Wednesday, June 11, 2014



ENDELEA KUTIZAMA MECHI ZAIDI KWA KUBOFYA HAPA CHINI





MCHEZAJI mstaafu wa timu ya soka ya KMKM Ali Issa Simai, amefariki dunia jana wakati wa magharibi baada ya kuugua kwa muda mfupi, na kuzikwa leo huko Chukwani Wilaya ya Magharibi Unguja.

Marehemu, ambaye alijulikana zaidi kwa jina la ‘Kepteni’ kutokana na kuwa nahodha wa KMKM kwa muda mrefu, alikutwa na mauti nyumbani kwake Fuoni baada ya kurudi kutoka katika shughuli zake za kawaida.

Mwaka 1974, kiungo huyo mshambuliaji alijiunga na timu ya kikosi cha wanamaji wakati huo ikiitwa Navy na kudumu nayo hata ilipobadilishwa jina na kuitwa KMKM (Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo), akitokea klabu ya Ujamaa yenye maskani yake mtaa wa Rahaleo.

Mmoja wa wanasoka waliocheza pamoja naye Abdalla Maulid, ameliambia gazeti hili kuwa, marehemu alikuwemo kwenye kikosi cha washika magendo hao kilichoshiriki michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati mwaka 1974 yaliyofanyika mjini Dar es Salaam, yakiwa katika mwaka wake wa kwanza.

Maulid alifahamisha kuwa, mwaka 1975, kepteni huyo aliitwa katika timu ya taifa ya Zanzibar iliyoshiriki mashindano ya Chalenji kwa vijana, yaliyofanyika uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam, na ubingwa kuchukuliwa na Kenya.

Aidha mwaka huo wa 1975, marehemu aliyesifika kwa umahiri wake wa kumiliki mpira na mbinu za kufumania nyavu, aliteuliwa katika timu kubwa ya taifa iliyokuwa chini ya kocha Muingereza George Dunga.

Pamoja na kuibeba vyema klabu yake katika ligi kuu ya muungano kuanzia mwaka 1976 na kufanikiwa kutwaa ubingwa mwaka 1984, marehemu Ali Issa pia aliisaidia Navy (sasa KMKM) kucheza klabu bingwa Afrika mwaka 1978, ambapo walifika hatua ya nne bora.

Nahodha huyo alidumu na KMKM hadi mwaka 1990 alipoamua kutundika madaluga, na kuendelea kuchezea timu ya maveterani, Wazee Sports.

Mazishi ya marehemu huyo aliyeacha watoto kumi, yalihudhuriwa na mamia ya wananchi na wanamichezo mbalimbali, ambapo mwili wake ulisaliwa katika msikiti uliopo karibu na uwanja wa Amani, na baadae kupelekwa malazoni Chukwani.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu pahala pema Peponi. Amin.


Roy Hodgson ana matumaini makubwa Alex Oxlade-Chamberlain atakuwa fiti kucheza Mechi ya England ya Pili ya Kundi D la Fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Uruguay.
Winga huyo wa Arsenal hataweza kucheza Mechi ya Kwanza na Italy hapo Jumamosi Juni 14 huko Manaus, Brazil baada ya kuumia Goti walipocheza na Ecuador huko Miami, Florida Nchini Marekani Wiki iliyopita.
Akithibitisha kwa Mchezaji huyo mwenye Miaka 20 kuweza kuikabili Uruguay huko Sao Paulo, Hodgson alisema: “Anaendelea vizuri sana na Mazoezi yake binafsi Wiki yote hii!”
Wakati huo huo kuliibuka Ripoti kuwa Nahodha wa England Steven Gerrard ana maumivu ya Nyonga lakini Kocha wa England, Hodgson, amezipiga chini stori hizo.

Amesema: “Tulifanya Mazoezi Jana na kutenganisha wale Wachezaji waliocheza Jumamosi na wale ambao hawakucheza ili kuwapa Programu tofauti. Mwishoni, Steven alifanya Mazoezi ya ziada. Hana tatizo na sielewi Stori hizo!”



ENGLAND KWENYE KUNDI
KUNDI D

14 Juni: England v Italy, Manaus
19 Juni: England v Uruguay, Sao Paulo
24 Juni: England v Costa Rica, Belo Horizonte


The Cameroon national team has arrived in Galeao Aerial Base safely.
Here, a few pics from their arrival:

That’s the head coach, Finke above there


Ekotto!


Refa NISHIMURA Yuichi na wasaidizi wake SAGARA Toru na NAGI Toshiyuki
REFA kutoka Japan Yuichi Nishimura amepangwa kuchezesha Mechi ya Ufunguzi ya Fainali zaKombe la Dunia kati ya Wenyeji Brazil na Croatio itakayochezwa Alhamisi Juni 12 huko Arena Corinthians, Jijini Sao Paulo.

Wasaidizi wake ni kutoka Japan ambao ni Toru Sagara na Toshiyuki Nagi huku Alireza Faghani wa Iran akiwa ni Refa wa Nne.
Sambamba na hao, FIFA pia imetangaza Marefa wa Mechi 3 nyingine za mwanzoni.
Nishimura, mwenye Miaka 42, anakuwa Refa wa Tatu kutoka Japan kuchezesha Fainali za Kombe la Dunia mara mbili wengine wakiwa Shizuo Takada (1986 na1990) na Toru Kamikawa (2002 na 2006).
Kwenye Fainali za 2010 huko Afrika Kusini, Nishimura alichezesha Mechi 4 ikiwemo Robo Fainali kati ya Netherlands na Brazil.
Mwaka 2012, Yuichi Nishimura alitajwa kuwa ndie Refa Bora wa Mwaka wa AFC, Shirikisho la Soka la Asia.



KOMBE LA DUNIA
RATIBA-Mechi za Ufunguzi:

Alhamisi 12 Juni 2014
KUNDI A

23:00 Brazil v Croatia
-REFA: Yuichi Nishimura [Japan]

Ijumaa 13 Juni 2014
19:00 Mexico v Cameroon
-REFA: Wilmar Roldan [Colombia]

KUNDI B
22:00 Spain v Netherlands
-REFA: Nicola Rizzoli [Italy]
01:00 Chile v Australia
-REFA: Noumandiez Doue [Ivory Coast]

waliotembelea blog