Thursday, February 6, 2014

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger ameondoa uwezekano wa kumsajili Luis Suarez kutoka Liverpool katika majira ya kiangazi baadae mwaka huu. Arsenal walijaribu kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay wakati wa usajili msimu uliopita huku Suarez mwenyewe akitaka kuondoka Anfield. Lakini Wenger amekanusha tetesi mpya zilizozuka kuwa bado wanahitaji huduma ya nyota huyo ambaye yuko katika kiwango cha juu msimu huu. Wenger amesema uhamisho wa mara ya kwanza wa Suarez haukufanikiwa hivyo mchezajihuyo hajawahi kuwa wa kwao na itabakia hivyo. 
 
Suarez mpaka sasa amefanikiwa kufunga mabao 23 katika mechi 19 alizoichezea 
Liverpool na kuwawezesha kuwepo katika nafasi nne za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini Uingereza. Arsenal wanatarajiwa kukwaana na Liverpool katika Uwanja wa Anfiled Jumamosi ambapo wanaweza kuongeza pengo la alama kufikia 11 kama Daniel Sturridge of Liverpool is congratulated by teammates after scoring his team's third goal



Afisa Mahusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde (wa pili kushoto) akiongelea umuhimu wa promosheni ya Mimi ni Bingwa muda mfupi baada ya kukabidhi shilingi milioni moja kwa baadhi ya washindi wa promosheni hiyo (waliopo pichani). Kushoto ni Bw. Ramdhani Wefa, Kulia ni Philemon Nathaniel Mgaya akifuatiwa na Bw. Msemwa Makuzi ambaye pia ni mshindi wa tiketi na wote wakiwa wanatokea Dar es salaam.

Afisa Mahusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde (kulia) akikabidhi kitita cha shilingi milioni moja kwa mmoja kati ya washindi wa milioni moja Bw. Msemwa Makuzi ambaye pia ni mshindi wa tiketi ya kwenda kushuhudia moja kati ya mechi za Manchester United nchini Uingereza kwenye uwanja wa Old trafford.Mpaka sasa zaidi ya shilingi milioni 150 zimeshatolewa kwenye promosheni hiyo.
======== ======== ========
Washindi wa promosheni ya Mimi ni Bingwa waipongeza Airtel
Wakati Kampuni ya mitandao ya simu za mkononi ya Airtel ikisubiria kuchezesha droo kubwa ya shilingi Milioni 50 kupitia promosheni ya Mimi ni Bingwa, baadhi ya washindi waliokwishapatikana wamejitokeza wakiisifia kampuni hiyo kwa kuratibu promosheni zenye kulenga maendeleo kwa watanzania walio wengi nchini.

Washindi hao wameainisha hayo muda mfupi baada ya kukabidhiwa pesa zao mapema wiki hii kwenye ofisi za makao makuu ya Airtel ziilizopo Morocco jijini Dar es salaam.


Washindi hao wamedai kuwa mara nyingi watu huwa hawaamini promosheni zinazoendeshwa na kampuni ya simu kama Airtel na hivyo kujikuta wakibaki nyuma kwa kuogopa kuthubutu.


“Mi binafsi sikuwahi kumuambia mke wangu kwamba nashiriki kwenye promosheni ya Mimi ni Bingwa sababu huwa akijua nashiriki ananikasirikia na kusema nina matumizi mabaya ya pesa, lakini leo nimeibuka mshindi wa shilingi milioni moja yeye akishuhudia na vilevile nimeshinda tiketi ya kwenda kushuhudia mechi ya Manchester United kwenye uwanja wa Old Trafford,” alisema mshindi huyo Bw. Msemwa Makuzi mkazi wa Dar es salaam.

Mshindi huyo aliendelea kwa kusema, kwa hali ya kawaida ilikuwa ni ngumu kuamini kwamba ameshinda shilingi milioni Moja na tiketi ya kwenda nchini Uingereza kushuhudia mechi ya Manchester United kwenye uwanja wa Old Trafford.

“Kweli mimi kama mtu mwingine yeyote wa kawaida iliniwia vigumu kuamini kwamba nimeibuka mshindi wa pesa hizo na tiketi. Na imenichukua muda kuamini mpaka sasa baada ya kukabidhiwa hizi milioni moja ndo naamini kweli mimi ni mshindi,” alimalizia Bw. Makuzi.

Aidha washindi wengine wamewaasa wananchi kote nchini kujitokeza kwa wingi katika promosheni hiyo kwani ina manufaa makubwa kwa maendeleo ya mtu binafsi na taifa zima.

“Kwa kweli mi nawaambia watanzania wenzangu wasidhani hivi vitu ni masihara, watu wanashinda kweli na maisha yao yanabadilika kupitia hizi pesa tunazopewa. Mimi hapa naiwinda hiyo milioni 50 kwani nina uhakika nikishinda nitakuwa nimesahau kabisa umasikini,” alisema Ramadhani Wefa ambaye ni mshindi wa milioni moja kutoka Kinondoni jijini Dar es salaam.

Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde alisema bado Airtel inatambua na itaendelea kutambua umuhimu wa wateja wake hivyo haina budi kuhakikisha inatoa huduma bora na zenye manufaa kwa wananchi wote kiujumla.

“Airtel inaelewa fika kuwa wateja ndio kiini cha maendeleo ya kampuni hiyo na hivyo inajitahidi kuhakikisha inatoa huduma bora za kuwanufaisha wateja wake na kuleta maendeleo kwa taifa zima kiujumla,” alisema Jane.


Washiriki wa michezo ya Sochi
Serikali ya Marekani imeonya mashirika ya ndege yanayofanya safari za kwenda Urussi kwamba magaidi huenda wakajaribu kuingiza kimagendo vilipuzi vilivyofichwa ndani ya neli za dawa ya kusugua meno.
Afisa mmoja wa idara ya usalama nchini Marekani amesema vifaa kama hivyo huenda vikatumiwa kujenga bomu ndani ya ndege au baada ya kuwasili katika mashindano ya Olimpiki ya msimu wa baridi ambayo yataanza Ijumaa katika mji wa milimani wa Sochi.
Afisa huyo hata hivyo alisema kuwa serikali yake haina ushahidi wa tishio la moja kwa moja wa mashindano hayo ya Olimpiki ya Sochi .
Vikosi vya usalama vya Serikali ya Urussi viko katika hali ya tahadhari kuu baada ya makundi ya wanamgambo na magaidi kutishia kufanya mashambulizi katika mashindano ya Olimpiki ya msimu wa baridi ya Sochi.
Vikosi vya usalama katika jimbo la Dagestan nchini Urussi vimemuua kwa kumpiga risasi mwanamgambo wa kiislamu katika mji wa Izberbash.
Dzhamaldin Mirzayev mwenye umri wa miaka thelathini anashukiwa kuandaa mashambulizi ya bomu ya kujitoa mhanga katika mji wa Volgograd mwezi Disemba.
Watu thelathini na wanne waliwauwa katika shambulizi hilo.
Inadhaniwa kuwa Mirzayev ndiye aliyewapa mafunzo washambulizi wawili wa kujitoa mhanga .

Luiz Suarez
Miaka imebadilika na kuwa miezi na sasa ni miezi nne pekee , kabla ya mashindano ya kombe la dunia huko Brazil kuanza.
Makocha wanaendelea na maandalizi kuhakikisha timu zao zimekamilika idara zote ima ni safu ya ushambulizi ,ya kati na safu ya ulinzi kabla ya kipenga cha kuanza kwa kombe la dunia .
Kulingana na tafiti za ushabiki ,kombe la dunia ndilo lenya ufuasi mkubwa zaidi kote duniani .
Edison Cavani
Kocha wa Uruguay Oscar Tabarez , amesema kuwa washambulizi wa timu hiyo Luis Suarez na Edinson Cavani wapo katika umri bora wa kushamiri katika kinyanganyiro cha Kombe la dunia huko Brazil.
Tabarez anamatumaini kuwa kuwa washambulizi wake wanaujuzi na uwezo wa kutwaa kombe hilo baada ya kufuzu kwenye hatua ya nusu fainali katika kombe la duna la 2010.
Uruguay ambayo imewahi kushinda kombe hilo mara mbili iko katika kundi D na Costa Rica, Uingereza, Italia na wenyeji Bra



Biashara haramu ya pembe za Ndovu hufaidi zaidi Bara Asia
Tani tatu ya pembe za Ndovu zitateketezwa hii leo Nchini Ufansa ili kuonyesha kujitolea kwa serikali ya taifa hilo katika vita dhidi ya biashara hiyo haramu.
Wizara ya mazingira itatekeleza uchomaji huo wa shehena ya pembe za Ndovu zilizonaswa katika uwanja wa ndege wa Charles de Gaulle.
Ufaransa ni taifa la kwanza barani Uropa kuharibu na kuchoma hadharani pembe haramu za Ndovu.
Muungano wa kimataifa wa uhifadhi wa mazingira, umesema kwamba takriba ndovu elfu 22 mwaka 2012.
Pembe haramu za ndovu huuzwa sana Nchini China na kwingineko barani Asia.
China ndio taifa kubwa lenye kufaidi kutokana na biashara haramu ya pembe za Ndovu

Bunge la Tanzania
Serikali ya Tanzania imekanusha taarifa za vyombo vya habari zilizodai kuwa wabunge wa nchi hiyo watalipwa kiasi cha zaidi ya dola laki moja za kimarekani watakapomaliza muda wao wa kipindi cha miaka mitano yakiwa malipo ya kiinua mgongo.
Taarifa ya wizara ya fedha imesema habari hiyo ni ya upotoshaji kwa kuwa Waziri wa fedha ,hakuwahi kuzungumza na mwandishi yeyote kama inavyodaiwa kuwa alithibitisha taarifa hizo.
Baada ya kuzuka kwa taarifa hizo baadhi ya wabunge waliozungumza na vyombo vya habari walikiri kuwepo kwa mipango hiyo huku wengine wakikanusha kuwa hawajawahi kupitisha mapendekezo kama hayo bungeni.
Naye naibu spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ameiambia BBC kuwa habari hizi si za kweli '' nipende kusema kuwa jambo hilo kwa kweli si la kweli.Si la kweli kwa sehemu mbili,kwanza kwa utaratibu wa utawala wetu bora Tanzania, hakuna mtu mwenye mamlaka ya kujiongezea yeye mwenyewe kipato chake katika utumishi wa uma.kila ambaye ana mshahara au marupurupu ya aina fulani lazima yaidhinishwe na mamlaka au chombo kingine, ndio utaratibu wa utawala wetu.Kwa hiyo na sisi Bunge hatuna mamlaka ya kujipangia posho ya aina yoyoyte au mshahara wa aina yoyote kwa wabunge au viongozi wa Bunge''.
Pia naibu spika Ndugai amesema madai ya baadhi ya Wabunge kuwa kulikuwa na mpango huo si ya kweli na hayajawahi kujadiliwa katika Bunge hilo.
Taarifa hizo zilisababisha malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu hatua ya serikali kuwapatia wabunge kiasi hicho kikubwa cha fedha huku ikidai kuwa haina fedha za kutekeleza miradi kwa ajili ya huduma nyingine za umma.

Mbwa aliyekamatwa laikuwa anatumiwa 'na kikosi maalum cha jeshi la Marekani nchini Afghanistan
Kundi la wapiganaji wa Taleban limesema kuwa limemkamata Mbwa kutoka kwa wanajeshi wa Marekani Mashariki mwa Afghanistan.
Picha waliyoiweka kwenye akaunti yao ya Twitter, inaonyesha Mbwa mdogo wa hudhurungi akiwa na kamba ndogo shingoni.
Taliban wanasema kuwa Mbwa huyo kwa jina, 'Kanali' alikamatwa usiku wakati wa msako uliofanywa mwezi Disemba.
Mbwa huyo alikuwa na tochi ndogo, kamera na kifaa cha GPS.
Pia walionyesha silaha walizonasa wakati wa msako huo, ambazo hutumiwa na kikosi maalum cha jeshi la Marekani.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa kumekuwa na taarifa za kiongozi wa Taliban katika eneo hilo kuonekana akiwa na Mbwa huyo ambaye sasa ni mfungwa wa kivita.


ami.
 short stint at PSG before quitting the game last summer.

David Beckham announced he's the owner of Miami's new MLS franchise

Beckham was handed a black and blue scarf at the end of the press conference

 Beckham was joined by MLS commissioner Don Garber (left) and mayor Carlos Gimenez

 Beckham arriving to unveil his new Major League Soccer franchise in Miami

The former England captain has bought the franchise for a fraction of the normal price

The former midfielder was happy to speak to confused local TV reporters

Beckham is expected to raid the Premier League for loan players

Beckham was met by a wall of media when he arrived in Miami



Edison Cavani

Kocha wa Uruguay Oscar Tabarez, amesema kuwa washambulizi wa timu hiyo Luis Suarez na Edinson Cavani wapo katika umri bora wa kushamiri katika kinyanganyiro cha Kombe la dunia huko Brazil.
Tabarez anamatumaini kuwa kuwa washambulizi wake wanaujuzi na uwezo wa kutwaa kombe hilo baada ya kufuzu kwenye hatua ya nusu fainali katika kombe la duna la 2010.

Uruguay ambayo imewahi kushinda kombe hilo mara mbili iko katika kundi D na Costa Rica, Uingereza, Italia na wenyeji Brazil.
 
 Kikosi cha Uruguay
 
 
Miaka imebadilika na kuwa miezi na sasa ni miezi minne pekee , kabla ya mashindano ya kombe la dunia huko Brazil kuanza.


Makocha wanaendelea na maandalizi kuhakikisha timu zao zimekamilika idara zote ima ni safu ya ushambulizi ya kati na safu ya ulinzi kabla ya kipenga cha kuanza kwa kombe la dunia .

Kulingana na tafiti za ushabiki ,kombe la dunia ndilo lenya ufuasi mkubwa zaidi kote duniani .
 
Home is where the heart is: Poyet will be supporting Uruguay when they take on England on June 19 Gus Poyet kuwaongoza!

waliotembelea blog