Friday, July 5, 2013




Leo ni siku ya kimataifa ya kupambana na dawa za kulevya na biashara haramu ya dawa hizo. Umoja wa Mataifa umeitenga siku hii kuuhimiza ulimwengu kupambana na janga hili ambalo linaathiri hasa vijana kote duniani.





 Ni jukumu la kila mmoja kupambana na dawa
Bado kiwango cha matumizi ya dawa kama vile Heroin, cocaine na amphetamine hakijashuka lakini mtindo huu wa kuwepo kwa aina mpya za dawa za kulevya unatia wasiwasi.
Takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya watu walioambukizwa virusi vya HIV kupitia kujidunga sindano miongoni mwa waraibu wa dawa za kulevya ilikuwa milioni 1.6 mwaka 2011.
Papa Francis
Wachambuzi wanasema kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis ameongeza nguvu zaidi katika kushughulikia kashfa zilizoigubika benki ya Vatican kwa kumuondoa viongozi wa juu wa tasisi hiyo.
Paolo Cipriani na Massimo Tulli, mkurugenzi na naibu wake katika benki hiyo ya Vatikan walitoa rasmi barua za kujiuzulu kwao jumatatu iliyopita kwa maslahi ya taasisi hiyo na makao makuu ya kanisa hilo kwa ujumla. Rais wa benki ya Vatican Ernst von Freyberg, amepokea maamuzi hayo kwa ili kufanikisha upatikanaji wa viongozi wapya kwa lengo kuifanya benki hiyo kukidhi vigezo vya kimataifa dhidi ya uwekezaji wa fedha haramu.
Wataalamu wa masuala ya kidini na mahakama wamesema makao makuu ya kanisa Katoliki Vatican yamelazimika kuwaondoa maafisa wawili ambao walinusurika katika sakata lililomuondoa mkuu wa zamani wa benki hiyo, Ettore Gott Tedeschi, alishutumiwa kwa uongozi duni lakini pia kugubikwa na ripoti ya uwekezaji wa fedha haramu.


Hatua muhimu ya Vatican
waumini wakihudhuria misa iliyoongozwa na Papa Francis
  

Kwa mujibu wa mtaalamu, Fionrena Sarzanini kufukuzwa kwao ni hatua muhimu kwa Vatican kwa kuwa viongozi hao waliojiuzulu Cipriani na Tuli wapo katika orodha ya watu wanaofuatiliwa na tume ya waendesha mashitaka ya Roma iliyoundwa mwaka 2010 kwa ajili ya kuchunguza madai ya fedha haramu.
Fiorenza amesema uchunguzi huo uliopangwa kumalizika katika kipindi cha siku chache zijazo ungalipenda kuona wakishitakiwa kutokana na shutuma za kuruhusu vitendo haramu kufanyika. Mbali na hayo mkurugenzi huyo na naibu wake waliojizulu hivi karibuni wanahusishwa pia kuwa na uhusiano wa karibu na Nunzio Scarano, ambae amefanya kazi kama muhasibu mwandamizi wa benki ya Vatican ambae alikamatwa ijumaa iliyopita kwa tuhuma za njama za kusafirisha fedha haramu kutoka Uswis na kuziingiza nchini Italia.
Mtaalamu mwingine wa masuala ya kidini Marco Politi amesema pamoja na kuwepo kwa minong'ono kwamba makaoa makuu ya kanisa katoliki yanataka kuachana na taasisi hiyo kabisa lakini Papa Francis anaonekana si mwenye nia ya kufanya hivyo kutokana na umuhimu wa ke kwa utendaji wa majukumu ya kanisa.
Kutokana na mfululizo wa taarifa za vyombo vya habari vya Italia kuhusu kuwepo kwa akaunti ambazo wamiliki wake hawajulikani zinazotumiwa na wafanya uhalifu wa kupanga na wanaosafarisha fedha kwa njia za haramu taarifa nyingi zaidi zinatarajiwa kuwekwa hadharani kuhusu utendaji wa benki hiyo.


 Kipre (katikati) wakati akipokea tuzo yake usiku huu. Kushoto ni Waziri Dk Fenella na kulia Mkurugenzi wa masoko wa Vodacom, Kevin Twisa.


SC, Kevin Patrick Yondan ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2012/2013 na kuzawadiwa donge nono la Sh. Milioni 5.
Hata hivyo, katika hafla ya kutoa zawadi za washindi wa Ligi Kuu msimu uliopita kutoa wadhamini, Vodacom Tanzania zilizofanyika katika hoteli ya Double Tree, Masaki, Dar es Salaam, usiku huu, Yondan hakuwepo na tuzo yake alipokelewa na Ofisa Habari wa klabu hiyo, Baraka Kizuguto, kutoka kwa mgeni rasmi, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara.
Yondan ambaye alikuwa katika msimu wake wa kwanza Yanga SC, yuko kwenye kambi ya timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayojiandaa na mchezo dhidi ya Uganda Julai 13, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kipa chipukizi wa Tanzania Prisons FC ya Mbeya, David Burhan alishinda tuzo ya kipa bora wa Ligi Kuu na kupewa Sh. Milioni 5, wakati mfungaji bora, Kipre Herman Tchetche raia wa Ivory Coast  wa Azam FC alipewa Milioni 5 pia na Fully Maganga wa JKT Mgambo alipewa tuzo ya mchezaji mwenye nidhamu na kuzawadiwa Milioni 5.
Kocha mpya wa Simba, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibadeni’ ameshinda tuzo ya kocha bora kwa kazi nzuri aliyoifanya akiwa na Kagera Sugar msimu uliopita na kuzawadiwa Milioni 7.5 sawa na refa bora, Simon Mbelwa.
Yanga SC pamoja na kuzawadiwa Sh. Milioni 70 za kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu, waliongezewa Milioni 15 kwa kuwa timu yenye nidhamu zaidi kwenye ligi hiyo msimu uliopita, hivyo kuondoka na jumla ya kiasi cha Sh. Milioni 85.
Azam FC washindi wa pili kwa msimu wa pili mfululizo, walizawadiwa Sh. Milioni 35, Simba SC washindi wa tatu Milioni 25 na Kagera Sugar washindi wa nne walipewa Milioni 20.
Kwa upande wa zawadi za wachezaji wa timu za vijana za klabu za Ligi Kuu, Hamisi Saleh (JKT Ojoro), Abdulrahman Mussa (Ruvu Shooting), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Chande Magoja (Mgambo JKT), Tonny Kavishe (Mgambo JKT) na Rajab Zahir (Mtibwa Sugar), wote wamezawadiwa Sh. Milioni 1 kila mmoja.
Zawadi za wachezaji wa timu za vijana, walizozawadiwa kwa kuzichezea mechi nyingi timu zao za wakubwa katika Ligi Kuu, zimetoka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Rajab Zahir amesaini Yanga SC na tayari amejiunga nayo.
Gari la kubeba maiti likiwasili katika eneo la Mvezo Resort kuchukua mabaki ya miili ya watoto watatu wa Nelson Mandela iliyokuwa imezikwa kinyemela katika eneo hilo na mjukuu wa kiongozi huyo, Mandela.
Kwa ufupi
  • Hilo ni kosa na ni kinyume cha sheria za nchi. Maeneo ya makaburi yanalindwa na sheria hivyo ukienda kuchimbua mabaki ya marehemu pasipo kibali kinachokubalika kisheria kufanya hivyo ni matatizo na ndicho kilichotokea kwa sababu sheria hazikufuatwa (Profesa Gutto.)

Hatua hiyo inatokana na uamuzi wa Mahakama wa kuamuru miili ya watoto wake watatu iliyohamishiwa Mvezo, ifukuliwe na kwenda kuzikwa tena Qunu
Pretoria. Vita ya wapi atakapozikwa  Rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela imefikia tamati na sasa ni rasmi kwamba atazikwa Qunu uamuzi ambao umeacha ufa na uhasama mkubwa katika familia ya kiongozi huyo.
Jana, mabaki ya miili ya watoto watatu wa Mandela ambao ni marehemu ilitarajiwa kuzikwa upya katika eneo la Qunu, yakiwa ni mazishi ya mara ya tatu tangu walipofariki dunia katika vipindi tofauti, ukiwa ni utekelezaji wa amri ya Mahakama Kuu ya Eastern Cape.
Uamuzi huo ulimaanisha kushindwa kwa mjukuu wa Mandela, Mandla ambaye jana katika mkutano wake na waandishi wa habari alisema: “Sikusudii kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama,” lakini akahusisha ugomvi katika familia ya babu yake kwamba ni vita ya fedha na mali za Mandela.
Mabaki hayo ni ya mtoto wa kwanza wa kiume wa kiongozi huyo, Makgato aliyefariki dunia 2005, binti yake wa kwanza Makaziwe (mkubwa) ambaye alifariki akiwa mchanga mwaka 1948 na mtoto wake wa pili wa kiume, Madiba Thembekile aliyefariki katika ajali ya gari 1969.
Mahakama Kuu ya Eastern Cape ilitoa uamuzi uliowapa ushindi wanafamilia 16 wa Mandela ambao walifungua madai wakiongozwa na shangazi yake Mandla, Makaziwe.
Jaji Lusindiso Pakade katika hukumu yake, mbali na kutoa amri hiyo alitaja vitendo vya Mandla kuwa ni vya aibu visivyo vya kibinadamu hivyo kutoa amri ya kufukuliwa miili hiyo na kisha kurejeshwa Qunu. Mabaki hayo yalihamishwa kutoka kijiji cha Mvezo ambako yalizikwa mara ya pili kwa kificho miaka miwili iliyopita na mjukuu mkubwa wa Mandela, Mandla ambaye pia ni kiongozi wa kimila katika kijiji hicho.
Kazi ya kufukua makaburi ya watoto wa Mandela katika eneo la Mvezo ilifanyika hadi juzi usiku chini ya ulinzi wa polisi baada ya madalali wa mahakama kutumia sururu kuvunja lango (geti) kuu la kuingia katika makazi ya Mandla.
Kwa mujibu wa msemaji wa polisi wa eneo hilo, Luteni Kanali Mzukisi Fatyela, uchimbuaji wa makaburi ulifanywa na wataalamu wa Kituo cha Afya cha Mthatha na baadaye kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha kituo hicho juzi usiku na jana asubuhi mabaki ya marehemu hao yalifanyiwa uchunguzi wa kimaabara kabla ya kupelekwa Qunu kwa maziko.
Madaraka au fedha?
Makaziwe (60) ambaye ni binti mkubwa  wa Mandela na wenzake 15 kutoka katika familia hiyo, walifungua madai wakitaka kurejeshwa kwa mabaki ya miili hiyo Qunu wakisema Mandla aliyahamisha bila makubaliano ya familia. Mandla katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika Mvezo jana alisema ugomvi uliopo ni wa kimasilahi na kwamba familia inawania fedha za babu yake.
Alisema chimbuko la kuandamwa linatokana na msimamo wake wa kukataa kuondolewa katika bodi ya ya mfuko wa Mandela baadhi ya watu wakiwamo Wakili George Bizos na Waziri wa Makazi Tokyo Sexwale. “Sasa wameamua kunilenga mimi kama mlengwa dhaifu.”
Kabla ya familia kuamua kufungua kesi Juni 28, mwaka huu kiliitishwa kikao cha familia na Mandla alihojiwa na kutakiwa arejeshe mabaki ya miili hiyo Qunu lakini hakukubali na badala yake alitoka na kuacha kikao kikiendelea, hatua ambayo ilitafsiriwa kuwa ni kudharau familia hiyo.
Mvutano baina ya Mandla na shangazi yake Makaziwe anayewaongoza wanafamilia wengine unatafsiriwa na baadhi ya watu kwamba ni vita ya kuwania madaraka na fedha ikiwa Mzee Mandela atafariki dunia. Juzi, Msemaji Mkuu wa chama tawala cha ANC, Jackson Mthembu alisema chama hicho hakiwezi kuingilia masuala ya familia hiyo na kwamba kinaamini wana uwezo wa kuyamaliza... “Tunasikitishwa na hali hiyo, inaweza kuharibu sifa ya Mandela ndani na nje ya nchi, lakini tunaamini kwamba familia ina uwezo wa kuyamaliza.” Inaaminika kuwa Mandela mara kadhaa alisema akifa angependa azikwe Qunu ambako kuna makaburi ya familia yakiwamo ya watoto wake, hivyo Mandla aliyahamishia Mvezo ikiwa ni hatua ya kushawishi babu yake (Mandela) azikwe katika eneo hilo ambalo yeye ni kiongozi wake.
Uamuzi wa Mahakama una maana kwamba kaburi la Mandela litakapokuwa ni dhahiri ndipo makumbusho yake yatakapojengwa, hivyo kama atazikwa Qunu basi makumbusho hayo yatakuwa mikononi mwa familia yake na kama atazikwa Mvezo yatakuwa chini ya usimamizi wa Mandla ambaye ni dhahiri tayari amekosa nafasi hiyo.
Katika hati yake ya kiapo iliyowasilishwa mahakamani Mthatha, Mandla alidai kwamba anataka Mandela azikwe Mvezo kwani ndiko alikozaliwa na kwamba eneo hilo lina umuhimu wa kipekee katika historia ya babu yake.
Hivi sasa mjukuu huyo wa Mandela ambaye pia ni Mbunge wa Eastern Cape, ana hoteli kubwa ya kitalii yenye thamani ya mamilioni ya Dola za Marekani katika Kijiji cha Mvezo. Mwaka jana mmoja wa wanakijiji wa Mvezo alimfungulia mashtaka kwa tuhuma za kufukua makaburi kwa lengo la kujenga hoteli, lakini kesi hiyo hadi sasa haijasikilizwa.
Mgawanyiko wa familia
Ni dhahiri kwamba uamuzi wa juzi wa Mahakama umeiacha familia hiyo ya Mandela vipande kwani Mandla anakabiliwa na kesi nyingine mbili za jinai ambazo huenda zikafunguliwa siku chache zijazo katika Mahakama Kuu ya Western Cape baada ya uchunguzi wa kipolisi kukamilika.
Kesi hizo ni ile inayotokana na wanafamilia kutaka polisi wachunguze madai kwamba Mandla ‘alichezea’ makaburi hali ambayo inaweza kusababisha uharibifu wa mazingira kinyume cha sheria za Afrika Kusini na pili uchunguzi unaolenga kubaini iwapo taratibu za kisheria kwa maana ya afya zilifuatwa wakati wa uhamishaji wa mabaki ya marehemu hao miaka miwili iliyopita. Polisi kwa upande mmoja na kituo cha afya kwa upande mwingine katika eneo la Mthatha wamethibitisha kuanza kwa upelelezi huo dhidi ya Mandla na ikiwa wataridhika, watamfungulia mbunge huyo mashtaka ya jinai.
Mandla kwa upande wake jana aliweka bayana kuwa baadhi ya watu siyo wanafamilia wa Mandela akiwarushia vijembe shangazi zake kwa maelezo kuwa walishaolewa na kupoteza jina hilo kwani walikuwa wakitumia majina ya waume zao.
“Sasa inaonekana kwamba kila mtu anaweza kusema kwamba yeye ni Mandela kudai kuwa mwanafamilia ili kushiriki katika uamuzi wa kifamilia, wameamua kuzikimbia familia zao na kurukia katika ‘jahazi’ la Mandela.”
Afya ya Mandela
Mandela hivi sasa yu mahututi kwa siku ya 28 na amelazwa katika Hospitali ya Magonjwa ya Moyo, Medclinic iliyopo Pretoria akisumbuliwa na tatizo la figo kushindwa kufanya kazi na hali yake inaelezwa kuwa ni mbaya.
Kesi hiyo iliwezesha kufahamika kwa hali ya afya yake kwani kwa mara ya kwanza, ilithibitika kwamba anapumua kwa msaada wa mashine na hiyo ni kwa kujibu wa hati ya kiapo ya Makaziwe aliyoiwasilisha mahakamani katika kesi hiyo ambayo pia inasema: “Matarajio ya kifo chake yamejengwa kwenye msingi wa uhalisia.” Hati hiyo ya Juni 28, mwaka huu ambayo pia inawahusisha wanafamilia wengine akiwamo mke wa Mandela Graca Machel na mtalaka wa Mandela, Winnie inasema afya ya Mandela haitii matumaini huku ikiweka bayana kwamba hati ya kiapo ya daktari ingewasilishwa mahakamani kuthibitisha kwamba anasaidiwa na mashine kupumua.
Kadhalika, hati hiyo inathibitisha kwamba lengo la kesi hiyo ni kuhakikisha Mandela anazikwa katika eneo ambalo wanafamilia wengine wakiwamo watoto wake wa kuwazaa wamezikwa na kwamba wanafamilia wanaamini kwamba hatua ya kuhamishwa makaburi matatu kwenda Mvezo kulifanyika kwa masilahi ya kifedha.
Hata hivyo, Mandla katika kiapo chake mahakamani alipinga hoja kwamba Mandela yu mahututi na kwamba hata kama ni kweli suala hilo halina uhusiano na mahali atakapozikwa.
“Ugonjwa hauna uhusiano wowote na mahali atakapozikwa na hakuna maelekezo maalumu ya wasia ambayo yanasema Mandela anataka azikwe Qunu,” inasomeka sehemu ya kiapo cha Mandla.
Kwa mujibu wa sheria za Afrika Kusini zinazosimamia masuala ya mila na desturi, Mandla asingeweza kushinda kesi hiyo.
Gazeti la Mail & Guardian lilimnukuu Mtaalamu wa Sheria na Katiba nchini hapa Profesa Shadrack Gutto akisema kuwa sheria zinamtaka Mandla ambaye ni kiongozi wa kimila wa Mvezo, Eastern Cape kufuata taratibu kabla ya kuhamisha masalia hayo.
Profesa Gutto alisema ni dhahiri kwamba Mandla hakufuata sheria na taratibu hizo kwani akiwa kiongozi wa Mvezo, alipaswa kushauriana, kisha kukubaliana na kiongozi wa Qunu kabla ya kufanya alichokifanya.

waliotembelea blog