Monday, June 1, 2015


Adidas imekizindua kiatu maalum cha Lionel Messi kwa ajili ya mchezo wa fainali ya Uefa Champions League kati ya timu yake ya Fc Barcelona dhidi ya Juventus.
Messi atakitumia kiatu hicho pia kwenye mashindano ya Copa America.



Mlinda wa mlango wa Manchester United, David De Gea ameshindwa kutegua kitendawili kilichotanda juu ya mstakabali wake katika klabu hiyo na kuzipa nguvu tetesi za yeye kuhamia Real Madrid anakohusishwa nako kwa muda mrefu sasa.

Real Mdrid inayotazamiwa kumtangaza Rafa Benitez kama mrithi wa Carlo Anceloti katika klabu hiyo yenye maskani yake Santiago Bernabeu, imekuwa ikihaha kunasa dole gumba la mlinda lango huyo na kumrudisha katika jiji alilozaliwa na kuwa mrithi wa Ika Cassilas anayeonekana kuhitaji mbadala katika klabu hiyo.
Kocha mtarajiwa wa Real Madrid

David De Gea amebakisha mwaka mmoja katika kandarasi yake Old Trafford na ameshindwa kuweka wazi iwapo atabakia United au ataelekea Madrid wanaohitaji huduma yake kwa udi na uvumba katika kipindi hiki cha usajili.

“Tutaona nini kitatokea juu ya mstakabali wangu,” De Gea aliliambia gazeti la AS la nchini Hispania aliko mapumzikoni kwa sasa baada ya kwisha kwa msimu wa ligi na kuisaidia United kushika nafasi ya nne na kurudi katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Licha ya sintofahamu hiyo, kocha wa mashetani wekundu Manchester United bado ana matumaini kuwa De Gea atabaki Old Trafford na kuisaidia United kushinda mataji katika msimu ujao.
De Gea(24) aliyejiunga na United akitokea Atletico Madrid kwa ada ya uhamisho wa pauni million 17.8, ameshaichezea Man United michezo 132 mpaka sasa na ameonekana kuzivaa vema ‘gloves’ za Mdachi Edwin Van De Sar aliyestaafu baada ya fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya mwaka 2008.
Kama De Gea ataondoka United, itamlazimu Luis Van Gaal kuingia sokoni na kutafuta mlinda mlango atakayechukua nafasi ya Mhispania huyo licha ya kuwepo kwa Mhispania mwingine Victor Valdes aliyesajiliwa katikati ya msimu uliopita kutoka Fc Barcelona.Tayari walinda lango kama Hugo Loris (Spurs), Asmir Begovic(Stoke City) na Jasper Cillesen(Ajax) wametajwa kama tazamio la Luis Van Gaal kama warithi wa mikoba ya De Gea kama kweli atahamia kwa mabingwa hao mara 10 wa Ulaya.


Tanzania imepata mwaliko wa kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Taifa ya Rwanda kati ya Juni 6, 7 mwaka huu jijini Kigali, kwenye kumbukumbu ya mauaji ya kimbali, Tanzania itapeleka kikosi cha vijana U23 katika mchezo huo utakaochezwa mwishoni mwa wiki.
Kufuatia kupata mwaliko huo kikosi cha U23 kitaondoka nchini ijumaa tarehe 5, Juni 2015 kuelekea nchini Rwanda kikiwa na wachezaji 18 chini ya kocha Salum Mayanga.
Kocha wa Mtibwa Sugar Mecky Maxime ameongezwa kwenye benchi la ufundi litakalokwenda Ethiopia kisha nchini Misri kufuatia kocha Salum Mayanga kuwa na timu ya U23 nchini Rwanda.


Bondia Francis Cheka (kulia) akipambana na Kiatchai Singwancha wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Cheka alishinda kwa T.K.O ya raundi ya nane
Bondia Francis Cheka (kulia) akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Kiatchai Singwancha wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba Cheka alishinda kwa T.K.O ya raundi ya nane

Bondia Shabani Kaoneka (kulia) akimtupia konde la nguvu Zumba Kukwe wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Kaoneka alishinda mpambano huo kwa pointi

Bondia Seleman Zugo (kushoto) akipambana na Twaha Kiduku wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita
Bondia Francis Cheka (kulia) akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Kiatchai Singwancha wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika Ukumbi wa P.T.A Sabasaba Cheka alishinda kwa T.K.O ya raundi ya nane



Afisa habari wa Yanga Jerry Muro (katikati) akimkabidhi jezi kiungo mshambuliaji wao mpya, Balimi Busungu (kulia) aliyekuwa akichezea Mgambo JKT ya Tanga kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kumtambulisha kwa wandishi wa habari leo. Kushoto ni meneja wa timu ya Yanga, Hafidh Salehe. (Picha na Rahel Pallangyo)


UONGOZI wa Yanga umemtambulisha mchezaji mpya waliyemsajili Malimi Busungu huku wakitamba kuhamia katika usajili wa kimataifa.
Busungu ambaye msimu uliopita alifanya vizuri akiitumikia Mgambo Shooting, alisajiliwa mwishoni mwa wiki kama mchezaji huru kwa mkataba wa miaka miwili baada ya mkataba wake na Mgambo kumalizika mwishoni mwa msimu.
Akizungumza jana na waandishi wa habari Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga Jerry Muro alisema walivutiwa na kiwango cha Busungu alichoonesha katika timu yake ya Mgambo na hivyo kuamini kuwa atawasaidia katika mechi za kimataifa.
“Sisi kama Yanga tunapenda kusema kuwa tulivutiwa na kiwango cha Busungu, kazi tuliyopewa tumaimaliza na tumempa jezi namba 16 ambayo aliichagua mwenyewe,”alisema.

Uongozi pamoja na Wafanyakazi wa kituo cha radio ya EFM 93.7 kwa pamoja wakikata keki kusherehekea kutimiza mwaka mmoja wa kituo hicho ambacho kwa sasa kinakuja kwa kasi jijini Dar na kwingineko,hafla hiyo ilikwenda sambamba na kuadhimisha miaka 16 ya msanii Mkongwe wa muziki wa kizazi kipya Juma Nature,katika tamasha lililoitwa KOMAA CONCERT,ambalo lilifanyika ndani ya kiota cha maraha cha Dar Live,Mbagala jijini Dar mwishoni mwa wiki na kuhudhuriwa na maelfu ya mashabiki na wapenzi wa muziki .

Lengo la kuwaburudisha Mashabiki wa Juma Nature na wasikiliazaji wa 93.7 EFM ilikuwa pia ni sehemu ya kuwashukuru mashabiki kwa ushirikiano wao kwa miaka kumi na sita ya muziki tangu kuanza msanii huyo Juma Nature aingie kwenye game ya Muziki nchini Tanzania.

Baadhi ya Wasanii walioshiriki kulinogesha tamasha hilo ni pamoja na Profesa Jay, Shetta, Snura, Makomando, Msagasumu na wengine wengi. Katika tamasha hilo lililowavutia wakazi wa Mbagala na vitongoji vyake,kiingilio kilipangwa kuwa ni shilingi 7,000 tu.

Meneja Mwasiliano na mambo ya Sheria wa EFM 93.7 Deniss ssebo alisema kuwa wanaamini Msanii Juma nature ni msanii mwenye kipaji kikubwa na aliyewahamasisha wasanii kibao kuingia katika muziki huu wa kizazi kipya hivyo anastahili kupewa heshima kubwa kwa mchango wake mkubwa katika kukuza muziki wa kizazi kipya,alisema na kuongeza kuwa lakini kwa Efm huyo ni msanii wa Kwanza tu na itaendelea kufanya hivyo kwa wasanii wengine kwa kuwa wanaaamini Muziki unaongea.

Mkurugenzi wa Efm Dj Majay akiongoza jopo la wafanyakazi wenzake kukata keki

Pichani kulia ni Meneja Mwasiliano na mambo ya Sheria wa EFM 93.7 Deniss Ssebo akizungumza jambo mbele ya mwashabiki na wapenzi wa muziki na pia wasikilizaji wakubwa wa kituo hicho kuhusiana na utaratibu mzima wa sherehe hiyo,kulia ni Mkurugenzi wa Efm Dj Majay akigawa keki kwa mashabiki waliofika kushuhudia tukio hilo ndani ya Dar Live.

Msanii Mkongwe wa muziki wa kizazi kipya Juma Nature akitumbuiza jukwaani mbele ya mashabiki wake,pia akiwashukuru kumpa sapoti ya kutosha tangu ameanza muziki na sasa anatimiza miaka 16 katika tasnia hiyo adhimu.

Wakongwe pamoja Juma Nature na Prof.Jay wakishoo love kwa mashabiki wao.

Msanii Snura na Madansa wake wakilishambulia jukwaa la KOMAA CONCERT


Msanii wa muziki wa kizazi kipya atambulikae kwa jina la kisanii Shetta akitumbuiza mbele ya mashabiki kibao waliofika kwenye tamasha la KOMAA CONCERT.

Makamuzi yalikuwa yakiendelea jukwaani.

Amsha amsha za hapa na pale zikiendelea jukwaani.


Mashabiki walikuwa kibao.


Deejay Spar akionesha uwezo wake kwa mashabiki.

Shabiki wa ukweli kwa Juma Nature

Burudani ilipangwa sawa bin sawia huku Ma -Mc wakinogesha shughuli


Mashabiki na mandhari ya Dar Live kwa usiku huo ndani ya jicho la samaki

Dar Live palinoga usiku huo wa KOMAA CONCERT

waliotembelea blog