Wednesday, June 29, 2016

Mkali wa Bongo fleva, Harmonize ambaye ni msanii wa kwanza kusainiwa kwenye lebo ya Diamond Platnumz (WCB), amekaa kwenye interview hii na Millard Ayo na amezungumzia kuhusu kujiendeleza zaidi katika masuala ya lugha, Harmonize amesema…
>>>’Kuna mwalimu pale ofisini WCB anafundisha lugha lakini kuiongea lugha kabla haujaijua vizuri si kitu kizuri kiiungwana, kuna mwalimu pale special kabisa  kwa sababu msanii yoyote wa WCB kwa sababu tunahitaji kutanua mziki wetu ufike tuwe na market ya nje pia’
>>>’hatuwezi kuwa na biashara ya nje, unawezaje kuwa na biashara nje na wakati international language hauwezi kuiongea, inakuwa ni vigumu kwa hiyo tunajaribu na management ililiona hilo mapema na likaishughulikia kuna mwalimu pale anatufundisha lugha vizuri tu‘- Harmonize


Liverpool wamekamilisha kumsaini Sadio Mane kwa Dau la Pauni Milioni 34 kutoka Southampton na kumpa Mkataba wa Miaka Mitano.
Dau hilo linaweza kupanda na kufikia Pauni Milioni 36 likizidi lile la Mchezaji alienunuliwa na Liverpool kwa ghali kupita yeyote walipotoa Pauni Milioni 35 kumnunua Andy Carroll Mwaka 2011.
Dili hii imemfanya Mane, anaetoka Senegal, kuwa ndie Mchezaji wa Bei ghali kupita yeyote katika Historia akilipiku lile la Januari 2015 ambalo Man City walilipa Pauni Milioni 28 kwa Swansea City kumnunua Wilfried Bony.

Mane, ambae alifunga Bao 21 katika Gemu 67 za Ligi Kuu England alizochezea Southampton tangu ahamia hapo kutoka Salzburg Mwaka 2014, anakuwa Mchezaji wa Tatu kusainiwa na Meneja Jurgen Klopp katika kipindi kufuatia Kipa wa Germany Loris Karius na Beki wa Cameroon Joel Matip. Mane anafuata mlolongo wa Wachezaji kadhaa wa Southampton walionunuliwa na Liverpool tangu 2014 na wengine ni Adam Lallana, Dejan Lovren, Rickie Lambert na Nathaniel Clyne.
Leo June 29 2016 Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imetengua matokeo ya ushindi yaliyompa Ubunge, Onesmo Nangole ‘CHADEMA’  jimbo la Longido kutokana na udanganyifu.
Akisikiliza kesi hiyo Jaji Sivangilwa Mwangesi amesema fomu zilizotumika kuandika matokeo ni fomu 21b za udiwani badala ya kutumia fomu 21c za ubunge hivyo uchaguzi utarudiwa.
Kesi hiyo ilifunguliwa mnamo June 29 2016 mahakama kuu Arusha na aliyekuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ jimbo la Longido Dk. Steven Kiruswa.
Baada ya ushindi wa kesi hiyo dhidi ya Onesmo Nangole ‘CHADEMA’ Dk. Kiruswa ‘CCM’ amesema…..>>>’tunangojea wenzetu kama wana sababu ya kukata rufaa, wakate baada ya hapo tutaenda uwanjani kuanza upya….tulikuwa na madai mengi ya msingi lakini moja ni kuwepo kwa kasoro katika utaratibu waliotumia kuhesabu, kujumlisha na kutangaza matokeo ya uchaguzi

June 28 2016 ziliripotiwa taarifa kuwa watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalamu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania.
Leo June 29 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli kupitia account yake ya tweeter amepost akizungumzia ugunduzi huo huku akitoa wito kujipanga katika eneo la mikataba…….



Imeripotiwa kuwa watu 36 wameuawa katika shambulio la kujitoa muhanga katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Ataturk Istanbul nchini Uturuki na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa, shughuli za usafirishaji katika uwanja huo zimesitishwa huku shughuli ya uokoaji na huduma ya kwanza vikiendelea.
Gavana wa mji wa Istanbul amethibisha kuuawa watu haona idadi hiyo ya majeruhi. Mashuhuda wanasema waliwaona washambuliaji watatu ambapo mmoja kati yao alikuwa akifyatua risasi kabla ya kujitoa muhanga kwa kujilipua kwa bomu na kufa.
DM GRAB - Ataturk Airport International Terminal terrorists images appeared on the departures floor. Images of the Russian national airline Aeroflot experienced moments of horror in front of the bank where the check-in office and this was reflected in the cameras. (Haberturk News Centre)
Hata hivyo mashambulizi hayo yalihusisha katika eneo la kuingia katika uwanja huo. Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan amelaani shambulio hilo na kusisitiza umoja katika kutokomeza vitendo hivyo.
.
.
.
.
.
.
.n
.n
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Mgodi wa dhahabu wa Geita ‘GGM’ June 28 umetoa vifaa vya msaada katika hospitali ya Muhimbili vyenye thamani ya shilingi milioni 23 ili kusaidia jitihada za serikali katika kuboresha huduma za afya katika kitengo cha watoto Muhimbili.
Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na Bp Mashine 10, Infusion Pump 2, Thermometers 110, Standing weghing scale 6, lying down weghing scale 6, nebulises 3 na pulse oxymeter. GGM imechangia ili watoto na kina mama wanaofika hospitalini hapo kupata huduma hizo muhimu



Baada ya kuwepo na taarifa mbalimbali zinazozagaa kwenye mitandao ya kijamii zinazotokana na habari iliyoandikwa na kuchapishwa kwenye gazeti la Jambo leo la June 24 2016, toleo namba 2482 yenye kichwa cha habari “Sasa ukimwi kupimwa nyumba kwa nyumba”.
June 28 2016 Ofisi ya Taifa ya Takwimu ‘NBS’ imetoa ufafanuzi kwamba UKIMWI hautapimwa nyumba kwa nyumba bali itafanya utafiti wa viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania kuanzia September 2016 ambapo UKIMWI utapimwa kwenye kaya chache ambazo zimechaguliwa kitaalam nchi nzima ili ziweze kuwakilisha kaya nyingine nyingi ambazo hazitahusika moja kwa moja katika utafiti huo.
Taarifa iliyotolewa na NBS imesema utafiti huu utajumuisha kaya zipatazo 16,000 ambazo ni sampuli iliyochaguliwa kisayansi kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar na utahusisha watu wazima wasiopungua 40,000 wakiwemo watoto takribani 8,000.
Aidha, taarifa hiyo imeeleza kuwa katika utafiti huo kutakuwa na kupima homa ya ini, kupima wingi wa chembechembe za damu yaani CD4, kupima wingi wa virusi katika damu na kupima kiwango cha ufanisi wa dawa za kufubaza VVU kwa watu wanaotumia dawa hizo.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa, utafiti huo wa viashiria na Matokeo ya UKIMWI wa mwaka 2016 unafanyika nchini kwa mara ya 4 ambapo utafiti wa kwanza ulifanyika mwaka 2003, wa pili ulifanyika mwaka 2007 na wa tatu ulifanyika mwaka 2011.
Hivyo, Ofisi ya Taifa ya Takwimu inapenda kuwatoa hofu wananchi kwakuwa utafiti huu sio mpya katika nchi yetu na watanzania ambao wamekuwa wakipitiwa na utafiti huu, wamekuwa wakitoa ushirikiano kwa zaidi ya asilimia 90.

June 28 2016 klabu ya Dar es Salaam Young Africans ilicheza mchezo wake wa pili wa Kundi A wa Kombe la shirikisho barani Afrika dhidi ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, katika mchezo huo Yanga ilifungwa goli 1-0, goli amble lilifungwa na Merveille Bope dakika ya 74.

waliotembelea blog