Saturday, November 14, 2015



Jina Joseph Kimwaga sio geni katika soka la Tanzania hususani katika vilabu vya Azam FC na Simba, Kimwaga alianza kusikika katika soka akiwa katika klabu ya Azam FC kabla ya dirisha la usajili lililofungwa mwezi August 2015 kuomba kwenda katika klabu ya Simba kwa mkopo wa muda mrefu.
Kimwaga ambaye ana umri wa miaka 19 ni miongoni mwa mastaa chipukizi wa mchezo wa soka wanaofanya vizuri kwa sasa, stori za ushirikina katika soka zipo na zimewahi kumfikia Joseph Kimwaga ila yeye huwa anaamini katika dini yake ya kikristo na kuvaa rozari, licha ya kuwa rozari hukatazwa mchezaji kuvaa wakati wa mechi Kimwaga huwa anaifunga katika bukta yake ili refa asijue kwa imani yake anaamini inamlinda.
IMG_20151113_215912
Staa huyo ambaye amewahi kuingia katika headlines baada ya kufunga goli la ushindi kwa klabu yake ya Azam FC dhidi ya Yanga amepewa rozari hiyo iliyotoka kwa Papa kutoka Italia na padri wake, ndio aliompatia hivyo kwa sababu imebarikiwa na Papa sio rahisi kwa vitu vya imani za giza kumpata Kimwaga.
“Kuna majaribu ambayo yanatokea katika soka kiukweli ila kama una roho fupi unaweza ukaacha lakini ni vitu ambavyo mimi na imani kwa sababu nikikumbuka tu msemo mmoja nilioambiwa na paroko kuwa ukiingia tu katika imani ndio majaribu yatakavyozidi kwa hiyo mimi na imani na ndio maana navaa rozari muda wote” >>> Joseph Kimwaga



Mshindi wa shindano la Trace Music Stars Africa, Mtanzania Nalimi Mayunga anaziandika headlines za leo kwenye kurasa za Bongo Fleva. Baada ya kushinda shindano hilo kubwa la kusaka vipaji, Mayunga aliondoka na mkataba wa kurekodi na Universal Studio wenye thamani ya dola 500,000 ambayo kwa pesa ya sasa inagonga mpaka Tzs bilion 1!
MAYUNGA2
Good news kwako mtu wangu, mtu wetu Mayunga anatarajiwa kuondoka Tz siku ya Jumatatu tarehe 16 November 2015 kwenda Marekani kwa ajili ya mafunzo ya muziki pamoja na kurekodi single yake na Akon ambaye kwenye shindano la Trace Music Stars Africa alikuwa miongoni wa majaji.
MAYUNGA3
Akiongea na CloudsFM radio leo kupitia kipindi cha XXL, Mayunga aligusia pia kuhusu safari yake ya Marekani
>>> “Marekani naenda Jumatatu na ninachoenda kukifanya kule ni kile kinachoongelewa kwenye media, kuwa naenda kwa ajili ya mafunzo, kufanya wimbo, na vilevile kushoot video ya wimbo nitakaoenda kuurekodi… japo kusema kweli sijajua wimbo huo utakuaje kwa sababu mpaka sasa bado sijaupata na wala sijausikia. Dili ni kwamba Akon anakuandikia wimbo mwenyewe, sema sijaupata ili niweze kujipanga, so nahisi kama anataka kunipima aone uwezo wangu…” Mayunga.
MAYUNGA

waliotembelea blog