Saturday, May 9, 2015


Stoke City XI: Butland, Cameron, Shawcross, Muniesa, Pieters, N'Zonzi, Whelan, Walters, Adam, Arnautovic, Diouf.
Akiba: Sorensen, Bardsley, Ireland, Odemwingie, Sidwell, Crouch, Wollscheid.

Tottenham XI: Lloris; Dier, ChiricheÈ™, Fazio, Vertonghen; Bentaleb, Mason; Lamela, Eriksen, Chadli; Kane.
Akiba: Vorm, Rose, Yedlin, Dembele, Stambouli, Townsend, Soldado.


Timu ya Simba Sports Club imeibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya JKT Ruvu na kushika nafasi ya 3 katika Ligi Kuu ya Vodacom iliyomalizika leo. ‪#‎VPL2015‬
Timu za Polisi Moro na Ruvu Shooting zimeshuka daraja.



Kutoka chini ya kwa chini ni kuhusu Kocha wa Bayern Munich kwenda Ligi Kuu England msimu Ujao wa 2015/2016 kufundisha Timu ya Man City.

 


Jermain Defoe dakika ya 85 kipindi cha pili aliwafungia bao Sunderland na kufanya 2-0 dhidi ya Everton. Ushindi huu umeipandisha Sunderland nafasi ya 14 wakiwa na pointi 36 huku Everton wakiwa nafasi ya 11 na pointi zao 44. Ukumbuke mpenzi wa bukobasports Sunderland wanamchezo wao mkononi hivyo mchezo wao wa leo ni 35, Everton wao wamecheza mchezo wao wa 36.
Danny Graham wa Sunderland  dakika ya 53 anaifungia bao Sunderland na kufanya 1-0 dhidi ya Everton kipindi cha pili.


 Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Tanga, Bw. Gabriel masanja  (wapili kulia) akipeana mkono na Bw. Rajpaul Singh Dhani (kulia) dereva wa gari ya mashindano iliyoiwakilisha benki hiyo katika mchezo wa mashindano ya magari uliyofanyika mkoani Tanga hivi katibuni. Wengine katika picha ni wafanyakazi wa benki hiyo tawi la Tanga.

Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Tanga, Bw. Gabriel masanja  (wa kwanza kushoto) pamoja na Bw. Rajpaul Singh Dhani (Wa tatu kushoto) dereva wa gari (iliyopo mbele yao)ya mashindano iliyoiwakilisha benki hiyo katika mchezo wa mashindano ya magari uliyofanyika mkoani Tanga hivi katibuni. Wengine katika picha ni wafanyakazi wa benki hiyo tawi la Tanga. 


Tayari Ligi Kuu Vodacom inae Bingwa, Yanga, Mshindi wa Pili, Azam FC, na Mshindi wa Tatu, Simba, lakini kazi kubwa ipo leo hii Jumamosi kwenye Mechi za mwisho kabisa za Msimu kuamua Timu ipi moja itaungana na Polisi Moro kuteremka Daraja.
Yanga walishatwaa Ubingwa tangu Wiki iliyopita na Msimu ujao watawakilisha kwenye CAF CHAMPIONS LIGI na Azam FC, ambao wamepoteza Taji lao, wameshika Nafasi ya Pili na hivyo watacheza Mashindano ya CAF ya Kombe la Shirikisho.
Kwa Msimu huu Timu mbili zitashushwa Daraja na Timu 4 kupandishwa ili kufanya idadi ya Timu za Ligi Kuu Vodacom kuwa 16 Msimu ujao badala ya 14 za sasa.
Timu 4 zilizofuzu kupanda Daraja na kucheza Ligi Kuu Vodacom Msimu ujao ni Majimaji ya Songea, Mwadui ya Shinyanga, African Sports ya Tanga na Toto Africans ya Mwanza.
Timu moja ambayo itaungana na Polisi Moro kuporomoka Daraja kutoka Ligi Kuu Vodacom ni moja kati ya Timu 5 ambazo ni Ruvu Shooting, Prisons, Stand United, Ndanda FC na Mgambo JKT.
Ligi Kuu Vodacom itamalizika Jumamosi hii Mei 9, 2015
LIGI KUU VODACOM
RATIBA
Jumamosi Mei 9
Ratiba hiyo!Mwali wa Yanga SC


Manchester United wakipanda train kuelekea Ugenini tayari kucheza mchezo wao ugenini na Crystal Palace
Jonny Evans, Marouane Fellaini, Phil Jones, Luke Shaw, Radamel Falcao na Andreas Pereira walipofana mazoezi kujiandaa na Mchezo wao wa leo dhidi ya Crystal Palace.
Jones nae alipasha hiyo jana ijumaa kwenye Uwanja wa Mazoezi wa Aon complex

Radamel Falcao na Robin van Persie

Marcos Rojo na James Wilson

Juan Mata, Antonio Valencia na Rooney
Valencia kushoto, Rooney kwenye mazoeziEvans na Jones wakiwa pamoja na Smalling


LIGI KUU ENGLAND Wikiendi hii inaanza safari yake ya kumalizia Raundi zake 3 za mwisho wakati Bingwa, Chelsea, anatarajiwa kukabidhiwa Kombe lao Jumapili Uwanjani kwao Stamford Bridge wakicheza na Liverpool ambayo bado ina matumaini ya kufuzu 4 Bora.
Jumamosi zipo Mechi 7 ambazo nyingine ni muhimu kwa Timu zinazotaka kujinusuru kutoshushwa Daraja na hizo, kimahesabu, ni Timu 9 ambazo zipo kwenye hatari hiyo.Timu hizo ni kuanzia Crystal Palace, iliyo Nafasi ya 12, zikifuatia West Bromwich Albion, Aston Villa, Newcastle, Leicester City, Hull City na zile 3 za mkiani, Sunderland, QPR na Burnley.
Huko juu, baada ya Chelsea kutwaa Ubingwa na kujihakikishia kuwa moja ya Timu 4 zitakazocheza Ulaya kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu ujao, vita imebaki kupatika 3 zipi nyingine zitaungana nao.
Ingawa Man City na Arsenal wana nafasi nzuri sana kuwemo 4 Bora, kimahesabu lolote linaweza kutokea na hivyo wanahitaji ushindi ili kujihakikishia kuwemo.
Kazi kubwa ipo kwa Man United, walio Nafasi ya 4, wakiwa Pointi 4 mbele ya Timu ya 5 Liverpool na ambao pia, kimahesabu wanaweza kupitwa na hata Tottenham, walio Nafasi ya 6 na Southampton, walio Nafasi ya 7.
Jumamosi, Man United wako Ugenini huko Selhurts Park kuivaa Crystal Palace wakitafuta ushindi wao wa kwanza baada kudundwa Mechi 3 mfululizo.
Ikiwa Man United watashinda Mechi hiyo na Liverpool kutetereka huko Stamford Bridge wakicheza na Mabingwa Chelsea, basi uhakika wa Man United kucheza UEFA CHAMPIONS utakuwa wa matumaini ya kutosha.

LIGI KUU ENGLAND
RATIBA
Jumamosi Mei 9

14:45 Everton vs Sunderland
17:00 Aston Villa vs West Ham
17:00 Hull vs Burnley
17:00 Leicester vs Southampton
17:00 Newcastle vs West Brom
17:00 Stoke vs Tottenham
19:30 Crystal Palace vs Man United

Jumapili Mei 10
15:30 Man City vs QPR
18:00 Chelsea vs Liverpool
Jumatatu Mei 11
22:00 Arsenal vs Swansea

waliotembelea blog