Thursday, September 10, 2015



Matarajio yalikuwa ni kwamba Steven Gerrard atarejea Liverpool kwa mkopo Mei, mwakani.


Lakini inaonekana hilo halitakuwepo na kiungo huyo nyota wa zamani wa Liverpool, mwenye miaka 35 sasa, ataendelea kubaki na klabu yake mpya ya LA Galaxy.

Kawaida wachezaji wengi wanaokwenda kucheza Marekani wamekuwa wakirejea England kwa mkopo.

Lakini Kamishna wa Ligi Kuu Marekani (MLS), Don Garber amesema haoni kama kuna sababu ya Gerrard kurudi Liverpool.


Tena akaongeza kwamba wachezaji kuondoka MLS kumekuwa kukiishusha hadhi akitolea mfano wa David Beckham alivyoondoka LA Galaxy na kwenda AC Mnilan.

Mchezaji mpya wa Manchester city, Kevin De Bruyne amekutana na wenzake kwa mara ya kwanza baada ya kuanza mazoezi arasmi jana.


Mchezaji huyo amekutana na wenzake katika uwanja wa mazoezi huku akionekana ni mwenye furaha.

City imemnunua raia huyo wa Ubelgiji kwa kitita cha pauni milioni 52 na kumfanya kuwa mmoja wa wachezaji ghali duniani.

Je, umewahi kuwaona wachezaji kama Vincent Kompany, David Silva, Raheem Sterling na wengine wanaingia mazoezini Ciy kabla ya mazoezi. Cheki mapichaz.







MAYWEATHER NA BERTO...
 Floyd Mayweather ameeeleza kwa nini aliamua kutomchagua bondia Mwingereza, Amir Khan katika pambano la 49.
Mayweather amechagua kuzichapa na Andre Berto katika pambano litakalopigwa Jumapili.


Swali hilo limetokana na tiketi kutokuwa zimenunuliwa na haki za runinga kutogombewa hadi sasa wakati inaonekana siku zimeisha.

Khan alionekana ana nafasi ya kupigana na Mmarekani huyo mara tatu tofauti lakini aliikosa nafasi hiyo.

“Si suala la binafsi, nianchoangalia ni kazi au sema biashara. Sina matatizo na Khan lakini ndiyo niliona hivi ni sahihi kwa ajili ya biashara,” alisema Mayweather.



SASA ndiyo imekuwa gumzo, binti wa Hans van der Pluijm na Jose Mourinho, nani mkali?


Makocha wote wawili ni raia wan chi za bara la Ulaya, Ureno na Uholanzi. Wote timu zao ni mabingwa wa nchi.

Jose Mourinho ambaye aliingoza Chelsea kutwaa ubingwa wa England msimu uliopita anaonekana akiwa katika picha akiwa na binti yake walipokwenda kuhudhuria tuzo.

Pluijm, anaonekana pia akiwa na binti yake siku ambayo Yanga ilibeba Ngao ya Hisani kwa kuitwanga Azam FC kwa mikwaju ya penalti.

Wengi wanasifia muonekano wa binti wa Pluijm ambaye mama yake ni Mwafrika raia wa Ghana.
Lakini wako wanaovutiwa zaidi na vazi la binti wa Mourinho.


Hata hivyo ni vigumu kujua nani kashinda kwa kuwa hakuna sehemu ambayo kura zinahesabiwa na picha hizo zimekuwa zikisambaa sehemu mbalimbali.



Azam Media Limited imeingia mkataba wa miaka minne na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kudhamini michuano ya Kombe la Shirikisho.


Michuano hiyo ambayo ilijulikana kama Kombe la Fat  au FA itadhaminiwa na kampuni hiyo kuwa ya mambo ya habari kwa thamani ya Sh bilioni 3.3.

Rais wa TFF, Jamal Malinzi ameshindwa kuficha furaha yake kutokana na udhamini huo mnono wa Azam Media.
KOCHA WA FRIENDS RANGERS, ELLY MZOZO AKIULIZA SWALI

Timu 64 zitashiriki michuano hiyo kwa mtindo wa mtoano.

Sehemu ya udhamini inaonyesha kuwa bingwa wa mashindano hayo atabeba kitita cha Sh milioni 50 na wakati wa safari kucheza ugenini timu itapata Sh milioni 3 huku mwenyeji akipa Sh milioni moja. Kumbuka mechi zitapigwa nyumbani na ugenini.

Akizungumza katika halfa fupi ya mkataba huo kwenye Ukumbi wa mikutano wa Jengo la Kisenga LAPF, Kijitonyama jijinai , Dar es Salaam, Rais wa TFF, Jamal Malinzi, amesema:


Malinzi amesema kwamba duniani kote maendeleo ya soka yanatokana na kuwepo na mashindano mbalimbali yakiwemo ya Kombe la Shirikisho la nchi, ambayo yanashirikisha na klabu za chini hadi zile zinazoshiriki Ligi Kuu.

“Udhamini huu utachangia soka kukua kwa kiasi kikubwa, nashukuru sana kuona mambo yamefikia hapa, ahsante kwa Azam Media kwa uamuzi wao wa kuingia kukuza mpira wa Tanzania,” alisema Malinzi.





RATIBA YA RAUNDI YA KWANZA YA KOMBE LA FA

Ruvu Shooting vs Cosmopolitan

Abdajalo Dar vs Transcamp

AFC vs  Polisi Mara

Polisi Tabora vs Green Warriors

Kariakoo Lindi vs Changanyikeni Dar

Mkamba Rangers vs Ruvuma FC ya Kigoma

Rhino ya Tabora vs Alliance FC ya Mwanza

Panone vs Cocacola Kwanza ya Mbeya

Sabasaba Utd vs Abdajalo ya Tabora

Magereza Iringa vs Polisi Dar

Mirambo vs Town Small Boys Ruvuma

JKT Rwamkoma vs Villa Squad

Wenda vs Madini Sports Arusha

Pamba vs Polisi Dodoma.

Singida Utd vs Bulyhanhulu

Polisi Moro vs Mshikamano Sports



Wakati viongozi wengi wa siasa na wale wa serikali wanaona michezo ni kama burudani tu, England imefanikiwa kuingiza mamilioni ya fedha kwa mwaka jana tu na kujiongeza kiuchumi kupitia soka.


Watalii wanaofikia 800,000 kutoka nje ya England wametembelea nchini hiyo kwenye viwanja mbalimbali vya mpira wa miguu na kuisaidia England kuingiza pauni milioni 684.

Fedha hizo zingeweza kuinua kwa kiasi kikubwa uchumi wa Tanzania kama ingezipata kupitia fedha.

Fedha hizo ni zaidi ya zile ambazo Tanzania huingiza kupitia utalii hapa nchini.

Uwanja unaomilikiwa na Manchester United wa Old Trafford wenyewe ndiyo umetembelewa zaidi sawa na ule wa Emirates wa Arsenal. Kila mmoja umetembelewa na watalii 109,000.

Pamoja na kuyumba katika ligi, lakini watalii 99,000 walitembelea Anfield wa Liverpool na Chelsea ikapanda kwa kupata watalii 89,000 kupitia Stamford Brigde.


Hii inaonyesha kiasi gani mchezo wa soka ukiendelezwa unavyoweza kugeuka na kuwa kitegauchumi kwa watu binafsi lakini hata serikali.


LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
Jumamosi Septemba 12

14:45 Everton v Chelsea
17:00 Arsenal v Stoke
17:00 Crystal Palace v Man City
17:00 Norwich v Bournemouth
17:00 Watford v Swansea
17:00 West Brom v Southampton
19:30 Man United v Liverpool

Jumapili Septemba 13
15:30 Sunderland v Tottenham
18:00 Leicester v Aston Villa

Jumatatu Septemba 14
22:00 West Ham v Newcastle


SIMBA SC inafunga safari leo kutoka Zanzibar kwenda Tanga tayari kwa mchezo wa ufunguzi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumamosi dhidi ya wenyeji wao, African Sports. Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema baada ya maandalizi ya tangu Julai, anaamini kabisa kikosi sasa kipo tayari kwa Ligi Kuu. “Mwalimu alipatiwa kila alichohitaji katika maandalizi. Ushauri wake ulifuatwa katika uundwaji wa timu na matayarisho kwa ujumla. Kambi ya aina gani, wakati gani kila alipohitaji alipata. Mechi za aina gani za majaribio na wakati gani, kila alipohitaji alipata, na kila mchezaji aliyesajiliwa alipitia mikononi mwake kwanza akamuangalia na kumuidhinisha. Nadhani upande wetu kama viongozi, tumecheza vizuri katika eneo letu,”amesema Poppe.
Basi la Simba SC litawapokea wachezaji wa SImba SC bandarini Dar es Salaam kuwapeleka Tanga tayari kwa mechi na African Sports Jumamosi
Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), amesema anaamini kabisa sasa ni wakati wa benchi la Ufundi na wachezaji nao kufanya kazi yao ili kuwapa raha wana Simba SC. “Ushindi tu hadi ubingwa, hiyo ndiyo kiu ya wana Simba wote na ndiyo maana tumetumia gharama kubwa ya kuiandaa timu, kuanzia kambi ya Lushoto na baadaye Zanzibr kwa miezi miwili,”amesema.   Msimu mpya wa Ligi Kuu unaanza Jumamosi, na mbali na Smba SC na African Sports Mkwakwani,  Ndanda FC watakuwa wenyeji wa Mgambo Shooting Uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara, Majimaji FC wataikaribisha na JKT Ruvu Uwanja wa Majimaji, Songea na Azam FC wataikaribisha Prisons Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Stand United watakuwa wenyeji wa Mtibwa Sugar Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Toto Africans wataikaribisha Mwadui FC Uwanja wa Kambarage Shinyanga na Mbeya City watakuwa wenyeji wa Kagera Sugar Uwanja wa Sokoine, wakati Jumapili mabngwa watetezi Yanga SC wataanzia nyumbani na Coastal Union Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Simba SC inaingia katika msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara chini ya kocha mpya, Muingereza Dylan Kerr aliyeanza kazi mapema Julai, baada ya kuachana na Mserbia, Goran Kopunovic aliyetaka dau kubwa ili kuongeza Mkataba.

Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited, Rhys Torrington (kulia) akibadilishana mikataba na Rais wa TFF, Jamal Malinzi leo 

RATIBA YA MECHI ZA RAUNDI YA KWANZA 

AFC vs  Polisi Mara Polisi Tabora vs Green Warriors Kariakoo Lindi vs Changanyikeni Dar Mkamba Rangers vs Ruvuma FC ya Kigoma Rhino ya Tabora vs Alliance FC ya Mwanza Panone vs Cocacola Kwanza ya Mbeya Polisi Moro vs Mshikamano Sports Sabasaba Utd vs Abdajalo ya Tabora Magereza Iringa vs Polisi Dar Mirambo vs Town Small Boys Ruvuma Abdajalo Dar vs Transcamp Ruvu Shooting vs Cosmopolitan Singida Utd vs Bulyhanhulu JKT Rwamkoma vs Villa Squad Wenda vs Madini Sports Arusha Pamba vs Polisi Dodoma.
Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
KAMPUNI ya Azam Media Limited leo imesaini Mkataba wa miaka minne na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa ajili ya kudhamini michuano ya Kombe la Shirikisho, zamani (FA) wenye thamani ya Sh. Bilioni 3.3.
Katika halfa iloyofanyika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa jengo la Kisenga LAPF, Kijitonyama, Dar es Salaam, Rais wa TFF, Jamal Malinzi, amesema kwamba amefurahia kufanikisha azma ya kurejesha mashindano hayo.
Malinzi amesema kwamba duniani kote maendeleo ya soka yanatokana na kuwepo na mashindano mbalimbali yakiwemo ya Kombe la Shirikisho la nchi, ambayo yanashirikisha na klabu za chini hadi zile zinazoshiriki Ligi Kuu.
“Nitafurahi sana kuona klabu ya Daraja la Pili inashinda Kombe hilo, duniani kote Kombe hili lipo na klabu za chini zimekuwa zikiwapiga ‘visu’ wale wakubwa,” alisema Malinzi.
Aliongeza kuwa bingwa wa mashindano hayo atajinyakulia kitita cha Sh. Milioni 50 wakati kila timu itakayokwenda kucheza ugenini itapata Sh. Milioni tatu za safari na mwenyejii atapewa Sh. Milioni 1 ya maandalizi.
“Tumeona bingwa wa michuano hii apate Sh. Milioni 50 kwa sababu atakuwa amecheza mechi saba na yule wa Vodacom anayecheza michezo 30 anapata Sh. Milioni 70,” Malinzi aliongeza.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya TFF, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ alisema jana kuwa mashindano ya mwaka huu yatashirikisha klabu 64 na yataendeshwa kwa njia ya mtoano.
Kaburu, ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Simba SC, amezitaja timu hizo kuwa ni pamoja klabu 16 zinazoshiriki Ligi Kuu ya Bara, timu 24 za Daraja la Kwanza na idadi kama hiyo za Daraja la Pili.
Alisema kwamba mshindi wa kombe hilo atapata nafasi ya kuiwakilisha nchi katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAF) mwaka 2017.
Torrington (kulia) wakitiliana saini Mkataba na Malinzi 
Malinzi akichezesha droo ya kuchagua timu za Raundi ya kwanza 
Meneja Masoko wa TFF, Peter Simon akitaja timu za kumenyana katika Raundi ya kwanza




ORODHA YA MABINGWA WA KOMBE LA FA: 

1967 Yanga SC (Dar es Salaam)
1985 Maji Maji (Songea)   
1995 Simba SC (Dar es Salaam)
1996 Sigara (Dar-es-Salaam)
1997 Tanzania Stars (Dar es Salaam)
1998 Tanzania Stars (Dar es Salaam)
1999 Yanga SC (Dar-es-Salaam)
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC (Dar-es-Salaam) 
2002 JKT Ruvu Stars (Pwani)
Alieleza kuwa timu 16 za Ligi Kuu ya Bara zenyewe zitaanzia raundi ya pili itakayoshirikisha klabu 32 na kuongeza kwamba wiki ya mechi za Kombe la FA hakutakuwa na michezo ya Ligi ya Bara.
Hii ni mara ya kwanza kihistoria michuano ya Kombe la FA kuwa na udhamini na miaka ya imekuwa ikiibuka na ‘kuyeyuka’ tangu mwaka 1967 kabla ya kupotea moja kwa moja mwaka 2002. Mara ya mwisho Kombe la FA lilifanyika mwaka 2002 na JKT Ruvu Stars ya Pwani ikaibuka bingwa baada ya kuifunga Baker Rangers ya Magomeni kwenye fainali. Bingwa wa kwanza wa Kombe la FA enzi hizo likiitwa Kombe la FAT ilikuwa Yanga SC mwaka 1967, na michuano hiyo haikufanyika tena hadi 1985 Maji Maji ya Songea ilipotwaa Kombe. Kombe la FAT likayeyua tena kabla ya kurejea miaka 10 baadaye, 1995 na Simba SC ikatwaa ubingwa kabla ya kupokonywa na Sigara mwaka 1996, ambao nao walilitema kwa Tanzania Stars mwaka 1997 iliyofanikiwa kulitetea 1998 kabla ya kupokonywa na Yanga SC 1999. Ubingwa wa FA mwaka 2000 ulikwenda kwa  Simba SC, waliopokonywa na Yanga SC mwaka 2001 kabla ya JKT Ruvu kuwa bingwa wa mwisho wa mashindano hayo mwaka 2002.
Klabu ya Tottenham Hotspur ambayo makao makuu yake ni jiji la London imemzuia winga wa kimataifa wa Korea Kusini Son Heung-Min kununua gari lenye rangi nyekundu. Spurs ambao wanajiandaa na mchezo wa Ligi Kuu weekend hii dhidi ya Sunderland wametoa sharti hilo kwa Son Heung-Min.
Kwa mujibu wa mtandao wa mirror.co.uk Son Heung-Min anatajwa kuwa mchezaji ghali zaidi katika historia ya soka kutokea bara la Asia, lakini amethibitisha kuzuiwa na viongozi wa Spurs kununua gari lenye rangi nyekundu kwa sababu ni rangi ambayo inatumiwa na wapinzani wao Arsenal.
Son-Heung-Min-signs-for-Tottenham
“Viongozi wa Tottenham tayari wameniambia siruhusiwi kununua gari lenye rangi nyekundu, nina furaha kucheza mechi yoyote ile dhidi ya Arsenal  na ninapenda kushinda kwa sababu mimi ni mshambuliaji, rekodi yangu ya ufungaji itaongea kwa ajili yangu”>>> Son Heung-Min
Heung-Min-Song
Son Heung-Min alisajiliwa na klabu ya Tottenham Hotspur kwa dau la pound milioni 22 akitokea klabu ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani na kusaini mkataba wa miaka mitano, Son Heung-Min amecheza mechi 87 na kufunga magoli 29 akiwa na klabu ya Bayer Leverkusen.



.
.
Kazi yangu ni kuhakikisha nakusogezea kila stori inayonifikia na hapa ninayo stori iliyochukua headlines Sept 9,2015 ya msanii wa Hip Hop kutokea 96.0 (Tanga) Roma Mkatoliki ambaye single yake mpya ilizuiliwa kwenye baadhi ya vituo vya radio nchini.
Msanii huyo alipokutana na ripota wa millardayo.com aliweza kuelezea sababu zilizopelekea kuzuiliwa kwa single yake mpya iitwayo Viva Roma na kusema..’Kiukweli jana ndio ilikuwa tarehe 9 mwezi wa tisa ambayo nilitoa ahadi kwa watu kuwa nitaachia wimbo wangu mpya unaoitwa Viva Roma na asubuhi mapema kabisa kwenye ukurasa wangu wa instagram nilipost picha ikionesha napaki CD zangu nikiwa tayari kuisambaza kazi yangu mpya mimi na timu yangu nzima ya Tongwe Records; – Roma Mkatoliki
.
.
‘Ilikuwa saa saba nianze na Eatv Radio kwenye kipindi cha Planet Bongo, saa nane nitaenda XXL ya Clouds FM, halafu nitaenda Times FM, halafu nitaenda E FM, na Magic FM so nilikuwa natoa ratiba ya kuitambulisha wimbo wangu katika vituo mbalimbali vya radio’ – Roma Mkatoliki
‘Ila mpaka sasa tunavyoongea tumeshaisambaza katika vituo vyote mbalimbali sehemu ambayo bado ni kwenye mitandao tu kama blogs, website na nchi za jirani ila jibu nililopewa na baadhi ya vituo vya radio ni kwamba wameikataa kuicheza ngoma yangu kwasababu wanachodai kwamba ina maneno makali huku vituo vingine vikiwa vinacheza verse moja tu kiukweli imenisikitisha lakini kwa upande wa mashabiki wanasema wimbo ni mzuri na sio kama ninalaumu vituo vya radio ila ndio maamuzi yao


Kila siku team ya Hekaheka kutoka Clouds FM imekua ikituletea matukio mbalimbali yanayotokea ndani ya familia zetu.
Hekaheka ya leo inatokea Kahama ambapo mtoto wa miezi mitano aling’atwa na punda na kisha kukimbia naye umbali wa mita kama 300.
Shuhuda wa tukio hilo amesema mtoto huyo alikua amelala pembeni ya kibanda cha mama yake ambaye alikua anapika mara ghafla punda mmoja akaja kisha akamng’ata, akaanza kukimbia naye.
Mama wa mtoto amesema alikuwa amemkalisha chini huku yeye anapika, lakini akashangaa punda amemchukua mtoto wake na kuanza kukimbia naye.
Anasema baada ya mwendo mrefu yule punda alikutana na mtu mwenye fimbo ndipo akamuachia yule mtoto lakini akiwa tayari na majeraha mbalimbali na mpaka sasa amelazwa katika hospitali ya Kahama.
Daktari wa mifugo amesema punda pia anaweza kupata kichaa cha mbwa hivyo ni vyema wananchi wakajua hilo, pia anaweza kufanya hivyo akiwa katika wakati wa kutaka kujamiana.
Baada ya tukio lile wananchi wenye hasira waliwakamata wale punda wote wawili na kuwachoma moto.



Cristiano Ronaldo ni staa mkubwa kwenye soka, YES… Dunia inamjua, hii ni kumaanisha kwamba hata wasio na ushabiki kwenye soka jina lake wanalijua !!
1900832
Mastaa kama Michael Jordan wamestaafu kwenye Michezo lakini majina yao yako juu bado kutokana na kujiingiza pia kwenye biashara kubwakubwa Duniani… Ronaldo anahitaji hata ikitokea leo anaachana na soka, jina lake likumbukwe pia tena kwenye uzito wake !!
Ni dili juu ya dili kwa Cristiano Ronaldo… baada ya kuingia Mikataba mingi ikiwemo ya kutengeneza nguo na viatu vyenye jina lake, safari hii amezindua perfume zenye jina la ‘Legacy‘ na tayari zimesogezwa sokoni kuuzwa.
Hapa nimekuwekea Pichaz na Video, Ronaldo na watu wake wa karibu wakati wa uzinduzi huo…
ron
ron2
ron3
ron4
ron6
Hiki ni kipande cha Video ambacho ni tangazo la perfume yenyewe, sekunde 31 tu mtu wangu hiki hapa..

waliotembelea blog