipocheza na AS Roma.
The City squad prepare for their flight to the Russian capital to take on CSKAMsimu uliopita, hapo hapo Arena Khimki, City waliichapa CSKA Bao 2-1 kwa Bao za Aguero lakini Mchezaji wao Yaya Toure alikumbana na adha ya kuandamwa na kauli za Kibaguzi.

UEFA CHAMPIONS LEAGUE
RATIBA

Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku isipokuwa inapotajwa
Jumanne Oktoba 21

KUNDI E
19:00 CSKA Moscow vs Man City
AS Roma vs Bayern Munich
KUNDI F
APOEL Nicosia vs Paris St-Germain
Barcelona vs Ajax
KUNDI G
Chelsea vs NK Maribor
FC Schalke 04 vs Sporting Lisbon
KUNDI H
BATE Borisovs vs Shakhtar Donetsk
FC Porto vs Athletic Bilbao

Dakika ya 87 Daley Blind aliisawazishia bao Man United na kufanya 2-2 na kuwaokoa Man United huko Hawthorns kwa sare hiyo ambayo aikuleta mabadiliko kwa timu zote mbili licha ya kugawana pointi moja. Sare hii inambakisha Man United nafasi ya 6 na pointi zake 12 huku West Brom Albion wakibaki nafasi ya 15 na pointi zao 9. Dakika ya 66 kipindi cha pili Saido Berahino aliwachomoka mabeki wa United na kuwafunga bao la pili na kufanya 2-1 dhidi ya United baada ya kutanguliziwa pasi na Chris Brunt.Kipindi cha pili dakika ya 48 Marouane Fellaini aliwasawazishia bao safi Man United baada ya kupata krosi kutoka kwa Di Maria na Fellaini aliingia ndani ya Dimba akitokea benchi kuchukua nafasi ya Ander Herrera katika kipindi cha pili dakika ya 46.Fellaini akishangilia bao lakeStéphane Sessegnon akiruka juu kwa kushangilia baada ya kufunga bao la mapema dakika ya nane. Mpaka dakiks 45 zinakatika za kipindi cha kwanza West Brom Albion ndio walikuwa wanaongoza kwa bao 1-0 dhidi ya Manchester United.Stéphane Sessegnon  akishangilia bao lake mapema kipindi cha kwanza baada ya kuweka 1-0 dhidi ya Man United.Dakika ya 8 kipindi cha kwanza West Brom wanafanya shambulizi kali na kupata bao la kuongoza kupitia kwa Stéphane Sessegnon baada ya kupata pasi safi kutoka kwa Andre Wisdom.

KIUNGO wa zamani wa Arsenal Ray Parlour amesema Msimu huu Klabu yake hiyo ya zamani isiwe na matumaini yeyote zaidi ya kumaliza Nafasi ya 3 au ya 4 kwenye Ligi Kuu England. Matokeo hayo yamewaacha Arsenal wakiwa Nafasi ya 6 wakiwa Pointi 11 nyuma ya Vinara Chelsea na Pointi 6 nyuma ya Timu ya Pili, Manchester City, ambao ni Mabingwa Watetezi.
Hivi sasa huko England ipo dhana kubwa kuwa mbio za Ubingwa kwa Msimu huu ni kati ya Timu mbili tu, Chelsea na Man City, huku Arsenal, Man United, Liverpool na Tottenham zikitajwa kuwa ndizo zitakazogombea Nafasi za 3 na 4.
Ray Parlour, akiongea kwenye Kipindi cha Weekend Sports Breakfast cha talkSPORT, amesema: “Nadhani Arsenal wanapigania Nafasi ya 3 au ya 4. Ukiwatazama Chelsea na City wapo Ligi tofauti na Arsenal. Wako juu ya Timu zote Arsenal, Man United, Liverpool na Tottenham. Hizi ndio zinapigania Nafasi mbili, wanapigania Nafasi za 3 na 4!”


Louis van Gaal amesema wapo kwenye hali njema wakati anaitayarisha Timu yake Manchester United Jumatatu Usiku kwenda huko The Hawthorns kuivaa West Bromwich Albion kwenye Ligi Kuu England.
Akiongea Jana na Wanahabari kuhusu Mechi hiyo, Meneja huyo alisema hivi sasa ni Wachezaji Wanne tu ambao ndio Majeruhi na Ijumaa aliweza kuwa na Wachezaji wengi wa Timu ya Kwanza kiasi cha kutolazimika kuchukua Wachezaji wa Timu ya Pili ili kuja kuongeza idadi kwenye Mazoezi.Louis van Gaal amesema wapo kwenye hali njema wakati anaitayarisha Timu yake Manchester United Jumatatu Usiku kwenda huko The Hawthorns kuivaa West Bromwich Albion kwenye Ligi Kuu England.
Akiongea Jana na Wanahabari kuhusu Mechi hiyo, Meneja huyo alisema hivi sasa ni Wachezaji Wanne tu ambao ndio Majeruhi na Ijumaa aliweza kuwa na Wachezaji wengi wa Timu ya Kwanza kiasi cha kutolazimika kuchukua Wachezaji wa Timu ya Pili ili kuja kuongeza idadi kwenye Mazoezi.
Alieleza: “Asubuhi hii hatukuhitaji Wachezaji wa Timu ya Pili na hii ni habari njema. Nina furaha hatuna Majeruhi zaidi kutoka Mechi za Kimataifa. Tupo hali njema. Wapo Wachezaji wanaoendelea kupona na tutaangalia hadi Jumatatu Kikosi kitakuwa kipi. Hivi sasa tuna Wachezaji Wanne tu majeruhi. Hii ni safi.”
Wachezaji ambao bado ni Majeruhi ni Mabeki Jonny Evans na Paddy McNair na Mawinga Jesse Lingard na Antonio Valencia lakini pia Man United itamkosa Nahodha Wayne Rooney ambae anatumikia Kifungo chake cha Mechi 3 kwa Kadi Nyekundu.
LEO Jumatatu, Van Gaal anasaka ushindi wake wa kwanza wa Ugenini dhidi ya WBA ambayo imeshinda Mechi zao mbili za Nyumbani zilizopita dhidi ya Burnley na Hull City.

Van Gaal ameeleza: “Nadhani WBA ni Timu ngumu kuifunga hasa Nyumbani kwao. Wanacheza Pasi ndefu lakini pia wanazuia nafasi. Ni Wapinzani hatari. Lakini kila Mpinzani Ligi Kuu ni mgumu. Tunataka tuanze na ushindi baada ya mapumziko ya Mechi za Kimataifa.”



Mmoja wa askari waliokuwa wamepangwa katika suala zima la kusimamia usalama ndani ya tamasha la Fiesta 2014 akihakikisha usalama wa kutosha unakuwepo katika eneo hilo,na watazamaji wanapata burudani iliyokusudiwa kutoka kwa wasanii mbalimbali waliotumbuiza usiku wa kuamkia leo katika tamasha la Fiesta 2014 lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya Lidaz Kinondoni jijini Dar.

Shaa na madansa wake wakilishambulia jukwaa.

Pichani kulia ni Msanii kutoka nchini Nigeria ajulikanae kwa jina la Kisanii Davido sambamba na Diamond Platnum kwa pamoja wakilishambulia jukwaa la fiesta 2014 usiku wa kuamkia leo.

Msanii kutoka THT,Barnaba akiimba wimbo wake wa Wahalade sambamba na madansa wake kwenye jukwaa la fiesta 2014,katika viwanja vya Lidaz Kinondoni jijini Dar.

Sehemu ya umati wa watu waliokuwa wakishuhudia yaliyokuwa yakijiri kwenye jukwaa la Fiesta usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya Lidaz Kinondoni jijini Dar.

Ilikuwa ni shoo moja nzuri kutoka nyumba ya vipaji ya THT

Pichani msanii Linah (nyeupe) akiwa na skwadi lake mara baada kumaliza kulishambulia jukwaa kwa pamoja.

Anaitwa Ally kiba ambaye inaelezwa kutoka kwa mashabiki kuwa alifanyo shoo nzuri na iliyowavutia,na kuthibitisha uwezo wake kuwa ni kweli amerejea kwenye kiti chake cha usanii.

Msanii kutoka nchini Marekani Clifford Haris a.k.a T.I akilishambulia jukwaa la Fiesta vilivyo

Msanii kutoka nchini Marekani T.I akiwaimbisha mashabiki wake

PICHA NA MICHUZI JR,

waliotembelea blog