Wednesday, May 28, 2014



ALIEKUWA Meneja wa Southampton Mauricio Pochettino  ameteuliwa kuwa Meneja mpya wa Tottenham Hotspur kwa Mkataba wa Miaka Mitano.
Pochettino, mwenye Miaka 42, aliteuliwa kuwa Meneja wa Southampton hapo Januari 2013 alipombadili Nigel Adkins na Msimu huu amewafikisha Nafasi ya 8 kwenye Ligi Kuu England iliyomalizika Mei 11, na kabla uteuzi huu wa Leo wa kwenda Tottenham, alijiuzulu wadhifa wake wa Southampton.
Pochettino anamrithi Tim Sherwood alietimuliwa mapema Mwezi huu. 

Raia huyu wa Argentina anakuwa Meneja wa 10 wa Tottenham tangu Mwaka 2001.
Waliokuwa Wasaidizi wa Pochettino huko Southampton, Jesus Perez, aliekuwa Meneja Msaidizi, Kocha wa Timu ya Kwanza, Miguel D'Agostino, na Kocha wa Makipa, Toni Jimenez, wote wanaungana nae huko Spurs.
Roberto Soldado kuuzwa?

KUHUSU POCHETTINO:

-Kazaliwa 2 Machi 1972 huko Santa Fe, Argentina
-Alichezea Klabu za Newell's Old Boys, Espanyol, PSG na Bordeaux
-Akiwa na Espanyol alitwaa Copa del Rey mara 2: 1999/2000 na 2005/06
-Ameichezea Argentina mara 20 na kufunga Bao 2
-Aliteuliwa Meneja wa Espanyol Januari 2009.
-Aliteuliwa Meneja wa Southampton hapo Tarehe 18 Januari 2013
-Alifanikiwa kuzitwanga Manchester City, Liverpool na Chelsea kwenye Ligi


UEFA imewafungulia Mashitaka Kocha wa Atletico Madrid Diego Simeone na Kiungo wa Real Madrid Xabi Alonso kwa kuwatuhumu kufanya Utovu wa Nidhamu kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI iliyochezwa Jumamosi iliyopita huko Lisbon, Ureno na Real Madrid kuichapa Atletico Madrid Bao 4-1.
Wote hao wawili wameshitakiwa kwa makosa ya kuvamia Uwanja.
Mara mbili Diego Simeone aliingia Uwanjani wakati wa Dakika za Nyongeza 30 kwenda kumkabili Beki wa Real Raphael Varane na ikabidi azuiwe na Wasaidizi wake.
Pia Simeone alionyesha kukasirishwa na Refa Bjorn Kuipers wa Holland. Nae Xabi Alonso, ambae alikosa kucheza Fainali hiyo kwa sababu alikuwa Kifungoni, alionekana akikimbia nje ya Uwanja baada ya Mechi hiyo.
UEFA imetamka kuwa Kesi za wawili hao zitasikilizwa hapo Julai 17 na wakipatikana na hatia baadhi ya Adhabu zao ni kuzikosa Mechi za UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao.
Vile vile, UEFA imezifungulia Mashitaka Klabu zote mbili, Real Madrid na Atletico Madrid, kwa kuzoa Kadi za Njano 5 kila moja katika Fainali hiyo.
Kwenye Mechi hiyo, Wachezaji 7 wa Atletico na 5 wa Real walipewa Kadi za Njano.


Cardiff City imemsaini Straika wa Manchester United Federico Macheda kwa Mkataba wa Miaka Mitatu.
Macheda, mwenye Miaka 22, anakuwa Mchezaji wa 3 kusainiwa na Cardiff kwa ajili ya Msimu ujao na atahamia bila malipo kuanzia Julai 1 wakati Mkataba wake na Man United utakapoisha. 

Macheda aliwahi kufanya kazi huko Man United chini ya Bosi wa Cardiff, Ole Gunnar Solskjaer, alipokuwa Kocha wa Timu ya Rizevu.
Macheda alijiunga na Timu ya Vijana ya Man United Mwaka 2007 akitokea Lazio na kuwa Mfungaji Bora wa Timu ya Vijana ya chini ya Miaka 18 katika Msimu wake wa kwanza tu Old Trafford kwa kufunga Bao 12 katika Mechi 21.
Mwaka 2009, akiwa na Miaka 17 tu, Macheda aling’ara katika Mechi yake ya kwanza tu na Timu ya Kwanza ya Man United walipokuwa nyuma kwa Bao 2-1 na Aston Villa, Cristiano Ronaldo akasawazisha, na Macheda kupiga Bao la ushindi katika Dakika za Majeruhi na kuisaidia sana Man United kwenye mbio zao za Ubingwa Msimu huo.
Msimu huo, Macheda aliendelea kuonekana mara kadhaa kwenye Timu ya Kwanza na alifunga Bao lake la Pili kwa Man United Sekunde 45 tu baada ya kumbadili Dimitar Berbatov kwenye Mechi na Sunderland.

Msimu huo, Macheda alitunukiwa Tuzo ya Jimmy Murphy ambayo hupewa Mchezaji Bora wa Mwaka toka Chuo cha Soka cha Man United.
Lakini Msimu uliofuatia, Macheda akaanza kuzongwa na Majeruhi ya mara kwa mara na maendeleo yake kuathirika.
Misimu iliyofuatia, Macheda akawa anacheza nje ya Man United kwa Mkopo kwenye Klabu za Sampdoria, Queens Park Rangers, VfB Stuttgart, Doncaster Rovers na Birmingham City, ambako alifunga Bao 10 katika Mechi zake 18.

waliotembelea blog