Monday, September 15, 2014



Manchester United  wameshinda Mechi yao ya kwanza Msimu huu kwenye Ligi Kuu England wakati Kikosi chao kipya kikiisambaratisha QPR kwa Bao 4-0 ndani ya Old Trafford huku Angel De Maria aking’ara na Wachezaji wapya Marcos Rojo na Daley Blind wakicheza Mechi yao ya kwanza na kuleta uhai mkubwa.Manchester United v QPRJuan Mata akifanya yake..Manchester United v QPR
Bao 3 kabla ya Mapumziko, zilizofungwa na Di Maria, Ander Herrera na Wayne Rooney ziliwaua QPR na kuwamaliza kabisa pale Kipindi cha Pili Juan Mata alipofunga Bao la 4.Manchester United v QPRRadamel Falcao akikimbiza mpira mwishoni kipindi cha pili..Manchester United v QPRRadamel Falcao chupuchupu afunge! Kipa wa QPR aliutema mpira..
Manchester United v QPR
Straika mpya, Radamel Falcao, alikuwa Benchi na kuingizwa Dakika ya 67 na alionyesha matumaini na nusura afunge Bao kama si uhodari wa Kipa wa Robert Green. Bao la nne lilifungwa na Juan Mata katika dakika ya 58 kipindi cha pili baada ya kupata pasi kutoka kwa Ángel Di María.
Ander Herrera akishangilia bao lake la pili kwa United.Angel Di Maria alifunga Bao la Kwanza kwa frikiki murua na ni yeye alietengeneza Bao la Pili kwa kukokota ngoma Mita 60 na kumpasia Rooney aliepiga Shuti lililookolewa na kumrudia Herrera na kufunga.Manchester United v QPRDakika ya 24 Di Maria anaipachikia bao la kwanza Manchester United..1-0 dhidi ya QPR. Ni Frii kiki ya Di Maria ya umbali wa  yadi  30 na kutinga moja kwa moja hadi langoni mwa QPR.Ander Herrera  alitupia la pili na kufanya 2-0 dhidi ya QPR katika dakika ya 36 kipindi cha kwanza baada ya kupata mpira kutoka kwa Wayne Rooney. Bao la tatu lilifungwa na Wayne Rooney katika dakika ya 44 kwa shuti kali lililomzidi kipa wa QPR Green na kuzama langoni moja kwa moja na ni kwa ushirikiano wa Ander Herrera aliyetoa pasi kwa Rooney.Manchester United v QPRFalcao alichukua nafasi ya Juani Mata kipindi cja pili dakika ya 67Manchester United v QPRRojo kwenye patashika na Matt Philips wa QPRManchester United v QPRFer wa QPR akichuana na Angel Di MariaRio Ferdinand kwenye wasiwasi kutoka kwa timu yake ya zamani UnitedRadamel Falcao kaanzia benchiManchester United v QPRRio Ferdinand akipewa zawadi yake mapema kabla ya mtanange..Louis van GaalVan Gaal kati..Radamel FalcaoTayari kwa kipute...
Daley Blind na Radomel Falcao wakiingia Old Trafford...yasemekana Falcao kuingia kipindi cha pili..dhidi ya QPR.Wachezaji wa Man United wakiwa tayari kwa kipute na QPR jioni hii kwenye uwanja wa Old Trafford. United wanatarajia kuchezesha wachezaji wao wapya katika mtanange huu.
Daley Blind na Radomel Falcao wa  Manchester United wakiwasili kwenye Uwanja wa Old Trafford, Tayari kwa mtanange huo.
Luke Shawna  Ander Herrera wakishuka kwenye basi kuingia Uwanjani Old Trafford.
Meneja wa Man United Louis van Gaal akiwsiliWachezaji wa QPR wakiwa kwenye Uwanja wa  Old Trafford
Mashabiki nao ndio kwanza wanaanza kuingia kuchukua nafasi zao Uwanjani Old Trafford.
VIKOSI:


Kikosi cha Simba sc kilichokwenda Mtwara jumamosi na kutoka suluhu pacha ya bila kufungana (0-0) dhidi ya wenyeji Ndanda fc

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
WEKUNDU wa Msimbazi , Simba SC, wanaenda kuweka kambi tena Visiwani Zanzibar kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya ligi kuu soka  Tanzania bara inayotarajia kuanza kutimua vumbi septemba 20 mwaka huu.
Simba chini ya kocha Mzambia Patrick Phiri wataanza kampeni za kusaka ubingwa walioukosa kwa misimu miwili dhidi ya Wagosi wa Kaya, Coastal Union, septemba 21 mwaka huu uwanja wa Taifa , Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘kaburu’ Perez amesema:  “Leo timu inaelekea Zanzibar kwa ajili ya mkakati wa mwisho wa kujiandaa na ligi kuu na jumamosi timu itarudi Dar es salaam kwaajili ya mchezo wa jumapili dhidi ya Coastal Union uwanja wa Taifa.”
Hii itakuwa mara ya pili Simba kujificha Zanzibar kwasabababu ilikuwa huko kabla ya kuja Dar es salaam kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya, septemba 6 mwaka huu uwanja wa Taifa.
Katika mechi hiyo ya kimataifa ya kirafiki, mabao mawili ya Paul Kiongera na moja la Ramadhani Singano ‘Messi’ yalitosha kuwapa Simba ushindi wa 3-0.
Baada ya mechi hiyo,  Simba waliendelea kubakia Dar es salaam badala ya kurudi Zanzibar kama ilivyokuwa imeelezwa awali na alikuwa inafanya mazoezi katika uwanja wa Boko Veterani.
Ijumaa ya wiki iliyopita, Simba ilicheza mechi ya pili ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya URA ya Uganda na kulala bao 1-0.
Kesho yake (jumamosi) ya wiki iliyopita, Simba ilisafiri kwenda Mtwara ambapo ilicheza mechi ya kirafiki na Ndanda fc katika uwanja wa Nangwanda Sijaona na kutoka suluhu pacha ya bila kufungana.
Baada ya mechi hiyo, jana wachezaji walipewa mapumzikio, na leo jumatatu wanaanza mazoezi kabla ya kuelekea Zanzibar.
Simba wamekuwa wakiijenga timu upya chini ya kocha Phiri na usajili wao unawafanya wapinzani wawe na wasiwasi.
Wachezaji wa kigeni waliopo Simba wameonekana kuwa na ubora wa kutosha, hivyo kujenga imani kwa mashabiki wao.
Warundi, Amissi Tambwe, Pierre Kwizera, Mkenya, Paul Kiongera na Waganda Joseph Owino na Emmanuel Okwi wameonekana kuwa na msaada mkubwa kwa Simba.
Pia wapo wazawa waliosajiliwa kama, kipa Hussein Sharrif, Shaaban Kisiga, Elius Maguli,Joram Mgeveke, Tshabalala, na wengineo.

Wachezaji hawa wameonakana kuelewana na kucheza mpira mzuri kama walivyoonekana kwenye mechi dhidi ya Gor Mahia na URA.

waliotembelea blog