Saturday, September 13, 2014


Martín Demichelis ndie aliyewasawazishia bao na kufanya 2-2 katika dakika ya 83 baada ya kazi nzuri ya Aleksandar Kolarov kutoa pande kwa Demichelis.Jack Wilshere akishangilia bao lake. Jack Wilshere dakika ya 63 aliisawazishia Arsenal na dakika ya 74 kipindi hicho cha pili Alexis Sánchez aliwapa bao la pili Arsenal na kufanya 2-1 dhidi ya City baada ya kazi nzuri ya Jack Wilshere.Sergio Agüero akishangilia bao lake la dakika ya 28 kipindi cha kwanza dhidi ya Arsenal.
Dakika ya 28 kipindi cha kwanza Sergio Agüero anaipachikia bao safi timu yake ya Man City  na kufanya 1-0 dhidi ya Arsenal ambao ndio wenyeji kwenye Uwanja wao wa Emirates. Hadi Mapumziko City ndio walikuwa wanaongoza kwa bao 1-0.



Pichani kati msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka THT, Rachael akiwa na madansa wake wakilishambulia jukwaa kwa namna ya kipekee usiku huu kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga.

Mmoja wa wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,atambulikae kwa jina la kisanii Ommy Dimpo akiwaimbisha mashabiki huku akisherehekea siku yake ya kuzaliwa na wakazi wa mji huo usiku katika tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage

Mmoja wa wasanii wa Bongofleva anaefanya vyema katika muziki huo atambulikae kwa jina la Young Killer a.k.a Msodoki akiimba jukwaani usiku huu kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga.


Pichani juu na chini ni umati wa wakazi wa mji wa Shinyanga waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage,usiku huu.

Wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Ney Wa Mitego (pichani kulia) na Stamina wakilishambulia jukwaa kwa wimbo wao wa Huko Kwenu vipi,huku makele ya shangwe yakiwa yametawala kila kona ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga usiku huu.

Sehemu ya mashabiki wa Fiesta wakishangilia yaliyokuwa yakijiri kwenye jukwaa la Fiesta 2014 ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga.

Mwanadada Linah akionesha umahiri wake wa kucheza wimbo wake wa Ole Temba juu ya jukwaa la Fiesta 2014 usiku huu kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage.

Ukipenda muite Mr Blue,msanii wa muziki wa kizazi kipya juu ya jukwaa la Fiesta 2014 usiku huu ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga.

Mmoja wa wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,atambulikae kwa jina la kisanii Ommy Dimpo akiimba mbele ya mashabiki wimbo wake wa ani kama mama usiku huu katika tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage

Wanajiita Wakata Mkaa kutoka kundi la Wanaume TMK,Chege na Temba kwa pamoja wakilishambulia jukwa la fiesta mbele ya umati wa watu (hawapo pichani) ndani ya tamasha la Fiesta lililofanyika usiku huu ndani ya uwanja mdodog wa Kambarage mjini Shinyanga.

Wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya Khadija anaetamba na wimbo wake wa maumivu akiwa sambamba na mwanadada Rachael anaetamba na wimbo wake wa Ole temba,kwa pamoja wakilishambulia jukwaa la Fiesta usiku huu ndani ya uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Mmoja wa wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,atambulikae kwa jina la kisanii Ommy Dimpo akiwaimbisha mashabiki wimbo wake wa nani kama mamaa,usiku huu kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage

Sehemu ya umati wa watu wakishangweka na na Fiesta usiku huu.

Mmoja wa wakali wa kukamua mangona kutoka Clouds FM,Dj Zero akikamua ngoma jukwaani mbele ya umati wa wakazi wa Shinyanga kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage

Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Shinyanga wakiwa ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage,wakishuhudia tamasha la Fiesta 2014 likifanyika usiku huu.

Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Shinyanga wakiwa ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage,wakishuhudia tamasha la Fiesta 2014 likifanyika usiku huu.



Daley Blind signs for Manchester United
Louis van Gaal anaamini kumaliza kwenye Tatu Bora katika Ligi Kuu England Msimu huu ni lengo ambalo linaweza kufikiwa.
Msimu uliopita, chini ya Meneja alietimulia David Moyes, Man United walimaliza Nafasi ya 7 na kukosa kucheza Mashindano ya UEFA Ulaya.Juzi, akiongea na Wawekezaji na pia kutangaza Mapato ya Rekodi, Makamu Mwenyekiti Mtendaji wa Man United, Ed Woodward, alisema Bajeti zao zijazo zimeweka na kukadiriwa kwa Misingi ya kumaliza katika Nafasi 3 za juu.

Jana Meneja wa Man United, Louis van Gaal, ameunga mkono lengo hilo na kusema: “Sidhani kama ni lengo ambalo haliwezekani. Klabu kama Manchester United ni lazima iweke malengo. Hata mie naweka malengo. Kuwemo 3 bora ni sahihi kwa sababu Manchester United inataka kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI!”

Wakiwa na Pointi 2 tu na Goli 2 katika Mechi zao 3 za kwanza za Ligi, Man United inabidi washinde Mechi yao ya Jumapili dhidi ya QPR Uwanjani Old Trafford na Mechi hii huenda ikiwaona Wachezaji wao wapya Radamel Falcao, Marcos Rojo, Daley Blind na Luke Shaw, wakicheza kwa mara ya kwanza huku mpya mwingine, Angel Di Maria, akicheza kwa mara ya kwanza Uwanjani Old Trafford.

LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
Jumamosi Septemba 13

14:45 Arsenal v Man City
17:00 Chelsea v Swansea
17:00 Crystal Palace v Burnley
17:00 Southampton v Newcastle
17:00 Stoke v Leicester
17:00 Sunderland v Tottenham
17:00 West Brom v Everton
19:30 Liverpool v Aston Villa

Jumapili Septemba 14
18:00 Man United v QPR
Jumatatu Septemba 15
22:00 Hull v West Ham


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kesho Jumamosi (Septemba 13 mwaka huu) saa 4 asubuhi litaendesha mafunzo ya matumizi ya tiketi za elektroniki kwa wadau wa mpira wa miguu Dar es Salaam.
Mafunzo hayo Uwanja wa Taifa, na kushirikisha wasimamizi wa mechi, viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na makatibu na maofisa habari wa klabu za Azam na Yanga.
Washiriki wengine wa mafunzo hayo ni Meneja wa Uwanja wa Taifa na msaidizi wake, wasimamizi wa milangoni (stewards), waandishi wa habari wa Dar es Salaam maofisa usalama wa TFF.
Mafunzo hayo yatahitimishwa Jumapili (Septemba 14 mwaka huu) kwa mechi ya Ngao ya Jamii kati ya Azam na Yanga kuanzia saa 10 kamili jioni.
Tiketi zimeanza kuuzwa jana (Alhamisi) kupitia M-Pesa, CRDB Simbanking na maduka ya Fahari Huduma.

BONIFACE WAMBURA
MKURUGENZI WA MASHINDANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

MAKOCHA YANGA, AZAM FC LEO KUKUTANA NA WANAHABARI
Makocha wa Timu za Azam FC na Young Africans SC watakutana na Waandishi wa Habari hii Leo.
Mkutano huo utafanyika Leo Jumamosi (Septemba 13 mwaka huu) Saa 5 Asubuhi katika Ofisi za TFF zilizopo ghorofa ya tatu kwenye Jengo la PPF Tower.
Makocha hao watazungumzia jinsi walivyoandaa vikosi vya kwa ajili ya mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) itakayochezwa Jumapili (Septemba 14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



ARSENE Wenger kesho anawakabili mabingwa watetezi wa ligi kuu soka nchini England, Manchester City katika mchezo wa ligi kuu uwanja wa Emirates.
Baada ya kumsajili Danny Welbeck, je, kikosi kitakakuwa kama inavyoonekana pichani juu?
Kuna majeruhi wachache waliojitokeza kwenye mechi za kimataifa ambao ni Aaron Ramsey, Mikel Arteta na Mesut Ozil.
Lakini inaonekana Wenger ana chaguo kubwa la wachezaji na wataweza kumsaidia katika mechi ya kesho.


 Danny Welbeck akiwa katiika mazoezi ya Arsenal uwanja wa London Colney leo

Arsene Wenger ana wachezaji wengi wanaoweza kumsaidia kwenye mechi dhidi ya Manchester City kesho jumamosi.

LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:

Jumamosi Septemba 13
14:45 Arsenal v Man City
17:00 Chelsea v Swansea
17:00 Crystal Palace v Burnley
17:00 Southampton v Newcastle
17:00 Stoke v Leicester
17:00 Sunderland v Tottenham
17:00 West Brom v Everton
19:30 Liverpool v Aston Villa
Jumapili Septemba 14
18:00 Man United v QPR
Jumatatu Septemba 15
22:00 Hull v West Ham



Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akimkabidhi Ngao ya Jamii nahodha wa timu ya KMKM, Khasim Ali baada ya kuifunga Shaba ya Pemba 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar juzi. Kulia ni Meneja Mauzo wa kinywaji cha Grandmalt, Kassiro Msangi. (Na Mpiga Picha Wetu)
Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na mmoja wa wachezaji wa timu ya soka ya KMKM wakati akikagua timu hizo kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii baina ya KMKM na Shaba ya Pemba kabla ya ufunguzi wa ligi kuu ya soka ya Grandmalt inayotarajiwa kuanza jumatatu tarehe 15/09/2014, KMKM ilishinda kwa mabao 2:0 dhidi ya shaba ya Pemba.

Sehemu ya washabiki waliofurika kwenye Uwanja wa Amani mjini Zanzibar kushudia mchezo kati ya KMKM na Shaba kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii.



Aliyekuwa Rais wa Bongo Movie, Steve Nyerere.
Rais wa Bongo Movie, Steve Nyerere ametangaza kujiuzulu cheo hicho kupitia ukurasa wake wa instagram. Amedai kuna mbinu chafu dhidi yake.

MENEJA wa Swansea City Garry Monk ameshinda Tuzo ya Wadhamini Barclays ya Ligi Kuu England na kutajwa ndie Meneja Bora wa Mwezi baada ya kuongoza Timu yake kushinda Mechi zote Tatu za Ligi Kuu England.
Swansea wamefungana kileleni na Chelsea ambao wako juu kwa ubora wa Magoli na Meneja wao Jose Mourinho alikuwemo kwenye kugombea Umeneja Bora wa Agosti.


Diego Costa akiwa amebeba tuzo yake ya Mwezi Agosti
Kwa upande wa Wachezaji Straika wa Chelsea Diego Costa, ambae ameifungia Timu yake Bao katika kila Mechi ya Ligi waliyocheza, ndie amechaguliwa Mchezaji Bora na kumbwaga mwenzake wa Chelsea Cesc Fabregas na Nathan Dyer pamoja na Gylfi Sigurdsson wa Swansea, na Andreas Weimann wa Aston Villa.

Jumamosi Swansea na Chelsea zitakutana USO KWA USO huko Stamford Bridge.

WACHEZAJI WALIOKUWA WANAGOMBEA NAFASI HIYO:
Diego Costa (Chelsea)
Cesc Fabregas (Chelsea)
Nathan Dyer (Swansea)
Gylfi Sigurdsson (Swansea)
Andreas Weimann (Aston Villa)


LOUIS van Gaal amesema Danny Welbeck aliuzwa Arsenal kwasababu hakuwa mzuri sana kwa Manchester United, lakini amekataa kuwa klabu imeharibu sera yake ya soka la vijana.
Majira ya kiangazi, United walitumia paundi milioni 150 katika usajili wa wachezaji wapya, wakiwemo Angel di Maria na Radamel Falcao.
Kitendo hicho kimezua maswali kuwa klabu hiyo imewageuzia mgongo wachezaji vijana waliokulia katika akademi yao, hususani baada ya kumuuza mshambuliaji wa England, Welbeck kwenda klabu ya Arsenal kwa dau la paundi milioni 16.

Lakini katika mkutano na waandishi wa habari wa kuwatambulisha Falcao na Daley Blind jana alhamisi, Van Gaal alidai kuwa United bado itajikita kuwakuza wachezaji vijana.


Wachezaji wapya waliosajiliwa na Arsenal (kutoka kushoto) Mathieu Debuchy, Calum Chambers, David Ospina, Danny Welbeck na Alexis Sanchez katika uwanja wa mazoezi wa London Colney jana alhamisi. 
Van Gaal alieleza sababu za kumuuza Mzaliwa wa Manchester, Welbeck ambaye ameichezea klabu hiyo toka utotoni, akisema kuwa rekodi ya mshambuliaji huyo ya mabao 29 katika mechi 142 haikaribiani na ya Wayne Rooney au Robin van Persie.
"Niliwapa wachezaji wote nafasi ya kunishawishi," alisema Van Gaal. "Unapouliza kuhusu Welbeck, alikuwepo hapa tangu akiwa na miaka 9 na baada ya kwenda kwa mkopo Sunderland, alicheza misimu mitatu United, lakini hajawa na rekodi kama ya Van Persie au Rooney. Ndio maana tulimuacha aende".


Rio Ferdinand will return to former club Manchester United with Queens Park Rangers on Sunday
Kesho jumapili, Rio Ferdinand atarudi katika klabu yake ya zamani, Manchester United akiichezea Queens Park Rangers 

RIO Ferdinand anarudi Manchester United kwa mara ya kwanza kesho jumapili, lakini amelalamika kuwa klabu hiyo aliyoichezea kwa miaka 12 kamwe haikumpa nafasi ya kuaga kabla ya kujiunga na QPR.
Ferdinand aliichezea United mechi 455 na alitoa mchango mkubwa katika mafanikio ya Sir Alex Ferguson, lakini Mkurugenzi msaidizi Ed Woodward alimuambia baada ya mechi ya mwisho dhidi ya Southamptom msimu uliopita kuwa hataongezewa mkataba.
Baada ya kuambiwa hivyo, beki huyo mwenye miaka 35 aliondoka Old Trafford na kujiunga na QPR mwezi julai mwaka huu.
"Nilikuwa na mafanikio makubwa Old Trafford," alisema Ferdinand. "Sijawahi kupata nafasi ya kuaga nilipoondoka. kilikuwa kitendo kibaya, kwahiyo nitapata fursa ya kuwaaga watu wengi walionisapoti na kunisaida"
The defender linked up with Harry Redknapp at Loftus Road in the summer after 12 years at Old Trafford
Beki huyu alijiunga na Harry Redknapp katika dimba la Loftus Road majira ya kiangazi baada ya kutumika kwa miaka 12 Old Trafford
Ferdinand represented Man United with distinction for over a decade, winning six Premier League titles
Ferdinand aliiwakilisha vyema Manchester United  kwa muongo mmoja na alibeba makombe sita ya ligi kuu 

waliotembelea blog