Monday, July 27, 2015



 Katibu wa Mipango na Mikakati wa Chama cha ACT-Wazalendo, Habibu Mchange (kushoto), akimkabidhi kadi ya chama hicho, aliyekuwa mbunge wa Viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Iringa mjini, Chiku Abwao baada ya kuhamia rasmi ACT-Wazalendo Dar es Salaam leo mchana.
 Mbunge Chiku Abwao (kulia), akionesha kadi ya chama cha ACT-Wazalendo baada ya kukabidhiwa.
  Mbunge Chiku Abwao (kulia), akizungumza na wanahabari baada ya kukabidhiwa kadi ya chama cha ACT-Wazalendo.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo
MITAZAMO MBALI MBALI JUKWAANI Tuachane uroho wa madaraka kwa kuwadanga na kuwahadaa wananchi. Leo tunawaonyesha wezi na kuwafikisha mahabusu halafu kesho tunakula nao na kuwasifia kwa kazi zao. Wengine wanasema ety ana wafuasi wengi, hivi tunataka kushika madaraka au tunataka kuwa na serikali bora itakayolinda na kutetea maslahi ya wananchi??? Lusifa ana wafuasi wengi sana hapa duniani hata kufikia hatua ya kumjaribu Mungu lakini kamwe Mungu hakuwai kumfikiria kumrejesha Lucifa kuwa malaika wa sifa kama alivyokuwa awali, Nitakuwa wa mwisho kuunga mkono usanii na udanganyifu wa kisiasa unaotaka kutokea ndani ya nchi yangu. By Mesaya #‎HABARI‬ LOWASSA AKARIBISHWA RASMI UKAWA Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) umesema umemkaribisha rasmi Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Lowassa kujiunga nao katika harakati za kuking'oa Chama cha Mapinduzi (CCM). Mbatia: Tunamkaribisha rasmi aliyekuwa waziri mkuu mstaafu, Edward Ngoyaye Lowasa kujiunga na UKAWA, ni mchapakazi makini na mtekelezaji wa majukumu, UKAWA ndio tumaini la Tanzania, tusikubali kunyamaza pale ambapo sauti zetu zinazimwa kwa lazima. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki UKAWA, UKAWA ndio tumaini letu. Mbatia: Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu, Mwanzoni wa mwezi wa nane(wiki ijayo) tutamtangaza mgombea wetu kwa mbwembwe, tumeshapiga hatua ambayo ni nzuri Lipumba: "Lowasa alishasema yeyote mwenye ushahidi aulete..hapa tumekaribisha Watanzania wote kujiunga. Kuhusu CUF kusuasua UKAWA: Chama chetu hakijasusua bali kilikuwa kinafuata taratibu za chama na mkutano mkuu umebariki, yeyote atakaechaguliwa kupitia UKAWA, mimi nitamuunga mkono, chama kimebariki maamuzi haya, unapozungumza na mwenyekiti wa CUF basi ndio unazungumza na CUF.

Copy and WIN : http://ow.ly/KNICZ

 

LowassaNi wiki ya mtikisiko. Hivi ndiyo unavyoweza kuelezea hali itakavyokuwa nchini kutokana na matukio makubwa ya kisiasa yanayotazamiwa kutokea ndani ya wiki inayoanza leo ambayo yanaweza kubadili mwelekeo wa siasa za Tanzania.
Hali hiyo inatokana na vuguvugu la kisiasa linalohusisha viongozi wenye ushawishi kuhama vyama vyao vya siasa na kutimkia kwenye vyama vingine, ikiwa ni siku chache kabla ya kufanyika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, mwaka huu.
Ni wiki ambayo itapambwa na matokeo ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi wa CUF kilichofanyika jana mjini Zanzibar kuhusu mustakabali wake ndani ya Ukawa, ikizingatiwa kuwa hivi karibuni chama hicho kiliamua kujiweka kando ya vikao vya umoja huo hadi vikao vya juu viamue. 
Hata hivyo, habari ambazo gazeti hili limezipata zinasema kuwa uwezekano wa chama hicho kujitoa ndani ya Ukawa ulikuwa mdogo kutokana na kuogopa hasira za wananchi wenye matumaini na umoja huo.
Aidha, kulikuwa na taarifa kuwa kikao cha jana kilikuwa kinaangalia jinsi watakavyoshiriki katika umoja huo na kwamba kulikuwa na matumaini makubwa.
Vile vile, hii ni wiki ambayo kura za maoni zinazoendelea katika vyama vikubwa vya siasa, kuonyesha baadhi ya vigogo wakiangushwa na kujaribu kutafuta upenyo wa madaraka katika vyama vingine.
Pia, ni wiki ambayo chama kikuu cha upinzani, Chadema kimeamua kusogeza mbele tarehe za kuchukua na kurejesha fomu za kuomba kuteuliwa kugombea urais kutoka jana hadi Ijumaa, katika kile kinachotazamwa kama kusubiri mchakato wa kumpata mgombea urais.
Kana kwamba hiyo haitoshi, hii ni wiki ambayo minong’ono ya waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa ambaye jina lake limekatwa katika orodha ya wasaka urais wa CCM anaweza kuhamia Chadema.
Tayari baadhi ya viashiria vya hali hiyo vimeanza kuonekana ambapo wiki iliyopita wabunge wawili wa chama tawala cha CCM, James Lembeli na Ester Bulaya waliachana na chama hicho na kujiunga na Chadema huku chama hicho cha upinzani kikitamba kujiandaa kuwapokea vigogo wengine zaidi.

Kiashiria kingine cha mtikisiko ni hatua ya madiwani 18 wa CCM wilayani Monduli na wengine 10 wa UDP na CCM Bariadi kuhamia Chadema.
Lakini pia wapo wabunge na madiwani wanaohama Chadema kwenda chama cha ACT-Wazalendo.

Vuguvugu hilo la kisiasa limekolezwa na kauli za wanasiasa wawili vijana kwa nyakati tofauti, Godbless Lema na Zitto Kabwe kuwa wiki hii itakuwa ya mshikemshike kutokana na mambo yaliyopangwa kufanyika.






mail.google.comn
Mwanariadha wa Polisi Tanzania Fabian Nelson (wa pili) akipambana na wanariadha wengine katika mbio za kilomita 10000 katika uwanja wa Mavuso nchini Swaziland wakati wa Michezo ya majeshi ya polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika(SARPCCO) yanayoendelea nchini Swaziland.Fabian Nelson alishinda medali ya Fedha baada ya kushika nafasi ya pili katika mbio hizo.
(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi, Swaziland).
t
Mwanariadha wa Polisi Tanzania Fabian Nelson (kushoto) akishangilia na wanariadha wenzake kutoka Zimbabwer baada ya  kuvalishwa medali ya fedha baada ya kushika nafasi ya pili  katika mbio za kilomita 10000 katika uwanja wa Mavuso nchini Swaziland wakati wa Michezo ya majeshi ya polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika(SARPCCO) inayoendelea nchini Swaziland.nafasi ya kwanza na ya tatu ilikwenda kwa wanariadha kutoka Jeshi la Polisi la Zimbabwe.
IMG_5796
Baraka Kizuguto msemaji wa TFF
Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na kati maarufu kama CECAFA limetangaza mabadiliko ya muda wa kuanza kwa mechi za robo fainali ya michuano hiyo.. CECAFA imetangaza mabadiliko hayo kupitia kwa msemaji wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) Baraka Kizuguto.
cecafa
Mabadiliko yaliotangazwa hapo ni ya mechi za robo fainali, mchezo wa kwanza utapigwa saa 7:45 ambapo itakuwa mechi kati ya APR ya Rwanda dhidi ya Al Khartoum ya Sudan na mchezo wa pili utapigwa saa 9:45 utakutanisha timu ya  Gor Mahia ya Kenya dhidi ya Malakia ya Sudan Kusini, michezo hiyo itapigwa July 28.
KMKM-vs-Gor-Mahia-1
Kikosi cha Gor Mahia ya Kenya
July 29 itapigwa michezo miwili wa kwanza utakuwa mchezo kati ya KCCA ya Uganda dhidi ya AL Shandy ya Sudan saa 7:45 na mchezo wa pili ni kati Azam FC  dhidi ya Yanga saa 9:45 michezo yote itapigwa katika Uwanja wa Taifa Dar Es Salaam na hakutakuwa na dakika 30 za nyongeza kama timu zitatoka suluhu bali zitapigiana mikwaju ya penati.
NUTTALL-THINK
Kocha wa Gor Mahia Frank Nutall
Sambamba na mabadiliko hayo CECAFA pia imewaandikia barua ya kuwapa onyo klabu ya Gor Mahia ya Kenya na kocha wao Frank Nutall kwa utovu wa nidhamu kwa kutumia mlango ambao hawakupaswa kutumia wakati wa kuingia na kutoka vyumbani.
accrareport_didier-drogba-retires-from-international-football
Mshambuliaji wa kimataifa wa Ivory Coast Didier Drogba ambaye pia amewahi kuitumikia klabu ya Chelsea ya Uingereza kwa miaka kadhaa sasa ameamua kuendeleza maisha yake ya soka Canada na ataanza kuonekana katika Ligi Kuu ya Marekani MLS.
DidiFinale12
Taarifa zimethibitisha kuwa Drogba amekubaliana na klabu Montreal Impact  na atajiunga na timu hiyo kwa mkataba wa miezi 18, Drogba amekuwa akiwindwa na timu zinazoshiriki Ligi Kuu Marekani toka mwaka 2012 na alikataa mshahara wa dola milioni 7.5 kwa mwaka na kutimkia China.
Didier Drogba celebrates Chelsea goal in FA Cup semi final win over Tottenham 2012
Rais wa klabu ya Montreal Impact Joey Saputo amethibitisha Drogba kujiunga na kikosi chao.
“Ni heshima kumkaribisha Drogba katika klabu ya Montreal Impact, toka mazungumzo yetu ya kwanza nazungumza nae, nilijisikia kwamba kiukweli alitaka kuichezea Montreal”>>>Joey Saputo 
CK8CB_rWgAAQBAz
Picha ya July 27 Drogba alipo kutana na Neymer Ibiza Airport


Wojciech Szczesny akiwa na Scarf ya Klabu ya As Roma baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Leonardo da Vinci International


.Internazionale hawakupata kitu katika mtanange huu hii leo, Wakinyukwa bao 3-0 na Real.
BAO za Real Madrid zilifungwa na
Jese dakika ya 29 kipindi cha kwanza na bao mbili kipindi cha pili zilizofungwa na Raphaël Varane dakika ya 56 na lile la James Rodríguez dakika ya 88'
Cristiano Ronaldo kwenye Patashika
Dakika ya 46 Real Madrid waliwapumzisha, Cristiano Ronaldo, Keylor Navas, Gareth Bale, Pepe na Sergio Ramos na kuwaingizwa Denis Cheryshev, Bale, Lucas Vázquez, Nacho Fernandez na Raphael Varane.
Raphaël Varane, katika Dakika ya 56, aliwapa Real Bao lao la pili alipomalizia Mpira safi ndani ya Boksi na Bao la 3 kufungwa kwa Frikiki kali ya James Rodriguez.
Isco na JeisonJeisco na Gareth BaleJuan Jesus akiwekea kigingi na RonaldoMarcelo Mateo na Denis Kovacic www.bukobasports.comRafael Benitez kwenye Ukodak

1285139-27695451-1600-900
Kocha wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho anajulikana kwa majigambo, kujisifia lakini pia anapenda kitu kizuri kiwe kwake.
Kama utakua unakumbuka vizuri Mourinho ni kocha anayependa mfumo wa kujihami kwa lugha za mpira wanaita kupaki Bus yaani ni mfumo ambao timu inashambulia kwa kushtukiza na kujihami kwa kiasi kikubwa… Lakini cha kushangaza aliwahi kukutana na timu yenye tabia zaidi ya zake alilalamika.
1358693-29167764-1600-900
Sasa basi Mourinho amerudi tena kwenye headlines, kwa kuanza kejeli zake tena kwa kusema kuwa timu pinzani zina jaribu kununua mataji. Mourinho ameyasema hayo kufuatia klabu vya Manchester United kufanya usajili mkubwa msimu huu, kwa wachezaji kama Matteo Darmian, Memphis DepayBastian Schweinsteiger na Morgan Schneiderlin vivo hivyo kwa upande wa Man City na Klabu ya Liverpool ambao nao wamefanya usajili kwa kutumia fedha nyingi.
jose_mourinho_22
Licha ya kukiri kuwa hata mwaka 2003 mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich alikuwa ananunua mataji klabuni hapo baada ya kuanza kununua wachezaji kwa gharama ya juu, kauli ya Mourinho inatafsirika kama hapendezwi na usajili wanaofanya timu pinzani licha ya kuwa soka limebadilika wamiliki wananunua wachezaji kwa gharama za juu.
MANCHESTER, ENGLAND - OCTOBER 26:  Chelsea Manager Jose Mourinho shouts orders during the Barclays Premier League match between Manchester United and Chelsea at Old Trafford on October 26, 2014 in Manchester, England.  (Photo by Alex Livesey/Getty Images)



Mshambuliaji wa Yanga, Amisi Tambwe akishangilia kwa staili ya aina yake baada ya kuifungia timu yake bao pekee katika mchezo wa Kombe la Kagame dhidi ya Khartoum ya Sudan uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kushoto ni mshambuliaji wa timu hiyo, Malimi Busungu. (Picha na Francis Dande)

Msuva akimiliki mpira.

Malimi Busungu akichuana na beki wa Khartoum ya Sudan.

Golikipa wa Khartoum ya Sudan, Mohamed Ibrahimakiokoa moja ya hatari langoni mwake.

Simon Msuva akichuana na beki wa Khartoum.

Mshambuliaji wa timu ya Yanga, Simon Msuva akitafuta mbinu za kumfunga kipa wa Khartoum ya Sudan, Mohamed Ibrahim katika mchezo wa Kombe la Kagame uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Simon Msuva akiwatoka wachezaji wa Khartoum ya Sudan.

Amisi Tambwe akimtoka beki wa Khartoum, Hamza Daoud.


Chelsea na Paris Saint-Germain zimetoka 1-1 katika Mechi ya Kirafiki ya michuano ya International Champions Cup huko Bank of America Stadium, North Carolina lakini Chelsea wamepata ushindi baada kupigiana Penati kwa kupata Penati 6-5.
Majuzi, Chelsea walitwangwa Bao 4-2 katika Mechi yao ya kwanza na New York Red Bulls.
Bao za mechi hii zilifungwa na Zlatan Ibrahimovic, Dakika ya 25, kwa PSG na lile la Chelsea kufungwa na Victor Moses katika Dakika ya 65.

Kwenye Mikwaju ya Penati, KIpa wa Chelsea, Thibaut Courtois, aliokoa Penati mbili.
Zikiwa zimebki Dakika 25, Meneja wa Chelsea Jose Mourinho alimuingiza Straika wao mpya alietoka kwa Mkopo kutoka AS Monaco, Radamel Falcao.
Kipa wa Chelsea akiachia na kumfunga kipa mwenzake wa PSGAkiokoa mkwaju wa PenatiRadamel Falcao akipigana vikumbo kuutafuta mpira dhidi ya MarquinhosviesKipa wa Chelsea Thibaut akiokoa jahazi langoni mwakeThiago Motta na John TerryBlaise Matuidi na Nemanja MaticWachezaji wa PSG wakimpongeza mwenzao Zlatan baada ya kufunga bao kipindi cha kwanza

waliotembelea blog