Monday, August 10, 2015


www.bukobasports.comChelsea wamekubaliwa kumsaini Beki wa Ghana Baba Rahman.
Beki huyo mwenye Miaka 21 anaichezea Klabu ya Germany FC Augsburg na atagharimu Pauni Milioni 20 huku Pauni Milioni 14 zikilipwa kwanza na nyingine Pauni Milioni 6 zitalipwa akifikisha Mechi 100.
Baba Rahman amenunuliwa baada ya Chelsea kutonywa na Meneja wao wa zamani Avram Grant ambae sasa ni Kocha wa Timu ya Taifa ya Ghana.
Fulbeki huyo wa Kushoto analetwa kuziba pengo la Filipe Luis ambae ameuzwa kwa Atletico Madrid.


Kepteni wa Lazio ya Italy Lucas Biglia ameafika Mkataba wa Miaka Minne Klabu hiyo ya England.
Ripoti hizo, ambazo chanzo chake ni Wasambaza Habari wa France Le10sport.com, zimedai Kiungo huyo alishaafikiana maslahi yake binafsi na Man United na kilichobaki ni Klabu husika kukubaliana Ada ya Uhamisho.
Imedaiwa Man United imetoa Ofa ya Pauni Milioni 17 lakini Lazio wanataka Pauni Milioni 25 kwa Kiungo huyo mwenye Miaka 29.
Kuhusu Pedro, inasemekana Man United na Barcelona tayari wana makubaliano ila Barca wanataka Fowadi huyo abakie kwao hadi wamalize kucheza na Sevilla kwenye Fainali ya UEFA SUPER CUP itakayochezwa Jumanne huko Tbilisi, Georgia.
Klabu hizo mbili zimekubaliana Ada ya Uhamisho ya Pauni Milioni 18.1 ambayo itapanda kwa Pauni Milioni 4.2 kutokana na Bonasi mbalimbali za mafanikio ya Fowadi huyo.Ikiwa Pedro na Biglia watatua Old Trafford basi Wachezaji hao watafanya Man United iwe imepata Wapya 7 katika kipindi hiki kuelekea Msimu mpya kufuatia kusainiwa Memphis Depay, Matteo Darmian, Morgan Schneiderlin, Bastian Schweinsteiger na Sergio Romero.


www.bukobasports.comBao la tatu limefungwa kipindi cha pili dakika ya 59 na Vincent Kompany kwa kichwa baada ya kupigwa kona na David Silva. Picha hapo juu ni Fernandinho akimpongeza Yaya Toure baada ya kuipa bao tena. Ushindi huu mwepesi kwa City umewapandisha juu kileleni na kuanza msimu vyema na kwa kupata bao nyingi kuliko wengine walianza msimu rasmi tangu hapo jumamosi agosti 8. Mechi inayofuata kwa City ni huko kwao Etihad kuwakaribisha Mabingwa wa England Chelsea jumapili agosti 16.Yaya Toure akipongezwa baada ya kuipa City bao la piliYaya Touré dakika ya 9 anaipa bao la kuongoza Man City kwa kufanya 1-0 dhidi ya West Brom Albion. Bao la pili lilifungwa pia na huyo huyo Yaya Touré dakika ya 24 na mtanange kwenda mapumziko City ikiwa mbele ya bao 2-0 dhidi ya Wenyeji West Brom.VIKOSI:
West Brom wanaoanza 11:
Myhill, Chester, Dawson, Lescott, Brunt, Morrison, Gardner, Fletcher, McClean, Berahino, Lambert
WBA Akiba: Rose, Olsson, Yacob, McManaman, Sessegnon, Anichebe, Ideye
Manchester City wanaoanza 11: Hart, Sagna, Kompany, Mangala, Kolarov, Toure, Fernandinho, Navas, Silva, Sterling, Bony
Man City Akiba: Caballero, Zabaleta, Denayer, Demichelis, Nasri, Iheanacho, Aguero

MABINGWA wa zamani wa England, Manchester City wameanza vyema msimu mpya wa Ligi Kuu kwa ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya West Bromwich Albion usiku wa kuamkia leo.
Shujaa wa mechi alikuwa na kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast, Yaya Toure aliyefunga mabao mawili, lingine likifungwa na beki Mbelgiji, Vincent Kompany.
Mwanasoka bora Afrika, Yaya Toure alianza kuifungia Manchester City dakika ya tisa baada ya shuti lake la umbali wa mita 20 kumbambatiza Boaz Myhill na kutinga nyavuni, kabla ya kufunga la pili dakika ya 24.
Nahodha wa Man City, Vincent Kompany akakamilisha ushindi mnono katika mchezo wa kwanza wa timu yake kwa kufunga bao la tatu dakika ya kwa kichwa 59.  
Mchzeaji mpya, Raheem Sterling aliyesajiliwa kutoka Liverpool, alicheza vizuri katika kikosi cha City jana, lakini akapoteza nafasi nzuri na ya wazi ya kufunga.
Kikosi cha West Brom kilikuwa: Myhill, Chester, Dawson, Lescott, Brunt, Morrison, Gardner, Fletcher, McClean/Yacob dk46, Lambert/Anichebe dk73 na Berahino/McManaman dk79.
Man City; Hart, Sagna, Kompany, Mangala, Kolarov, Toure/Demichelis dk79, Fernandinho, Jesus Navas, Silva, Sterling/Nasri dk73 na Bony/Aguero dk62.

Yaya Toure akifumua shuti kuifungia Man City nbao la kwanza buku kiungo wa Baggies, James Morrison akijaribu bila mafanikio kuzuia
Manchester City captain Vincent Kompany celebrates putting his side into a 3-0 lead against West Brom on Monday night
Manchester City captain Vincent Kompany celebrates putting his side into a 3-0 lead against West Brom on Monday night

Yaya Toure fires City on their way and into a 1-0 lead as Baggies midfielder James Morrison fails to block the Ivorian's low drive 
City midfielder David Silva (third left) flicks the ball through the legs of West Brom's Craig Dawson as the visitors take a 1-0 lead
City midfielder David Silva (third left) flicks the ball through the legs of West Brom's Craig Dawson as the visitors take a 1-0 lead
Baggies goalkeeper Boaz Myhill looks on in desperation as the deflected shot trickles agonisingly over the line 
Baggies goalkeeper Boaz Myhill looks on in desperation as the deflected shot trickles agonisingly over the line 


TIMU ya Esperance ya Tunisia imefufua matumaini ya kusonga mbele Kombe la Shirikisho Afrika kufuatia ushindi wa bao 1-0 ugenini jana dhidi ya wenyeji Stade Malien mjini Bamako, Mali.
Shukran kwake, mfungaji wa bao hilo pekee, Mnigeria, Samuel Eduok huo ukiwa ushindi wa kwanza kwa ‘Damu na Dhahabu’ na kumaliza wimbi la kufungwa mechi tatu.
Mechi hiyo ya nne ya Kundi A, ililazimika kuchezwa siku mbili baada ya mchezo wa kwanza Jumapili jioni kuvunjika dakika ya 49 kufuatia mvua kubwa iliyonyesha na kuharibu eneo la kuchezea Uwanja wa Modibo Keita.
Na kwa mujibu wa sheria, mechi hiyo ikaendelea jana kuanzia pale iliposimamia kwenye Uwanja huo huo na Esperance wakaibuka na ushindi unaompa ahueni Mfaransa Jose Anigo sasa.
Zikiwa zimebaki mechi mbili kukamilisha hatua ya makundi, mabingwa hao mara mbili Afrika wana nafasi ya kwenda Nusu Fainali licha ya kuzidiwa pointi sita na vinara, Etoile du Sahel ya Tunisia pia. Mabingwa watetezi, Al Ahly ya Misri wapo nafasi ya pili wakiwa na pointi saba na Stade Malien ina pointi nne.

MSIMAMO WA MAKUNDI KOMBE LA SHIRIKISHO

Kundi A



PWDLGFGAGDPts
1ES Sahel (Tunisia)43013129
2Al Ahly (Misri)42114137
3Stade Malien (Mali)411223-14
4Esperance (Tunisia)410326-43

Kundi B



PWDLGFGAGDPts
1Orlando Pirates43015239
2Zamalek (Misri)43015239
3AC Leopards (Kongo)411224-24
4CS Sfaxien (Tunisia)401315-4

Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa kituo cha Redio cha EFM,  Denis Ssebo (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu  kuendelea kufanyika kwa Tamasha la Muziki Bar kwa Bar baada ya kumalizika kwa tamasha hilo kwa awamu ya kwanza. Kulia ni Mtangazaji, Dina Marios.
 Mtangazaji, Dina Marios akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu  kuendelea kufanyika kwa Tamasha la Muziki Bar kwa Bar baada ya kumalizika kwa tamasha hilo kwa awamu ya kwanza. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa kituo cha Redio cha EFM,  Denis Ssebo.
Waandishi wa habari wakimsikiliza Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa kituo cha Redio cha EFM,  Denis Ssebo katika mkutano uliofanyika makao makuu ya EFM-Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
BAADA ya kumalizika kwa Tamasha la musiku mnene Bar kwa bar awamu ya kwanza, na mashabiki kuomba Burudani hiyo iendelea tena, Uongozi Efm umekubali ombi hilo na sasa Tamasha hilo linarudi tena kwa kishindo likiwa  limeboreshwa kwakuongeza wigo wa kuwafikia watu wengi zaidi.
Muziki mnene bar kwa bar awamu hii bila kuwasahamu wasikilizaji na mashabiki wa EFM katika wilaya za Kinondoni, Temeke na Ilala kwa umuhimu wake na Wilaya mpya katika mkoa wa Dar es salaam, Muziki mnene sasa utapelekwa pia katika mkoa wa Pwani.
Maeneo ambayo wanatakiwa kukaa tayari  kwa Muziki mnene bar kwa bar utakaoporomoshwa  na Madjs wakali wa Efm, ni pamoja na Kibaha, Mlandizi, Mkuranga, Bagamoyo, Kisarawe,  Kigamboni na maeneo mengine mengi kwa ajili ya kuhakikisha tunakonga nyoyo za mashabiki wetu.
Muziki Mnene bar kwa bar mwaka huu inatarajiwa kuanza rasmi tarehe 5/09/2015 . Lakini katika kuelekea huko efm imeanza na Muziki mnene bango katika sehemu yako ya biashara ambako bwana E anapita na ukiwa umeweka bango la EFM na unasikiliza matangazo yetu basi utapata kifurushi chenye zawadi kibao.
Na kama ilivyokawaida yetu, mwishoni tutakuwa na Tamasha kubwa la hitimisho ambalo litafanyika jijini Dar es salaam ambalo safari hii limeboreshwa na kuongezwa vionjo vingi sana.
“Ninawaomba wasikilizaji wetu wakae mkao wa kula maana tutawafikia na kuwamiminia Burudani ambayo pia itarushwa live kutoka eneo husika kupitia kituo chao cha 93.7 EFM. Njoo tuonane, tufahamiane na tuijenge Radio yetu efm ambayo kwetu Muziki unaongea”.
LAKINI jambo la pili ambalo ndugu zangu wanahabari tungependa kuwajulisha ni kwamba katika kuhakikisha tunaendelea kukupa kilicho bora zaidi kupitia vipindi vyetu mbalimbali,sanjari na kuwa na watangazaji wenye ushawishi na uwezo mkubwa. leo hii tunamtambulisha kwenu mtangazaji Dina Marios ambaye wengi uwezo wake mnaujua na sasa ameungana na wenzake  wenye uwezo mkubwa katika familia ya Efm.
Mwisho niwashukuru sana kwa mwitikio wetu na kwakuwa tumeendelea kushirikiana mara nyingi hivyo naomba tuendelee kushirikiana hivi hivi.  Asanteni sana kwakunisikiliza.


dr

Daktari wa klabu ya Chelsea Eva Carneiro amewashukuru masabiki wa klabu hiyo ambao walichukua muda wao na kutuma ujumbe wa kumuunga mkono baada ya kocha wa klabu hiyo Jose Mourinho kumshutumu kufuatia tukio lililojitokeza kwneye mchezo wa kwanza wa ligi kuu ya England kwa mabingwa hao dhidi ya Swansea.
Huku matokeo yakienda kinyume na matarajio ya kocha huyo kwenye mchezo huo dhidi ya Swansea ambako Chelsea walibanwa na kutoka sare ya 2-2, Mourinho alimshutumu daktari wa timu baada ya kitendo cha kwenda kumtibu Eden Hazard wakiwa akiwa ameumia .
Daktari wa Chelsea akiwashukuru mashabiki walioonyesha kumuunga mkono.
Daktari wa Chelsea akiwashukuru mashabiki walioonyesha kumuunga mkono.
Mourinho alisema kuwa Daktari huyo alikosea kwa alichofanya kwani kwenda kumtibu kiungo Eden Hazard kuliifanya timu yake ibaki na wachezaji nane uwanjani hali ambayo iliwafanya wacheze kwa mazingira magumu .
Wakati kitendo hicho kinatokea Chelsea ilikuwa imebaki na wachezaji 9 uwanjani baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu kwa kipa Thibaut Courtois na daktari huyo kwenda kumtibu Hazard ambaye sheria zinalazimu mchezaji kutoka nje kabla ya kurudishwa uwanjani kwa ruhusa ya refa kuliifanya Chelsea kubaki na watu 8 tu kwa takribani dakika mbili.
Mourinho akionyesha kukerwa wakati wa mchezo kati ya Chelsea na Swansea.
Mourinho akionyesha kukerwa wakati wa mchezo kati ya Chelsea na Swansea.
Mourinho alimshutumu daktari huyo kwa kusema kuwa baadhi ya watu wanaokaa kwenye benchi la ufundi wanapaswa kuelewa jinsi ambavyo mchezo wa soka unakwenda huku akiongeza kuwa Hazard hakuwa ameumia alikuwa amechoka na alihitaji kuachwa na angenyanyuka mwenyewe.
Mourinho alikasirika baada ya daktari wa chelsea kwenda kumtibu Eden Hazard.
Mourinho alikasirika baada ya daktari wa chelsea kwenda kumtibu Eden Hazard.
Watu wengi wametafsiri tukio hili kama dharau toka kwa Mourinho na wamekuwa wakimtumia daktari huyo ujumbe wa kumuunga mkono ktiando ambacho kimemgusa daktari huyo ambaye amejijengea umaarufu mkubwa akiwa daktari pekee wa kike kwenye timu kubwa.
sergio-ramos-cruz-azul-real-madrid-fifa-world-club-cup-12162014_bz7pe05jv18h1haakqqlo63s6

Beki wa kati wa klabu ya Real Madrid Sergio Ramos anatarajia kusaini mkataba mpya na klabu yake mpaka kufikia alhmis ya wiki hii baada ya kufikia muafaka na uongozi wa klabu hiyo katika mazungumzo ambayo yamedumu kwa muda wa mwezi mzima.
Kusaini kwa mkataba mpya kwa beki huyu kunafikisha ukomo kwa tetesi kadhaa ambazo zilimhusisha na kuihama Real Madrid huku Manchester United ikitajwa kuwa timu ambayo ingemsajili.
Beki huyo ameteuliwa kuwa nahodha mpya wa Madrid baada ya kuondoka kwa Iker Casillas na kwa nyakati tofauti rais wa klabu Florentino Perez na kocha Rafa Benitez wamekuwa wakisisitiza umuhimu wa mchezaji huyo kwa timu hiyo na kuwa hatauzwa kwa bei yoyote ile.
Ramos alidaiwa kutoridhishwa na mshahara wa Euro milioni 6 kwa mwaka ambao amekuwa akiupata kiwango ambacho mwakilishi wake na kaka yake Rene Ramos amekuwa akisisitiza kuwa hakilingani na mchango wa beki huyo kwa Madrid katika miaka ambayo ameitumikia .


Leo Usiku Mabingwa wa zamani wa England Manchester City wanaingia Ugenini The Hawthorns kucheza na West Bromwich Albion katika Mechi yao ya kwanza kabisa ya Msimu mpya wa Ligi Kuu England.
Hii ni Mechi ya mwisho ya Raundi ya kwanza kwa Timu 20 za Ligi Kuu England ambazo zilianza mbio zao za Msimu mpya hapo Jumamosi na Jana Jumapili huku ikishuhudiwa Mabingwa Chelsea kutoka Sare 2 kwa 2 na Swansea City, Man United kuifunga Spurs 1-0 na Arsenal wakitandikwa kwao Emirates 2-0 na West Ham.Hali za Wachezaji
West Brom, chini ya Meneja Tony Pulis, huenda wakamkosa Beki wao ambae ni Mchezaji wa zamani wa Man City, Joleon Lescott, ambae ana maumivu lakini Wachezaji wao wapya, Rickie Lambert, James McClean na James Chester wapo tayari kucheza isipokuwa Serge Gnabry kutoka Arsenal ambae Uhamisho wake haukukamilika kwa wakati.
Manchester City, chini ya Meneja Manuel Pellegrini, itawakosa Gael Clichy na Fabian Delph wote wakiwa na maumivu lakini David Silva, Samir Nasri na Sergio Aguero, ambao walikuwa wagonjwa, wako fiti kuanza Mechi hii.

Uso kwa Uso
-Manchester City hawajafungwa na WBA katika Mechi zao 5 zilizopita Uwanjani The Hawthorns, wakishinda 4 kati ya hizo.
-City, wakicheza kwao Etihad na hapo The Hawthorns, wameifunga WBA mara 7 mfululizo.

Mike Dean refa atakayechezesha mpambano huo utakaopigwa usiku huu saa nne kamili kwa saa za hapa Tz.
Referee: Mike Dean Assistants: S Long, M Perry Fourth Official: M Clattenburg 
LIGI KUU ENGLAND
Jumatatu Agosti 10

22:00 West Brom v Man City
Ijumaa Agosti 14
22:45 Aston Villa v Man United
Jumamosi Agosti 15
14:45 Southampton v Everton
17:00 Sunderland v Norwich
17:00 Swansea v Newcastle
17:00 Tottenham v Stoke
17:00 Watford v West Brom
17:00 West Ham v Leicester


.Huku Wachambuzi wakimnyooshea kidole Kipa mpya wa Arsenal Petr Cech kwa kufanya makossa yaliyoruhusa Bao zote walipopigwa 2-0 Leo kwao Emirates na West Ham katika Mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu England kwa Msimu mpya, Meneja Arsene Wenger amekataa kumshushia lawama Kipa huyo.
Cech, alienunuliwa kutoka Chelsea, aliutokea Mpira wa Frikiki ili aupanchi lakini akaukosa na kutoa mwanya kwa Cheikhou Kouyate kufunga kilaini kwa Kichwa Bao la kwanza na kisha shuti la mbali la Mauro Zarate kumhadaa Cech kwenye Posti yake ya karibu na kutinga.

Lakini Wenger, akiongea mara baada ya kipigo hicho, ameeleza: “Ni kutokuwa makini kwa pamoja. Kuna vitu vingi hapo. Nilijua kama ile frikiki itapigwa vizuri basi tutakuwa mashakani kutokana na tulivyojipanga, tulijiua wenyewe. Sijaongea na Cech lakini sikuona Mchezaji mwingine yeyote akicheza kwa kufurahisha hii Leo hivyo ni ngumu kumlaumu mmoja.” 
Aliongeza: “Pasi zetu hazikuwa nzuri. Leo lazima tujitazame wenyewe. Hatukuwa wazuri.”
Mara baada ya Wikiendi iliyopita kuwafunga Mabingwa Chelsea Bao 1-0 huko Wembley na kutwaa Ngao ya Jamii, Wachambuzi wengi huko England waliipa nafasi kubwa Arsenal kuwemo rasmi kwenye kinyang’anyiro cha Ubingwa Msimu huu lakini kichapo hiki cha Leo kimeleta fikra nyingine.



Oxford alimkaba Mtu mzima Mesut Ozil wa Arsenal na aliyenunuliwa £42.5million leo jumapili kwenye Uwanja wa Emirates, West Ham wameshinda bao 2-0 dhidi ya Arsenal.
Chipukizi Reece Oxford wa West Ham ameweka rekodi kwa kuwa mchezaji mchanga zaidi wa saba na umri wa miaka 16.

Oxford alipumzishwa na Meneja mpya wa West Ham Slaven Bilic kipindi cha pili dakika ya 79.
Reece Oxford leo wakati anacheza na Wakongwe Arsenal
Leo ameweka Historia kwenye Uwanja wa Emirates alipoisaidia Timu yake West Ham kuifunga Arsenal Bao 2-0 katika Mechi ya kwanza ya Msimu mpya wa Ligi Kuu England kwa Timu hizo.
Reece anakuwa miongoni mwa Kijana mdogo kucheza Ligi Kuu England yeye akiwa na Miaka 16 na Siku 236 akiwa nyuma ya Mchezaji mdogo kabisa, Matthew Briggs, ambae alicheza Mechi yake ya kwanza kwa Klabu yake Fulham ilipofungwa 3-1 na Middlesbrough Mei 2007.
Siku hiyo, Briggs alikuwa na Umri wa Miaka 16 na Siku 65.
Oxford Reece alianzia Soka lake hapo hapo West Ham na Leo Meneja mpya Slaven Bilic alimpa nafasi ya kuanza Mechi hii ya Ligi dhidi ya Arsenal akicheza kama Kiungo Mkabaji mbele ya Difensi yake ya Mtu 4 akimudu kuwakalisha Mastaa kina Santi Cazorla, Mesut Ozil na Olivier Giroud.

Reece alicheza Mechi hiyo kwa Dakika 79 hadi alipobadilishwa na kuingizwa Mkongwe Kevin Nolan ambae ni mkubwa wake kwa Miaka 17.
Kinda huyo, mwenye Urefu wa Futi 6 na Inchi 3, kama ingekuwa Afrika bila shaka Watu wangetilia wasiwasi umri wake lakini Meneja wake, Bilic, ameeleza: “Kama Messi angekuwa mbele yangu ningekuwa na mchecheto lakini si yeye.”
Bilic aliongeza: “Watu wananiuliza: ‘Una hakika ana Miaka 16?’ Ni hatari kumchezesha lakini niliamini ana uwezo. Nasikia fahari kwake. Kwenye Karatasi tu ndio ana Miaka 16. Huyu ni sehemu ya kizazi hiki kipya!”
Nae Mchezaji mwingine mzoefu wa West Ham, Winston Reid, amesema: “Ni Kijana mdogo wa Miaka 16 lakini ana umbo kubwa kupita mie! Pengine ana uwezo Zaidi kupita mie!”
Hata Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, ameungama kuwa Reece Oxford ni Kijana Jembe.



James Milner, Martin Skrtel, Emre Can na Roberto Firmino wakifurahia bao la Philippe Coutinho kwenye dakika za mwishoni kwenye Uwanja wa Stoke City Britannia Stadium1-0 full time!
Akiachia shuti kali lililozama moja kwa moja langoni

Jordan Henderson akipagawa baada ya kukosa nafasi ya wazi kufunga bao

Mchezaji wa Stoke  Glen Johnson akituliza kiuzuri mpira mbele ya Meneja wa Liverppool Brendan Rodgers

Mchezaji mpya wa Liverpool, Milner, akioneshwa kadi ya njano na refa Anthony Taylor kwa kumfanyia rafu mbaya Charlie Adam

Henderson chini akijiuguza baada ya kufanyiwa ndivyo sivyo!

Joe Gomez  dhidi ya Straika  Jonathan Walters kwenye Uwanja wa  Britannia ambapo Liverpool walishinda bao lao na kujinyakulia pointi 3 muhimu dakika ya 86.

Martin Skrtel na  Simon Mignolet wakichuana vikaliBrendan Rodgers akijionea wapya aliosajili msimu huu.
Philippe Coutinho dakika ya 86 aliipa bao la ushindi na kuibuka na pointi 3 muhimu leo kwenye ufunguzi msimu mpya ulioanza rasmi jana Benteke akiendesha mpira...kipindi cha kwanza.



Full time, Arsenal 0 vs 2 West Ham United
Meneja mpya Slaven Bilic ameanza Ligi Kuu England kwa kuiongoza Timu yake West Ham kuitandika Arsenal 2-0 kwenye Dabi ya Jiji la London huko Emirates na kumfanya Meneja wa Arsenal Arsene Wenger kutoamini kilichomkuta na kubaki kushika kichwa, West Ham, ambao walimchezesha Kijana wa Miaka 16 Reece Oxford, walifunga Bao lao la kwanza baada ya Kipa wa Arsenal Petr Cech kuitokea Frikiki na kuikosa na kumruhusu Cheikhou Kouyate kufunga kwa kichwa katika Dakika ya 43.
Nafasi pekee waliyokaribia Arsenal kufunga katika Kipindi cha Kwanza ni pale Aaron Ramsey alipopiga Posti.

Zarate dakika ya 57 aliwachapa bao la pili Arsenal na kuipa bao la pili West Ham dhidi ya Wenyeji wao Arsenal kwenye Uwanja wa Emirates na kufanya Gunners wachanganyikiwe na kumuingiza Alexis Sanchez ili awaokoe lakini mambo yakaenda kombo.Bao la West Ham lilifungwa kipindi cha kwanza dakika ya 43 kupitia kwa Cheikhou Kouyaté alipolifunga kwa kichwa kupitia mpira wa adhabu uliopigwa na Dimitri Payet na kisha Cheikhou Kouyaté kuunganisha vyema hadi langoni mwa Arsenal.Santi Cazorla akilindwa na msitu wa West Ham United katika kipindi cha kwanza.

waliotembelea blog