Saturday, May 23, 2015



Mkufunzi wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho ametangazwa kuwa mkufunzi bora katika ligi ya Uingereza kwa mara ya tatu.
Akihudumia kipindi chake cha pili katika kilabu hiyo rais huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 52 aliiongoza Chelsea kubeba taji lao la kwanza la ligi ya Uingereza katika kipindi cha miaka mitano pamoja na kombe la Ligi.

Jose Mourinho ameiongoza Timu ya Chelsea na kuibuka na Ushindi

John Terry akifurahia Ubingwa wao mapema mwezi wa tano kwenye tarehe 3 waliposhinda Mechi na kutwaa Ubingwa wa England kwa mara nyingine.
Gary Cahill nae alifurahia

Kiungo wa kati wa Chelsea Eden Hazard ambaye aliifungia Chelsea mabao 20 alitangazwa kuwa mchezaji bora wa ligi ya Uingereza msimu huu.


Klabu ya Ligi Kuu England Sunderland hivi karibuni imetembelea Tanzania ikiongozwa na Mkuu wao wa Kuendeleza Soka Kimataifa, Graham Robinson, ambae alizuru Migodi Miwili inayomilikiwa na Acacia Mining ili kutoa Mafunzo ya Soka kwa Jamii zinazoishi jirani na Migodi hiyo.
Acacia Mining plc, ndiyo inayomiliki Migodi ya Dhahabu ya Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara.
Ziara hiyo ya Graham ni Mradi wa pamoja wa Klabu ya Sunderland na Acacia Mining ili kutoa Mafunzo ya Soka na Ukocha kwa Timu za Migodi hiyo na Makocha wao.

Mafunzo hayo yalifanyika Bulyanhulu Mine School yakijumuisha Makocha wa Timu ya Acacia pamoja na Makocha kutoka Vijiji jirani.
Akiongelea kuhusu Mafunzo hayo, Graham alisema: "Tulitoa mafunzo ya vitendo kadhaa na Makocha walishiriki kikamilifu na kuuliza maswali mengi."
"Soka ya Jamii ndio chanzo cha Wachezaji wengi na kupitia Washirika wetu Barani Afrika tuna Miradi ya muda mrefu na tunasifika kwa kuwekeza katika Programu za Elimu katika Jamii."
Baada ya Kipindi cha kutoa Mafunzo, Graham alishuhudia Mechi kati ya Shule ya Sekondari ya Bugarama na Shule ya Sekondari ya Bulyanhulu ambapo Msafara wa Sunderland ulitoa Mipira Miwili na Bendera.
Graham aliongeza: "Tunathamini sana kuhusu uhusiano mzuri ambao tunao na Tanzania na tunalenga kujitwika kwenye Jamii ambazo tunafanya nazo kazi ili kufikisha malengo huku tukiboresha maisha ya Watu."
Katika sehemu ya Ziara yake ya Tanzania, Graham pia alikutana na Maafisa wa Symbion Power na kutembelea eneo ambalo litajengwa Kituo cha Vijana cha Rais Jakaya M. Kikwete (Jakaya M. Kikwete Youth Park) pale Kidongo Chekundu Jijini Dar es Salaam.
Kituo hicho kinagharamiwa na Symbion Power na Klabu ya Sunderland inatoa msaada wa Kiufundi na wa Vitendo.

waliotembelea blog