Monday, February 24, 2014

Mratibu wa Mbio za Uhuru Marathon, Innocent Melleck akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati akizungumzia maandalizi ya uzinduzi wa Mbio hizo kwa Mwaka 2014,ambapo mwaka huu Mbio hizo zitazinduliwa kwenye Kijiji cha Butiama,Mkoani Mara.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Selemani Nyambui akinzungumza kwenye Mkutano huo.

MBIO za Uhuru (Uhuru Marathon) zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi katika kijiji cha Butiama mkoani Mara, Agosti mwaka huu, huku lengo kubwa likiwa ni kudumisha amani, umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa Uhuru Marathon, Innocent Melleck alisema, wameamua kuzindulia Butiama ili kumuenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambaye katika uhai wake alipigania mno mambo hayo.

“Tukumbuke Mwalimu Nyerere alipigania mno amani, umoja na mshikamano miongoni mwetu, pia ndiye muasisi wa Taifa hili, hivyo tuliona bora tukazindulie Butiama ili kumuenzi.”

Alisema, mara baada ya uzinduzi huo wanatarajia kuzunguka nchi nzima kuanzia ngazi ya wilaya, ili kuzitambulisha mbio hizo na kuwakumbusha Watanzania umuhimu wa amani, umoja na mshikamano miongoni mwetu.

Melleck alisema, kiini cha kuanza kampeni ya kuzindua mbio hizo mapema imekuja, kwani zenyewe zimebeba ujumbe wa amani, umoja na mshikamano, hivyo ni vyema kuwakumbusha Watanzania umuhimu wa kutunza na kuenzi mambo hayo.

“Amani ya nchi yetu katika siku za hivi karibuni inaonekana kwenda vibaya hasa kutokana na baadhi ya vyama vya siasa kufanya siasa kwa visasi badala ya kujenga hoja kukabiliana na changamoto za kisiasa, hivyo ni jukumu letu kuilinda,” alisema.

Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Selemani Nyambui alisema, kuanza maandalizi mapema kwa mbio hizo ni faraja kwao na watahakikisha wanakabiliana na changamoto zote ili ziweze kufana.

Mbio hizo zinatarajiwa kufanyika Desemba 8, mwaka huu na kwa mara ya kwanza zilifanyika mwishoni mwa mwaka jana na kushirikisha wanariadha kutoka nchi mbalimbali.

Mratibu wa Mbio za Uhuru Marathon, Innocent Melleck akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati akizungumzia maandalizi ya uzinduzi wa Mbio hizo kwa Mwaka 2014,ambapo mwaka huu Mbio hizo zitazinduliwa kwenye Kijiji cha Butiama,Mkoani Mara.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Selemani Nyambui akinzungumza kwenye Mkutano huo.

MBIO za Uhuru (Uhuru Marathon) zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi katika kijiji cha Butiama mkoani Mara, Agosti mwaka huu, huku lengo kubwa likiwa ni kudumisha amani, umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa Uhuru Marathon, Innocent Melleck alisema, wameamua kuzindulia Butiama ili kumuenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambaye katika uhai wake alipigania mno mambo hayo.

“Tukumbuke Mwalimu Nyerere alipigania mno amani, umoja na mshikamano miongoni mwetu, pia ndiye muasisi wa Taifa hili, hivyo tuliona bora tukazindulie Butiama ili kumuenzi.”

Alisema, mara baada ya uzinduzi huo wanatarajia kuzunguka nchi nzima kuanzia ngazi ya wilaya, ili kuzitambulisha mbio hizo na kuwakumbusha Watanzania umuhimu wa amani, umoja na mshikamano miongoni mwetu.

Melleck alisema, kiini cha kuanza kampeni ya kuzindua mbio hizo mapema imekuja, kwani zenyewe zimebeba ujumbe wa amani, umoja na mshikamano, hivyo ni vyema kuwakumbusha Watanzania umuhimu wa kutunza na kuenzi mambo hayo.

“Amani ya nchi yetu katika siku za hivi karibuni inaonekana kwenda vibaya hasa kutokana na baadhi ya vyama vya siasa kufanya siasa kwa visasi badala ya kujenga hoja kukabiliana na changamoto za kisiasa, hivyo ni jukumu letu kuilinda,” alisema.

Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Selemani Nyambui alisema, kuanza maandalizi mapema kwa mbio hizo ni faraja kwao na watahakikisha wanakabiliana na changamoto zote ili ziweze kufana.

Mbio hizo zinatarajiwa kufanyika Desemba 8, mwaka huu na kwa mara ya kwanza zilifanyika mwishoni mwa mwaka jana na kushirikisha wanariadha kutoka nchi mbalimbali.

Mwonekano wa kiwanja cha Aliianz Riviera mjini Nice nchini Ufaransa
Timu ya taifa ya Scotland na Jamuhuri ya Ireland zimepangwa katika moja ya makundi magumu katika michuano ya kufuzu kwa ajili ya fainali za mataifa barani ulaya mwaka 2016.
Katika kundi lao nchi nyingine zinazoungana nazo ni Ujerumani, Poland, Georgia na Gibraltar.
Uingereza itakutana na Switzerland, Slovenia,Estonia,Lithuania na San Marino, huku Wales ikiwa kundi moja na Bosnia-Hercegovina,Belgium,Israel,Cyprus na Andorra.
Ireland kaskazini iko kundi F pamoja na Ugiriki,Hungary, Romania, Finland na Faroe Islands.
Michuano ya Euro mwaka 2016 itahodhiwa na Ufaransa, ambayo moja kwa moja imefuzu, michuano ambayo itahusisha mataifa 24, kutoka idadi ya nchi 16 katika michuano iliyopita.



Sherehe za kufunga rasmi michezo ya Olimpiki ya Sochi
Michezo ya ishirini na mbili ya Olimpiki ya majira ya baridi, iliyodumu kwa siku 17, imemalizika Jumapili katika mji wa kitalii wa Sochi, kwa wenyeji Urusi kuibuka wa kwanza
Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki Thomas Bach alifunga rasmi michezo hiyo katika tafrija iliyodumu kwa dakika 130.
Urusi ilimaliza ya kwanza katika jedwali la medali, ikiwa na medali 13 za dhahabu 11 za fedha na 9 za shaba.
Norway ilimaliza ya pili na medali 11 za dhahabu 5 fedha na 10 za shaba.
Canada ilikamilisha orodha ya tatu bora na jumla ya medali 10 za dhahabu 10 za fedha na 5 za shaba.
Korea Kusini ilikabidhiwa bendera ya Olimpiki ikiwa ni ishara ya kuandaa michezo hiyo mwaka 2018, itakayofanyika katika mji wa Pyeongchang.
Mashindano ya Urusi yaligharimu dola bilioni 30, ambacho ni kitita kikubwa zaidi katika historia ya mashindano ya Olimpiki duniani IOC.
Rais wa shirikisho la Olimpiki duniani (IOC) Thomas Bach ameitaka dunia kuitizama Urusi kwa mtazamo mpya kwani wameonyesha uwezo wa hali ya juu katika kuandaa michezo hiyo na kukidhi matarajio ya washiriki wengi walioshiriki mashindano ya msimu wa baridi Sochi.
Alisema wanaondoka Sochi wakiwa marafiki bila ya kumbukumbu ya changamoto zilizokuwepo awali.

Performers form the Olympic rings during the closing ceremony for the 2014 Sochi Winter Olympics, February 23, 2014. REUTERS/Pawel Kopczynski (RUSSIA - Tags: OLYMPICS SPORT)
Former President of the International Olympic Committee (IOC) Jacques Rogge, Claudia Bach, International Olympic Committee (IOC) President Thomas Bach and President of Russia Vladimir Putin look on during the 2014 Sochi Winter Olympics Closing Ceremony at Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014 in Sochi, Russia. (Photo by Ryan Pierse/Getty Images)Thomas Bach (L), President of the IOC and Russian President Vladimir Putin (R) attend the 2014 Sochi Winter Olympics Closing Ceremony at Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014 in Sochi, Russia.Dancers form the Olympic rings during the 2014 Sochi Winter Olympics Closing Ceremony at Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014 in Sochi, Russia.Dancers form the Olympic rings during the Closing Ceremony of the Sochi 2014 Winter Olympics at Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014 in Sochi, Russia. Russian athletes perform the Russian national anthem with a choir during the closing Ceremony of the Sochi Winter Olympics at the Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014.
Flag bearers parade ahead of athletes during the Closing Ceremony of the Sochi Winter Olympics at the Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014.SOCHI, RUSSIA - FEBRUARY 23: Athletes enter the 2014 Sochi Winter Olympics Closing Ceremony at Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014 in Sochi, Russia.US nordic flag bearer, ice hockey player Julie Chu enters the stadium during the Closing Ceremony of the Sochi Winter Olympics at the Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014.Athletes carry their national flags as they take part in the Closing Ceremony of the Sochi Winter Olympics at the Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014. AFP PHOTO / DAMIEN MEYERDAMIEN MEYER/AFP/Getty ImagesSOCHI, RUSSIA - FEBRUARY 23: The flags of the competiting nations enters the arean during the 2014 Sochi Winter Olympics Closing Ceremony at Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014 in Sochi, Russia.Children from the Pan-Russian Choir sing during the Closing Ceremony of the Sochi Winter Olympics at the Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014.SOCHI, RUSSIA - FEBRUARY 23: A band performs during the 2014 Sochi Winter Olympics Closing Ceremony at Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014 in Sochi, Russia. France's flag bearer, biathlete Martin Fourcade (R) and Italy's flag bearer, short track skater Arianna Fontana (L) enter the stadium during the Closing Ceremony of the Sochi Winter Olympics at the Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014.
Performers take part in the closing ceremony for the Sochi 2014 Winter Olympic Games February 23, 2014. 
German athletes parade during the Closing Ceremony of the Sochi Winter Olympics at the Fisht Olympic Stadium on February 23, 2014.
Flagbearers arrive holding their national flags in the closing ceremony for the Sochi 2014 Winter Olympic Games February 23, 2014.
Mandatory Credit: Photo by Gong Bing/REX (3592384f) Russia national flag is raised in the stadium at the closing ceremony for the 22nd Winter Olympic Games Sochi 2014 Winter Olympic Games, Russia - 23 Feb 2014.


Michuano ya UEFA CHAMPIONS LIGI, yanaendelea tena kesho Jumanne na Jumatano wiki hii kwa Mechi nyingine za kwanza 4 za Raundi hiyo ambapo Timu mbili za England, Mabingwa Manchester United na Chelsea, zitakuwa Ugenini kuanza kampeni zao.
Wiki iliyopita, Timu nyingine mbili za England zilianza vibaya kwa zote kufungwa Mechi zao za Nyumbani wakati Man City walipochapwa kwao Etihad 2-0 na Barcelona na kumaliza Mechi wakiwa Mtu 10 baada ya Beki wao, Martin Demichellis, kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Hali kama hiyo iliwakuta Arsenal walipopigwa 2-0 Uwanjani kwao Emirates na Bayern Munich na kumaliza Mechi hiyo Mtu 10 baada Kipa wao Wojciech Szczesny kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.

Wiki hii, Man United watakuwa huko Ugiriki kucheza na Olympiacos na Meneja wao, David Moyes, licha ya kukiri ni Mechi ngumu, amesema wao wamepania ushindi wa huko huko Ugenini.
Wachezaji wa United wakishangilia moja ya bao juzi kwenye mtanange wao na Crystal Palace walipoifunga bao 2-0 ugenini.Solid: David Moyes saw his team pick up a hard earned 2-0 victory at Selhurst ParkKocha David Moyes wa United
VIKOSI VINATARAJIWA KUWA HIVI: Olympiakos (4-4-1-1): Roberto, Salino, Manolas, Papadopoulos, Bong, Maniatis, Samaris, Campbell, Fuster, Saviola, Scepovic
Manchester United (4-4-2): De Gea, Smalling, Ferdinand, Vidic, Evra, Valencia, Fellaini, Carrick, Januzaj, Rooney, Van Persie
Nao Chelsea watakwenda huko Uturuki kupambana na Klabu Kigogo ya huko, Galatasaray Spor Kulübü, ambayo Straika wake ni Didier Drogba, Gwiji wa zamani wa Chelsea, ambae Mechi yake ya mwisho na Klabu hiyo ya England ni kuifungia Penati ya mwisho katika Mikwaju ya Penati 5 walipoitoa Bayern Munich kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI huko Munich Mwaka 2012 na kutwaa Ubingwa.Lakini Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho, amesema urafiki na Drogba utakuwa haupo kwa Dakika 90.Patakuwa hapatoshi...ni Drogba dhidi ya  kocha wake wa zamani

RATIBA:
Jumanne Februari 25
20:00 Zenit St. Petersburg v BV Borussia Dortmund
22:45 Olympiacos v Manchester United
Jumatano Februari 26
22:45 Schalke 04 v Real Madrid CF
22:45 Galatasaray Spor Kulübü v Chelsea FC

UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
MATOKEO:
Jumanne Februari 18
Manchester City 0 FC Barcelona 2
Bayer 04 Leverkusen 0 Paris Saint-Germain 4
Jumatano Februari 19
AC Milan 0 Atletico de Madrid 1
Arsenal FC 0 Bayern Munich 2

RATIBA:
Jumanne Februari 25
20:00 Zenit St. Petersburg v BV Borussia Dortmund
22:45 Olympiacos CFP v Manchester United
Jumatano Februari 26
22:45 Schalke 04 v Real Madrid CF
22:45 Galatasaray Spor Kulübü v Chelsea FC

MARUDIANO
Jumanne Machi 11
22:45 Bayern Munich v Arsenal FC
22:45 Atletico de Madrid v AC Milan
Jumatano Machi 12
22:45 FC Barcelona v Manchester City
22:45 Paris Saint-Germain v Bayer 04 Leverkusen
Jumanne Machi 18
22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor Kulübü
22:45 Real Madrid CF v Schalke 04
Jumatano Machi 19
22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg
22:45 Manchester United v Olympiacos CFP


Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya mawasiliano ya Airtel Tanzania Ijumaa hii itachezesha droo kubwa ya promosheni yake ya 'Mimi Ni Bingwa' ambayo itamfanya mmoja wa wateja wake kujishindia zawadi ya kitita cha shilingi milioni 50.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Afisa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde alisema droo hiyo itakayobadilisha maisha ya mtu, imepangwa kuchezeshwa katika ofisi za makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.


"Baada ya miezi kadhaa iliyojaa zawadi kwa wateja wetu waaminifu, Ijumaa hii itakuwa ndiyo kilele cha promosheni yetu ya Mimi Ni Bingwa ambapo tutamtafuta na kumtangaza mshindi wa zawadi yetu kubwa," alisema.


Jane alisema kuwa mshindi atakayebahatika atapatikana kwa kuchezesha droo ya bahati na sibu utakaokuwa chini ya uangalizi na usimamizi wa afisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania na kushuhudiwa na wafanyakazi wa Airtel na vyombo vya habari.

"Ningependa kuwashukuru wateje wetu kwa kushiriki promosheni hii na kuwakumbusha wateja wote wa Airtel ambao bado hawajajiunga na mchezo huu kwamba bado wanaweza kujiunga na wanaweza wakawa na bahati ya kushinda zawadi kubwa ya shilingi milioni 50 kwa sababu wote waliojisajili katika promosheni wataingizwa katika droo hii kubwa na ni namba moja tu itakayobahatika. Hii ina maana kuwa kadri uchezavyo ndipo unapata nafasi kubwa ya kuibuka mshindi,” alisema.

Alisema kuwa wakati wa promosheni, wateja wa Airtel walijishindia pesa taslim ya zaidi ya shilingi milioni 324 na zaidi ya tiketi 36 kwa ajili ya safari iliyogharamiwa kila kitu ya kwenda kuangalia mechi ya klabu ya Manchester United katika uwanja wa Old Trafford zilitolewa.


"Promosheni ya Airtel ‘Mimi Ni Bingwa' imeweza kubadilisha maisha ya wateja wake kwa kuwazawadia zaidi ya shilingi milioni 324 pesa taslim na kuwapa watanzania 36 nafasi ya kipekee katika maisha yao ya kuitembelea klabu kubwa ya soka ulimwenguni ya Manchester United pamoja na kuitembelea uwanja wao wa Old Trafford na pia kuwa sehemu ya mashabiki wa soka wanao angalia mechi ya Manchester United moja kwa moja ‘live’ uwanjani," alisema.


“Kwa mara nyingine tena, hii ni nafasi kwa wateja wengine wa Airtel ambao hawakujisajili kwenye promosheni kuingia kwa kutuma ujumbe mfupi (SMS) wenye neno “BINGWA” kwenda namba 15656, na kujibu maswali mengi iwezekanavyo, unaweza jishindia zawadi kubwa ya pesa taslim ya shilingi milioni 50,” alisema.


Promosheni ya Airtel ‘Mimi ni Bingwa’ iliyoanza mwezi Novemba mwaka jana, ni matokeo ya ushirika baina ya klabu ya Manchester United na kampuni hii ya mawasiliano, ambayo hailengi tu kuwazawadia wateja wake pekee lakini pia kuwaunganisha washiriki wa promosheni hii na soka la kimataifa ambapo itasaidia kuamsha ari ya michezi miongoni mwa watanzania, hasa katika soka.


Wakati wa promosheni hiyo, washindi wawili wa Mimi Ni Bingwa walijishindia zawadi ya shilingi milioni moja kila moja kwa kila siku, washindi wawili walijishindia zawadi ya shilingi milioni 5 kila mmoja kila wiki na mshiriki mmoja alikuwa anajishindia tiketi mbili kila wiki kwa ajili ya safari iliyogharamiwa kila kitu ya kwenda Old Trafford.


Kundi la awamu ya kwanza la washindi wa tiketi tayari walifurahia safari yao na imebainisha kuwa kundi la pili na la tatu watasafiri kwenda Manchester ifikapo mwezi Machi wakati Manchester United ikitarajiwa kucheza tena katika uwanja wake wa Old Trafford.

rooney 1ae1b
£160,000 - Hii ndio fedha ambayo itabaki kwenye akaunti ya Rooney kwa wiki - baada ya kulipia kila kitu, kodi na bima.
victor_d832d.png
HATIMAYE rais Victor Yanukovych wa nchini Ukraine amekimbia mji wa Kiev baada ya bunge la nchi hiyo kupitisha kura ya kumwondoa madarakani rais huyo kutokana na shinikizo la waandamanaji.
Aidha, aliyekuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Bw. Yulia Tymoshenko ameachiwa huru baada ya kutumikia kifungo cha miaka miwili jela wakati wa utawala wa Rais Yanukovych ambaye ni hasimu mkubwa wa rais huyo.
Kwa mujibu wa BBC, Naibu wa kikosi cha ulinzi wa mipaka wa taifa hilo amenukuliwa akisema kuwa ndege ya kukodiwa iliyokuwa imemchukua rais Yanukovych imenyimwa ruhusa ya kuondoka kutoka uwanja wa Donetsk, mji ambao uko mashariki mwa Ukraine ambao ni ngome ya wafuasi wake.
Akizungumza katika runinga moja ya mji wa Kharkiv, rais Yanukovych ameeleza kuwa vitendo vinavyofanyika dhidi ya serikali yake ni vya mapinduzi.
Hata hivyo, Magavana wa majimbo ya mashariki mwa Ukraine wamefanya mkutano katika mji wa Kharkiv, na kuhudhuriwa na maafisa wa Urusi kuzungumzia udhibiti haramu wa mji mkuu wa Kiev.
Wakati huohuo, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Ukraine, Yulia Tymoshenko ameachiwa huru na kupokelewa kwa hisia tofauti baada ya kuwahutubia maelfu ya waandamanaji waliokusanyika katikati ya mji mkuu wa Kiev.
Akiwa ameketi katika kiti cha magurudumu, amewaambia waandamanaji kwamba wanasiasa nchini humo hawana thamani ya 'tone la damu yao' iliyomwagika wakati wa maandamano hayo.
Hata hivyo, hali katika mji wa Kiev imekuwa ya utulivu jana asubuhi siku moja baada ya kushuhudiwa mabadiliko makubwa katika mgogoro wa kisiasa wa taifa hilo.(E.L)

waliotembelea blog