Wednesday, September 23, 2015



Simba imekuwa ikiendelea na mazoezi yake katika kambi maalumu mjini Zanzibar.

Simba inajiwinda tayari kwa mechi yake dhidi ya watani wake wa jadi Yanga, Jumamosi.

Yanga inakutana na Simba katika mechi hiyo ya kwanza ya msimu kwa timu hizo kukutana.
 

Chini ya Kocha Mkuu, Dylan Kerr, Simba imekuwa ikifanya mazoezi mara mbili kwa siku.

Mazoezi yake yanaonekana kuwa ni ya mpira zaidi ingawa siku walipotua Zanzibar, mazoezi ya kwanza walianza na kutafuta stamina.

Tayari Simba imeshinda mechi zake zote tatu za mwanzo ikianza kwa kuitwanga African Sports bao 1-0, ikaishindilia Mgambo Shooting 2-0, halafu ikarejea Dar es Salaam na kuituliza Kagera Sugar 3-0 huku mshambuliaji wake, Hamisi Kiiza aking’ara.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog