Monday, October 19, 2015

Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa Stars iliyoteuliwa hivi karibuni na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Bwana Farough Baghozah amekutana na waandishi wa habari katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam na kuitambulisha rasmi kamati hiyo.

Katika kamati hiyo ya Taifa ya Stars wapo Michael Wambura – Makamu Mwenyekiti, Bi Teddy Mapunda – Katibu, Wakili Imani Madega – Mweka Hazina, na wajumbe wengine ni Juma Pinto, Isaac Chanji, Salum Abdalla na Moses Katabaro.
Pia Mwenyekiti amechukua fursa hiyo kutangaza kamati ndogondogo na wajumbe wake kama ifuatavyo:

 1. Maandalizi ya timu, zikiwemo huduma kwa timu ya Taifa stars
 Mwenyekiti – Imani Madega
 Wajumbe – Msafiri Mgoyi,Teddy Mapunda.

2. Uhamasishaji wa mchezo (Michezo ijayo) na Masoko
 Mwenyekiti – Juma Pinto
 Wajumbe – Baraka Kizuguto, Mlamu Ng’ambi, Charles Hamka, Hashim  Lundenga, Maulid Kitenge, Shaffih Dauda, Salehe Ally, Peter Simon,  Edo Kumwembe na Mahmoud Zubeiry.

 3. Kamati ya Fedha
Mwenyekiti – Farough Baghozah
Wajumbe – Teddy Mapunda, Michael Wambura, Imani Madega,          Juma Pinto,        Isaac Chanji, Moses Katabaro na Edgar Masoud.

4. Mikakati ya ushindi – itakuwa na kamati ndogondogo na zitakuwa na wajumbe mbalimbali wakiwemo Mwenyekiti Farough Baghozah, Teddy Mapunda, Mohamed Nassoro, Philemon Ntahilaja, Isaac Kasanga, Cresencius Magori.

Pia kamati imetangaza kauli mbiu ya ushindi inayosema “NCHI YETU, TIMU YETU, TAIFA LETU, USHINDI WETU” itakayoanza kutumika kuanzia leo hii.  Pia Kamati imemteua Bi Teddy Mapunda kuwa msemaji mkuu wa kamati hiyo.

Timu inatarajia kuweka kambi Nje ya Nchi kwa takribani siku 12 ili kujiandaa na mechi dhidi ya Algeria Novemba 14 Dar es salaam, na Novemba 17 nchini Algeria.
Aidha Mwenyekiti alitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania wote warudishe imani kwa timu yao, wajitokeze kwa wingi kwenye mechi ijayo tarehe 14 November dhidi ya Algeria hapa nyumbani.  Pia akatoa wito kwa Watanzania Wote kuchangia timu kwa hali na mali (Madawa, Maji, vifaa vya michezo na kadhalika)…aliongeza ‘Mwenyekiti wa Kamati Bwana Farough Baghouzah.



9:45 PM - BATE Borisov vs Barcelona
9:45 PM - Bayer Leverkusen vs AS Roma
9:45 PM - Arsenal vs Bayern Munich
9:45 PM - Dinamo Zagreb vs Olympiakos
9:45 PM - Dynamo Kiev vs Chelsea
9:45 PM - FC Porto vs Maccabi Tel-Aviv
9:45 PM - Valencia vs KAA Gent
9:45 PM - Zenit St Peters burg vs Lyon


Bojan akichonga penati Bojan Krkic kaipatia bao la kuongoza Stoke mapema dakika ya 4 kwa mkwaju wa penati.

Kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast anayeichezea klabu ya Manchester City ya Uingereza Yaya Toure, October 19 kauli yake imeingia katika vyombo vya habari vingi, kutokana na wengi wao hawakuitarajia, Toure ambaye alijiunga na Man City mwaka 2010 akitokea klabu ya FC Barcelona ya Hispania amethibitisha kutokuwa na furaha  klabuni hapo.
Manchester City's Ivorian midfielder Yaya Toure celebrates after scoring his team's third goal and completing his hattrick during the English Premier League football match between Manchester City and Fulham at the Etihad Stadium in Manchester, northwest England, on March 22, 2014. AFP PHOTO / ANDREW YATES RESTRICTED TO EDITORIAL USE. No use with unauthorized audio, video, data, fixture lists, club/league logos or live services. Online in-match use limited to 45 images, no video emulation. No use in betting, games or single club/league/player publications. (Photo credit should read ANDREW YATES/AFP/Getty Images)
Toure ambaye toka awasili klabuni hapo akitokea FC Barcelona ya Hispania amefanikiwa kuisaidia Man City kutwaa mataji mawili ya Ligi Kuu Uingereza, Kombe la FA na Kombe la Capital One, amekiri kuwa licha ya kulipwa mshahara mkubwa na kutwaa mataji, amekuwa hana furaha klabuni hapo kutokana na vyombo vya habari vya Uingereza vimekuwa vikimsema.
2D827B3500000578-0-image-a-5_1445244027069
“Mara kadhaa nimekuwa sijisikii furaha, wakati najiunga na Man City mwaka 2010 nilisikia watu wakizungumza kuwa nakuja kuua mpira hapa na waandishi wa habari walikuwa wakizungumzia sana mshahara wangu mkubwa lakini nimekuwa na mchango mkubwa katika timu na kuisadia kushinda mataji”>>> Yaya Toure

Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali vya Habari katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakiwa Jijini Mwanza katika Semina ya siku tatu (Octoba 19 hadi 22) juu ya VYOMBO VYA HABARI NA UCHAGUZI iliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA.
Wanahabari watapata fursa ya Kujadili yale yanayoendelea katika kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Octoba 25 mwaka huu na nanma Vyombo vya Habari/ Waandishi wa Habari wanavyoripoti habari za Uchaguzi Mkuu kwa kuzingatia haki sawa kwa pande zote ikiwemo wagombea, wapiga kura huku suala la gender balance pia likizingatiwa.

Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali vya Habari katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakiwa Jijini Mwanza katika Semina ya siku tatu juu ya VYOMBO VYA HABARI NA UCHAGUZI iliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA.

Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali vya Habari katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakiwa Jijini Mwanza katika Semina ya siku tatu juu ya VYOMBO VYA HABARI NA UCHAGUZI iliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA.(P.T)

Majadiliano yakiendelea

Majadiliano yakiendelea

Beatrice Bandawe (Kushoto) ambae ni Mhariri wa Gazeti la Nipashe akiwa pamoja na Godfrida Jola (Kulia) ambae ni Afisa Programu TAMWA wakitoa ufafanuzi juu ya Semna kwa wanahabari inayofanyika Jijini Mwanza.

Leonida Kanyuma ambae ni Afisa Habari TAMWA akizungumza katika Semina kwa Wanahabari juu Vyombo vya Habari na Uchaguzi inayofanyika Jijini Mwanza.



Na Saleh Ally
INAWEZEKANA kabisa ikawa ni vigumu sana kwa watu wengi kuona ni miujiza kwa kampuni kubwa wanayoijua kusikia imefeli na mwisho inafungwa kabisa. Yote yanawezekana ndiyo maana maduka makubwa ya bidhaa maarufu kama Uchumi Supermarket, yamefilisika.

Biashara inahitaji nidhamu ya juu sana, inahitaji kuwasoma wateja ambao sawa na wamiliki, wanataka nini, kwa wakati gani lakini pia kusikiliza shida au kero zao.

Mimi siamini kama Kampuni ya DSTV imekuwa ikisikiliza kero za wateja wake hasa kwa Tanzania, wengi wanalia na wako wameanza kuweka chuki kabisa.

Wote wanaolia ni kuhusiana na bei, kwamba zimekuwa kubwa sana hadi kufikia kuona kama ni sehemu ya kuwakomoa. Wako wanaoamini DSTV hawawajali wazalendo zaidi ya kuangalia kile wanachoingiza.

Maoni mengi huenda tumekuwa tukiyapata kwa kuwa wengi ambao wamekuwa wakiyatuma ni watu wa michezo, wanajua Championi ndiyo makao makuu ya michezo kama utazungumzia magazeti ya michezo, kweli hapa ndiyo nyumbani.
 
RAIS JAKAYA KIKWETE AKIWA NA MMILIKI WA AZAM MEDIA, SAID SALIM BAKHRESA PAMOJA NA BAADHI YA WAFANYAKAZI WA AZAM TV SIKU YA UZINDUZI WAKE, MIEZI MICHACHE ILIYOPITA. TAYARI AZAM TV IMEKUWA GUMZO KUTOKANA NA UBORA WA KAZI YAKE LAKINI BEI AMBAZO WAZALENDO WENGI WANAWEZA KUZIMUDU.
Wapenda soka wengi hasa barani Afrika ni watu masikini, lakini mpira au soka ni zaidi ya kabila na wengine ni zaidi hata ya dini, wanaupenda hadi kufikia kiwango cha kuonekana kama wendawazimu.

Ndiyo starehe kuu na tulizo la moyo, kama ukitokea kuwaingizia kero, hamtaelewana milele. Ndiko hili suala linapokwenda, kwamba itafikia DSTV na Watanzania wapenda soka au michezo wasiwe na urafiki hata kidogo.

Hii inatokana na kilio cha malipo ya mwezi, hasa kwa wale wanaotaka kuangalia Ligi Kuu England. Ili mtu apate nafasi ya kuangalia michezo ya moja kwa moja ya ligi hiyo, basi lazima alipe takribani dola 100 (wakati mwingine ni zaidi ya Sh 200,000). Kwa Mtanzania wa kawaida hakika ni fedha nyingi sana.

DSTV wanafanya biashara, hili hakuna anayeweza kukataa lakini bado kuna kila sababu ya kuangalia mbinu za kibiashara na kuwapunguzia Watanzania kwa kuwa wanapenda soka.

Nina rafiki zaidi ya watatu ambao wameamua kuhamishia mapenzi yao Hispania. Wanaamini La Liga ni bora kuliko Premier League lakini imekosa matangazo ya kutosha. Wanaona DSTV sasa inaitumia EPL kama silaha ya kuwakandamiza wanyonge na inawezekana kupunguzwa kwa bei.
KING'AMUZI CHA DSTV...
Wanajua kuwa Afrika Kusini kuna unafuu mkubwa wa bei ukilinganisha na hapa nyumbani Tanzania. Wanaendelea kuamini La Liga ambayo sasa wanaweza kuipata kwenye ving’amuzi vya Azam TV tena ikichambuliwa kwa lugha ya Kiswahili, itakata kiu yao.

Nina rafiki ambao sasa wanaangalia Premier League kupitia mitandao ambayo mtu anaweka ‘bando’ yake ya intaneti na kuangalia moja kwa moja mechi hizo.

Hawa ni wale wanaoondoka taratibu katika himaya ya DSTV ambao wanaona haiwezekani lakini nawasisitizia kadiri siku zinavyosonga wanaotafuta njia mbadala watakuwa wengi na watazidi kuachana nayo.

Azam TV ambayo pamoja na gharama za uendeshaji kuwa kubwa kama DSTV wanavyosema, lakini imejitahidi kuwapa Watanzania karibu kila kitu ambacho wanatoa DSTV na huenda zaidi, lakini gharama ziko chini.

Hii inafanya Watanzania wazidi kuongeza mapenzi na upande wanaoona unawajali. Najua kuna gharama kubwa kupata uonyeshaji wa EPL lakini bado kuna njia zinaweza kutumika kuwasaidia Watanzania katika suala la gharama za malipo ya mwezi.

Mara zote, mtu anamjali anayemjali. Hata kama kweli wanafanya biashara, DSTV wanatakiwa kuonyesha wanawajali Watanzania. Wajiulize, siku Azam TV wakipata nafasi ya kuonyesha moja kwa moja mechi za EPL, wao itakuwaje?


 Mwenyekiti wa Kamati ya kuisaidia Taifa Stars, Farouk Baghouza amewaomba Watanzania kujitokeza na kuichangia kamati yake ili iweze kufanikisha lengo la kuisaidia Stars.

Akizungumza leo na waandishi wa habari, pamoja na kutangaza kamati kubwa na ndogondogo kwa ajili ya kuisaidia Stars, Farouk alisisitiza suala la Watanzania kujitolea.
“Mwenye maji, mwenye dawa tunakaribisha michango. Lengo ni kuisaidia timu, lakini lengo ni kuonyesha umoja na utaifa wetu.
“Taifa Stars inatuwakilisha Watanzania wote hata wasio wapenda soka, tafadhari tuungane pamoja katika kipindi hiki kuhakiksha tunaing’oa Algeria,” alisema.
Stars inakutana na Algeria Novemba 14 katika mechi ya kwanza iatakayochezwa jijini Dar es Salaam kabla ya kurudiana Novemba 17 nchini Algeria.
Mechi hiyo ni ya kuwania kucheza Kombe la Dunia nchini Urusi mwaka 2018.
Stars imepata nafasi hiyo baada ya kuing’oa Malawi kwa jumla ya mabao 2-1 ikiwa imeanza na ushindi wa mabao 2-0 jijini Dar es Salaam, ikapoteza 1-0 mjini Blantyre.
Algeria ndiyo timu bora kuliko zote Afrika, pia ndiyo timu ya Afrika iliyofanya vizuri zaidi katika michuano ya kwanza ya Kombe la Dunia nchini Brazil, mwaka jana.



MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA STARS, FAROUKH BAGHOZA AKIMSIKILIZA KATIBU WAKE, TEDDY MAPUNDA.
Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa Stars iliyoteuliwa hivi karibuni na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Bwana Farough Baghozah leo hii amekutana na waandishi wa habari katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam na kuitambulisha rasmi kamati hiyo.

Katika kamati hiyo ya Taifa ya Stars wapo Michael Wambura – Makamu Mwenyekiti, Bi Teddy Mapunda – Katibu, Wakili Imani Madega – Mweka Hazina, na wajumbe wengine ni Juma Pinto, Isaac Chanji, Salum Abdalla na Moses Katabaro.
Pia Mwenyekiti amechukua fursa hiyo kutangaza kamati ndogondogo na wajumbe wake kama ifuatavyo:
 1. Maandalizi ya timu, zikiwemo huduma kwa timu ya Taifa stars
 Mwenyekiti – Imani Madega
 Wajumbe – Msafiri Mgoyi,Teddy Mapunda.
SALEH ALLY NA EDO KUMWEMBE
2. Uhamasishaji wa mchezo (Michezo ijayo) na Masoko
 Mwenyekiti – Juma Pinto
 Wajumbe – Baraka Kizuguto, Mlamu Ng’ambi, Charles Hamka, Hashim  Lundenga, Maulid Kitenge, Shaffih Dauda, Salehe Ally, Peter Simon,  Edo Kumwembe na Mahmoud Zubeiry.
 
3. Kamati ya Fedha
Mwenyekiti – Farough Baghozah
Wajumbe – Teddy Mapunda, Michael Wambura, Imani Madega,          Juma Pinto,        Isaac Chanji, Moses Katabaro na Edgar Masoud.
4. Mikakati ya ushindi – itakuwa na kamati ndogondogo na zitakuwa na wajumbe mbalimbali wakiwemo Mwenyekiti Farough Baghozah, Teddy Mapunda, Mohamed Nassoro, Philemon Ntahilaja, Isaac Kasanga, Cresencius Magori.
Kamati ya kuisaidia Taifa Stars imetangaza kauli mbiu ya ushindi inayosema “NCHI YETU, TIMU YETU, TAIFA LETU, USHINDI WETU” itakayoanza kutumika kuanzia leo hii. 


Kamati hiyo chini ya uenyekiti wa Farouk Baghoza  imemteua Bi Teddy Mapunda kuwa msemaji mkuu wa kamati hiyo.
Timu inatarajia kuweka kambi Nje ya Nchi kwa takribani siku 12 ili kujiandaa na mechi dhidi ya Algeria Novemba 14 Dar es salaam, na Novemba 17 nchini Algeria.
Aidha, Mwenyekiti alitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania wote warudishe imani kwa timu yao, wajitokeze kwa wingi kwenye mechi ijayo tarehe 14 November dhidi ya Algeria hapa nyumbani.  

Pia akatoa wito kwa Watanzania Wote kuchangia timu kwa hali na mali (Madawa, Maji, vifaa vya michezo na kadhalika)…aliongeza ‘Mwenyekiti wa Kamati Bwana Farough Baghouzah.

Mwandishi wa Gazeti la Championi, Nicodemus Jonas wa pili kulia akiwa na vyeti alivyochukuwa kwa niaba ya Blog ya Salehjembe na Kampuni ya Global Publishers vilivyotolewa na Asasi ya Somi katika Tamasha la Majimaji Selebuka. Kulia ni Mkurugenzi Mwenza wa Asasi ya Somi, Prof. Julian Murchison, Dk Damas Ndumbaro- mkurugenzi mwenza wa Somi na Mkuu wa Jumba la Makumbusho mjini Songea, Balthazar Namusya.
Katika kule kilichoonekana Blogu ya Saleh Jembe ndiyo blog pendwa kwa michezo nchini, imetunukiwa cheti na Asasi ya Songea –Mississippi (Somi) kwa kutambua mchango wake katika Tamasha la Majimaji Selebuka 2015, lililohitimishwa juzi Jumamosi.

Tamasha hilo lililenga kudumisha uhusiano wa Jimbo la Songea na Mississippi ya nchini Marekani kiuchumi kwa kuwaninua wajasiriamali pamoja na kudumisha sekta ya michezo mkoani Ruvuma.
Akizungumza wakati wa kufunga tamasha hilo, kwenye Uwanja wa Makumbusho ya Mashujaa wa Vita vya Majimaji mjini Songea, Mkurugenzi Mwenza wa Somi, wakili Dk Damas Ndumbaro alisema: “Saleh Jembe blog ilikuwa bega kwa bega nasi, mwanzo mpaka mwisho wa tamasha hilo.
“Tunashukuru watu wengi wamehamasika na wamekuwa wakitufuatilia kupitia blogu hii, hivyo ni lazima tulipe fadhaira kwake.”
Tovuti na Global Pulishers, nayo ilitunukiwa cheti kama hicho kwa sapoti ya kuripoti matukio yote yaliyojili kwenye tamasha hilo, ambayo ni: Riadha, maonyesho ya ngoma za asili, maonyesho ya wajasiriamali, mbio za baiskeli pamoja na utalii wa ndani.



  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwasikiliza wananchi wa jimbo la Buchosa mapema walipokuwa wakishamgilia mara baada ya kupanda jukwaani na kuwasalimia,mkutano huo wa kampeni umefanyika mapema leo asubuhi katika kijiji cha Nyehunge wilayani Sengerema mkoani Mwanza.Pamoja na mvua kunyesha hapa hapa na pale katika maeneo hayo,Dkt Magufuli anatarajia kuhutubia mkutano mkubwa wa kampeni katika jimbo la Geita Vijjini katika kijiji cha Nkome.
  Wakazi wa jimbo la Buchosa wakishangilia jambo wakati Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi mbele yao kuomba kura za kutosha ifikapo Oktoba 25 kwenye uchaguzi mkuu
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa jimbo la Buchosa mapema leo asubuhi katika kijiji cha Nyehunge wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
 Wakazi wa jimbo la Buchosa wakishangilia jambo wakati Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi mbele yao kuomba kura za kutosha ifikapo Oktoba 25 kwenye uchaguzi mkuu
Wakazi wa jimbo la Buchosa wakiwa wamekusanyika kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli uliofanyika mapema leo asubuhi kijiji cha Nyehunge wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli akimnadi Mgmbea Ubunge jimbo la Buchosa,Dkt Charles Tizeba mapema leo asubuhi kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Nyehunge wilayani Sengerema mkoani Mwanza
 Magufuli akiwasili kwenye mkutano wa kampeni,Nyehunge jimbo la Buchosa mapema leo mchana huku akishangiliwa .
 Dkt Magufuli akiwasalimia wananchi wa Nyehunge jimbo la Buchoasa kwenye kutano wa kampeni wilayani Sengerema.
.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Kamanga mapema leo asubuhi aliposhuka akitokea mkoani Mwanza kuelekea wilayani Sengerema kuendelea na Mikutano yake ya kampeni
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa kijiji cha Lwezera mara baada ya kupokelewa na viongozi mbalimali wa chama cha CCM mkoa wa Geita,akielekea jimbo la Geita Vijijini kuhutubia wananchi kwenye kutano wa kampeni
 Wanamsikiliza Mgombea Urais wa CCM alipokuwa akimwaga sera zake kwa wakazi wa kijiji cha Lwezera,Geita vijijini


Uwe Rosler
Uwe Rosler Aliiongoza Leeds karibu mechi 11 za Championship msimu huu 2015-2016Rosler aliteuliwa mwanzoni mwa msimu huu kuiongoza Leeds
Steve Evans anajiandaa kuendesha timu hiyo baada ya Rosler kutimuliwa


Arsenal hawana njia yoyote ila kuwashambulia Bayern Munich Uwanjani Emirates Jumanne Usiku kwenye Mechi ya Kundi F la UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, kwa mujibu wa Meneja wao Arsene Wenger.
Arsenal wamechapwa Mechi zao zote mbili za Kundi F kutoka kwa Dinamo Zagreb na Olympiakos na wapo mkiani mwa Kundi hilo na Mechi zao 2 zinazofuata ni dhidi ya Mabingwa wa Germany Bayern Munich.Ikiwa Arsenal watafungwa na Bayern basi wapo hatarini ya kutofuzu kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL kwa mara ya kwanza katika Miaka 16.
Hii si Mechi rahisi kwa Arsenal kwani Bayern watatinga Jijini London Uwanjani Emirates wakiwa na wimbi la ushindi la Mechi 12 mfululizo.

Lakini hilo halimtishi Wenger ambae amesema: “Sasa tupo katika hali nzuri na mkazo kwetu ni Mechi hii ya Jumanne.”
Arsenal hivi sasa wapo kwenye wimbi zuri la ushindi kwenye Ligi Kuu England ambalo limewapaisha hadi Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 2 tu nyuma ya Vinara Man City.

Mara ya mwisho kwa Arsenal na Bayern kukutana kwenye UCL ni Mwaka Jana walipotoka 1-1 huko Allianz Arena Jijini Munich na Bayern kushinda 2-0 Uwanjani Emirates katika Mechi yao ya kwanza.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE
MAKUNDI
Jumanne Oktoba 20
KUNDI E

BATE Borislov v Barcelona
Bayer Leverkusen v AS Roma

KUNDI F
Arsenal v Bayern Munich
Dinamo Zagreb v Olympiakos

KUNDI G
Dynamo Kiev v Chelsea
FC Porto v Maccabi Tel Aviv

KUNDI H
Valencia v KAA Gent
Zenit Saint Petersburg v Lyon

Jumatano Oktoba 21
KUNDI A

Malmö FF v Shakhtar Donetsk
Paris St Germaine v Real Madrid

KUNDI B

CSKA v Man United
VfL Wolfsburg v PSV

KUNDI C

Atletico Madrid v FC Astana
Galatasaray v Benfica

KUNDI D

Juventus v Borussia Mönchengladbach 

Man City v Sevilla



MSIMAMO ULIVYO: Barclays Premier League
PosLogo &TeamPWDLGDPts
1Manchester CityManchester City97021621
2ArsenalArsenal9612919
3Manchester UnitedManchester United9612719
4West Ham UnitedWest Ham United9522817
5Leicester CityLeicester City9441216
6Crystal PalaceCrystal Palace9504215
7Tottenham HotspurTottenham Hotspur9351414
8SouthamptonSouthampton9342313
9EvertonEverton9342113
10LiverpoolLiverpool9342-213
11ChelseaChelsea9324-311
12West Bromwich AlbionWest Bromwich Albion9324-411
13Swansea CitySwansea City8242010
14WatfordWatford9243-410
15Stoke CityStoke City8233-29
16Norwich CityNorwich City9234-69
17BournemouthBournemouth9225-68
18Newcastle UnitedNewcastle United9135-76
19Aston VillaAston Villa9117-74
20SunderlandSunderland9036-113

waliotembelea blog