Monday, October 20, 2014


UEFA CHAMPIONS, Kesho Jumanne Usiku inaanza Mechi zake za Tatu za Makundi ambapo safari hii Timu zitakazocheza zitakuwa zinacheza nje ndani, yaani kukutana Wiki hii na kurudiana Timu hizo hizo katika Ratiba inayofuata.Wachezaji wa City wakipasha
Wachezaji wa Man City wakipasha kujiandaa na kipute cha kesho kwenye UEFA champions dhidi ya
CSKA Moscow.
CSKA MOSCOW vs MANCHESTER CITY
Mabingwa wa England, Man City wanaenda huko Moscow, Urusi kucheza na CSKA Moscow huku Timu zote hizi zikisaka ushindi wa kwanza katika Kundi lao.

Fresh from scoring four against Tottenham, Sergio Aguero also trained with City team-matesTimu zote zinaingia kwenye Mechi hii wakitokea kwenye ushindi wa kishindo kwenye Ligi zao Siku ya Jumamosi kwa City kuibamiza Tottenham Bao 4-1 huku Bao zote zikifungwa na Sergio Aguero na CSKA ikiichapa Kuban Krasnodar 6-0.
Lakini Mechi hii ya UCL ndani ya Arena Khimki itachezwa bila ya Watazamaji baada ya UEFA kuiadhibu CSKA kwa vurugu Mwezi uliopita walipocheza na AS Roma.
The City squad prepare for their flight to the Russian capital to take on CSKAMsimu uliopita, hapo hapo Arena Khimki, City waliichapa CSKA Bao 2-1 kwa Bao za Aguero lakini Mchezaji wao Yaya Toure alikumbana na adha ya kuandamwa na kauli za Kibaguzi.

UEFA CHAMPIONS LEAGUE
RATIBA

Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku isipokuwa inapotajwa
Jumanne Oktoba 21

KUNDI E
19:00 CSKA Moscow vs Man City
AS Roma vs Bayern Munich
KUNDI F
APOEL Nicosia vs Paris St-Germain
Barcelona vs Ajax
KUNDI G
Chelsea vs NK Maribor
FC Schalke 04 vs Sporting Lisbon
KUNDI H
BATE Borisovs vs Shakhtar Donetsk
FC Porto vs Athletic Bilbao

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog