Tuesday, November 10, 2015


Utamaduni wa wanafunzi kuwatunga majina waalimu wao ulikuwepo toka zamani na mara nyingi mwalimu anaweza kutungwa jina ambalo yeye halijui ila kutokana na tabia na muonekano wake basi wanafunzi hupenda kumtunga jina linaloendana na tabia zake kama ni mkali usishangae ukisikia akipewa jina la ajabu kama mnoko na kadhalika.
PAY-Man-United-arrive-at-The-Lowry-Hotel
Stori zilizotoka mtandaoni ni kuwa wachezaji wa klabu ya Manchester United wameamua kumtunga jina kocha wao raia wa Uholanzi Louis van Gaal, wachezaji wa Man United wamempa jina kocha wao la “Daisy” kutokana na tabia yake ya kuendesha gari taratibu akiwa anawasili katika uwanja wa mazoezi wa timu hiyo Carrington na kukwepa vishimo vidogo vidogo.
_82305410_man_united_reuters
Jina hilo la ‘Daisy’ linatoka katika movie iliyowahi kutamba miaka ya nyuma ya ‘Driving Miss Daisy’ wachezaji hao wamempa jina la utani kocha huyo ambaye pia wanamtaja kama muoga na anaendesha gari taratibu sana na mwendo wa gari yake ukifananishwa na mwendo wa Konokono. Hata hivyo Louis van Gaal ni kocha ambaye anafahamika kwa tabia yake ya ukali na misimamo.


Leicester City forward Jamie Vardy poses with the October Barclays Player of the Month trophy
Fowadi wa Leicester City Jamie Vardy akipozi kupata picha na Tuzo yake ya Mwezi Oktoba, 2015
Manchester United youngster Anthony Martial won the award in September 2015 before VardyMwezi wa Septemba Mchezaji wa Manchester United Anthony Martial ndiye aliyetwaa hiyo tuzo



Msafara wa timu ya Taifa ya Algeria (The Desert Warriors) unatarajiwa kuwasili nchini siku ya Alhamis kwa ndege binafsi ya kukodi, ukiwa na jumla ya watu 65 wakiwamo wachezaji 24 tayari kwa mchezo wa Jumamosi Novemba 14 dhidi ya wenyeji Tanzania katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Kocha mkuu wa timu hiyo Iitakayofikia hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Kempsinki, Christian Gourcuff raia wa Ufaransa ametaja kikosi cha wachezaji 24, wakiwemo wachezaji 18 wanaocheza katika klabu za Ulaya kwa ajili ya kuikabili Tanzania.
Wachezaji wanaotarajiwa kuwasili Alhamisi ni walinda mlango, Doukha Izeddine (JS Kabliye), M’bolhi Rais (Antalyaspor), Asselah Malik (CR Belouizdad), walinzi Zeffane Mehdi (Rennes), Medjani Carl (Trabzonspor), Ziti Mohamed (JS Kabliye), Mesbah Eddine (Sampordia), Bensebaini Ramy (Montpeller), Belkarou Hichem (Club African), Ghoulam Faouzi (Namples), Mandi Aissa (Reims).
Viungo ni Guedioura Adlane (Watford), Boudebouz Ryad (Montpeller), Taider Saphir (Bologna), Abeid Mehdi (Panathinacos), Bentaleb Nabil (Tottenham), Ghezzal Rachid (Lyon), Melsoub Walid (Lorient), Marhez Ryad (Leicester).


Kiungo wa zamani wa timu za Arsenal na Manchester City, Patrick Vieira ameteuliwa kuwa kocha mpya wa timu ya New York City.
Vieira mwenye umri wa miaka 39 amesaini mkataba wa miaka mitatu kuifundisha timu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini Marekani.
Kocha huyu alikua anakifundisha kikosi cha vijana wa chini ya umri wa 21 cha Manchester City. Vieira ni miongoni mwa nyota wa timu ya taifa ya ufaransa waliotwaa Kombe la Dunia mwaka 1998.
Vieira ataanza majukumu yake rasmi Januari 1, 2016 akiwa na kibarua cha kuingoza timu hiyo kufanya vizuri katika ligi ya Marekani.



Ratiba ya michuano ya Kombe la Challenji kwa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa Senior Challenger Cup) imetoka jana ambapo timu ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Star’ imepangwa kundi moja na wenyeji Ethiopia.
Katika taarifa ya CECAFA iliyotolewa jana, Kilimanjaro Star imepangwa kundi A pamoja na wenyeji Ethiopia, Somali na waaalikwa wa michuano hiyo timu ya Taifa ya Zambia ‘Chipolopolo’.
Kundi B lina Bingwa mtetezi timu ya Kenya, Uganda, Burundi na Djibouti, huku kundi C likiwa na timu za Rwanda, Sudan, Sudan Kusini na Zanzibar.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Novemba 21 nchini Ethiopia katika mji wa Addis Ababa na kumalizika Disemba 6 mwaka huu.



David Moyes ametimuliwa kazi kama Meneja wa Klabu ya La Liga inayosuasua ya Real Sociedad ikiwa ni Siku 1 tu kabla hajatimiza Mwaka mmoja Klabuni hapo.
Moyes, mwenye Miaka 52, alitwaa wadhifa wa Umeneja wa Klabu hiyo ya Spain hapo Tarehe 10 Novemba 2014 na kuiokoa Klabu hiyo kuporomoka wakati ikiwa katika hali mbaya na kukamata Nafasi ya 12 kwenye La Liga Msimu uliopita.

Lakini Msimu huu mambo ni yale yale kwa Real Sociedad baada ya Ijumaa kuchapwa 2-0 na Las Palmas ikiwa ni kipigo cha 4 katika Mechi zao 5 zilizokwisha za La Liga.
Real Sociedad imetangaza Moyes na Msaidizi wake, Billy McKinlay, wote wamefukuzwa.
Kuhamia kwa Moyes huko Sociedad Mwaka Jana ilikuwa ni kibarua chake cha kwanza tangu atimuliwe Man United Mwezi Aprili 2014 baada ya kudumu Miezi 10 tu hapo Old Trafford.

Moyes, ambae kabla ya kutua Man United alikuwa Meneja wa Everton kwa Miaka 11, alikuwa ni Meneja wa 4 kutoka Uingereza katika Historia ya Real Sociedad.
Wengine waliomtangulia Klabuni hapo ni Harry Lowe alieingia Mwaka 1930 na kukaa Miaka 5, John Toshack alieiongoza Klabu hiyo kwa vipindi vitatu tofauti na cha mwisho kilikuwa Mwaka 2002 wakati Chris Coleman alikaa kwa Miezi 7 baada ya kuteuliwa Julai 2007.
Real Sociedad, ambao wako Nafasi ya 17 katika La Liga, watapambana na Sevilla, Mabingwa wa UEFA EUROPA LIGI, na kisha Barcelona, Mabingwa Watetezi wa La Liga na pia UEFA CHAMPIONS LIGI, katika Mechi zao 2 za La Liga zifuatazo mara baada ya La Liga kurejea tena Wikiendi ya Novemba 21 baada kupisha Mechi za Kimataifa.

Mchezo wa mpira wa miguu ni miongoni mwa kazi zinazotajwa kulipa mishahara mikubwa zaidi duniani, siku hizi imekuwa kawaida kusikia mchezaji huyu na yule kuwa na mshahara wenye tofauti kubwa. Kwa sasa Ligi Kuu soka Tanzania bara inatajwa kuwa ni moja kati ya Ligi zinazoongoza kwa kulipa mishahara mikubwa tofauti na baadhi ya Ligi za nchi jirani.
henry1
November 9 nakusogezea karibu yako sehemu ya exclusive interview ya Henry Joseph ambapo amezungumza kuhusiana na mishahara na jinsi alivyoingia Simba. Henry aliingia Simba mwaka 2006 baada ya kumaliza kidato cha nne ilikuwaje? mkataba wake je? mshahara wake?
“Ilitokea tu kama bahati nikaitwa na mwenyekiti wa Simba alikuwa Wambura wakati ule na kocha Julio nikacheza mechi ya majaribio, baadae nikapigiwa simu, Nikapewa mkataba wa miaka miwili nikasaini hata bila kuusoma Simba tena, mshahara wakati huo bwana wachezaji wote tulikuwa tunalipwa sawa laki moja na ishirini tofauti na siku hizi” >>> Henry Joseph
????????????????????????????????????
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Henry Joseph ni kiungo wa zamani wa klabu ya Simba na timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars lakini amewahi kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Kongsvinger ya Norway ila kwa sasa yupo katika klabu ya Mtibwa Sugar ya Manungu  Turiani.

waliotembelea blog