Monday, September 22, 2014


Steven Gerrard looked out of sorts in Liverpool's disappointing 3-1 loss against West Ham on Saturday
Steven Gerrard alionekana mweny huzuni baada ya kuchapwa 3-1 na West Ham 

BRENDAN Rodgers ametetea kiwango cha Steven Gerrard, akisisitza kuwa nahodha huyo mkongwe wa Liverpool hahitaji kupumzika zaidi.
Gerrard mwenye miaka 34, amecheza kila dakika msimu huu, zikiwemo mechi tatu katika wiki na kushuhudia Liverpool akipoteza michezo miwili ya ligi kuu mbele ya  Aston Villa na West Ham.
Pia alicheza na kufunga penalti katika mechi ya ligi ya mabingwa dhidi ya wakali wa Bulgaria, Ludogorets.
Rodgers  na wasaidizi wake wanafahamu kuwa katika mechi zote za ligi kuu Gabriel Agbonlahor na Stewart Downing walifanikiwa zaidi na kumzidi kete Gerrard ambaye alishindwa kugawa mipira kama alivyozoeleka.
Reds manager Brendan Rodgers hands out instructions to his skipper from the sidelines at Upton Park
Kocha wa wekundu wa Anfield, Brendan Rodgers akimpa maelekezo nahodha wake katika uwanja wa  Upton Park
Liverpool host Middlesbrough on Tuesday in the Capital One cup, with Grant Leadbitter (left) in great form for the North East club
Liverpool wataikaribsiaha Middlesbrough leo jumanne katika mechi ya  Capital One cup, ambayo itamtumia nyota wake  aliye katika kiwango cha juu, Grant Leadbitter (kushoto) 


Nahodha huyo wa zamani wa England alikosea pasi 11 dhidi ya West Ham katika kipindi cha kwanza na alishindwa kumiliki mpira mara 14.
Rodgers alikuwa na mipango ya kumpumzisha Gerrard wakati Liverpool inacheza mechi ya Capital One leo dhidi ya Middlesbrough, lakini kila kitu kimevurugika baada ya Jordan Henderson na Philippe Coutinho kupata majeruhi.
Alipoulizwa kiwango cha nahodha wake jana, Rodgers alisema: "Hakuna tatizo. Ni mchezaji muhimu kwetu. Kiwango cha timu hakikuwa kizuri. Tumejitahidi kuimarisha kiwango chake kwa misimu miwili iliyopita na wakati huo alikuwa anacheza soka la kimataifa. Ukiangalia idadi ya mechi alizocheza, amekuwa mzuri sana".
"Yupo katika umri ambao tunatakiwa kumtunza yeye binafsi. Tunamtaka kuhusika katika mechi kubwa kwasababu ya uzoefu wake na siku zote tutafanya kila linalowezekana kumfanya awe bora"
"Tutawafahamisha kama atapumzishwa. Baadhi ya wachezaji vijana watahusishwa katika kikosi".


Mathieu Debuchy atakuwa nje ya Uwanja kwa Miezi Mitatu baada ya kufanyiwa operesheni ya Enka yake.
Debuchy, mwenye Miaka 29, aliumia na kutolewa nje kwa Machela Arsenal walipocheza na Manchester City na kutoka Sare 2-2 hapo Septemba 13.

Akithibitisha habari hizi, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amesema operesheni ya Mchezaji huyo wa Kimataifa wa France ilienda vyema lakini kuwepo nje kwake kwa muda mrefu ni pigo kubwa sana kwao.
Debuchy alinunuliwa kutoka Newcastle mapema Julai mahsusi kumbadili Bacary Sagna aliehamia Man City mwanzoni mwa Msimu huu baada ya Mkataba wake kumalizika na mwenyewe kukataa kuongeza.

Wenger amesema: “Tutajua baadae pigo hili ni kubwa kiasi gani tukishajua tumembadilisha kivipi. Lakini ndio maana tulimnunua Calum Chambers!”


Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Stamina na Ney wa Mitego wakilishambulia jukwaa mbele ya umati wa wakazi wa mji wa Morogoro mapema jana ndani ya uwanja wa Jamhuri.

Msanii wa Bongo Fleva Vanessa Mdee a.k.a V-Money akitumbuiza mashabiki waliokuwa wamefurika kwenye Uwanja wa Jamhuri Morogoro kwenye Tamasha la Fiesta 2014.

Mmoja wa mashabiki aliyekuwa kwenye Tamasha la Fiesta akishangilia huku akiwa amebebwa na mwenzake.

Vanessa Mdee akipagawisha jukwaani.

Umati uliyokuwa umefurika kwenye Tamasha la Fiesta 2014, ukishangilia moja ya burudani zilizokuwa zikitolewa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Umati uliyokuwa umefurika kwenye Tamasha la Fiesta 2014, ukishangilia moja ya burudani zilizokuwa zikitolewa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mashabiki wakishangweka

Makomando wakiwajibika jukwaani hapo.

Ommy Dimpoz akiimba na mmoja wa mashabiki aliyekuwa akiimba kwenye nafasi ya Vanessa Mdee katika wimbo wa Me & U.


Bondia Saleh Said wa Magereza 'kulia' akioneshana umwamba na Sudi Mohamed wa Mavituzi wakati wa mpambano wa kumi bora yanayoendelea kila jumamosi katika ukumbi wa Manyara Park Manzese Dar es salaam Said alishinda mpambano huo 

Bondia Iddi Juma wa Midizini akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Jumanne Mashombo wa Ndame wakati wa mpambano wa kumi bora uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika ukumbi wa Manyara Park Mahombo alishinda kwa point


Leicester City wameifunga Manchester United bao 5-3 kwenye uwanja wao wa nyumbani King PowerRobin Van Persie na Di Maria ndio wameifungia bao United kipindi cha kwanza..Di Maria akishangilia bao lake la pili kwa United ugenini huko King PowerKipindi cha kwanza dakika ya 13 Robin Van Persie anaipachikia bao la kichwa Manchester United baada ya kuunganisha krosi safi kama kona kutoka kwa Radame Falcao.
Dakika ya 16 Ángel Di María alipachika bao la pili na kufanya 2-0 lakini nao Leicester walipata bao lao nao dakika ya 18 kupitia kwa L. Ulloa bao la kichwa baada ya kupata ushirikiao kutoka wa krosi kkutoka kwa  Jamie Vardy na kufanya 2-1.Leicester nao walifanikiwa kufunga bao lao dakika ya 18 kupitia kwa José Ulloa.
 Kipindi cha pili dakika ya 57 Ander Herrera alipachika bao la tatu muda punde nao  Leceister walipatabao la pili kupitia penati ya utata na kufanya 2-3 mkwaju uliopigwa na D. Nugent katika dakika ya 62.
Dakika ya 64 E. Cambiasso aliwasawazishia bao kwa kufanya 3-3 Leceister City.
Jamie Vardy aliwachapa bao la nne na kufanya 4-3 baada ya kuwatoka mabeki wa United na kutupia baada ya kutanguliziwa mpira na Ritchie De Laet. bao la tano lilifungwa kwa mkwaju wa penati tena kupitia kwa José Ulloa dakika ya 83.

VIKOSI:Leicester: Schmeichel, De Laet, Morgan, Moore, Konchesky, Cambiasso, Nugent, Drinkwater, Hammond, Vardy, Ulloa.
Akiba: James, King, Hamer, Schlupp, Mahrez, Wasilewski, Wood.

Manchester United: De Gea, Da Silva, Evans, Blackett, Rojo, Blind, Ander Herrera, Di Maria, Rooney, Falcao, Van Persie.
Akiba: Shaw, Mata, Januzaj, Smalling, Lindegaard, Fletcher, Valencia.
Refa: Mark Clattenburg


Frank Lampard alikataa kushangilia baada ya kuisawazishia bao Manchester City dhidi ya klabu yake Chelsea aliyoitumikia karibu miaka 13.

Lamapard akipongezwa na  David Silva pamoja na  Jesus Navas, a,bapo swala la kushangilia kawaachia wenzake!

Lampard akitupia na kufunga bao usawa wa penati

Andre Schurrle akishangilia bao lake kwa Chelsea kipindi cha pili kwenye uwanja wa  Etihad leo hii walipotoka sare na wenyeji wao Man City.

Schurrle akifunga bao huku akiwa anaangaliwa na Eden Hazard kama kipa  Joe Hart ataweza kuutoa  lakini hatimaye ikawa bao na kuwa 1-0 dhidi City.

Eliquim Managala kaweka kizuizi lakini mambo yakawa tofauti!

Schurrle akishangilia mbele ya Umati wa mashabiki kwenye Uwanja wa Etihad.

1-0 Schurrle  akishangilia mbele ya wapiga picha..

Pablo Zabaleta akioneshwa kadi nyekundu na mwamuzi Mike Dean baada ya kukwaruzana na staa  Diego Costa kwenye kipindi cha pili.

Zabaleta akikwaruzana na Diego Costa

Zabaleta kimya kimya akitoka nje ya Uwanja na kuwaacha Mtu 10 City.

John Terry dhidi ya  Edin Dzeko huku nae Cesar Azpilicueta akiruka juu kwa juundani ya box

wachezaji watatu wakimkaba Nemanja Matic, James Milner kulia  Fernandinho na Vincent Kompany 
Edin Dzeko na Vincent Kompany wakimkaba Diego Costa pamoja na  Branislav Ivanovic


Jose Mourinho says Frank Lampard's love story with Chelsea ended when he joined a title competitor5
Jose Mourinho anasema mapenzi ya Frank Lampard kwa Chelsea yalikwisha baada ya kujiunga na washindani wake

JOSE  Mourinho amesema mapenzi ya Frank Lampard kwa Chelsea yamekwisha baada ya jana kuifungia Manchester City bao la kusawazisha katika dakika za majeruhi uwanja wa Etihad.
Nyota huyo mwenye rekodi ya kufunga mabao mengi kwa muda wote Chelsea, alitokea benchi na kuiadhibu timu yake hiyo ya zamani, lakini Mourinho aligoma kukubali kuwa mchezaji huyo anayecheza kwa mkopo Man City ana mapenzi ya kweli kwa Chelsea.
Alisema: "Frank ni mchezaji wa Man City, siamini hadidhi zake na mapenzi ya moyoni kwake, labda mimi ni mshamba wa mpira"
Lampard slots home from inside the penalty area to send the City fans into ecstasy against his former employers5
Lampard akiteleza katika eneo la penalti na kuifungia City bao.

"Alipoamua kwenda kwa washindani wa moja kwa moja na Chelsea, mapenzi kwa timu yalikwisha. Alifanya kazi yake kiuweledi.
"Alipokelewa vizuri England na hii ndio England na hii ndio Chelsea. Watu wa Chelsea kamwe hawasahau kile watu wa Chelsea walifanya".
"Iliwahi kunitokea hata mimi  nikiwa kocha wa Inter. Ni utamaduni na uzuri wa Chelsea".

waliotembelea blog