Saturday, January 21, 2017



Ni taarifa rasmi kutoka IKULU Dar es salaam juu ya maamuzi mapya ya Rais John Pombe Magufuli ambaye leo January 21 2017 amemteua Anne Kilango Malecela kuwa Mbunge kwenye bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Cheo cha mwisho alichopewa Anne Kilango kilikua ni ukuu wa mkoa wa Shinyanga lakini April 11 2016 Rais Magufuli alitengua uteuzi wake na katibu tawala wa mkoa Abdul Rashid Dachi baada ya mkoa huo kutoa taarifa zisizo sahihi kuwa hauna Watumishi hewa.
Taarifa ya IKULU leo imesema baada ya Anne Kilango kuteuliwa, ataapishwa kwa mujibu wa taratibu za bunge.

ULIPITWA? TAZAMA WANAJESHI WA TANZANIA WAKIONYESHA UWEZO WAO MBELE YA RAIS MAGUFULI


Usiku wa January 21 2017 wawakilishi pekee wa ukanda wa Afrika Mashariki katika michuano ya mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON 2017, timu ya taifa ya Uganda ilitolewa rasmi katika michuano ya mataifa ya Afrika yanayoendelea nchini nchini Gabon.
Uganda wameaga mashindano hayo baada ya kukubali kipigo cha goli 1-0 dhidi ya timu ya taifa ya Misri katika mchezo wao wa pili wa Kundi D, Uganda wanaaga mashindano hayo na kuwa wanasubiria mchezo wao wa kukamilisha ratiba dhidi ya Mali, hawana uwezo wa kufuzu hatua ya robo fainali hata wakipata ushindi wa aina yoyote ile.
Abdallah El Said wa Misri ndio alihitimisha safari ya Uganda katika michuano ya AFCON 2017, baada ya kufunga goli dakika ya 89 kwa kutumia vyema assist iliyotolewa na Mohamed Salah, kwa mujibu wa rekodi Uganda ni dhaifu kwa Misri, kwani leo wanakuwa wamefungwa kwa mara ya 16 na mara ya mwisho Uganda



Ay ambaye ni staa wa smash hit ya ‘zigo’ na kwasasa akiwa ana brand new single na Nyasinski amechukua time yake na kuwaandikia Wasanii wenzake yafuatayo >>>> ‘Ndugu zangu Wasanii wa kibongo, Wadau na Mashabiki wa muziki nimeona sio vibaya kuwashirikisha na nyie jambo hili
Ili Producers wa Kibongo waweze kubadilisha Tunes kwa beats zao na waendelee kutisha KULIKO JANA nawaomba wasanii wenzangu muweke utaratibu wa kusafiri nao mnavyotoka nje ya Afrika Mashariki wakienda, wakiona, wakijifunza na kujiongeza LAZIMA TUTATISHA SANA‘ – AY
Nimeona sana Afrika Magharibi wana hesabu hizo ndio maana wana Tunes za kila aina,Tuna Producers wazuri sana ila wanahitaji kusafiri zaidi,Mfano mzuri ni @majani187 @nahreel@hermyb na @marcochali wamepata exposure ndio maana wana Tunes Unique‬ all the time #ZEE – @AyTanzania kwenye Instagram
UMEPITWA? Kijana aliyemshtua Mama Kanumba, Dully Sykes kuhusu ushirikiano na Alikiba je? tazama kwenye hii video hapa chini kujionea kila kitu


January 21 2017 Mabingwa watetezi wa Kombe la ASFC klabu ya Dar es Salaam Young Africans ilishuka dimba kuanza kutetea taji lake hilo, kwa kucheza dhidi ya Ashanti United katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, katika mchezo huo Yanga walifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 4-1.


1-1Juan Mata kawapa zawadi Stoke City dakika ya 19 ya kipindi cha kwanza.Mata kajifunga bao dakika ya 19 na kuwapa zawadi Stoke City kipindi cha kwanza. mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika United 0 Stoke City 1.Man United kwenye harakati za kupunguza pengo na kusonga mbele...




Bao za liverpool zilifungwa na Roberto Firmino dakika ya (55' na dakika ya 69') Huku bao za Swansea City zikifungwa na Fernando Llorente dakika ya (48' na dakika ya 52')
Kipindi cha pili Gylfi Sigurdsson akiwafungia bao la ushindi dakika ya (74') na mtanange kumalizika dakika 90 kwa Swansea kujikwamua mkiani na kupanda juu na kuwashangaza Mashabiki wa Majogoo na kwenye Uwanja wao.



Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi kuwa Mjumbe wa Kamati ya Maendeleo ya soka ya FIFA kwa miaka minne ijayo. Uteuzi huo unaanza mwaka huu 2017 hadi 2021.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Januari 18, 2017 iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa FIFA, Fatma Samoura inasema: “Tuna faraja kukufahamisha kuwa umeteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Maendeleo ya FIFA. Tunachukua nafasi hii kukupongeza kwa uteuzi huu,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa hiyo ilifafanua kuwa Kamati hiyo inayoongozwa na Sheikh Salman Bin Ebrahim Al Khalifa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Bara la Asia, ina majukumu ya kusimamia mipango ya maendeleo ya mpira wa miguu duniani kote.
Wajumbe wengine wote watatangazwa kwenye tovuti ya FIFA ambayo ni www.FIFA.com.
Huu ni mfululizo wa Tanzania kupata nafasi katika vyombo vikubwa vinavyoendesha soka FIFA na CAF. Mwishoni mwa mwaka jana, CAF – Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika lilimteua Rais Malinzi kuwa mmoja wa wajumbe wa kamati maalumu inayoongozwa na Rais wa CAF, Issa Hayatou ya kuboresha mfumo wa uongozi wa CAF.
TFF inamshukuru Rais Gianni Infantino na kamati yake ya ushauri kwa kumteua Malinzi katika nafasi ya ujumbe katika kamati hiyo muhimu ya maendeleo ya soka ulimwenguni.


Ligi Kuu England
RATIBA
Jumamosi Januari 21

15:30 Liverpool v Swansea City
18:00 Bournemouth v Watford
18:00 Crystal Palace v Everton
18:00 Middlesbrough v West Ham United
18:00 Stoke City v Manchester United
18
:00 West Bromwich Albion v Sunderland
20:30 Manchester City v Tottenham Hotspur
Jumapili Januari 22
15:00 Southampton v Leicester City
17:15 Arsenal v Burnley
19
:30 Chelsea v Hull City

MANCHESTER City sasa wameruhusiwa kumtumia Staa Mbrazil wa Miaka 19 Gabriel Jesus kwenye Mechi yao ya EPL, Ligi Kuu England, ya kesho Jumamosi dhidi ya Tottenham Hotspur.
City walishafikia makubaliano na Klabu ya Brazil Palmeiras tangu Mwezi Julai Mwaka Jana kumnunua Kinda huyo wa Brazil mwenye Miaka 19 kwa Dau la Pauni Milioni 27 na pia kukubali Mchezaji huyo abakie Palmeiras hadi Msimu wa Brazil utakapoisha Mwezi Desemba.
Jesus amekuwa Kambini na City kwa Wiki 3 sasa lakini ukiritimba umekwamisha Uhamisho wake kukamilika rasmi na hivyo kusitisha kuichezea rasmi City.
Kinda huyo ndio kwanza amechomoza kwenye Soka la Dunia akiwa na Msimu wa Pili tu na Palmeiras lakini akaiongoza Klabu hiyo kutwaa Ubingwa wa Taifa Mwezi Novemba baada ya kutwaa Medali ya Dhahabu akiichezea Brazil kwenye Michezo ya Olimpiki, RIO 2016, Mwezi Julai.
Jesus alianza kukichezea Kikosi cha Kwanza cha Timu ya Taifa ya Brazil Mwezi Septemba Mwaka Jana na kufunga Bao 4 katika Mechi zake 6.
Hivi sasa Man City wapo Nafasi ya 5 kwenye EPL, wakiwa Pointi 10, nyuma ya Vinara Chelsea baada ya kufungwa Mechi 2 kati ya 3 walizocheza mwisho.


JE WAJUA?
-Jesus alijilukana kama Gabriel Fernando alipoanza kuichezea Palmeiras akiwa na Miaka 17.

-Akiwa huko alipewa Jezi Namba 33 [Umri wa Yesu Kristu] na mmoja wa Maafisa Habari wa Klabu hiyo akammwambia atumie Jina la Gabriel Jesus.

-Akiwa na Man City, Jesus pia atavaa Jezi Namba 33 ambayo awali ilivaliwa na Nahodha wa City Vincent Kompany.

waliotembelea blog