Wednesday, July 24, 2013

sintaSIKU chache baada ya msanii wa filamu na muziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, kutishia kumpa kisago msanii mwenzake ambaye pia ni mtangazaji, Christina John ‘Sinta’, mtangazaji huyo amefunguka na kumtaka aache mambo ya kizamani.
Shilole, majuzi kupitia mitandao ya kijamii, aliandika kukerwa na Sinta kwa kumbeza kuwa hawezi kuimba na mwanamuziki maarufu wa Marekani J. Lo na kuwa hizo ni ndoto za mchana, hivyo anamsaka na popote wakikutana atampa kipigo cha mbwa mwizi.
Akizungumza kwa simu na mtandao wa Gumzo la Jiji, Sinta alisema amekuwa akiambiwa na watu hasa wanaofuatilia mitandao kuwa eti anatafutwa kupigwa na Shilole, jambo linalomshangaza, kwani msanii huyo anapajua nyumbani kwake.
“Ninachoshangaa…huyo Shilole anapafahamu kwangu, aje basi anipige au ofisini kwangu anapajua, namkaribisha vizuri sana jamani!” alisema Sinta na kuongeza: “Mimi huwa sio mtu wa maneno, yeye aje tu anipige na sio kutangaza kwenye mitandao kuwa ananitafuta anipige, hayo mambo ya bifu siku hizi watu wanayachukulia upuuzi.
“Kutafuta pesa ndio mpango mzima, hivyo mimi namshauri Shilole kama ‘underground’ wa sanaa nchini, aachane na bifu, badala yake akazane kwenye mambo yake ya kutafuta pesa kwa ajili ya maisha yake na familia, kwani uzee unakuja.”
Chanzo cha ugomvi huo ulitokana na Sinta kuandika habari kwenye mtandao wake kuwa Shilole hawezi kuimba na Jennifer Lopez wa Marekani, bora hata Linah wa THT, kwa hiyo Shilole aache kuidanganya jamii.
Aidha mashabiki mbalimbali hasa wasomaji wa kwenye mitandao, wamemuunga mkono Sinta kuhusu kauli yake.
“Ni kweli jamani, Shilole hawezi kuimba na Jennifer Lopez, hayo ni masihara jamani, kwenda Marekani ndio aje kuongea ulojo kiasi hicho; kwanza ikumbukwe kuwa wasanii wote wa Tanzania kule Marekani hawajulikani hata, hasa kwa sisi tunaofuatilia tunajua,” alisema shabiki aliyejitambulishia kwa jina la Hamu Juma.
Dereva wa gari la JWTZ lililopata ajali katika eneo la Mwanakwerekwe wakati wa wakielekea kwenye mazishi ya wanajeshi wawili wa Zanzibar waliofari Darfur akishushwa kwenye gari katika hospitali ya Mnazi mmoja kwa ajili ya kupatiwa matibabu.Wanajeshi wakimshusha majeruhi wa ajali ya gari ya JWTZ iliotokea Mwanakwerekwe , katika hospitali ya Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar. (Picha na Makame Mshenga Maelezo Zanzibar).

STAA wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ ameingia matatani akidaiwa kuingia mitini na simu tatu za mkononi alizoaminiwa nchini Afrika ya Kusini alikokwenda kufanya shoo.


Msanii huyo alikumbwa na kasheshe hilo Julai 19, 2013 nyumbani kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sinza Mori, Dar.
Siku hiyo Diamond alikuwa akifuturisha na aliwaalika watu mbalimbali wakiwemo mastaa lakini nusura futuru iingie doa kufuatia zogo hilo.
Mfano wa aina ya simu anazo daiwa kuiba Shilole

ISHU ILIKUWAJE?
Ndugu wa Diamond aitwaye Majaliwa Majuto ‘Q Boy’ alidai ndiye mwenye simu hizo. Alisema miezi kadhaa iliyopita, Shilole alikwenda nchini humo kufanya shoo ya muziki. Wakati wa kuondoka alimpa simu tatu, Ipad, Samsung Galaxy na Blackberry ili akifika Bongo ampe Diamond lakini msanii huyo hakufanya hivyo.
 

“Alikuja Sauzi kufanya shoo, wakati wa kuondoka nilimpa simu tatu amletee Diamond lakini nashangaa hakufanya hivyo na mimi tangu nirudi Bongo simpati, kila nikimpigia simu hapokei, leo ndiyo tumekutana hapa kwa Diamond,” alilalama Q Boy.
DIAMOND ALIAMBIWA SIMU ANAZO SHILOLE
Alisema awali akiwa nchini humo baada ya kumkabidhi mali hizo, alimpigia simu Diamond na kumtaarifu kuwa ‘mzigo’ anao Shilole, akashangaa staa huyo kujibu kwamba hajazipata wala hajamwona Shilole.

SHILOLE AJITETEA
Katikati ya mzozo huo, Shilole alijitetea kwa kusema: Mi namdai rafiki yake fedha yangu ya shoo iliyobaki, kama shilingi laki nane hivi ndiyo maana nikaamua kuzizuia simu za huyu (Q Boy) hadi nimaliziwe pesa yangu.
Hata hivyo, katika sakata hilo ilielezwa kuwa Shilole na Q Boy hawakuwa na makubaliano yoyote kuhusu shoo hiyo na simu hizo hivyo madai ya mwigizaji huyo ni ‘usanii’ tu.

MAMA DIAMOND AINGILIA KATI KUOKOA
Zogo hilo lilipopamba moto na kuashiria kuvurugika kwa amani, mama mzazi wa Diamond, Sanura Kasim ‘Sandra’ aliamua kuingilia kati na kuagiza suala la kudaiana simu lifanyike kesho yake (Jumamosi) kwa vile siku hiyo haikuwa muafaka.
“Jamani! Jamani! We nani, Shilole na we Majaliwa, naomba kwa leo muepusheni shetani kwani hapa si mahali pake, ila kesho tutaitana na kumaliza suala hili, mimi mwenyewe nitalisimamia,” alisema bi mkubwa huyo na kumaliza henyahenya iliyoibuka.

JUMAMOSI YAFIKA, KIKAO VIPI?
Jumamosi, mapaparazi wetu walifuatilia ishu hiyo nyumbani kwa akina Diamond na kuulizia ili kujua kama kikao cha usuluhishi kilifanyika kama mama Nasibu alivyoagiza.
“Mh! Sijaona kikao chochote, kwanza Shilole mwenyewe akipigiwa simu hapokei,” alisema ndugu mmoja wa Diamond huku akiomba hifadhi ya jina lake.

MSIKIE DIAMOND
Juzi, Diamond alipopigiwa simu na kuulizwa kama anaijua ishu ya simu, alikubali.
Staa huyo alisema anashindwa kuingilia kati sakata hilo kwa sababu wahusika wote ni watu wake wa karibu kikazi.
“Yeah! Ishu ni kweli ipo, lakini mimi nilijiweka kando mapema, nikamwambia dogo (Q Boy) afuatilie mwenyewe baada ya kuona Shilole haeleweki.
“Unajua Shilole ni mwanamuziki mwenzangu, dogo yupo ndani ya Kampuni ya Wasafi Entertainment (ya Diamond), sasa kukomaa na ishu za simu tu nahisi itanishushia hadhi, napiga shoo za hela nyingi halafu leo nakomaa kwa hela ndogo, inakuwa siyo,” alisema Diamond.

SHILOLE TENA
Baada ya kuzungumza na Diamond, Shilole alipigiwa simu na kuomba kufafanua kwa undani ishu hiyo ambapo katika hali isiyotarajiwa, alimlalamikia paparazi wetu akidai anapendelea katika sakata hilo.
“Nyiye mnamtetea tu yule dogo, mimi sina tatizo, kama rafiki yake (aliyemuitia shoo Afrika Kusini) akinilipa hela yangu nawapa simu zao,” alisema Shilole.
Msanii huyo alikwenda mbele zaidi kwa kumwambia paparazi kuwa atatia timu kwenye Ofisi za Global Publishers ili kuzungumzia suala hilo na viongozi.
Baadaye Shilole alifika ofisini kwetu na kufafanua juu ya sakata hilo ambapo alirudia kukiri kuzuia simu hizo akidai kwamba anamdai Q Boy hivyo mpaka atakapomlipa ndiyo atampa simu zake.

Q BOY NAYE TENA
Kwa upande wake, Q Boy alipozungumza na paparazi wetu siku hiyo alisema amekusudia kwenda kufungua kesi kituoni ili apewe msaada zaidi wa kisheria kwa vile simu hizo zinamuuma hasa ukizingatia kuwa yeye siye aliyempeleka Shilole Afrika Kusini kufanya shoo.
“Mimi leo (Jumatatu) nimebanwa sana, kuna sehemu nakwenda na Diamond, nadhani nitamaliza jioni. Lakini kesho (Jumanne) nitaamkia polisi kufungua kesi nione watanisaidiaje?” alisema Q Boy.

POLISI AGUSIA ISHU
Risasi Mchanganyiko lilizungumza na askari mmoja kutoka Kituo cha Polisi cha Oysterbay na kummegea mtiririko wote, kisha kumuuliza kama kuna kesi ambapo alijibu:
“Japokuwa mimi si msemaji wa jeshi (la polisi), lakini ishu kama hiyo shitaka lake lipo, ni wizi wa kuaminiwa. Unajua wengi wanadhani kuibiwa lazima mtu uwe hujui, lakini mtu akifanya kama hivyo alivyofanya huyo msanii nani sijui (Shilole), kama ni kweli, kosa linakuwa wizi wa kuaminiwa endapo atafikishwa polisi.”

DIAMOND, Q BOY WALIFANYA MCHEZO?
Hata hivyo, baadhi ya watu walioshuhudia sakata hilo walikuwa na maswali kibao yaliyokosa majibu.
Swali la kwanza: Shilole alikwenda kufuturu kwa mwaliko wa Diamond na alijua staa huyo na Q Boy ni wamoja na simu alizopewa ilikuwa amletee msanii huyo, kwa nini alikwenda huku akijua ana msala?
Swali la pili: Kama Shilole alikwenda akijua Q Boy hayupo Bongo, je! Si kwamba ulikuwa mpango wa wawili hao kumwita ili wampe kibano ateme simu zao?
Swali la tatu: Je, ni kweli Shilole alizuia simu ili amaliziwe deni lake kwa mtu aliyemuitia shoo Afrika Kusini au shetani alimwingia baada ya kutua Bongo na kuamua kuzitumia hasa ikizingatiwa kuwa siku hizi mambo ya Instagram ndiyo habari ya mjini?


 


KIVAZI cha ndugu wa maharusi, kimesababisha patashika katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Peter, baada ya Paroko Msaidizi wa Kanisa hilo, Padri Paulo Haule, kusitisha ibada mpaka mhusika atoke akavae vizuri. 
“Ninatoa dakika 10 kwa aliyeingia na mavazi ambayo hayatakiwi kanisani humu kutoka mara moja akavae vizuri, la sivyo ndoa yao haitafungwa,” alisema Padri Haule wa Kanisa hilo lililoko Oysterbay, Dar es Salaam. 
Awali vurugu hizo zilizotokea Jumamosi iliyopita, zilianzia nje, wakati Katekista wa Parokia hiyo, Yohane Maboko, alipotangazia wanandoa na ndugu zao waliokuwa mabega wazi au kuvaa nguo fupi, kutafuta nguo za kujifunika au wasiingie kabisa kanisani. 
Maharusi walikubali kutekeleza ombi hilo, wakavishwa vitambaa mabegani vya rangi tofauti na gauni jeupe la harusi, wakaruhusiwa kuingia kanisani, tayari kufunga pingu zao za maisha. 
Hata hivyo, mmoja wa ndugu wa maharusi hao ambaye jina lake halikupatikana mara moja, alipotaka kulazimisha kuingia na kivazi chake cha mabega wazi, alizuiwa na Katekista Maboko. Katekista huyo alimfuata mwanamke huyo ili kumrudisha akavae vizuri, lakini aliibua zogo na kulazimisha kuingia na vazi hilo. 
Zogo hilo lilipoendelea, wanandugu waliingilia kati, wakitetea vazi hilo ambapo mmoja wa wanandugu, alimvua miwani Katekista Maboko na kuipiga chini ikavunjika huku yeye na wenzake wakimtolea maneno makali ya kumtaka asimzuie ndugu yao kuingia kanisani.  

Wakati ndugu hao wakimdhibiti Katekista Maboko, mwanamke huyo alitumia mwanya huo na kupenya hadi ndani ya Kanisa, ambamo Padri Haule, alikuwa akijiandaa kuanza ibada. 
Baada ya Padri Haule kupata taarifa, alitangaza kuwa ndoa ya maharusi wa msichana huyo, haitafungwa hadi awe ametoka.  
Licha ya Paroko kutangaza hivyo, bado ukaidi uliendelea jambo lililomfanya Katekista Maboko kumfuata tena dada huyo na kumwamuru atoke nje, ambapo aliendelea kupinga na baadaye akatekeleza amri hiyo ya Paroko. 
 Baada ya hapo shughuli za kufungisha ndoa ziliendelea kwa amani na utulivu hadi mwisho maharusi wakatoka kwenda kuendelea na mambo mengine.
 
Akizungumza na mwandishi wetu, Katekista Maboko alisema waumini hao walikiuka maadili ambayo Kanisa lina wajibu wa kulinda na kuyasimamia ili waumini wake wayafuate.  

Alisema miwani yake iliyovunjwa ilikuwa na thamani ya Sh 90,000 na baada ya ibada hiyo, aliyetenda kosa hilo alimwendea na kumwomba radhi na kulipa Sh 50,000 na kuahidi kumalizia kiasi kilichobaki wakati wowote. 
Maboko alisema uvaaji wa mavazi yasiyotakiwa kanisani hapo, umekuwa ukipigiwa kelele mara kwa mara, na hata katika mafundisho ya ndoa huambiwa lakini ukaidi unaendelea. 

“Maharusi wakati wa mafundisho ya ndoa tunawaambia kuhusu mavazi yao na hata ya ndugu zao watakaowasindikiza kanisani, kuwa wavae kistaarabu lakini hawasikii,” alisema Katekista Maboko. 

Makanisa mengi siku hizi yamekuwa yakipiga marufuku uvaaji wa nguo fupi na zinazoacha mabega wazi kwa wasichana na wanawake, wakati wa ibada za kawaida na za ndoa.

Hii ilikuwa siku ya jana baada ya kupata futari na ndugu,jamaa 
na marafiki na watu wasiojiweza
Presenter wa kipindi cha Take One Zamaradi ambae nae alikuwa 
mmoja wa wageni waalikwa aliamua 
kubadilisha mazingira na kuamua kunifanyia Interview mimi
 pamoja na familia yangu
juu ya mfungo huu wa ramadhani na Jinsi tunavyokabiria na mambo
 mbalimbali ya kidunia ndani ya mwezi huu...

Aliweza pia kuongea na Mama yangu mzazi Bi Sandrah,Cuzin
 Brother Rommy Jones,Dada zangu Esmah & Darlenee .....
Kuzungumzia mambo ya ndani ya kifamilia na n.k

Unaweza ukacheki picha kadhaa za nyuma ya pazia za Interview hiyo ya Take one special
ndani ya mwezi wa ramadhani iliyofanyika nyumbani kwangu sinza,bila kusahau
utaona kabisa kipindi kizima ndani ya TAKE ONE kwenye luninga yako kupitia
Channel ya CLOUDS TV...kila Jumanne saa 9:30 usiku...USIKOSEEEE..!!


Kuanzia ndani shuguli nzima ilianzia.....
Zamaradi akitangaza nje ya Nyumba .....
Nikiwakaribisha wageni wangu toka Take one na crew nzima ya Clouds Tv...
Mahojiano yalianzia nje na Zamaradi....




Baada ya kufturisha mimi na familia yangu kwa ujumla tuliweza kukaa chini na kufanya mahojiano na
zamaradi mketema......

Rommy Jones akizungumza jambo .....

Mama yangu alishindwa kuzungumza lolote kwa wakati ule......

Nikizungumza kwa Niaba ya Familia.....

Aunt Tahiya mtoto wa dada yangu akisoma Dua 
kutufungia zoezi zima la mahojiano na
Zamaradi...

Asante mungu kwa siku ya leo...........

waliotembelea blog