Friday, August 22, 2014

MMGM3002
Mshindi wa taji la Miss Temeke 2014,Sitti Mtemvu akipungia mkono mara tu baada ya kutangazwa rasmi kuwa ndie aliestahili kupata taji hilo katika shindano lililomalizika usiku huu kwenye Ukumbi wa TCC Club,Chang’ombe jijini Dar es salaam.Kushoto ni Mshindi wa pili,Salama Saleh na kulia ni Mshindi wa tatu,Neema Mollely.PICHA KWA HISANI YA MICHUZIBLOG
MMGM2844
Mwanalibeneke Othman Michuzi akimvisha taji la Michuzi Blog Miss Photogenic 2014 Mrembo Lilian Loth (9) kwa niaba ya Ankal,baada ya kuonekana ndie Mrembo pekee mwenye mvuto wa picha katika shindano la Miss Temeke 2014,lililomalizika usiku huu kwenye Ukumbi wa TCC Club,Chang’ombe jijini Dar es salaam
MMGM2906
Baadhi ya Warembo wa Miss Temeke 2014 wakiongozwa na Michuzi Blog Miss Photogenic,Lilian Loth wakiwa kwenye picha ya pamoja kusubiria kutangazwa mshindi wa jumla wa shindano hilo.

IMG_2829
Kikundi cha Platinum Dancers kikionyesha umahiri wao wakati wa shindano la kumsaka mshindi wa dansi la Serengeti fiesta, lililofanyika katika Ukumbi wa Klabu Lavida , mjini Tanga leo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya tamasha la Serengeti fiesta linalotarajiwa kufanyika kesho jumamosi Agosti 23 kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini humo.
IMG_2830
Majaji wa shindano la kumsaka mshindi wa  dansi la Serengeti fiesta wakifuatilia kwa makini namna wasanii wanavyotoana jasho ili kumpata mshindi wa shindano hilo.
IMG_2831
Kundi la Street Color, likionyesha umahiri wao katika  kinyang’anyiro hicho ambacho  mshindi aliondoka na kitita cha sh milioni  moja na kupata nafasi ya kutoa shoo katika tamasha la Serengeti fiesta katika Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
IMG_2832
Lucas Kaili wa kundi la Ice Cream naje akijaribu bahati yake wakati wa shindano hilo. 
IMG_2833
Kundi la Ice Cream likipozi kwa picha mara  baada ya kutangazwa  washindi wa dansi la Serengeti fiesta na kujishindia  zawadi ya sh milioni moja.


 

 Kocha Jose Mourinho akizungumza na Waandishi wa habari na akisema kuwa tayari wapo tayari na wako fiti kuikabiri Leicester.


Eden Hazards na Filipe Luis wakikabana leo kwenye mazoezi yao ya mwisho Stamford Bridge tayari kwa kuikaribisha timu iliyopanda Daraja msimu huu Leicester
Jon Obi Mikel na Mohamed Salah kwenye mazoezi leo huku Viongozi pamoja na Meneja Jose akiwaangalia..
Salah, Luiz na Hazard wakifanya mazoezi kwenye uwanja wao wa Nyumbani Stamford Bridge

Diego Costa, Nathan Ake, Oscar na Mikel


LA LIGA
RATIBA
Mechi za Ufunguzi
Jumamosi Agosti 23

20:00 Malaga CF v Athletic de Bilbao
22:00 Sevilla FC v Valencia
22:00 Granada CF v Deportivo La Coruna
2359 UD Almeria v RCD Espanyol
 

Jumapili Agosti 24
20:00 SD Eibar v Real Sociedad
22:00 FC Barcelona v Elche CF
22:00 Celta de Vigo v Getafe CF
23:59 Levante v Villarreal CF

Jumatatu Agosti 25
21:00 Real Madrid CF v Cordoba
23:00 Rayo Vallecano v Atletico de Madrid

Ijumaa Agosti 29
21:00 Getafe CF v UD Almeria
23:00 Valencia v Malaga CF


 
Kocha Msaidizi wa Tanzania XI, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ (kushoto) akizungumza na nyota wa zamani wa Real Madrid, Fernando Sanz Duran. 
 Kiungo wa zamani wa Real Madrid, Luis Figo akizungumza na waandishi wa habari jana (hawapo pichani). Wa kwanza kulia ni nyota mwingine wa Real Madrid, Christian Karembeu na katikati ni mratibu wa ziara ya wanasoka hao, Mkurugenzi wa Kampuni ya TSN, Farough Baghozah.


Heading for Merseyside? Former Chelsea striker Samuel Eto'o could be set to sign for Liverpool
Anakwenda Merseyside? Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Samuel Eto'o anaweza kujiunga na Liverpool.

MCAMEROON, Samuel Eto'o yuko tayari kukamilisha usajili wa ghafla kujiunga na Liverpool.
Mario Balotelli aliwasili Merseyside jana kujaribu kukamilisha uhamisho wa paundi milioni 16 kujiunga Anfield, lakini kama dili litashindikana, nafasi yake itachukuliwa na Mcameroon.
Inafahamika kuwa mshambuliaji huyo wa zamani wa Chelsea alipimwa afya na Liverpool akiwa mjini Paris jana ijumaa.
Eto'o mwenye miaka 33 ambaye anaishi mji mkuu wa Ufaransa, amekubali dili la miezi 12 (mwaka mmoja) kujiunga na Liverpool na anasubiri kupanda ndege kwenda kusaini mkataba.
Eto’o aliripotiwa kuvutiwa na Everton kwa siku chache zilizopita, lakini kigezo cha kucheza ligi ya mabingwa kimemfanya aichague Liverpool.
Mersey paradise: The Cameroon striker, pictured here at the World Cup, was also linked with Everton
Picha hii ya Mcameroon huyu alikuwa katika fainali za kombe la Dunia majira ya kiangazi mwaka huu nchini Brazil.


Na Baraka Mpenja
NUSU fainali ya klabu bingwa Afrika Mashariki na kati, Kombe ka Kagame iliendelea jana mjini Kigali, nchini Rwanda na kupata klabu mbili za kucheza fainali na hatimaye kupatikana bingwa atayechukua kombe lililoachwa na Vital’O ya Burundi.
Katika nusu fainali ya kwanza, El Merreikh ya Sudan ilitinga fainali baada ya kuifunga KCC ya Uganda kwa penalti 3-0.
Mshindi alipatikana kwa changamoto ya mikwaju ya penati kufuatia dakika 120 kumalizika kwa sare ya mabao 2-2.
Katika nusu fainali ya pili, APR walikutana na Wanyarwanda wenzao, timu ya Polisi.
Maafande wa APR walitinga fainali baada ya kushinda kwa penalti 4-3 kufuatia suluhu pacha ya bila kufungana ndani ya dakika 90.
Katika hatua ya robo fainali iliyomalizika juzi katika uwanja wa Nyamirambo, mechi moja tu ndio ilimalizika ndani ya dakika 90 baina ya KCC ya Uganda na Altabara ya Sudan Kusini.
Mechi ya Azam fc dhidi ya El Merreikh alimalizwa kwa penalti ambapo Wasudan waliibuka na ushindi wa penati 4-3 kufuatia dakika 90 kuhitimishwa kwa suluhu pacha ya bila kufungana.
Robo fainali nyingine iliwakutanisha Atletico ya Burundi dhidi Polisi ya Rwanda.
Polisi walishinda kwa penalty 9-8 kufuatia suluhu ya bila kufungana katika dakika 90, lakini rekodi iliyowekwa ni wachezaji wote 22 kupiga penalti.
Robo fainali nyingine iliyohitimishwa kwa mikwaju ya penalti ilikuwa baina ya APR na Rayon Sports. Katika dakika za kawaida timu hizi zilitoka sare ya mabao 2-2.
Katika hatua ya nusu fainali mechi zote mbili zilifikia hatua ya mikwaju ya penalti baada ya timu zote kukomaa ndani ya dakika 120.
Baada ya yote, APR dhidi ya El Merreikh watakutana kesho jumapili katika mchezo wa fainali utakaopigwa uwanja wa Amahoro mjini Kigali.
Mechi hii inatarajia kuwa na upinzani mkubwa kutokana na ubora wa vikosi vya timu zote.

Timu zote zimesheheni vijana wadogo wenye vipaji vya hali ya juu, hivyo kandanda safi linatarajiwa katika dimba hilo la Amahoro ambalo maana yake ni Amani.


Dakikaya 37 kipindi cha kwanza Thomas Müller anaifungia bao la kwanza Bayern Munich kwa kufanya 1-0 dhidi ya Wolfsburg baada ya kazi nzuri ya Arjen Robben kwa kukatiza ndani ya box na kupiga chenga mabeki na kutoa pasi iliyoguzwa na Muller na
kutinga nyavuni./media/images/homepage/fotogalerie-14-15/wolfsburg/FCB_WOB_09_GET_220814.jpgDakika 37 akishangilia bao lake/media/images/homepage/fotogalerie-14-15/wolfsburg/FCB_WOB_17_GET_220814.jpg1-0/media/images/homepage/fotogalerie-14-15/wolfsburg/FCB_WOB_15_GET_220814.jpg
Dakika ya 47 Arjen Robben aliwaipachikia bao la pili na kufanya 2-0 akipewa pasi na Robert Lewandowski.
Ivica Olic wa Wolfsburg aliwapachikia bao safi na kufanya 2-1 kipindi cha pili dakika ya 52 baada ya kupata pasi kutoka kwa Vieirinha./media/images/homepage/fotogalerie-14-15/wolfsburg/FCB_WOB_13_GET_220814.jpg/media/images/homepage/fotogalerie-14-15/wolfsburg/FCB_WOB_01_GET_220814.jpg/media/images/homepage/fotogalerie-14-15/wolfsburg/FCB_WOB_04_GET_220814.jpg/media/images/homepage/fotogalerie-14-15/wolfsburg/FCB_WOB_11_GET_220814.jpg/media/images/homepage/fotogalerie-14-15/wolfsburg/FCB_WOB_02_GET_220814.jpg

BUNDESLIGA
RATIBA/ MATOKEO
Mechi za Ufunguzi
Ijumaa Agosti 22
Bayern Munich 2 vs 1 VfL Wolfsburg

Jumamosi Agosti 23
16:30 Hannover 96 vs Schalke 04
16:30 Hertha Berlin vs  SV Werder Bremen
16:30 Eintracht Frankfurt vs SC Freiburg
16:30 FC Köln vs Hamburger SV
16:30 TSG Hoffenheim vs FC Augsburg
19:30 BV Borussia Dortmund v Bayer 04 Leverkusen

Jumapili Agosti 24
16:30 SC Paderborn 07 vs FSV Mainz 05
18:30 Borussia Mönchengladbach vs VfB Stuttgart

Mkurugenzi mtendaji wa Airtel Bwana Sunil Colasa akiongea na waandishi wa habari leo hii (hawapo pichani) akiwatangazia kuanza kutumika rasmi kwa huduma mpya ya kutuma na kupokea pesa kutoka kwenye mitandao mingine moja kwa moja kwenye akaunti  zao za Airtel money, (interoperability) huduma hii ni ya kwanza Duniani ambapo inaaminika kuwa itasaidia sana wateja wa Airtel Money na Wakala kuokoa muda wa kupata na kutoa huduma kwa haraka Zaidi. 
===========  ==========
  • Wateja Airtel Money sasa wanaweza kutuma na kupokea pesa kwenye akaunti zao za Airtel Money toka Tigo Pesa
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imezindua huduma itakayowawezesha wateja wake wa huduma ya Airtel Money kutuma na kupokea pesa kutoka kwenye mitandao mingine moja kwa moja kwenye akaunti  zao za Airtel money ,  huduma hii ni ya kwanza Afrika na duniani kwa ujumla na hivyo inaweka historia nchini kuzinduliwa ya kwanza kupitia njia ya  mtandao wa simu.

Huduma hii ya kwanza Duniani na Afrika inayohusisha makampuni ya simu Airtel na Tigo ulitangazwa kuwa itaanza kutumika mwishoni mwa mwezi wa Julai na sasa iko tayari ambapo wateja wa Airtel Money  wataweza kutumia  huduma hii kabambe na yenye utofauti kwa inaaminika kuwa ni  rahisi zaidi, salama na ina unafuu katika kutuma pesa kwa kutoka mteja mmoja kwenda mwingine na kuingia moja kwa moja katika (e-wallet) akaunti yake ya simu/mtandao anaotumia na kuweza kuitoa popote alipo.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo Mkurugenzi wa Airtel Bwana Sunil Colaso alisema” Tunayofuraha kushirikiana na makampuni mengine ya simu katika kuhakikisha tunaendelea kutoa huduma za kisasa, zenye ubunifu na kwa gharama nafuu. Ushirikiano huu utawawezesha wateja wa Airtel kutuma na kutoa pesa kutoka kwenye mitandao mingine . 

 Sasa wateja wetu watapokea pesa kutoka kwenye mitandao mingine na kuingia moja kwa moja kwenye (e-wallet) akaunti  zao za Airtel money hivyo kuondoa usumbufu ulikuwepo awali  ambapo mteja anapotumiwa pesa kutoka mtandao mwingine alitakiwa kuzitoa ndani ya siku 7.

Kwa uzinduzi huu  leo tunafanya huduma hii ya kifedha kwa njia ya mtandao kukidhi mahitaji ya wateja. Vile vile mawakala wetu pia wamerahisishiwa utoaji huduma  ambapo sasa hakutakuwa na haja ya wakala kupata udhibitisho wa ujumbe kutoka kwa simu ya mteja kabla ya kufanya malipo.  Tunaamini huduma hii itaongeza usalama wa mawakala na wateja nchini, Pia itamuongezea wakala muda wa kuhudumia wateja wengi Zaidi kwa uhakika, haya ni mapinduzi ya huduma za kifedha ambayo tunaamini ni maendelea makubwa ya maboresho ya huduma hii aliongeza kwa kusema Colaso.

Akiongea kuhusu huduma hiyo mmoja wa wakala ambae alijaribu wa Airtel Money Pasco Woiso alisema “Tunafurahia huduma iliyoanzishwa na Airtel kwa kushirikiana  na mitandao mingine,  leo nimeitumia huduma hii kwa mara ya kwanza lakini nimefurahishwa na ufanisi wake na jinsi wateja wanavyoipokea vizuri nikiwapasha habari kuhusu huduma hiii.  

Kwa sisi wakala awali tulikuwa na tatizo la kupata ujumbe wa malipo, kitambulisho cha malipo na pesa kurudi baada ya muda wa siku saba,  lakini kwa sasa ushirikiano huu umeifanya huduma hii ya pesa kwa mtandao kuwa bora zaidi na kupunguza muda niliokuwa nautumia kumuhudumia mteja moja na hivyo.



‘Mimi na Yanga tulikua na makubaliano ya mkataba na hakuna ukweli kwamba Mshahara niliokua nalipwa Yanga ni mdogo, mshahara usingekua unatosha nisingekubali kusaini mkataba‘
‘Ni kweli kuna mambo mengi hayapo sawa kati yangu na club yangu yaYanga ila ni mambo ya ndani ambayo nisingependa kuyazungumzia, ni mambo madogo ambayo nadhani yanaweza kuisha‘
‘Hakuna ukweli kwamba mimi nakwenda Ulaya, sijui hata imetoka wapi na nani kaanzisha hii ya Ulaya, mimi bado ni mchezaji halali wa Yanga na huwa naongea nao karibu kila siku, hata jana nimetoka kuongea na katibu mkuu na mambo yote yanaelekea vizuri hamna shida yoyote mpaka sasa hivi‘ - Hii ni kauli ya mshambuliaji wa Yanga, Emmanuel Anord Okwi.

Na Baraka Mpenja
NUSU fainali ya klabu bingwa Afrika mashariki na kati, kombe la Kagame inaanza kutimua vumbi leo mjini Kigali, Rwanda.
Timu mbili pinzani za nchini Rwanda, Polisi na APR zitachuana vikali ili kupata timu moja ya kucheza fainali.
Polisi walifuzu hatua hiyo kufuatia kuwatoa Atletico ya Burundi hatua ya robo fainali kwa penati 9-8.
Mikwaju ya penalti ilitumika kuamua mshindi katika mechi hiyo kwasababu dakika 90 zilimalizika kwa suluhu pacha ya bila kufungana.
Kwa upande wa APR, wao walifanikiwa kufuzu nusu fainali kufuatia kuwachapa wapinzani wao Rayon Sport kwa penati 4-3.
Penalti ziliamua mshindi katika mechi hiyo kwa vile dakika 90 zilimalizika kwa sare ya mabao 2-2.
Mechi hii imevuta hisi za mashabiki wengi nchini Rwanda kutokana na timu hizo kucheza ligi moja, hivyo zinajuana vizuri kwa ubora na udhaifu wao.
Mbali na mchezo huo, nusu fainali nyingine itawakutanisha KCC ya Uganda dhidi ya El Merreik ya Sudan katika uwanja wa Nyamirambo, Kigali.

KCC walifuzu kwa kuifunga Altabara ya Sudan kusini katika mchezo wa robo fainali, wakati El Merreik waliifunga Azam fc ya Tanzania.


 LIGI kuu soka Tanzania bara msimu wa 2014/2015 inatarajia kuanza kushika kasi septemba 20 mwaka huu kwa timu 14 kuwania ubingwa unaoshikiliwa na Azam fc. 
Kanuni inasema kuwa ratiba ya ligi inatakiwa kuanikwa hadharani angalau mwezi mmoja kabla ya ligi kuanza, ingawa inaweza kutangazwa hata miezi miwili kabla kama inavyotokea ulaya.
Waendeshaji wa ligi kwa maana ya Bodi ya ligi kuu (TPL Board) na Shirikisho la soka Tanzania, TFF wamekidhi matakwa ya kikanuni baada ya kufanikiwa kuweka hadharani ratiba septemba 20 mwaka huu ikiwa ni mwezi mmoja kabla ya michuano kuanza. 
Bodi ya ligi kuu Tanzania Bara (TPL Board) ndio wenye wajibu mkubwa wa kuratibu ligi kuu na ligi daraja la kwanza. 
Uchaguzi wa Bodi ya TPL ulifanyika Oktoba 25 mwaka jana. Oktoba 18 mwaka huo, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa wakati huo, Hamidu Mbwezeleni alitaja orodha ya mwisho ya wagombea waliokidhi vigezo katika uchaguzi huo. 
Nafasi ya Mwenyekiti alikuwa ni Hamad Yahya Juma (Mtibwa Sugar), Makamu Mwenyekiti ni Said Muhammad Said Abeid (Azam). Waliowania ujumbe wa Bodi ya Uendeshaji ni Kazimoto Miraji Muzo (Pamba) na Omary Khatibu Mwindadi (Mwadui). 
Baada ya uchaguzi kufanyika, Mbwezeleni aliwataja washindi ambapo Hamad Yahya Juma wa Mtibwa Sugar alishinda na kuwa mwenyekiti wa Bodi ya ligi kuu na Said Mohamed wa Azam fc alichaguliwa kuwa makamu mwenyekiti. 
Wagombea hao wawili wa nafasi mbili za juu walitangazwa kupata ushindi wa 100% ya kura zilizopigwa, lakini kwa mujibu wa Mbwezeleni baadhi ya wapiga kura katika uchaguzi huo waliondolewa kwasababu hawakukidhi vikezo.
Mwenyekiti huyo wa kamati ya uchaguzi aliwatangaza Kazimoto Miraji Muzo (Pamba) na Omary Khatibu Mwindadi (Mwadui fc).
Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi ya TFF, Hamid Mbwezeleni

Kwa mujibu wa Tangazo la uchaguzi wa Bodi ya Ligi lililotolewa Oktoba 14 mwaka 2013 zilitangazwa nafasi tatu kama zinavyoonekana hapo chini pamoja na masharti au sifa zinazotakiwa kuzingatiwa na waombaji:
1.          Nafasi zilizotangazwa kugombewa ni hizi zifuatazo:
(i)          Mwenyekiti  wa  TPL Board.
(ii)        Makamu Mwenyekiti wa TPL Board.
(iii)       Wajumbe wawakilishi wa Klabu za Ligi Daraja la Kwanza kwenye Kamati ya Uongozi ya TPL Board (TPL Board Management Committee), nafasi mbili (2).
2.          Mtu yeyote  anayeomba nafasi ya uongozi katika TPL Board lazima atimize masharti yafuatayo:
(i)          Awe Raia wa Tanzania
(ii)        Awe na kiwango cha elimu kisichopungua Kidato cha Nne na cheti cha kuhitimu elimu ya Sekondari.
(iii)       Awe na uzoefu wa uendeshaji wa Mpira wa Miguu uliothibitishwa wa angalau miaka mitano (5).
(iv)       Asiwe na hatia yoyote ya kosa la jinai na kuhukumiwa kifungo bila ya uchaguzi wa faini.
(v)         Awe na umri wa angalau miaka 21.
(vi)       Awe amewahi kuwa ama mchezaji Mpira wa Miguu, Kocha, Mwamuzi au kushiriki katika uendeshaji wa Mpira wa Miguu katika ngazi ya Mkoa au Ligi daraja la kwanza.
(vii)     Kwa nafasi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa TPL Board awe Mwenyekiti wa kati ya Klabu zilizoshika nafasi ya kwanza hadi ya sita kwenye Ligi Kuu kwa msimu uliopita (2012/13).
(viii)    Kwa nafasi za  Mjumbe mwakilishi wa Klabu za Ligi Daraja la Kwanza kwenye Kamati ya Uongozi ya TPL Board awe Mwenyekiti wa Klabu Daraja la Kwanza.

??????????
Mabingwa Azam fc walitoa kiongozi mmoja wa Bodi ya ligi kuu, Makamu mwenyekiti, Said Mohamed

Ukisoma  masharti yaliyotakiwa kuzingatiwa (namba vii) , inasema kwa nafasi ya mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa TPL Board, mgombea alitakiwa awe Mwenyekiti wa kati ya Klabu zilizoshika nafasi ya kwanza hadi ya sita kwenye Ligi Kuu kwa msimu wa mwaka juzi (2012/13). 
Kwa nafasi za Mjumbe mwakilishi wa Klabu za Ligi Daraja la Kwanza kwenye Kamati ya Uongozi ya TPL Board awe Mwenyekiti wa Klabu Daraja la Kwanza.
Hamad Yahya Juma (Mtibwa) na Said Mohamed  (Azam) walikidhi sharti hilo kwasababu msimu wa 2012/2013 timu zao zilikuwa katika nafasi sita za juu.
Kwa upande wa wajumbe, Kazimoto Miraji Muzo (Pamba) na Omary Khatibu Mwindadi (Mwadui fc), pia walifuzu kigezo hicho kwasababu timu zao zilikuwa ligi daraja la kwanza. 
Lakini katika msimu wa 2013/2014 kulitokea mabadiliko kwa timu zilizotoa viongozi hao.
Azam fc ilitwaa ubingwa kwa upande wa Ligi kuu wakati Mtibwa Sugar ilishika nafasi ya 7 katika Msimamo.
MSIMAMO WA LIGI KUU MWAKA JANA
Standings

Rnk

Team
MP
W
D
L
GF
GA
+/-
Pts


1

26
18
8
0
51
15
36
62


2

26
16
8
2
61
19
42
56


3

26
13
10
3
33
20
13
49


4

26
9
11
6
41
27
14
38


5

26
9
11
6
23
20
3
38


6

26
10
8
8
28
32
-4
38


7

26
7
10
9
30
31
-1
31


8

26
10
1
15
23
40
-17
31


9

26
6
11
9
16
20
-4
29


10

26
6
10
10
26
33
-7
28


11

26
6
8
12
18
35
-17
26


12

26
6
7
13
20
39
-19
25


13

26
3
10
13
19
37
-18
19


14

26
3
7
16
18
39
-21
16

Kwa kuzingatia msimamo huo, viongozi wa nafasi mbili za juu wa Bodi ya ligi kuu kwasasa wanatakiwa kutoka  klabu za Azam fc, Yanga, Mbeya City, Simba, Kagera Sugar na Ruvu Shooting.
Rais wa TFF, Jamal Emil Malinzi

Kwa kuzingatia sharti lilelile, Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi kuu, Hamad Yahya Juma (Mtibwa Sugar) amekosa sifa kwasababu timu yake msimu uliopita ilitoka nje ya timu sita za juu. Kwa upande wa Said Mohamed ameendelea kuwa na sifa ya kuiongoza bodi hiyo.
Kwa upande wa wajumbe, Pamba fc imeshuka daraja kutoka ligi daraja la kwanza, kwahiyo Kazimoto Miraji Muzo (Pamba) kwa mujibu wa masharti yaliyotangazwa amekosa sifa ya kuwa mjumbe.
Omary Khatibu Mwindadi (Mwadui fc), yeye anaendelea kuwa kiongozi halali kwasababu timu yake ipo ligi daraja la kwanza.
Kwa hiyo Bodi ya ligi kuu ina viongozi wawili ambao hawajakidhi masharti kwasababu ya timu zao kufanya vibaya msimu uliopita.
Tayari msimu mpya unatarajia kuanza septemba 20 na tayari Bodi ya ligi kuu imetangaza ratiba, lakini Mwenyekiti wa Bodi hiyo hatakiwi kuendelea kushika nafasi hiyo kwasababu timu yake haipo kwenye timu sita za juu.
Kwa maana hiyo ilitakiwa kabla ya ligi kuanza, ufanyike uchaguzi mwingine ili kuchagua viongozi wapya, au kama ni ngumu ungefanyika uchaguzi mdogo ili kuziba nafasi ya mwenyekiti ambaye hana sifa na mjumbe mmoja ambaye amekosa sifa kwa mujibu wa kanuni. 
Kitendo cha kuruhusu ligi ianze bila uchaguzi ina maana wanakiuka taratibu zilizowekwa.
Na kuzingatia masharti yaliyowekwa wakati wa uchuguzi, Bodi ya ligi haina mwenyekiti na inatakiwa uchaguzi ufanyike pamoja na kumpata mjumbe mmoja aliyepoteza sifa kutoka timu ya Pamba.
Hata wale wajumbe walioteuliwa na mwenyekiti wa Bodi kwa ajili ya kuingia kamati ya utendaji ya TFF hawana sifa.
Mwenyekiti wa Bodi anaingia moja kwa moja kwenye kamati ya utendaji kujadili mambo ya mpira, lakini inakuwaje aendelee kupata fursa hiyo wakati hana sifa?
Tatizo linabaki pale pale kuwa viongozi wanaoongoza mpira wa Bongo wana tabia ya kusahau mambo waliyojiwekea wenyewe.
Hamad Yahya alipoteza sifa, muda mfupi baada ya msimu kumalizika ilitakiwa mchakato wa uchaguzi uanze mapema ili apatikane mwenyekiti. 
Lakini ratiba imetoka na ligi inaelelekea kuanza  na kiongozi muhimu wa Bodi hana sifa. 
Ifike wakati tukubali kukaa katika misingi ya kanuni tuliyojiwekea, jambo lipo wazi na ukweli unafahamika, lakini kuna watu wachache wanavunga kama hawaoni hivi. 
Sidhani kama watu wote pale TFF wamesahau, lakini kutokana na mfumo wa kubebana kwa urafiki na masilahi binafsi, watu wasiokuwa na sifa wanaendelea kujadili na kuongoza mpira wa nchi hii. 

waliotembelea blog