Thursday, December 22, 2016


FIFA Leo hii imetoa Listi ya Ubora Duniani ambayo ni ya mwisho kwa Mwaka 2016 na Argentina wameendelea kushika Nambari 1 wakifuata Brazil.
Tanzania imepanda Nafasi 4 na sasa ipo ya 156 kutoka ile ya 160 ya Mwezi uliopita.
Mwezi Januari Mwaka huu Tanzania ilikuwa ya 126 na kupanda hadi 125 Mwezi Februari, kushuka 130 Aprili na kuyumba lakini Julai ikawa ya 123 na baada ya hapo mporomoko ukafuatia.

Kwa Bara la Afrika, Timu inayoshika Nafasi ya juu kabisa ni Senegal ambao ni wa 33 wakifuata Mabingwa wa Afrika Ivory Coast walio Nafasi ya 34 kisha Tunisia 35, Egypt 36 na Algeria 38.

10 BORA:
1. Argentina
2. Brazil
3. Germany
4. Chile
5. Belgium
6. Colombia
7. France
8. Portugal
9. Uruguay
10. Spain


KIUNGO wa Manchester United Henrikh Mkhitaryan Leo amezoa Tuzo yake ya 6 mfululizo kama Mchezaji Bora wa Mwaka kwa Nchi yake Armenia.
Hii ni Tuzo yake ya 7 tangu avuke Umri wa Miaka 20 na kumfanya awemo kwenye Rekodi za Mastaa wa Dunia waliozoa mara nyingi Tuzo za aina hiyo.
Anaeongoza kwa Tuzo aina hii kwa Nchi yake ni Mchezaji mwenzake Mkhitaryan huko Man United, Zlatan Ibrahimovic, ambae amechukua mara 11.
Wengine wanaomkimbiza Ibrahimovic ni Wachezaji toka Finland, Sami Hyypia, alietwaa mara 9 na Jari Litmanen, mara 8, na Kipa wa Czech Republic Petr Cech mara 8.

Lakini hao wote wamestaafu Timu za Taifa wakati Mkhitaryan bado anacheza akikimbizwa kwa karibu na wale ambao bado wanadunda Timu zao za Taifa kina Gareth Bale wa Wales na David Alaba wa Austria, wote wakiwa na Tuzo 6 kila mmoja.

Wengine waliowahi kutwaa Tuzo 6 enzi zao ni Andriy Shevchenko wa Ukraine na Aliaksandr Hleb wa Belarus.

Walotwaa mara 5 ni Marek Hamsik (Slovenia), Robert Lewandowski (Poland), Goran Pandev (Macedonia) na Mstaafu Kakha Kaladze (Georgia).

Kwenye baadhi ya Nchi Tuzo za Mchezaji Bora wa Mwaka zina mifumo tofauti kama vile Portugal ambako zipo za aina mbili za yule achezae Ligi ya ndani na yule achezae nje ya Nchi.

Huko, kwa Wachezaji wa nje, Cristiano Ronaldo amezoa mara 8 katika Miaka 10 iliyopita.

Na Argentina wana mfumo wa aina hiyo hiyo ingawa kabla haijabaguliwa Lionel Messi alibeba Tuzo mara 2 na ilipotofautishwa kati ya Wachezaji wa ndani na nje, Messi alipewa mara 8 kati ya 9 kwa wa nje tangu wakati huo.


Straika wa Mabingwa wa England Leicester City anaechezea England Jamie Vardy sasa atakosa Mechi 3 baada ya Rufaa yake kupinga Kadi Nyekundu aliyopewa Jumamosi Leicester ikitoka 2-2 na Stoke City kutupiliwa mbali.

Vardy, mwenye Miaka 29, atazikosa Mechi za Leicester dhidi ya Everton, West Ham na Middlesbrough.

Vardy alitolewa nje na Refa Craig Pawson katika Dakika ya 28 kwa Rafu ya Miguu Miwili kwa Straika wa Stoke Mame Diouf.


KILE Kifungo cha Real Madrid walichoshushiwa na FIFA cha kutosajili Wachezaji Wapya hadi Januari 2018 sasa kimepunguzwa na CAS, Court of Arbitration for Sport, Mahakama ya Usuluhishi Michezoni, na sasa wataruhusiwa kusajili Wapya kuanzia Julai, 2017.
Awali FIFA iliwafungia Real kutosajili Wachezaji Wapya kwa Madirisha Mawili ya Uhamisho ikimaanisha yale ya Januari 2017 na Julai 2017 kwa kosa la kusajili Wachezaji wa chini ya Miaka 18 kinyume na Kanuni za FIFA,
Vile vile, CAS imeipunguza Faini waliyotozwa Real kutoka Pauni 282,000 hadi Pauni 188,000.
Adhabu hiyo ya FIFA walipewa Real na pia wenzao wa Jiji la Madrid Atletico Madrid Mwezi Januari lakini Klabu hizo zilikata Rufaa na hivyo kupata mwanya wa Kusajili mwanzoni mwa Msimu Mwezi Julai.
Hata hivyo, FIFA ikazitupa Rufaa za Klabu hizo mbili na zote zikaamua kukata Rufaa kwa CAS.
Kupunguziwa Adhabu kwa Real kumetobolewa kupitia Tovuti ya Klabu hiyo lakini hamna habari yeyote kuhusu maamuzi ya CAS kwa Rufaa ya Atletico Madrid.



Miss Puerto Rico Stephanie Del Valle is crowned after winning the Miss World 2016 Competition in Oxen Hill, Maryland, U.S., December 18, 2016. REUTERS/Joshua Roberts
Miss Puerto Rico Stephanie Del Valle (C) reacts to being named Miss World as Miss Philippines Catriona Elisa Gray (L) and Miss Kenya Evelyn Njambi Thungu watch during the Miss World 2016 Competition in Oxen Hill, Maryland, U.S., December 18, 2016. REUTERS/Joshua Roberts
Winner of Miss World Miss Puerto Rico Stephanie Del Valle (C) stands with first runner up Miss Dominican Republic Yaritza Miguelina Reyes Ramirez (L) and second runner up Miss Indonesia Natasha Mannuela during the Miss World 2016 Competition in Oxen Hill, Maryland, U.S., December 18, 2016. REUTERS/Joshua Roberts
Winner of Miss World Miss Puerto Rico Stephanie Del Valle (C) stands with first runner up Miss Dominican Republic Yaritza Miguelina Reyes Ramirez (L) and second runner up Miss Indonesia Natasha Mannuela during the Miss World 2016 Competition in Oxen Hill, Maryland, U.S., December 18, 2016. REUTERS/Joshua Roberts
Miss Puerto Rico Stephanie Del Valle reacts after winning the Miss World 2016 Competition in Oxen Hill, Maryland, U.S., December 18, 2016. REUTERS/Joshua Roberts


RATIBA LIGI  KUU ENGLAND
Ijumaa Desemba 23

African Lyon v Yanga [Uhuru Stadium, Dar es Salaam]
 

Jumamosi Desemba 24
Mbeya City v Toto Africans [Sokoine, Mbeya]
Kagera Sugar v Stand United [Kaitaba, Bukoba]
Ndanda FC v Mtibwa Sugar [Nangwanda, Mtwara]
Simba v JKT Ruvu [Uhuru Stadium, Dar es Salaam]
Majimaji FC v Azam FC [Majimaji, Songea]
Mwadui FC v Mbao FC [Mwadui Complex, Mwadui]

Jumatatu Desemba 26

Ruvu Shooting v Tanzania Prisons [Mabatini, Mlandazi]


RATIBA YA LIGI KUU ENGLAND BOXING DAY
Jumatatu Desemba 26
15:30 Watford v Crystal Palace
18:00 Arsenal v West Bromwich Albion
18:00 Burnley v Middlesbrough
18:00 Chelsea v Bournemouth
18:00 Leicester City v Everton
18:00 Manchester United v Sunderland
18:00 Swansea City v West Ham United
20:15 Hull City v Manchester City

Jumanne Desemba 27
20:15 Liverpool v Stoke City

Jumatano Desemba 28
22:45 Southampton v Tottenham Hotspur

Ijumaa Desemba 30

2300 Hull City v Everton

Jumamosi Desemba 31
1800 Burnley v Sunderland
1800 Chelsea v Stoke City
1800 Leicester City v West Ham United
1800 Manchester United v Middlesbrough
1800 Southampton v West Bromwich Albion
1800 Swansea City v Bournemouth
2030 Liverpool v Manchester City

Jumapili Januari 1

16:30 Watford v Tottenham Hotspur
19:00 Arsenal v Crystal Palace

Jumatatu Januari 2
1530 Middlesbrough v Leicester City
1800 Everton v Southampton
1800 Manchester City v Burnley
1800 Sunderland v Liverpool
1800 West Bromwich Albion v Hull City
2015 West Ham United v Manchester United

Jumanne Januari 3
22:45 Bournemouth v Arsenal
23:00 Crystal Palace v Swansea City
23:00 Stoke City v Watford 20:00

Jumatano Januari 4
2300 Tottenham Hotspur v Chelsea

waliotembelea blog