Saturday, May 30, 2015


download (3) 
NA MWANDISHI WETU,TANGA.
Kikao cha Kamati ya Utendaji cha Coastal Union ambacho kimeketi
katikati ya wiki hii chini ya Makamu Mwenyekiti wa Coastal Union,
Steven Mguto kimeazimia kuwaacha baadhi ya wachezaji ambao muda wao
ulikuwa umemalizika huku wengine wakiongezewa mikataba ya kuendelea
kuitumikia timu hiyo kwa msimu ujao.
Kimsingi wachezaji hao wameachwa na sasa wapo huru kutumikia timu
nyengine ambazo zitahitaji huduma zao
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Ofisa Habari wa Coastal
Union,Oscar Assenga amesema
kuwa maamuzi hayo yalifikiwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya
klabu hiyo ambacho kilifanyika juzi mkoani hapa.
Amesema kuwa kimsingi katika kikao hicho kiliridhia kuwaacha wachezaji
waliomaliza mikataba yao ikiwemo Shabani Kado,Keneth Masumbuko,Yayo
Kato Lutimba, Seleimani Kibuta,Bakari,Razack Khalfani,Itubu Imbem na
Othumani Tamimu.
Aidha amesema kuwa wachezaji wengine ambao klabu imeamua kuwaacha ni
Hussein Sued, Mansour Alawi, Amani Juma, Mohamedi Mtindi na Mohamed
Hassani.
Hata hivyo amesema wachezaji ambao wamemaliza mikataba yao ambao klabu
ipo kwenye mazungumzo nao kwa ajili ya msimu ujao ni Bakari Mtama,Rama
Salim, Godfrey Wambura na Joseph Mahundi.
Wakati huo huo, uongozi wa Coastal Union umewapandisha timu wachezaji
wanne kutoka timu ya vijana kucheza timu ya wakubwa ambao ni Mtenje
Albano, Tumaini Karim, Mohamed Twaha Shekue “Djong”, Fikirini
Suleiman“Mapara”


Nahodha wa zamani wa England, Rio Ferdinand, ameamua kustaafu Soka.
Ferdinand, mwenye Miaka 36, alimpoteza Mkewe Rebecca aliezaa nae Watoto Watatu hapo Mei Mosi Mwaka huu baada kuugua kansa na kufariki.
Katika maisha yake ya Soka aliichezea Timu ya Taifa ya England mara 81 na pia kuwa Nahodha wake.
Kwenye Klabu, Ferdinand alizichezea West Ham, Leeds United, Man United na kumalizia Msimu huu akiwa QPR ambayo imeshushwa Daraja toka Ligi Kuu England.
Akiwa na Man United, Ferdinand alitwaa Ubingwa wa England mara kadhaa na pia UEFA CHAMPIONS LIGI pamoja na Klabu Bingwa ya Dunia.
Akitangaza kustaafu, Ferdinand alitoa shukran kwa Mameneja na Wafanyakazi wa Klabu alizopitia pamoja na Familia yake na hasa Mkewe.
Ferdinand akisherekea Ubingwa akiwa na Klabu ya  Manchester United mwaka  2003 Kwenye Ubingwa wa Ligi Kuu England akiwa na  David Beckham kwenye picha.

Ferdinand akipeana mkono  na Kaka yake  Anton walipokutana Uso kwa uso na  Manchester United dhidi ya West Ham huko Upton Park mnamo mwaka 2005.

Ferdinand akishangilia na  Wes Brown  2006. Man United walipoitwanga  Wigan bao 4-0

Siyo tu kwenye Ushindi Rio Ferdinand pia alipokuwa akiukosa ushindi Aliumia na hapa walitolewa nje England kwenye Kombe la Dunia

Cristiano Ronaldo mwezi wa tano mwaka  2007 huko  Old Trafford walipoutwaa ubingwa na hapa Ferdinand alipata picha ya pamoja.

Ferdinand akiwa na  Joe Cole mwaka 2008 hukoM oscow

Nemanja Vidic, Anderson, Patrice Evra, Edwin van der Sar, Carlos Tevez, Ferdinand, Brown, Ryan Giggs na Mikael Silvestre wakishangilia baada ya kuitwanga Chelsea huko Moscow mnamo mwaka 2008

Ferdinand akipozi na  Ferguson pamoja na  Giggs na kombe lao mwaka 2008
2009
Manchester United kwenye picha ya pamoja mwaka  2009 walipoibuka na Ubingwa.


This song"NANA"Has Been Produced By Naahreal From Tanzania And Writen By Diamond Platnumz And Mr Flavour'The Video Was Shoot In Cape Town,South Africa By Godfather Production. Diamond Quote:

waliotembelea blog