Thursday, September 10, 2015

Klabu ya Tottenham Hotspur ambayo makao makuu yake ni jiji la London imemzuia winga wa kimataifa wa Korea Kusini Son Heung-Min kununua gari lenye rangi nyekundu. Spurs ambao wanajiandaa na mchezo wa Ligi Kuu weekend hii dhidi ya Sunderland wametoa sharti hilo kwa Son Heung-Min.
Kwa mujibu wa mtandao wa mirror.co.uk Son Heung-Min anatajwa kuwa mchezaji ghali zaidi katika historia ya soka kutokea bara la Asia, lakini amethibitisha kuzuiwa na viongozi wa Spurs kununua gari lenye rangi nyekundu kwa sababu ni rangi ambayo inatumiwa na wapinzani wao Arsenal.
Son-Heung-Min-signs-for-Tottenham
“Viongozi wa Tottenham tayari wameniambia siruhusiwi kununua gari lenye rangi nyekundu, nina furaha kucheza mechi yoyote ile dhidi ya Arsenal  na ninapenda kushinda kwa sababu mimi ni mshambuliaji, rekodi yangu ya ufungaji itaongea kwa ajili yangu”>>> Son Heung-Min
Heung-Min-Song
Son Heung-Min alisajiliwa na klabu ya Tottenham Hotspur kwa dau la pound milioni 22 akitokea klabu ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani na kusaini mkataba wa miaka mitano, Son Heung-Min amecheza mechi 87 na kufunga magoli 29 akiwa na klabu ya Bayer Leverkusen.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog