Saturday, June 27, 2015

Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Moshi vijijini,Godlisen Maramia akipokea fomu kutoka kwa Deogratius Mushi ya kuwania nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi vijijini wakati liporudisha katika ofisi za chama hicho zilizopo Majengo.
Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Moshi vijijini ,Godlisen Maramia akimpongeza mtia nia Deuogratius Mushi kwa uamuzi wa kuingia katika kinya'ng'anyiri cha kuwania nafasi hiyo.
Mushi akipongezwa na makada wengine wa Chadema waliofika kumsindikiza ofisnini hapo.
Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Moshi vijijini,Godlisen Maramia akipokea fomu toka kwa Tally Kisesa ya kuwania Ubunge wa viti maalumu katika jimbola Moshi vijijini.

Mashindano ya Kombe la Meya Shinyanga 2015 (Pepsi Meya Cup 2015) yamezinduliwa rasmi leo na mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga.

Mashindano hayo ambayo yameandaliwa na mstahiki meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam na kudhaminiwa na kampuni ya Vinywaji baridi ya  Pepsi (SBC Tanzania Ltd) yanashirikisha timu 17 za kata zote za manispaa hiyo na timu ya polisi Shinyanga.

Mashindano ya Kombe la Meya Shinyanga yakihusisha mpira wa miguu yataendelea kufanyika hadi tarehe 25,Julai 2015 na yatakuwa yanafanyika siku tatu kwa wiki yaani Ijumaa,Jumamosi na Jumapili.

Mshindi wa kwanza katika mashindano hayo ataondoka na kitita cha shilingi milioni moja na laki tano,kombe na medali ya dhahabu,wa pili shilingi milioni moja,kombe dogo na medali ya fedha na wa tatu shilingi laki tano,kombe dogo na medali ya shaba.

Malunde1 blog ilikuwepo wakati wa uzinduzi huo,Kadama Malunde,ametuletea picha kutoka eneo la tukio....
Mstahiki meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam akizungumza wakati wa ufunguzi wa Pepsi Meya Cup Shinyanga 2015,ambapo alisema lengo la mashindano hayo ya mpira miguu kwa vijana yatakayoshirikisha timu 18 za manispaa ya Shinyanga ni kwa ajili ya burudani,ajira na kusaka vipaji kutoka kwa vijana katika manispaa ya Shinyanga.
Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh alisema mashindano hayo yatakuwa yatafanyika kwa muda wa mwezi mmoja na yatafanyika mara tatu kwa wiki katika viwanja vitatu vya Shycom,Kambarage na Polisi mjini Shinyanga.
Mashindano hayo yameanza leo Juni 26,2015 yatafikia tamati Julai 25,2015
Meza kuu wakiwa eneo la tukio.
Meneja mauzo wa Kampuni ya vinywaji baridi Pepsi kanda ya Ziwa Seni Makwaya akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kombe la Meya Shinyanga 2015 ambapo alisema katika mkoa wa Shinyanga ndiyo mara ya kwanza kwa kampuni ya Pepsi kudhamini mshindano ya meya,ingawa huu ni mwaka wa tatu nchini Tanzania tangu waanze kudhamini mashindano ya namna hiyo.
Meneja mauzo  wa kampuni ya vinywaji baridi SBC Tanzania Limited (Pepsi) bwana Promod  Nair akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano ya kombe la meya Shinyanga 2015 ambapo alisema wameamua kudhamini mashindano hayo ili kuinua vipaji kutoka kwa vijana katika manispaa ya Shinyanga.
Meneja mauzo kampuni ya Pepsi mkoa wa Shinyanga bwana Benson Tweve akizungumza katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga ambapo alizitaka timu za Stand United na Mwadui FC kutumia fursa ya mashindano hayo ya Meya Cup kuchukua vijana wenye vipaji kwa ajili ya kuinua mkoa wa Shinyanga kimichezo.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kombe la Meya Shinyanga 2015,ambapo pamoja na mambo mengine aliwataka vijana wa Shinyanga kutumia fursa ya mashindano hayo kuonesha vipaji vyao kwani michezo ni ajira.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro akikabidhi vifaa vya michezo kwa afisa mtendaji wa kata ya Masekelo yenye Timu ya Masekelo fc iliyocheza mechi ya ufunguzi na Ngokolo fc kutoka kata ya  Ngokolo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akikabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza katika mchezo wa mbio za baiskeli  Kulwa Ntyuki uliofanyika mjini Shinyanga wakati wa ufunguzi wa kombe la meya Shinyanga.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro akikabidhi vifaa vya michezo kwa afisa mtendaji wa kata ya Ngokolo.

Waamuzi wa mchezo wa ufunguzi wakikagua wachezaji wa timu ya Masekelo FC na Ngokol0 FC.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine akikagua timu ya Masekelo FC  kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya Masekelo FC na Ngokolo fc haijaanza katika uwanja wa mpira wa Shycom Mjini Shinyanga .
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine akikagua timu ya Ngokolo fc kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya Masekelo fc na Ngokolo fc haijaanza katika uwanja wa mpira wa Shycom Mjini Shinyanga.
Waamuzi wa mchezo wakiwa uwanjani.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine akizungumza na wachezaji wa timu ya Ngokolo fc  na  Masekelo fc na Ngokolo FC
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro akijiandaa kupiga penati huku meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam akiwa golini.
Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam akihangaika golini baada ya kufungwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.
Mechi kati ya Masekelo fc na Ngokolo fc ukiendelea ambapo hadi mwisho wa mchezo,Masekelo fc bao 2,na Ngokolo fc bao 2.
Wakazi wa Shinyanga wakishuhudia mechi.
Wengine walipaki na baiskeli zao uwanjani kujionea kilichokuwa kinajiri uwanjani.
Mchezo unaendelea.
Tunafuatilia kinachoendelea....
Wachezaji wa Masekelo fc wakishangilia goli lao la kwanza.

Wakazi wa Shinyanga wakiwa juu ya ukuta wakifuatilia mechi.
Tunafuatilia mechi......
Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam(mwandaaji wa Kombe la Meya Shinyanga 2015) akiteta jambo na  Meneja mauzo  SBC Tanzania Limited Pepsi bwana Promod  Nair( wadhamini wa kombe la meya Shinyanga 2015).
Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam akiteta jambo na msimamizi wa kituo cha Shycom bwana Geofrey Tibakenda,na mratibu wa Kombe la Meya bwana Paul Mganga,ambaye ni mkurugenzi wa Myklay Entertainment(katikati). 

Picha zote na Kadama Malunde.


Argentina wameingia Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Marekani ya Kusini, COPA AMERICA, baada ya kuitoa Colombia kwa Mikwaju ya Penati 5-4 kufuatia Sare ya 0-0 katika Dakika 90 kwenye Mechi ya Robo Fainali iliyochezwa Alfajiri hii.
Katika piga nikupige ya Penati, Timu zote zilifunga Penati zao 3 za kwanza kupitia Lionel Messi, Ezequiel Garay na Ever Banega kwa Argentina huku Colombia wakifunga kupitia James Rodriguez, Radamel Falcao na Juan Cuadrado.

Kwenye Penati ya 4, Muriel akakosa kwa Colombia na Lavezzi kuifungia Argentina na kufanya ngoma iwe 4-3.
Colombia wakafunga Penati yao ya 5 kupitia Cardona na Argentina, wakitakiwa kufunga Penati yao ya 5 ili wasonge, wakakosa Mpigaji akiwa Lucas Biglia na kufanya Bao ziwe 4-4.

Ndipo zikaja nyongeza za Penati moja moja kuamua Mshindi wa papo kwa papo na Colombia kukosa Mpigaji akiwa Zuniga lakini Argentina nao wakakosa ushindi baada ya Marcos Rojo kukosa pia.
Penati iliyofuatia ilipigwa na Colombia lakini Murillo akakosa na akaja Mchezaji mpya wa Boca Juniors ya Argentina, Carlos Tevez, alieanzia Benchi kwenye Mechi hii, na kufunga Penati ya mwisho iliyowapa Argentina ushindi wa Penati 5-4.


Straika wa Argentina Carlos Tevez amekamilisha Uhamisho wake kwenda Boca Juniors kutoka kwa Mabingwa wa Italy Juventus.
Tevez, mwenye Miaka 31, alianzia Soka lake huko kwao na Klabu ya Boca ambayo aliihama Mwaka 2004 kwenda Brazil kuchezea Corinthians na kisha kukaa Miaka 9 akichezea Klabu za Ulaya.
Huko Ulaya alizichezea Klabu za England, West Ham, Mwaka 2006-2007, Manchester United, 2007-2009, na Manchester City, 2009-2013, na kisha kwenda Italy kuichezea Juventus ambako msimu uliopita aliisaidia tena kutetea Taji lao la Ubingwa kwa kupiga Bao 20.
Majuzi Juventus walimbadili Tevez kwa kumsaini Straika wa Atletico Madrid ya Spain, Mario Mandzukic ambae anatoka Croatia.
Alfajiri hii, Tevez alitoa mchango mkubwa kwa Nchi yake Argentina pale alipofunga Penati ya mwisho katika Mechi ya Robo Fainali ya Copa America na kuifikisha Argentina Nusu Fainali baada ya kuibwaga Colombia kwa Penati 5-4 baada ya Sare ya 0-0 katika Dakika 90.
Akithibitisha Uhamisho huu, Rais wa Boca Juniors Daniel Angelici alisema: "Ni Siku ya furaha sana na ya kuridhisha. Kurudi kwa Tevez akiwa kwenye kilele cha mafanikio ni habari njema kwa Washirika na Mashabiki wote wa Boca na Soka la Argentina!"
Tevez, ambae alitwaa Ubingwa mara 3 huko England na mara 2 huko Italy, alifunga Bao 38 katika Mechi 110 alizochezea Boca alipokuwepo huko mara ya kwanza ambako pia alitwaa Ubingwa Mwaka 2003 na kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Marekani ya Kusini kwa mara 3 mfululizo.

waliotembelea blog