Monday, January 9, 2017


HAFLA ya FIFA ya kutunuku Tuzo za FIFA za Ubora Duniani kwa Mwaka 2016 zimefanyika Usiku huu huko Zurich, Uswisi na Cristiano Ronaldo kuibuka ndio Mshindi wa Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani.
Akitwaa Tuzo hii, Ronaldo, anaechezea Real Madrid na Nchi yake Portugal, aliwashinda kwa Kura Lionel Messi na Antoine Griezmann.

Ronaldo pia alitwaa, mapema Mwezi Desemba, Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani kwa 2016, Ballon d’Or, inayotolewa na Jarida la France, France Football, Tuzo ambayo kabla ya hapo, kwa Miaka 6, iliunganishwa na FIFA na kuitwa FIFA Ballon d’Or, lakini kuanzia safari hii wametengana.
Kwa upande wa Kinamama, Mchezaji Bora ni Carli Lloyd wa USA.

Kocha Bora Duniani kwa Wanaume ni Claudio Ranieri baada ya kuiwezesha Leicester City, bila kutegemewa, kutwaa Ubingwa wa England kwa mara ya kwanza katika Historia yao.
Nae Mohd Faiz Subri wa Penang, Malaysia ndie alitwaa Tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka. Kwenye Tuzo ya Mashabiki, Mashabiki wa Timu za Liverpool na Borussia Dortmund, kwa pamoja, wameshinda Tuzo hii kwa tukio la kuimba wote ‘Wimbo wa Taifa wa Liverpool’ -'You'll Never Walk Alone'- Uwanjani Anfield kabla ya Mechi yao ya Robo Fainali ya UEFA EUROPA LIGI Msimu uliopita. FIFA TUZO ZA UBORA – WAGOMBEA NA MSHINDI:
MCHEZAJI BORA WANAUME:
-Wagombea:
Cristiano Ronaldo, Antoine Griezmann, Lionel Messi
-Mshindi: Cristiano Ronaldo

MCHEZAJI BORA WANAWAKE:
-Wagombea: Melanie Behringer, Carli Lloyd, Marta
-Mshindi: Carli Lloyd wa USA.
KOCHA BORA WANAUME:
-Wagombea: Claudio Ranieri, Fernando Santos, Zinedine Zidane
-Mshindi: Claudio Ranieri wa Mabingwa wa England Leicester City

KOCHA BORA WANAWAKE:
-Wagombea: Jill Ellis, Silvia Neid, Pia Sundhage
-Mshindi: Silvia Neid [Germany]

GOLI BORA [Tuzo ya Puskas]:
-Wagombea: Marlone, Daniuska Rodriguez, Mohd Faiz Subri
-Mshindi: Mohd Faiz Subri wa Penang, Malaysia.
 

Tuzo hii inatokana na Kura za Mashabiki Duniani kote.
TUZO TOKA KWA MASHABIKI:

-Wagombea: Mashabiki wa Den Haag, Borussia Dortmund & Liverpool na Iceland.
-Mshindi: Mashabiki wa Borussia Dortmund & Liverpool

TUZO YA UCHEZAJI WA HAKI
-Mshindi:
Atletico Nacional ya Colombia
FIFA FIFPro World11 2016 – Kikosi Bora cha Mwaka 2016:
-Kipa: Neur
-Mabeki: Alves, Pique, Ramos, Marcelo
-Viungo: Modric, Kroos, Iniesta
-Mafowadi: Suarez, Ronaldo, Messi


DROO YA RAUNDI YA 4 ya EMIRATES FA CUP imefanyika Leo Usiku huko BT Tower Mjini London ikiendeshwa na Wachezaji wa zamani wa Kimataifa wa England Michael Owen na Martin Keown na Mabingwa Watetezi Manchester United kupangwa kucheza kwao Old Trafford na Wigan Athletics.

Man City na Arsenal zote zimepangwa kucheza Ugenini kwa Arsenal kuivaa Southampton au Norwich na Man City kucheza na Mshindi kati ya Crystal Palace na Bolton.
Liverpool, kama wataifunga Plymouth katika Mechi yao ya Marudiano baada ya Sare, watakuwa kwao Anfield kucheza na Wolves.
Vinara wa Ligi Kuu England, Chelsea, wao wako kwao Stamford Bridge kuivaa Brentford.
Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, Leicester City, watacheza Ugenini na Derby County wakati Tottenham wakicheza Nyumbani White Hart Lane na Wycombe.
Mechi 16 za Raundi ya 4 zitachezwa Wikiendi ya Januari 28 na 29.
DROO KAMILI TIMU 16:
Crystal Palace au Bolton v Manchester City
Middlesbrough v Accrington Stanley
Fulham v Hull City
Blackburn v Barnsley au Blackpool
Burnley au Sunderland v Fleetwood au Bristol City
Rochdale v Huddersfield Town
Millwall v Watford
Manchester United v Wigan Athletic
Chelsea v Brentford
Lincoln au Ipswich v Brighton
Southampton au Norwich v Arsenal
Plymouth au Liverpool v Wolves
AFC Wimbledon au Sutton v Cambridge au Leeds
Oxford United v Newcastle au Birmingham
Derby County v Leicester City
Tottenham v Wycombe



chato
chato-2

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika benchi la kibanda cha kupigia kiwi (Shoe Shine) pamoja na wakazi wengine wa Chato katika eneo maarufu kama Stendi za zamani Chato mkoani Geita. Kibanda hicho cha Kiwi ndicho Rais Dkt. Magufuli alichokuwa akisafishiwa viatu  vyake kabla ya kuwa Rais, pia ni sehemu ambayo alikuwa akipenda kukaa na  kubadilishana mawazo na wakazi wa Chato wakati akiwa mapumzikoni kipindi cha Nyuma.
chato-3chato-4chato-5
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Chato mkoani Geita. Shule hiyo ya Msingi Chato ndiyo Rais Dkt. Magufuli alisoma kuanzia darasa la kwanza mpaka Darasa la Saba. Rais Dkt. Magufuli amewaasa Wanafunzi hao kusoma kwa bidii kwasababu yeye pia alisoma shuleni hapo. Picha na Mpigapicha Maalum.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 9 Januari, 2017 amefanya ziara ya kushtukiza katika Shule ya Msingi Chato,ambapo ndipo aliposoma kuanzia darasa la kwanza hadi la saba na kuzungumza na walimu na wanafunzi wa shule hiyo.
Rais Dkt Magufuli ameahidi kujenga madarasa matatu na ofisi moja ya walimu katika Shule hiyo kufuatia ombi la Walimu kuwa shule hiyo inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa ikilinganishwa na idadi ya wanafunzi wanaosoma shuleni hapo.
Aidha Dkt.Magufuli amewaasa wanafunzi kutilia mkazo masomo ili waweze kufaulu na kuwataka walimu kuhakikisha wanatumia vyema fedha zinazotolewa na Serikali kila mwezi katika kutoa elimu bila malipo na pasiwe na wanafunzi hewa kama ilivyo kwa baadhi ya shule ambazo zimegundulika kuwa na wanafunzi hewa katika uhakiki uliofanywa na serikali.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Chato, Bwana Mwita Chacha amemshukuru Rais Dkt.Magufuli kwa msaada aliowapatia katika kukabiliana na uhaba wa madarasa uliokuwa unaikumba shule hiyo, pia kuitembelea Shule yao jambo ambalo limewatia moyo walimu na wanafunzi shuleni hapo.
Rais Magufuli pia ametembelea eneo la Stand ya zamani na kuzungumza na baadhi ya wananchi waliokuwepo eneo hilo na kutoa msaada kwa kikundi cha wasafisha viatu ili kuongeza mtaji wa biashara yao.

waliotembelea blog