Wednesday, May 28, 2014



ALIEKUWA Meneja wa Southampton Mauricio Pochettino  ameteuliwa kuwa Meneja mpya wa Tottenham Hotspur kwa Mkataba wa Miaka Mitano.
Pochettino, mwenye Miaka 42, aliteuliwa kuwa Meneja wa Southampton hapo Januari 2013 alipombadili Nigel Adkins na Msimu huu amewafikisha Nafasi ya 8 kwenye Ligi Kuu England iliyomalizika Mei 11, na kabla uteuzi huu wa Leo wa kwenda Tottenham, alijiuzulu wadhifa wake wa Southampton.
Pochettino anamrithi Tim Sherwood alietimuliwa mapema Mwezi huu. 

Raia huyu wa Argentina anakuwa Meneja wa 10 wa Tottenham tangu Mwaka 2001.
Waliokuwa Wasaidizi wa Pochettino huko Southampton, Jesus Perez, aliekuwa Meneja Msaidizi, Kocha wa Timu ya Kwanza, Miguel D'Agostino, na Kocha wa Makipa, Toni Jimenez, wote wanaungana nae huko Spurs.
Roberto Soldado kuuzwa?

KUHUSU POCHETTINO:

-Kazaliwa 2 Machi 1972 huko Santa Fe, Argentina
-Alichezea Klabu za Newell's Old Boys, Espanyol, PSG na Bordeaux
-Akiwa na Espanyol alitwaa Copa del Rey mara 2: 1999/2000 na 2005/06
-Ameichezea Argentina mara 20 na kufunga Bao 2
-Aliteuliwa Meneja wa Espanyol Januari 2009.
-Aliteuliwa Meneja wa Southampton hapo Tarehe 18 Januari 2013
-Alifanikiwa kuzitwanga Manchester City, Liverpool na Chelsea kwenye Ligi


UEFA imewafungulia Mashitaka Kocha wa Atletico Madrid Diego Simeone na Kiungo wa Real Madrid Xabi Alonso kwa kuwatuhumu kufanya Utovu wa Nidhamu kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI iliyochezwa Jumamosi iliyopita huko Lisbon, Ureno na Real Madrid kuichapa Atletico Madrid Bao 4-1.
Wote hao wawili wameshitakiwa kwa makosa ya kuvamia Uwanja.
Mara mbili Diego Simeone aliingia Uwanjani wakati wa Dakika za Nyongeza 30 kwenda kumkabili Beki wa Real Raphael Varane na ikabidi azuiwe na Wasaidizi wake.
Pia Simeone alionyesha kukasirishwa na Refa Bjorn Kuipers wa Holland. Nae Xabi Alonso, ambae alikosa kucheza Fainali hiyo kwa sababu alikuwa Kifungoni, alionekana akikimbia nje ya Uwanja baada ya Mechi hiyo.
UEFA imetamka kuwa Kesi za wawili hao zitasikilizwa hapo Julai 17 na wakipatikana na hatia baadhi ya Adhabu zao ni kuzikosa Mechi za UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao.
Vile vile, UEFA imezifungulia Mashitaka Klabu zote mbili, Real Madrid na Atletico Madrid, kwa kuzoa Kadi za Njano 5 kila moja katika Fainali hiyo.
Kwenye Mechi hiyo, Wachezaji 7 wa Atletico na 5 wa Real walipewa Kadi za Njano.


Cardiff City imemsaini Straika wa Manchester United Federico Macheda kwa Mkataba wa Miaka Mitatu.
Macheda, mwenye Miaka 22, anakuwa Mchezaji wa 3 kusainiwa na Cardiff kwa ajili ya Msimu ujao na atahamia bila malipo kuanzia Julai 1 wakati Mkataba wake na Man United utakapoisha. 

Macheda aliwahi kufanya kazi huko Man United chini ya Bosi wa Cardiff, Ole Gunnar Solskjaer, alipokuwa Kocha wa Timu ya Rizevu.
Macheda alijiunga na Timu ya Vijana ya Man United Mwaka 2007 akitokea Lazio na kuwa Mfungaji Bora wa Timu ya Vijana ya chini ya Miaka 18 katika Msimu wake wa kwanza tu Old Trafford kwa kufunga Bao 12 katika Mechi 21.
Mwaka 2009, akiwa na Miaka 17 tu, Macheda aling’ara katika Mechi yake ya kwanza tu na Timu ya Kwanza ya Man United walipokuwa nyuma kwa Bao 2-1 na Aston Villa, Cristiano Ronaldo akasawazisha, na Macheda kupiga Bao la ushindi katika Dakika za Majeruhi na kuisaidia sana Man United kwenye mbio zao za Ubingwa Msimu huo.
Msimu huo, Macheda aliendelea kuonekana mara kadhaa kwenye Timu ya Kwanza na alifunga Bao lake la Pili kwa Man United Sekunde 45 tu baada ya kumbadili Dimitar Berbatov kwenye Mechi na Sunderland.

Msimu huo, Macheda alitunukiwa Tuzo ya Jimmy Murphy ambayo hupewa Mchezaji Bora wa Mwaka toka Chuo cha Soka cha Man United.
Lakini Msimu uliofuatia, Macheda akaanza kuzongwa na Majeruhi ya mara kwa mara na maendeleo yake kuathirika.
Misimu iliyofuatia, Macheda akawa anacheza nje ya Man United kwa Mkopo kwenye Klabu za Sampdoria, Queens Park Rangers, VfB Stuttgart, Doncaster Rovers na Birmingham City, ambako alifunga Bao 10 katika Mechi zake 18.

Tuesday, May 27, 2014

Mbeya City Usiku huu imefungwa Bao 2-1 na AFC Leopards ya Kenya katika Mechi yao ya Pili ya KUNDI B la Mashindano ya CECAFA NILE BASIN CUP iliyochezwa huko Khartoum, Sudan.
Hadi Mapumziko, Mbeya City walikuwa nyuma kwa Bao 2-0 zilizofungwa na Mudde Musa katika Dakika ya 30 na Were Paul, Dakika ya 35.

Bao la Mbeya City lilifungwa na Deus Kaseke katika Dakika za Majeruhi.
Kwenye Mechi ya Kwanza, Mbeya City waliifunga Academie Tchite ya Burundi Bao 3-2 na Mechi yao ya mwisho ya KUNDI B ni hapo Jumatano dhidi ya Enticelles ya Rwanda.

VIKOSI VILIVYOANZA:

MBEYA CITY:
BARUAN David
MWAGANE Yeya (Nahodha)
KIBOPILE Hamad
JULIUS Deogratius
YOHANNA Morris
MATOGOLO Anthony
KASEKE Deus
MAZANDA Steven
NONGA Paul
KABANDA  John
THEMY Felix

Akiba:
LAMBON Ahery
YUSUPH Abdallah
YUSUPH Wilson
ABDALLAH Seif
KENNY Ally
SEMBULI Christian
KOCHA: MWAMBUSI Juma [Tanzania]

AFC LEOPARDS:
MATASI Patrick
WERE Paul (Nahodha)
WAFULA Edwin
MASIKA Eric Chemati
SHIKOKOTI Joseph
MUDDE Musa
IKENNE Austin
ABDALLAH Juma
SALEH Jackson
MANGOLI Benard
WAFULA Noah
Akiba:
MUSALIA Martin
IMBALAMBALA Martin
JUMAAN Khalid
KADENGE Oscar
OKWEMBA Charles
KHAMATI Michael
ETEMESI Augustine
KOCHA: Hendrik Pieter De Jong [Holland]


Mratibu Mtendaji wa tamasha hilo la ‘Love Concert –Kumbukumbu ya Mangwea’,  Kareeem Omary ‘KO’  (kushoto) akiwa na familia ya marehemu Albert Mangwea ‘Ngwair’ Mama mzazi wa Mangwea (Katikati) na  kaka wa Mangwea, Keneth Mangwea  (kulia).
Px2  
Mratibu Mtendaji wa tamasha hilo la ‘Love Concert –Kumbukumbu ya Mangwea’,  Kareeem Omary ‘KO’ .
Px3
Bana ya Love Concert
px4  
Taswira ya Nyumbani kwa Mama Mangwea kwa sasa.
Albert MangwairMangwea enzi za uhai  wake
..Mastaa kibao kujumuika katika ‘LOVE CONCERT’
..Afande Selle, Belle 9, Samir na wengineo –Moro
P-Funky, Mswaki, Chemba Squad kutikisa 
Na Andrew Chale
MASTAA mbalimbali nchini wakiwemo wanamuziki wanatarajiwa kushiriki kwenye tukio maalum la kumbukumbu ya mwaka mmoja tokea kifo cha  marehemu Albert Mangwea ‘Ngwair’ ,  litakalofanyika ndani ya ukumbi wa  Nyumbani Park (Samaki  samaki Spot) , Kihonda Morogoro mjini Juni 28.
Akizungumza na mtando huu , Mratibu Mtendaji wa tamasha hilo,  Kareeem Omary ‘KO’  alisema maandalizi ya tukio hilo litakalokuwa la kila mwaka, limepwa jina la ‘Love Concert – Kumbukumbu ya kifo cha Albert Mangwe’.
Kareem, aliwaomba wadau kujitokeza kwa wingi kuunga mkono kwenye tukio hilo kwani litakuwa la kipekee na la aina yake  ambalo pia litatoa fursa kwa wakazi hao pia mikoa jirani na watu kutoka nje ya Tannzania ambao watauzulia. 
“Nawaomba wadau kujitokeza kuonesha  upendo  wa pamoja. Kumbukumbu  kwa mpendwa wetu kama ilivyo utamaduni wetu.” alisema Kareem.
Na kuongeza kuwa, siku hiyo   Watu mbalimbali watapata kupiga picha na mastaa  pamoja na mama mzazi wa Mangwea  kama kumbukumbu.
Kareem aliwataja wasanii watakaotoa burundani, ni pamoja  na kutoka kwa kundi la Wanachemba ambalo pia aliwahi kuwa nalo marehemu Ngwair,  JSqueezer, P Funky Majani na Mswaki. Kwa upande wa wasanii kutoka Morogoro ni pamoja na Afande Sele, Team Racers, Mc Koba Chris wa Marya, Belle 9,  Samir, Zombie, President  Mirrow,  Jordan wa Dejavu na wengine wengi.
Katika siku hiyo ya Juni 28, ambayo ndiyo siku aliyopatwa na umati marehemu, Kareem alisema kabla ya matukio ya shoo ukumbini, itatanguliwa na ibada mbili maalum ikiwemo ya  Kanisani na ile ya nyumbani.
Aidha, Kareem alisema katika tukio hilo, ambalo linatarajia kuanza majira ya jioni ya saa 10 hadi saa 12 jioni, wametoa fursa kwa watoto kutoa burudani ikiwemo ya kuimba na nyinginezo  na baadae usiku wa kuanzia saa 2 hadi majogoo wasanii hao mbalimbali watatawala jukwaa na burudani ya nguvu ya kumbukumbu.
Marehemu ‘Ngwair’  alifariki  dunia akiwa  nchini Afrika kusini, alijizolea umaarufu kwa nyimbo kama Mikasi na Nisikilize Mi na nyingine nyingi alizowahi shirikishwa na wasanii mbalimbali nchini wakiwemo Professa Jay, Nuru, TID, Chidi Benz  na wengine wengi.


Open wide: David Luiz undergoing a medical check-up at the squad's Granja Comary training complex
Character: David Luiz poses on the doctor's bed as the Brazil squad settled down in Teresopolis
 Fundi: David Luiz akiwa amelala katika kitanda cha daktari.
Waiting patiently: David Luiz pulls a face as his ears are inspected during a medical check-up
Check-up: Thiago Silva gets inspected by the doctor as preparations step up ahead of the World Cup
Specimen: Dante is put through his paces on the treadmill, attached to a monitoring system
 Dante naye hakuwa mbali
Watchful eye: Bayern Munich gets his eyes checked out at the training complex
 Nyota huyo wa  Bayern Munich akichunguzwa jicho


DSC_4490Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
TIMU ya Taifa ya Tanzania chini ya kocha mkuu, Mholanzi, Mart Nooij inatarajia kujipima ubavu katika mechi ya kimataifa ya kirafiki jioni ya leo kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam dhidi ya timu ya Taifa ya Malawi (The Flames) kuanzia majira ya saa 11:00 jioni.
Taifa Stars iliyopiga kambi yake mjini Tukuyu jijini Mbeya inatarajia kuwasili asuhubi hii majira ya saa 4:00 katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa ndege ya Air Tanzania.
Wapinzani wa Taifa stars tayari wapo jijini Dar es salaam kwa ajili ya mechi hiyo muhimu kwa makocha kuangalia uimara wa timu zao kabla ya kwenda kucheza mechi za mashindano.
Stars na Malawi wanakutana kwa mara ya pili ndani ya mwezi mmoja kwani mei 4 mwaka huu walipambana tena katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na kutoka suluhu pacha ya bila kufungana.
Mechi hii itatumika na kocha mkuu wa Taifa stars, Nooij, kuangalia kama kuna maboresho katika kikosi chake kinachojiandaa na mechi ya marudiano dhidi ya Zimbabwe mjini Harare.
Mechi ya kwanza jijini Dar es salaam ambayo Stars ilishinda kwa bao 1-0 la John Bocco `Adebayor`, safu ya kiungo ilionekana kupwaya sana, hivyo leo hii itakuwa nafasi ya kocha kuona kama viungo wake wameimarika.
Pia safu ya ushambuliaji ilionekana kukosa nafasi muhimu za kufunga na kwa muda wote walipokuwa Tukuyu, Nooij alikuwa anahangaika kunoa makali ya washambuliaji wake.
Malawi (Flames) inayonolewa na mchezaji wake wa zamani Young Chidmozi nayo itakuwa inacheza mechi ya mwisho ya majaribio kabla ya kwenda N’djamena kuikabili Chad.
Shirkisho la soka Tanzania, TFF kupitia kwa Afisa habari wake, Boniface Wambura Mgoyo limewataka watanzania kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao ambayo kwa sasa inajengwa upya.
Wambura alitaja kiingilio katika mechi hiyo kuwa kitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa upande wa VIP B na C kiingilio kitakuwa sh. 10,000 wakati kwa VIP A itakuwa ni sh. 20,000.

Sunday, May 25, 2014


  • Mkutano kuonyeshwa moja kwa moja na Star TV
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akikagua jukwaa la wageni waalikwa kwenye uwanja wa People's Singida.
 Katibu wa NEC itikadi na Uenezi Nape Nnauye akikagua jukwaa la kuhutubia ,wengine pichani ni Maafisa wa Chama Makao Makuu Nyakia Ally (kushoto) na Octavian Kimario(kulia)
 Magari ya kurushia matangazo yakiwa tayari kwenye eneo la mkutano.
 Mafundi mitambo wa Star TV wakiweka sawa mitambo yao, mkutano huu utaenda live mnamo muda wa saa tisa mchana.
 Star TV wakiendelea kufunga vyombo vya kurushia matangazo ya mkutano moja kwa moja kutoka viwanja maarufu vya People's Singida.
 Uwanja wa People's unavyoonekana wakati wa maandalizi.




Nahodha wa Real Madrid, Iker Casillas akiwa ameinua Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuwafunga jirani zao, Atletico mabao 4-1 usiku huu Uwanja wa Luz mjini Lisbon, Ureno. Hilo linakuwa taji la 10 la michuano hiyo kwa Real.
Uplifting: Ronaldo gets his hands on the trophy in Lisbon after Real's extra time victory
Mfungaji wa bao la nne la Real, Cristiano Ronaldo akiwa ameinua Kombe
Landmark: Real Madrid's players celebrate their 10th European Cup triumph
Kikosi cha Real Madrid kikifurahia na Kombe hilo.

Wednesday, May 21, 2014



01_a939d.jpg
1_90ea0.jpg
2_a9106.jpg
3_0dd77.jpg
4_b7898.jpg
5_a1af1.jpg



 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi mteule wa Tanzania nchini Sweden Mhe,Dora Msechu , aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar leo,[
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein akifuatana na Balozi mteule wa Tanzania nchini Sweden Mhe,Dora Msechu , aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar leo,baada ya mazungumzo 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein akiagana na Balozi mteule wa Tanzania nchini Sweden Mhe,Dora Msechu , aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar leo,baada ya mazungumzo

Shirika la kutetea haki za binadamu Human rights watch limeishutumu serikali ya Somalia kwa kuwanyima wafungwa haki za uakilishi wa wakili na kuwashitaki raia wa kawaida chini ya mahakama za kijeshi.
Shirika hilo limesema kuwa mamia ya raia wanahukumiwa kwa sheria kali wasizoelewa. Human rights watch pia imesema kuwa raia wengi wamejikuta matatani baada ya kukamatwa katika msako wa kitaifa unaofanywa na mashirika ya kijasusi ya Somalia na mara nyingie wanazuiliwa kwa muda mrefu bila kufunguiwa mashtaka.
Kuzuiliwa kwa muda mrefu ni tatizo ndogo sana kwa raia hao wa Somalia ikilinganishwa na kufunguliwa mashtaka ya ugaidi na kutishia usalama wa nchi. Ukipatikana na hatia, hukumu ni kifo.
Licha ya kuwa mashirika ya haki za binadamu yamekuwa yakipinga kutolewa hukumu hii, Somalia ni mojawepo ya nchi chache Afrika ambayo bado inatoa huku hiyo.
Wasiwasi mkubwa ni kwamba, washukiwa hawapewi fursa ya kujitetea. Na wala mahakama hizi za kijeshi hazihitaji ushahidi mwingi kuamua kuwa una hatia.(P.T)
Human rights Watch imetaja katika ripoti yao kisa kimoja ambapo zaidi ya kesi 24 zilisikilizwa na kuamuliwa kwa chini ya siku 4.
Mahakama yajitetea
Lakini akijibu madai hayo, mwenye kiti wa mahakama za kijeshi wa Somalia Liban Cali Yarow ameambia BBC kuwa ni upuuzi mtupu na mwingilio wa jamii ya kimataifa katika mambo yasiyowahusu.
''Haya mashirika ni ya nje, na hayajui mambo yanayofanyika nchini kwetu. Inasikitisha kwamba hawazungumzii matatizo yetu ila wanapiga kelele tunapojaribu kujitatulia wenyewe. Ripoti hiyo imejaa madai yasiyo kweli.''
Human rights watch iliwahoji zaidi ya watu 30 na familia za watu walio shutumiwa, na wengi wao wamesema kuwa mahakama hizo haziwapi wafungwa nafasi ya kujitetea.
Mara nyingine hata kuwalazimisha kukiri mashtaka ambayo hawakufanya na hakuna ruhusa ya kukata rufaa. Hapa ndipo mwisho wa kesi.
Jamii ya kimataifa
Sasa shirika hilo limetoa wito kwa jamii ya kimataifa na hasa wafadhili kushinikiza Somalia kurejesha haki za wafungwa na kuzuia raia kushtakiwa katika mahakama za kijeshi.
Lakini mwenyekiti wa mahakama hiyo Liban Cali Yarow amepuuzilia mbali ripoti ya shirika hilo akisema kuwa imejaa madai ya uongo.
''Ningependa kumsihi yeyote ambaye ana malalamiko juu yetu awasilishe kwetu badala ya kuandika kwenye magazeti. Kuandika tu bila kutushauri ni sawa na kutuwekelea madai ya uongo.'' Amesema Liban Yarow.
Maafisa wa Somalia wametetea hatua ya kuwashtaki washukiwa wa ugaidi katika mahakama za kijeshi wakisema kuwa mahakama za kiraia hazina ulinzi wa kutosha na uwezo wa kusikiliza kesi zenye uzito mkubwa kiasi hicho.



 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akizungumza na ujembe wa watu kutoka Congo hawapo pichani waliomtembelea ofisini kwake kuwaalika wasanii kutoka Tanzania kushiriki katika sherehe za fiesta nchini Congo kwa lengo la kudumisha amani na mshikamano katika nchi za maziwa makuu. Kulia ni Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akifafanua jambo kwa wajumbe wa maandalizi ya fiesta kutoka Congo walipomtembelea ofisini kwake, kulia ni mratibu wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bw. Faso Mushigo Celestin na katikati ni Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara wapili kushoto akipokea zawadi kutoka kwa wajumbe kutoka Congo waliokuja nchini kuwaalika wasanii wa Tanzania kushiriki fiesta nchini Congo, kushoto ni Mkurugenzi Idara ya Utamaduni Profesa Hermas Mwansoko.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akiangalia CD iliyorekodiwa matukio mbalimbali ya fiesta ya mwaka jana ilivyokuwa nchini Congo. Kulia ni Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga.
Picha na: Genofeva Matemu – Afisa Mawasiliano Serikalini WHVUM

Na: Genofeva Matemu 
Wasanii wa muziki nchini waalikwa kushiriki katika sherehe za fiesta nchini Congo zinazotarajiwa kufanyika julai 16 hadi 26 mwaka huu.
Mwaliko huo umetolea na wajumbe kutoka Congo walioshiriki katika siku ya Uanuwai wa Utamaduni duniani iliyoadhimishwa kitaifa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja leo jijini Dar es Salaam na baadaye kumtembelea Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt Fenella Mukangala  ofisini kwake ambapo walimuomba wasanii wa muziki kutoka Tanzania kushiriki sherehe fiesta zitakazofanyika nchini Congo mwaka huu.
Akitoa ufafanuzi kuhusiana na sherehe hizo Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga amesema kuwa lengo la sherehe za fiesta mwaka huu ni kuwakutanisha wasanii wa Afrika wanaoishi nchi za maziwa makuu ili waweza kupata nafasi ya kupanda mti wa amani ikiwa na lengo la kuziwezesha nchi hizo kuwa na mazungumzo ya amani.
Bi. Gizenga amesema kuwa wanatarajia kupata wasanii wa muziki kutoka nchini Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi pamoja na wasanii wa Congo watakaoshiriki fiesta ndani ya mikoa miwili nchini Congo katika mkoa wa Kivu ya Kaskazini Goma pamoja na Kivu ya Kusini Bukavu.
“Tumezunguka nchi zilizopo katika maziwa makuu tukiwaomba wasanii wa nchi hizo kushiriki katika sherehe za fiesta nchini Congo ambazo mwaka huu tutahusisha upandaji wa mti wa amani tukizitaka nchi hizo ziwe na mazungumzo ya amani na mshikamano” alisema Bi. Gizenga.
Kwa upande wake waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara amewashukuru wajumbe hao kwa mwaliko na kuwahaidi kuwa wasanii kutoka nchini Tanzania watapata fursa ya kipekee hivo ni muhimu kwao kushiriki ili waweze kuiwakilisha Tanzania na kuweza kupata uzoefu kutoka nchi jirani.
Aidha Dkt. Mukangara amesema kuwa ni muhimu kwa Tanzania kushiriki katika sherehe hizo kwani Tanzania ilishiriki kwa kiasi kikubwa katika kuleta amani ya nchi ya Congo hivyo aina budi kushiriki na kuendeleza amani na mshikamano wa nchi hizo mbili.



 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu Kiongozi wa Japan, Yoshihiro Suga, wakati alipofika ofisini kwake Jijini Tokyo Japan leo Mei 21, 2014, akiwa katika ziara ya kikazi. Picha na OMR



Serikali ya Japan imeelezea nia yake ya kuendelea kuchangia bajeti ya Tanzania na kufafanua kuwa, inafanya hivyo kwa kutambua kuwa Tanzania ni mshirika mkubwa wa maendeleo na kwamba ni nchi yenye kutia matumaini katika kupiga hatua za kimaendeleo.
Akizungumza jana katika Ofisi yake jijini Tokyo, Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Japan Mheshimiwa Yoshihide Suga alisema, serikali ya Japan inaifahamu Tanzania kama mshirika wa maana katika maendeleo na kwamba inafahamu mchango wa Tanzania katika kuendeleza ushirikiano wa nchi za Afrika Mashariki. Katibu Mkuu huyo pia aliongeza kuwa, Tanzania imemudu kudumisha amani kwa kipindi kirefu huku ikipiga hatua za kimaendeleo na kwamba watu wake wamebakia wamoja kwa miaka mingi licha ya kuwa na tofauti za kitamaduni, kijiografia na kidini.
Kauli hiyo ya Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Japan, imetolewa kufuatia mkutano wake na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal ambaye yupo jijini Tokyo kwa ziara ya kikazi. Katibu huyo alisema, “tunaifahamu Tanzania kama nchi muhimu inayodumisha amani. Nchi yenu imeweza kudumisha Muungano kwa miaka 50, Japan inawapongeza sana. Tunafahamu mnafanya kazi kubwa katika kuwaendeleza wananchi wenu na sisi kama ndugu na rafiki zenu tuko tayari kabisa kushirikiana nanyi.”
Katibu Mkuu Suga alieleza pia kuwa, Tanzania ni nchi iliyo thabiti katika ukanda wa Afrika Mashariki na inayo nguvu katika kuhakikisha ukanda huu unaendeleza utengamano hali ambayo inachangia kuwepo maingiliano ya wananchi wa ukanda wa Afrika Mashariki sambamba na kutanua fursa kwa wawekezaji kutoka nje ya Afrika.
“Mko thabiti katika mambo mengi na hasa kuweza kumudu kuwa na amani na utulivu, mnategemewa sana na nchi za Afrika Mashariki na kwa hali hii sisi tupo tayari kuendelea kutenga fedha katika bajeti yetu kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali ya Tanzania katika ushirikiano wa serikali na sekta binafsi (PPP),” alisema.
Kwa upande wake Mheshimiwa Makamu wa Rais Dkt. Bilal alimueleza Katibu Mkuu Suga kuwa, Tanzania inapokea kwa heshima kubwa mchango wa Japan kwa kutambua hali yake ya utulivu na kwamba anatumia ziara yake Japan kuhamasisha wawekezaji kuja kuwekeza Tanzania.

“Tuna kazi kubwa mbele yetu katika kuwaendeleza Watanzania. Hatuwezi kufanya kazi hiyo peke yetu, hivyo basi nitumie nafasi hii kukuomba Mheshimiwa Katibu Mkuu kutusaidia kuhamasisha wawekezaji kutoka Japan ili waje kushirikiana nasi katika kuiendeleza Tanzania. Urafiki kati yenu na sisi ni wa siku nyingi na tungetegemea sasa tuubadili na utazame fursa za kuchangiana kiuchumi na hasa katika kuwekeza kwa kubadilishana teknolojia pamoja na mtaji,” Makamu wa Rais alisema.
Mheshimiwa Makamu wa Rais yuko nchini Japan kwa ziara ya kikazi na tayari amefanikiw akukutana na wakuu wa makampuni mbalimbali makubwa duniani yenye makao yake makuu nchini Japan na kisha kutumia nafasi hiyo kuelezea fursa za uwekezaji nchini Tanzanja sambamba na kubainisha umuhimu wa sekta binafsi kushiriki katika kusaidia maendeleo ya nchi zinazoendelea zilizopo Afrika, Tanzania ikiwa ni kipaumbele.





























Leo imetimia miaka 18 tangu ndugu zetu walipopata ajali na Meli ya MV. Bukoba 21 May 1996, na wengi kupoteza maisha! Ni tukio kubwa lililoua watu wengi nchini na kuacha huzuni kubwa kwa Watanzania. Comment R.I.P kwao ili waendelee kupumzika kwa aman..


Usajili wa wachezaji kwa hatua ya kwanza msimu huu (2014/2015) unaanza Juni 15 hadi
Agosti 3 mwaka huu wakati kipindi cha kutangaza wachezaji walioachwa au kusitishiwa
mikataba ni kuanzia Juni 15-30 mwaka huu.

Kipindi cha kwanza cha uhamisho wa wachezaji ni kuanzia Juni 15 mwaka huu hadi Julai
30 mwaka huu. Kupitia majina na kutangaza pingamizi ni kati ya Agosti 4 na 11 mwaka
huu. Kuthibitisha usajili hatua ya awali ni Agosti 12 hadi 14 mwaka huu.

Usajili hatua ya pili utakuwa kati ya Agosti 14 na 29 mwaka huu. Kupitia na kutangaza
majina ya pingamizi hatua ya pili ya usajili ni kuanzia Agosti 30 hadi Septemba 4 mwaka
huu. Uthibitisho wa usajili hatua ya pili ni Septemba 5 na 6 mwaka huu.

Kwa upande wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inatarajiwa kuanza Agosti 24 mwaka huu,
na ratiba inatarajiwa kutoka mwezi mmoja kabla (Julai 24 mwaka huu).



Kikosi cha timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) chenye watu 25 kinaondoka kesho alfajiri kwenda Nigeria kwa ajili ya mechi ya marudiano dhidi ya Nigeria (Flying Eagles).

Mechi hiyo itachezwa Jumamosi (Mei 24 mwaka huu) katika Jiji la Kaduna kwenye Jimbo la Kaduna ambalo lipo katikati ya Nigeria. Msafara wa timu hiyo unaoongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Ayoub Nyenzi unaondoka kwa ndege ya Ethiopian Airlines.

Ngorongoro Heroes inayonolewa na Kocha John Simkoko ilipoteza mechi ya kwanza iliyofanyika nyumbani jijini Dar es Salaam kwa mabao 2-0.

Mwamuzi Alhadi Allaou Mahamat wa Tchad ndiye atakayechezesha mechi hiyo. Atasaidiwa na Issa Yaya, Alfred Madjihoudel na Idriss Biani wote kutoka Tchad. Kamishna ni Aboubakar Alim Konate wa Cameroon.

TIMU YA U15 YAWASILI GABORONE
Timu ya Tanzania ya umri chini ya miaka 15 imewasili salama jijini Gaborone, Botswana kwa ajili ya michezo ya Afrika ambapo itacheza mechi yake ya kwanza Mei 22 mwaka huu dhidi ya Mali.

Kikosi hicho cha wachezaji 16 chini ya Kocha Abel Mtweve kimetua jijini Gaborone jana (Mei 19 mwaka huu) jioni kwa ndege ya South African Airways. Michezo hiyo itamalizika Mei 30 mwaka huu.

Wachezaji waliopo kwenye kikosi cha Tanzania ni Adam Shayo, Amani Ally, Amos Manguli, Amri Nyuki, Amede Amani, Baraka Rashid, David Uromi, Goodlove Mdumule, Hance Msonga, Kelvin Kamalamo, Makalius Amrin, Nasson Chanuka, Paulo Ngowi, Petro Shaban, Rajab Mohamed na Thomas Chindeka.

Nchi nyingine zinazoshiriki michezo hiyo kwa upande wa mpira wa miguu ni Afrika Kusini, Botswana, Nigeria, Mali na Swaziland.

Gabon na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) ambazo nazo zilikuwa zishiriki kwenye michezo hiyo zimejitoa dakika za mwisho.

10357474_634079413340945_8148690486284095511_nMechi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika mwakani nchini Morocco kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Zimbabwe iliyochezwa Jumapili katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 63,345,000.
Mapato hayo katika mechi hiyo iliyomalizika kwa Taifa Stars kuibuka na ushindi wa bao 1-0 yametokana na washabiki 11,079 waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 10,000 na sh. 20,000.
 
Mgawo wa mapato hayo ni asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 9,662,796.61, gharama za kuchapa tiketi sh. 6,000,000, asilimia 15 ya uwanja ni sh. 7,152,330.51, asilimia 20 ya gharama za mchezo sh. 9,536,440.68 na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kwa pamoja wamepata sh. 30,993,432.20.

waliotembelea blog