Wednesday, September 23, 2015


 Mkazi wa Wazo Hill, Tegeta Mary Joseph (Katikati) akipokea zawadi ya fulana toka kwa Msimamizi wa mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Ubungo, Mbezi na Tegeta Bw. Victor Mhindi (Kulia) wakati wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani iliyofanyika katika baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar es salaam. (Kushoto) ni mshereheshaji wa promosheni hiyo na Mtangazaji wa kipindi cha Ubaoni redio E-fm, Gadner Habash.



 Mkazi wa Tegeta Kibaoni na mpenzi wa bia ya Tusker Bi. Leonarda Shayo akiifurahia zawadi yake ya mfuko na fulana aliyokabidhiwa pale promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani ilipofunga kambi ndani ya baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar. Baa hiyo iliibuka mshindi wa wiki wa promosheni hiyo ambayo inadhaminiwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti. Akikabidhi zawadi hiyo (Kulia) ni Balozi wa bia ya Tusker Veronica Mbilinyi na (Kushoto) ni mshereheshaji wa promosheni hiyo Gadner Habash. 





 Mpenzi wa bia ya Tusker ambaye pia ni mkazi wa jiji la Mbeya Monalisa Makangila(Katikati) akipokea zawadi ya fulana na mfuko toka kwa balozi wa bia ya Tusker Veronica Mbilinyi (Kulia) wakati wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani katika baa ya Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar. Baa hiyo iliibuka mshindi wa wiki wa promosheni hiyo inayoendeshwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti. (Kushoto) ni mshereheshaji wa promosheni hiyo na mtangazaji wa redio Efm Gadner Habash.
Mkazi wa Tegeta, Uwanja wa Upanga ambaye pia ni Mwalimu wa shule ya Sekondari Max Richard akijiandaa kupokea zawadi ya fulana toka kwa Meneja Masoko wa bia ya Tusker Bi. Nandi Mwiyombella (Kulia) wakati wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani katika kiwanja cha baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar es salaam. Baa hiyo iliibuka baa ya wiki kwenye promosheni hiyo inayoendeshwa na bia ya Tusker yenye lengo la kuzihamasisha baa mbalimbali za mitaa inayotuzunguka kufanya kweli kwenye utoaji huduma kwa wateja. Promosheni hiyo ya nchi nzima inaendelea pia katika mikoa ya Arusha, Mwanza, Moshi, Morogoro na Mbeya.
Mkazi wa Segerea ambaye pia ni mjasiriamali Frank Ndumbalo (Kulia) akipokea zawadi yake ya fulana toka kwa Afisa Masoko anayejifunza kwa vitendo toka Kampuni ya bia ya Serengeti Bw. Josephat Shelukindo wakati wa kusherekea ushindi wa baa ya Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar es salaam. Baa hiyo iliibuka mshindi wa wiki kwenye promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani Kiwanjani inayodhaminiwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti.



UBA Tanzania staff during the jogging to bond event which took place on Saturday September 19, 2015.

UBA Tanzania staffs participate engaged in aerobics session during the jogging to bond event which took place on Saturday September 19, 2015

UBA Tanzania staffs participate in the aerobics session during the jogging to bond event which took place on Saturday September 19, 2015.

A cross section of UBA Tanzania staff in a group selfie after the exercises during the jogging to bond event which took place on Saturday September 19, 2015.



Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower( kushoto) akiendelea kutoa burudani ya nguvu huku msanii mwenzake Sony Masamba akiendelea kuzirundi ngoma ndani ya kiota cha Escape One, Mikocheni jijini Dar. Usikose leo siku ya Jumatano kwenye mkesha wa EID maana kuna vitu vingi vipya.

Mwimbaji wa Bendi ya Skylight, Natasha pamoja na mwenzake Kasongo Junior haya ni Majembe mapya ya bend ya Skylight yenye uwezo mkubwa wa katika uimbaji.

Sony Masamba ambaye ni mmoja wa waimbaji wa Skylight akiendelea kutoa burudani akisindikizwa na waimbaji wenzake.

Sam Mapenzi pamoja (kulia) akiimba pamoja na Ashura Kitenge wakiendelea kuwakonga nyoyo mashabiki wa Skylight Band waliofika siku ya Jumapili kwenye kiota cha Escape One Mikocheni na leo sio ya kukosa njoo tukeshe pamoja tukifurahi na mziki mzuri kutoka katika bendi hiyo.

Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower akiimba huku mashabiki wa bendi hiyo wakiserebuka kwa furaha na leo sio ya kukosa njoo na mwenzako uje kuona vitu vipya kutka kwenye bendi hiyo.
Mwimbaji wa Bendi ya Skylight, Natasha akiendelea kutuoa burudani kwa mashabiki wao waliofika kwenye kiwanja cha Escape One kujionea burudani ya nguvu kutoka katika bendi hiyo.


CAPITAL ONE CUP
Raundi ya 3
RATIBA
Jumatano Septemba 23

21:45 Crystal Palace vs Charlton
21:45 MK Dons vs Southampton
21:45 Newcastle vs Sheffield Weds
21:45 Norwich vs West Brom
21:45 Tottenham vs Arsenal
21:45 Walsall vs Chelsea
22:00 Liverpool vs Carlisle
22:00 Man United vs Ipswich Town



Simba imekuwa ikiendelea na mazoezi yake katika kambi maalumu mjini Zanzibar.

Simba inajiwinda tayari kwa mechi yake dhidi ya watani wake wa jadi Yanga, Jumamosi.

Yanga inakutana na Simba katika mechi hiyo ya kwanza ya msimu kwa timu hizo kukutana.
 

Chini ya Kocha Mkuu, Dylan Kerr, Simba imekuwa ikifanya mazoezi mara mbili kwa siku.

Mazoezi yake yanaonekana kuwa ni ya mpira zaidi ingawa siku walipotua Zanzibar, mazoezi ya kwanza walianza na kutafuta stamina.

Tayari Simba imeshinda mechi zake zote tatu za mwanzo ikianza kwa kuitwanga African Sports bao 1-0, ikaishindilia Mgambo Shooting 2-0, halafu ikarejea Dar es Salaam na kuituliza Kagera Sugar 3-0 huku mshambuliaji wake, Hamisi Kiiza aking’ara.


Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania (Twiga Stars) inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Taifa ya Wanawake ya Malawi tarehe 24 Oktoba, mwaka huu nchini Malawi.

Mechi hiyo kati ya Twiga Stars dhidi ya Malawi itachezwa jijini Lilongwe kufuatia mwaliko wa chama cha soka nchini Malawi (FAM) kuialika Twiga Stars kwenda nchini Malawi kwa ajili ya mchezo huo
Mchezo huo wa kirafiki ni sehemu ya maandalizi ya vikosi vya timu zote mbili za Wanawake Tanzania na Malawi kwa ajili ya michuano mbalimbali.
Viingilio vya mchezo wa watani wa jadi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania utakaochezwa Jumamosi katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam vimetangazwa leo ambapo kiingilio cha chini kitakua ni shilingi elfu saba (7,000).

Katika mchezo huo kiingilio cha juu kitakua ni shilingi Elfu Thelathini (30,000) kwa viti vya VIP A, Elfu Ishirini (20,000) kwa viti vya VIP B & C, huku kiingilio cha shilingi Elfu Saba (7,000) kikiwa ni kwa viti vyenye rangi ya Blu, Kijani na Orange.
Tiketi za mchezo ho zitaanza kuuzwa siku ya Ijumaa saa 2 kamili asubuhi katika vituo vifuatavyo: Karume – Ofisi za TFF, Buguruni – Oilcom, Dar Live – Mbagala, Uwanja wa Taifa, Luther House – Posta, Ferry – Kivukoni, Mnazi Mmoja, Ubungo – Oilcom na Makumbusho – Standi ya mabasi ya daladala.
TFF inawaomba wapenzi, wadau na washabiki wa mpira wa miguu nchin kununua tiketi katika magari yaliyopo kwenye vituo vya kuuzia tiketi ili kuondokana na kuuziwa tiketi zisizo sahihi.
Mchezo huo utachezeshwa na mwamuzi wa kimataifa mwenye beji ya FIFA, Israel Nkongo (Dsm) akisaidiwa na Josephat Bulali (Tanga), Ferdinand Chacha (Mwanza) mwamuzi wa akiba Soud Lila (Dsm) wakati kamisaa wa mchezo huo atakua Charles Mchau kutoka Kilimanjaro.
Michezo mingine ya Ligi Kuu ya Vodacom siku hiyo ya Jumamosi itakua ni kati ya Coastal Union dhidi ya Mwadui FC katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, Maafande wa jeshi la Magereza (Tanzania Prisons) watawakaribisha maafande wa Mgambo Shooting katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Maafande wa JKT Ruvu watakuwa wenyeji wa Stand United katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, huku wakata miwa wa Turiani Mtibwa Sugar watawakaribisha Majimjaji ya Songea katika uwanja wa Manungu wakati Kagera Sugar watakuwa wenyeji wa Toto Africans katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Ligi hiyo itaendelea siku ya Jumapili kwa michezo miwili ambapo waoka mikate wa Azam FC watawakaribisha Mbeya City katika uwanja wa Chamazi Complex, huku African Sports wakiwa wenyeji wa Ndanda FC kwenye uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.


Good news kwa watu wa nguvu ambao +254 Kenya  inayatambua majina yao ambayo yako kwa wino mzito kabisa kwenye Industry ya Entertainment Kenya, wa kwanza ni  Annabel Onyango ambae ni Mwanamitindo staa kabisa kutoka Kenya… mwingine ni Marek Fuchs ambae ni Manager wa Group la Mastaa wakali kabisa, Sauti Sol.
Majina ya wawili hao, yani Annabel na Marek sasahivi wanazungumziwa tofauti, wamekuwa kwenye uhusiano wa Kimapenzi kwa zaidi ya miaka nane na sasahivi ninazo pichaz mtu wangu, uthibitisho tosha kabisa kwamba wao sasahivi ni mtu na mume wake.
Kama bado hujakutana nazo, unaweza kuzicheki hapa mwanzo mwisho pamoja na baadhi ya mastaa wa +254 waliokula mwaliko wa nguvu kabisa ikiwemo Sauti Sol wenyewe !!
Anna-1
Mwenye suti nyeupe ndio bwana Harusi mwenyewe, Marek Fuchs na nyuma yake ni Bibi Harusi, Annabel Onyango mwenyewe katika ubora wao.
anna-2
anna-8
Bien-Aimé Baraza, moja ya Mastaa wa Sauti Sol.. camera ikawanasa kwenye story na mrembo wake pembeni.

waliotembelea blog