Wednesday, October 23, 2013



Msafara wa Magari ambao moja wapo (la mbele) likiwa limebeba jeneza lenye mwili wa marehemu Julius Nyaisanga ukiingia kwenye viwanja vya leaders muda huu kwaajili ya wakazi wa jiji la Dar kuweza kutoa heshima zao za mwisho kwa Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga kabla ya Kusafirisha Kwao Tarime Mkoani Mara




Baadhi ya Ndugu, Jamaa na marafiki wakibeba jeneza lenye Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga Kwaajili ya kupeleka sehemu husika tayari kwa kutoa heshima za mwisho kwa wakazi wa jiji la Dar waliofika katika viwanja vya leaders muda huu


Sehemu Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga litakapowekwa kwaajili ya wakazi wa jiji la dar kuweza kutoa heshima zao za mwisho kabla ya kusafirishwa kwenda Tarime Mkoani Mara




Baadhi ya wakazi wa jiji la dar waliojitokeza katika viwanja vya leaders muda huu






Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar wakisubiria Kutoa Heshima zao za Mwisho kwa Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga Kabla haujasafirishwa kupelekwa Kwao Tarime Mkoani Mara.

Hii stage bado ikiwa haijakamilika ikiwa bado kwenye kutengenezwa (Underconstruction) ni kati stage za kisasa ambayo itaonekana siku hiyo ya Serengeti Fiesta 2013 katika viwanja vya Leaders Club Jumamosi 26 Oktoba 2013 kwa kiingilio cha shilingi 10,000/= Tz kama ukikata tiketi yako mapema na mlangoni utalipa shilingi 15,000/= TZ huku ukipata nafasi ya kuwashuhudia wasanii wakimataifa zaidi ya mmoja ikiwa ni tofauti na Fiesta zote zilizopita, wasanii wakimataifa wannne kwa wakati mmoja hapa namzungumzia Iyanya, Davido, Alaine na Mohombi huku wakipigwa tafu na wasanii wakali kutoka nchini Tanzania. Stage inahitaji siku 10 mpaka kukamilika, kuna vitu vingi vya kustaajabisha kuhusiana na stage hii ni stage tofauti ni kubwa sana ambayo ina njia inayomfanya msanii atembee katikati akiwa amezungukwa na mashabiki kulia na kushoto kwake ndo maana Fiesta ya mwaka 2013 Ni Noma Saana!! Twenzetu — Usikose.
Hii ni nyumba ambayo itakuwa backstage ambayo itakuwa na bar na makochi comfortable ambayo yatatumiwa na watu watakao kuwepo katika eneo hilo wakiwemo wasanii huku wakisubiri kwenda kutoa burudani kwa mashabiki wa Serengeti Fiesta -- Noma Saana!! TWENZETU 

waliotembelea blog