Tuesday, June 3, 2014


Kikosi cha timu ya soka ya Panone fc ya Mkoani Kilimanjaro.
Wachezaji wa timu ya Panone fc ya mkoani Kilimanjaro wakishangilia baada ya kuifunga tmu ya Town Small Boys na kufanikiwa kutinga ligi daraja la kwanza.

Nderemo na shangwe

Furaha ya kutinga daraja la kwanza

Sapota wa Panone fc mkoani Mbeya wakishangilia mara baada ya timu hiyo kutinga ligi daraja la kwanza.

Mmoja wa wajumbe wa kamati ya ushindi ya Panone fc Shabani Machivya akishangilia mara baada ya timu yake kufanikiwa kutinga ligi daraja la kwanza.



Mashabiki wa timu ya soka ya Panone fc mkoani Mbeya wakishangilia baada ya timu hiyo kufanikiwa kutinga ligi daraja la kwanza.

Na Dixon Busagaga wa Globu
ya Jamii Kanda ya Kaskazini.


Heartbreak: Colombian striker Radamel Falcao will miss the World Cup in BrazilStraika hatari Radamel Falcao ameachwa kwenye Kikosi cha Wachezaji 23 kitakachocheza Fainali za Kombe la Dunia.
Falcao, anaechezea Klabu ya Monaco huko France, ndie alikuwa Mfungaji Bora wa Colombia akiwa na Bao 9 kwenye Mechi za Kundi la Marekani ya Kusini kwa ajili ya kufuzu Fainali za Kombe la Dunia walipomaliza Nafasi ya Pili nyuma ya Argentina na yeye kuwa nyuma tu ya Wafungaji Bora wa Kundi hilo, Luis Suarez na Lionel Messi.
Breaking the news: Falcao with manager Jose Pekerman at a press conference
Ingawa Falcao alikuwemo kwenye Kikosi cha Awali cha Wachezaji 30 ikiwa ni mara ya kwanza kwake kurudi Uwanjani tangu Januari alipofanyiwa operesheni ya Goti, alishindwa kuonyesha kama yuko fiti na atakuwa tayari kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia.
Staying behind: Amaranto Perea (left), Luis Muriel (second left) and Falcao (right) were all left out
Huko Brazil, Colombia wapo KUNDI C pamoja na Greece, Ivory Coast na Japan.

Kocha wa Colombia Pekerman akielezea kuhusu kikosi kinachoenda kushiriki kombe la Dunia Brazil 2014 huko Buenos Aires.Graphic: Colombia's final 23-man squad for Brazil. This image was posted by Seleccion Colombia on Twitter
COLOMBIA-KIKOSI KAMILI
Makipa: David Ospina (Nice), Faryd Mondragon (Deportivo Cali), Camilo Vargas (Independiente Santa Fe).
Mabeki: Camilo Zuniga (Napoli), Pablo Armero (West Ham), Cristian Zapata (Milan), Mario Yepes (Atalanta), Carlos Valdes (San Lorenzo), Santiago Arias (PSV), Eder Alvarez Balanta (River Plate).

Viungo: James Rodriguez (Monaco), Abel Aguilar (Toulouse), Carlos Sanchez (Elche), Fredy Guarin (Inter Milan), Juan Fernando Quintero (Porto), Aldo Ramirez (Morelia), Alex Mejia (Atleico Nacional), Victor Ibarbo (Cagliari), Juan Guillermo Cuadrado (Fiorentina).
Mafowadi: Jackson Martinez (Porto), Teofilo Gutierrez (River Plate), Carlos Bacca (Sevilla), Adrian Ramos (Borussia Dortmund).


Rais wa TFF, Jamal Malinzi
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha Mwakilishi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mara (FAM) katika Mkutano Mkuu wa TFF, William Chibura kilichotokea leo asubuhi (Juni 3 mwaka huu) katika Hospitali ya Mkoa wa Mara mjini Musoma.

Chibura aliyezaliwa mwaka 1969 alikuwa mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF akiwakilisha klabu za Mkoa wa Mara kupitia FAM. Aliwahi kuichezea Musoma Shooting, na baadaye kuwa kiongozi katika klabu hiyo na ile ya Polisi Mara iliyoko Ligi Daraja la Kwanza (FDL)
Hadi mauti yanamkuta alikuwa kiongozi wa Butiama FC, na mwakilishi wa klabu Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Butiama (MUFA) kwenye Mkutano Mkuu wa FAM.

Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu nchini kwani, Chibura enzi za uhai wake alitoa mchango mkubwa katika mchezo huu tangu akiwa mchezaji na baadaye kiongozi.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Chibura, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mara (FAM), Jeshi la Polisi Tanzania na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa na familia yake kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Tanzania- Mkoa wa Mara, kwani marehemu Chibura alikuwa mtumishi wa jeshi hilo. TFF tunasubiri taratibu hizo ili tujipange jinsi ya kushiriki katika msiba huo.
Bwana alitoa, na Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe. Amina
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

NA Mwandishi Wetu,Tanga.
Wasanii nguli wa mziki wa Bongo Fleva na Filamu ambao ni wazawa wa mkoa wa Tanga wanatarajiwa kushiriki kwenye Tamasha ya kuuchangia mfuko wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga ambayo inajiandaa na Ligi Kuu msimu ujao.
Tamasha hilo litafanyika mapema mwezi Agosti mwaka huu baada ya kumalizika mwezi wa ramadhani na kabla ya ligi kuu Tanzania bara haijaanza.

Akizungumza jana Mratibu wa Tamasha hilo,Salim Bawaziri alisema lengo kuu lake ni kutaka kuwakutanisha wadau mbalimbali ikiwemo wana michezo,wasanii,wafanyabiashara na wabunge wa mkoa wa Tanga ili kuweza kuisapoti timu hiyo kwa ajili ya harakati zake za ligi kuu.
Bawaziri alisema asilimia kubwa ya kuelekea maandalizi yake yanaendelea vema ambapo mazungumzo yanaendelea baina ya wasanii watakaotumbuiza siku hiyo wakiwemo Waziri Njenje na Hamisi Mwinyuma “Mwana FA” na wengine wengi.
Aliwataja wasanii ambao wanatarajiwa kutoa burudani siku hiyo kuwa ni Matonya,Tanga Clan,Parklane,Wagosi wa Kaya,TNG Squard,Abubakari Katwila Q.Chief,Rashid Makwiro “Chid Benzi”Nassoro Hamisi “Best Naso”
Ibrahimu Mussa “Roma Mkatoliki” wakiwemo King Majuto ,Rose Ndauka na Tito na wengine wengi.

Mratibu huyo alisema katika kuhakikisha suala hilo linapata mafanikio aliwashirikisha wadau wengine kwa ajili ya maandalizi hayo wakiwemo Mohamed Bawaziri na kiongozi mmoja wa ngazi za juu serikali ambaye
hakupenda kuliweka jina lake bayana.

Alisema katika tamasha hilo wanatarajia kumualika Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete kuwa mgeni rasmi lengo likiwa ni kuhakikisha mfuko wa Coastal Union unakuwa na
mafanikio.

Aidha alieleza kwa kuwashirikisha wasanii hao pamoja na watu maarufu waliopo nje na ndani ya Tanga kushiriki kwenye tamasha hilo ili kuchangia misaada mbalimbali.


Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Tanzania Silas Mwakibinga akiwaonesha waandishi wa habari uthibitisho wa malipo ya shilingi milioni 400 ikiwa ni sehemu ya pili ya malipo kwa ajili ya Ligi Kuu.


Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Azam Media Rhys Torrington (kulia) akimkabidhi Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Tanzania Silas Mwakibinga nakala ya uthibitisho wa malipo ya fedha kwa ajili ya Ligi Kuu ya Vodacom.

KAMPUNI ya Azam Media imetangaza kuwa tayari imeshatuma fedha kwa Bodi ya Ligi kwa ajili ya msimu wa ligi wa Vodacom kwa mwaka 2014/ 2015.
Fedha hizo zimetolewa mapema zaidi kwa ajili ya kusaidia maandalizi mapema kwa timu kama ilivyokubaliwa kwenye mkataba wa miaka mitatu ya udhamini wao katika ligi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Azam zilizopo Tazara, Dar es salaam, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Rhys Torrington, alisema kuwa kampuni hiyo inavutiwa na aina nzuri ya ushirikiano kati yake na bodi ya Ligi.
Alisema kuwa kupitia bodi hiyo Azam imepiga hatua kubwa katika kufanikisha adhma yake ya kuifanya Ligi hiyo ya Vodacom kuwa ya kuvutia zaidi.
“Ligi hii tunataka kuifanya kuwa ni moja kati ya ligi zinazovutia na kuonesha ushindani barani Afrika, ingawaje ninajua kuwa kuna mengi ambayo yanatakiwa kuendelea kufanywa ili kuipa nguvu zaidi ligi hii”alisema Torrington. Alisema kuwa kwa kutambua hilo ndio maana Azam Media imehakikisha kuwa klabu zote zinapata fedha mapema ili kusaidia suala zima la maandalizi.

Akizungumzia mikakati ya baadae ya Azam Media alisema kuwa inatarajia kuanza kuonesha soka la mitaani (street soccer) mbalimbali moja kwa moja (live) itakayokuwa ikiendelea kwenye nchi za Kenya na Uganda.

Alisema kuwa kwa sasa Azam Media imeanza kujikita katika nchi za Kenya, Uganda na Malawi ambapo itakuwa ikiuza ving’amuzi vyake katika nchi hizo. Aliongeza kuwa pia katika kuhakikisha kuwa inatoa mwanya zaidi wa vipindi vizuri na vya kuvutia inaendelea na vipindi vya michezo vya Morning Trumpet, sport@8 pamoja na Kwetu House.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya ligi, Mr Silas Mwakibinga alisema kuwa kwa hatua hiyo ya Azam ya kuhakikisha upatikanaji wa fedha hizo kwa wakati ni nzuri na itasaidia kuzipatia timu muda mzuri wa kujiandaa. Alisema kuwa bodi yake inavutiwa sio tu na utangazaji wa vipindi unaofanywa na Azam bali pia hata nia yao ya kuendeleza soka la Tanzania.

Azam Media ilisaini mkataba wa miaka mitatu na wenye thamani ya TSHS5,560,800,000 kuonesha mechi za live na za kurekodi mechi za Ligi Kuu na fedha hizo zinalipwa kwa awamu tatu.

Fainali za Kombe la Dunia ni uwanja mpana. Ni mahali ambapo vipaji na vipaji vya wanasoka duniani huonekana. Madalali wa kuvumbua na kununua wachezaji [scouts] hufurika kwenye mashindano kama haya wakijua wazi kabisa kwamba pale ndipo watakapoona “lulu” kwa ajili ya vilabu vyao. Kwa maana hiyo kuna kila aina ya harakati za kimichezo na kuonyesha na kuonyeshana vipaji. Hii sio kumaanisha kwamba wachezaji wote mahiri hapa duniani walicheza katika fainali za Kombe la Dunia.La. Wapo wasakata kabumbu kadhaa ambao hawakuwahi kugusa fainali hizi.Mfano ni George Opong Weah na watu kama kina George West nk.

Lakini wakati wengine wakionyesha vipaji ili wang’amuliwe na kubadilisha maisha yao ya kisoka,wapo wale ambao wanashuka dimbani tayari wakiwa na majina [superstars] na ambao dunia tayari inakuwa ikiwaangalia kwa makini kutaka kujua na kuona kile watakachokifanya. Kila timu huwa na mchezaji ambaye hutizamwa zaidi. Kwa umombo unaweza kumuita Key Player. Kila timu,kwa kupenda au kutopenda,huwa ina star player. Hii haimanishi kwamba katika timu hakuna wachezaji wengine wenye majina au wanaoweza pia kuwa stars.La. Ni sheria ya mmoja mmoja inayozingatiwa hapa.

Kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali wa soka,wachezaji hawa 32 [mmoja kutoka katika kila timu inayoshiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka huu] ndio watarajiwa kuchomoza zaidi huko Brazil. Mpangilio huu hapa ni kutokana na makundi ya FIFA World Cup 2014. NB: Orodha hii inaweza kubadilika kwani imeandikwa kabla timu zote hazijathibitisha wachezaji wake 23 iliyowachagua mwisho. Wengine wanaweza kuumia katika siku hizi za mwisho na hivyo kutokwenda Brazil.Zingatia.
Neymar-Brazil.
Hakuna ubishi kwamba Neymar anayechezea soka la kulipwa Barcelona nchini Spain ndio gumzo kubwa kwa timu ya Brazil. Anatarajiwa kuongoza mashambulizi ya The Kings Of Samba[Brazil]
Oribe Peralta-Mexico
Ingawa wachezaji wengine wa Mexico kama Chicharito na Giovani dos Santos wanatajwa kama ma-star,Oribe Peralta ambaye anacheza katika ligi ya nyumbani katika club ya Santos Laguna, ndiye anaaminika hivi sasa kuwa star zaidi
Luka Modric-Croatia
Hakuna shaka kwamba Luka Modric ndiye mchezaji star zaidi hivi sasa katika timu ya Croatia. Kiungo huyu ambaye hivi sasa anachezea timu ya Real Madrid nchini Spain ameonekana wazi kuwa tegemeo sio tu katika club bali nchi yake Croatia.

Charles Itandje-Cameroon
Ingawa ungetegemea mchezaji kama Samuel E’too kuendelea kuwa star na tegemeo zaidi katika timu ya Cameroon, golikipa Charles Itandje ndio tegemeo na ambaye wengi watapenda kumuona akiokoa mikwaji. Charles ambaye anachezea timu ya Konyaspor nchini Uturuki[kwa mkopo kutoka PAOK FC ya Ugiriki] aling’ara vilivyo katika mchezo dhidi ya Tunisia wakati wa kuwania nafasi ya kwenda Brazil.Google utaona alichofanya.
Diego Costa-Spain
Ingawa bado kuna utata kuhusu hali yake na kama atakuwa fit kabla ya kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia huko Brazil,Diego Costa mshambuliaji mahiri wa timu ya Atletico Madrid anatarajiwa kuwa nyota wa Spain. Lakini pia huenda akawa ndiye mchezaji atakayezomewa zaidi huko Brazil kwani Diego ni mzaliwa wa Brazil na angeweza kabisa kuchezea Brazil mwaka huu kama asingeamua kuchezea Spain[pia ni raia wa Spain].Wabrazil hawajaipenda hiyo.
Arjen Robben-Holland[The Netherlands]
Robben,mshambuliaji mahiri ambaye hivi sasa anaendelea kuwika na timu ya Bayern Munich nchini Ujerumani,ndiye mchezaji ambaye ni star zaidi na ambaye ameonyesha kuwa na kile kiwango kinachoitwa “cha dunia”. Ana miaka 30 hivi sasa.
HABARI ZAIDI BOFYA LINK HIYO HAPO

waliotembelea blog