Wednesday, March 25, 2015

Cristiano-Ronaldo
Rais wa ligi kuu ya soka nchini Hispania maarufu kama La Liga amesema kuwa Cristiano Ronaldo naweza akapata adhabu ya ukosefu wa nidhamu kutokana na aina ya ushangiliaji aliouonesha katika mechi ya El Classico dhidi ya Fc. Barcelona na hii ni mara baada ya kusawazisha goli katika mchezo uliochezwa siku ya Jumapili Nou Camp.
Ronaldo alionekana akitoa ishara ya kuwataka mashabiki wa Fc. Barcelona watulie mnamo dakika ya 31 aliposawazisha goli hilo kwa upande wa Real Madrid ndani ya El Classico Camp Nou.
Tebas wakati anaongea na waandishi wa habari alisema “Inatakiwa tuwe makini sana na ishara za ushangiliaji pindi mchezaji anapofunga goli au aina yoyoye ile ya ushaingiliaji wa ishara ambayo inaweza ikachochea vurugu kwa watazamaji”
“Tunaweza kutoa adhabu ya faini au kusimamisha mechi kadhaa, tutaliangalia hili suala”
Mamlaka ya ligi kuu ya Hispania wamekuwa wakiweka jitihada za ziada kuzuia aina ya ushangiliaji yenye ishara za ushawishi tangu tangu kufariki kwa mshambuliaji wa Derpotive La Coruna mwaka jana.
Mnamo mwezi wa 12 mwaka mwaka jana chama cha La Liga kiliripoti kuwa vilabu vitano Real Madrid, Fc. Barcelona, Derportive, Rayo Vallecano na Granada kutokana na aina ya ushangiliaji wa kukera ambapo pia Barcelona waliufanya kwa Cristiano Ronaldo walipomzomea na wakimuita ni mlevi wakati mchezo unaendelea”
Teabs ambaye alikuwa akiongea katika seminar huko Barcelona alisema ligi hiyo ni ligi bora duniani na ilie iendelee kuwa bora ni lazima iwe katika hali ya usalama zaidi hali ambayo itanyamazisha vilio na vurugu katika mpira.
Wakati huohuo kilabu ya Real Madrid imemmpiga marufuku moja kati ya mwanachama wake na kuiomba tume ya nchini humo kufanya uchunguzi kwa mashaiki wengine wawili ambao walionekana wakiwatukana matusi wachezaji kufutia mchezo wa Jumapili dhidi ya Barcelona.
Uongozi wa Real Madrid ulisema mapema jumatatu baada ya kugundua kupitia picha waliweza kumpia marufuku mmoja kati ya wanachama wao kuingia katika uwanja wa Santiago Bernabeu pamoja na kumfuta uanachama wa kilabu hiyo au sehemu yoyote ile itakayohusisha kilabu ya Real Madrid.
 pele mess
Na Amplifaya Amplifaya
Unapata maana ya kwamba Pele anatambua kile au ni kipi unataka kumuuliza hata kabla haujaanza kubuni maneno.
Labda ni kitu asili chenye muingiliano na uelewa sawa wenye athari kwa tabia za binadamu na jinsi gani anaweza kutumia hiyo fursa kwa faida yake ambayo imemfanya kuweza mchezaji mkubwa na mwenye historia kubwa duniani pia mwenye rekodi ya kuwa mfungaji mwenye magoli mengi duniani ambapo katika mchezo wa soka haijawahi kutokea.
Au labda kiurahisi ni kama sababu ya marejeo au kitu kisichoweza kuepukika kimazoezi.
Mchezaji huyo ambaye ni mshindi mara tatu wa kombe la dunia akiwa na timu yake ya Taifa ya Brazil labda hakumbuki amefanya mahojiano mara ngapi na vyombo vya habari na jinsi alivyotambulika katika umma wa watu duniani, magoli yake ambayo yanahesabika kuwa ni 1284 katika michezo yake yote aliyocheza na ikiwa kama amepata stashahada ya rekodi ya dunia.
Pele atakuwa anafikisha miaka 75 mwaka huu (amezeeka sasa) lakini haoneshi dalili yotote ya kupumzika na kuachana na masuala ya soka maana amekuwa akijumuishwa katika masuala mengi ikiwemo matangazo, projekiti nyingi kuhusiana na soka kiujumla huku akizunguka takribani dunia nzima.
Hauhitaji kujitambulisha mwenyewe na kila mtu anajua Pele ni nani.
Mwishoni mwa wiki iliyopita moja kati ya majukumu yaliyompeleka Pele Uingereza alikuwa ni mmoja kati ya wageni maalum pale Anfield ambapo Liverpool iliwakaribisha Manchester United na mchezo kumalizika kwa Liverpool kufungwa mechi hiyo katika ligi kuu ya Uingereza.
“Ni furaha kuwa hapa” Pele alisema wakati akiongea na mwandishi mmoja wa habari”
“Kuja Uingereza zaidi ya mara moja ni kitu cha kujivunia zaidi” Pele alisema.
Brazil huwa tuna kila mechi kila ifikapo mwisho mwa wiki kupitia video na Uingereza pia ambayo ni ligi moja muhimu sana hapa Duniani. AlisemaNeymar
Kunaweza kuwa na baadhi ya wachezaji wengi wa Kibrazil ambao wanatumikia maisha yao ya soka na vilabu ya Uingereza lakini nyota wakubwa watabakia kuwa nyota wa kipekee, na hapo ndipo mazungumzo yalipogeukia kwa Neymar ambaye ndiyo anaaminiwa na Pele kuwa ni nyota wa Barcelona hasa kwa hizi siku zijazo za usoni akiwa na maana ya miaka ijayo mbele.
“Hakuna jipya, nineongea sana kuhusu Neymar” Pele alisema
“Ni kama mtoto wetu tu, alichezea Santos, nilichezea Santos na mwanangu Edinho alichezea Santos kama golikipa na hivyo tunafurahia kuwa na Neymar
Nadhani kiwango chake tokea mwaka jana hadi sasa kimeimarika zaidi na bado ana mambo mengi zaidi ya kujifunza akiwa kama mchezaji japo ni mchezaji mzuri”  Pele alisema.
Kumbuka kuwa Pele alishawahi kuwa mmoja wa watu waliopinga sana Neymar asiondoke Barcelona ili kulinda kiwango chake ndani ya Kilabu cha Santos na sio Barcelona tu halikadhalika Real Madrid na vilabu vingine.
Itakuwa ni kitu cha kujivunia zaidi kucheza Barcelona sababu Barcelona sio timu tu bali ni Messi na Neymar, Pele alisema kuwa Messi ni mchezaji bora ambaye hajawahi kumuona katika maisha yake ya soka na anasema licha ya kuwa Barcelona bado kuna wachezaji wengine ambao ni nguzo ya timu kama Xavi na Iniesta jinsi wanavyocheza wana mchango mkubwa sana katika timu.
Pele pia alizungumzia suala la FIFA kubadili ratiba ya kombe la dunia kwa mwaka 2022 ambapo litakuwa linachezwa majira ya masika mwezi wa 12.
” nadhani wiki hii ndiyo wameamua kombe lichezwe mwezi wa 12 kipindi ambacho kitakuwa ni cha majira ya joto kwetu Brazil, kitu kizuri ni kuliweka kombe katika mazingira mazuri kwa watu, mahali na wakati sio jambo muhimu bali ni kitu ambacho kinachanganya mno, mabadilikobya kucheza mwezibwa 12 sio madogo kabisa” Pele alisema.
IMG_20150325_070626Na Augustino Mabalwe,Dar es salaam
Baada ya kukaa nje kwa muda mrefu akiuguza majeraha, hatimaye kiungo mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid James Rodriguez arejea mazoezini kufuatia matibabu mazuri aliyopatiwa na madaktari wa timu hiyo.
Rodriguez,23, alivunjika mfupa wa ndani katika mguu wake wa kulia mapema mwezi Februari katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Sevilla.
Mchezaji huyo aliyesajiliwa na matajiri hao msimu huu kwa ada ya paundi milioni 63 kutoka Monaco mpaka anapata majeraha hayo tayari alishaifungia klabu hiyo magoli 7 na kutoa pasi za mwisho 7 katika mechi 22 alizocheza kwenye michuano yote msimu huu.
Mshindi huyo wa tuzo ya goli bora (Puskas) la mashindano ya kombe la dunia mwaka 2014 amekosa mechi nyingi kipindi akiuguza majeraha yake na sasa amesema amerejea kwa kasi kuisaidia timu yake.
Aidha kuelekea mechi za robo fainali klabu bingwa dhidi ya Atletico Madrid mwezi ujao hii ni habari nzuri kwa kocha wa klabu hiyo Carlo Ancelotti ambaye amekuwa akimtumia mcolombia huyo katika nafasi tofauti ndani ya uwanja.
Omary-KatangaBaada ya kumalizika kwa michuano ya ligi ya mkoa wa Dar es salaam na timu za FFU na Zakhem kumaliza katika nafasi ya kwanza kwenye makundi yao,kesho 20/03/2015 utapigwa mchezo mmoja wa kusaka nafasi ya kuungana na mabingwa hao kushiriki michuano ya ligi ya mikoa.
Mchezo huo wa mtoano utakaopigwa katika uwanja wa Mizinga Kigamboni,utazikutanisha timu za Pan Africa dhidi ya Changanyikeni ambazo zimemaliza katika nafasi ya pili kwenye makundi yao.
Kwa mujibu wa kamati ya mashindano ya chama cha kandanda mkoa wa Dar es salaam,DRFA,baada ya kumpata mshindi katika mchezo huo, majina ya timu hizo tatu yatapelekwa shirikisho la soka la Tanzania TFF.
Aidha kamati hiyo chini ya mwenyekiti wake Kenny Mwaisabula,imewashukuru mashabiki waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja mbalimbali kushuhudua michuano ya ligi mkoa wa Dar es salam tangu ilipoanza kutimua vumbi.
IMG_3893Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa kushirikiana na Kilimanjaro Premium Lager wamezindua rasmi msimu mwingine wa tuzo za muziki Tanzania unaojulikana kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards (KTMA).
Meneja wa bia ya Kilimanjaro Pamela Kikuli amesema; “Kilimanjaro Premium Lager ni bia ya watanzania na imejikita katika kuwaletea burudani na pia kutoa majukwaa ambayo yanawapa Watanzania fursa ya kukuza vipaji mbalimbali.. hii tumeithibitisha kwa juhudi za makusudi za kutenga fungu kubwa na kuongeza ushiriki wa wataalaam mbali mbali kwenye fani husika ili kuziendeleza, kuzikuza na kuziongezea thamani tuzo hizi mwaka hadi mwaka sambamba na umaarufu kuongezeka kwenye medani za Kimataifa.”
Kampuni hiyo imewekeza zaidi ya Tshs. Bil.1 kuhakikisha ubora wa hali ya juu unajitokeza kwenye mchakato mzima wa tuzo hizi.
Msimu huu hauna mabadiliko makubwa sana katika vipengele wala mfumo wa kuwapata wasanii watakaoshiriki, kuna maboresha kwenye njia za upigaji kura kwa mfano kwa sasa ni watu wengi wanatumia Whatsapp, KTMA imewarahisishia kwa kuongeza njia hiyo kwenye mchakato wa kupendekeza na kupiga kura.
Kura za maoni zitaanza kupigwa tarehe March 30 ambapo shabiki ataweza kupendekeza nani ama nyimbo zipi ziwemo kwenye vipengele vyote vya KTMA 2015.
Watu watapiga kura kupitia mtandao, Whatsapp na SMS na utaratibu uliopo ni kwamba namba moja ya simu itatumika kupiga kura moja kwenye kila kipengele.


Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa na Masoko wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Nsao Shalua (kushoto), akikabidhi bendera ya taifa kwa mshindi wa Airtel Trace Music Stars, Mayunga Nalimi kwa ajili ya kwenda kuiwakilisha nchi katika fainali za Afrika za Airtel Trace Music Stars zitakazofanyika Jumamosi Machi 28, nchini Kenya na kushirikisha nchi 13, katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika kwenye ofisi za BASATA jijini Dar es Salaam jana. Anayeshuhudia (katikati), ni Meneja Masoko wa Airtel, Anet Muga.
Meneja Masoko wa Airtel, Anet Muga. akiongea wakati wa tukio la kumuaga na kumkabithi bendera ya taifa kwa ajili ya kwenda kuiwakilisha nchi katika fainali za Afrika za Airtel Trace Music Stars zitakazofanyika Jumamosi Machi 28, nchini Kenya na kushirikisha nchi 13, katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika kwenye ofisi za BASATA jijini Dar es Salaam jana. pichani katikati ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa na Masoko wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Nsao Shalua akifatiwa na mshindi wa Airtel Trace Music Stars, Mayunga Nalimi.
mshindi wa Airtel Trace Music Stars, Mayunga Nalimi akiwa ameshika bendera mara baada ya kukabithiwa na Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa na Masoko wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), kwaajili ya kuiwakilisha nchi katika mashindano ya muziki ya Airtel Trace Music Stars yatakayofanyika Jumamosi hii nchini Kenya.

Barasa la Sanaa Tanzania leo limemkabithi bendera mshindi wa shindano la Airtel Trace Music Stars Bwana Nalimi Mayunga anayeondoka leo nchi kwenda kuhudhuria mashindano ya Airtel Trace Afrika yatakayoshirikisha washiriki toka nchi 13 barani Afrika yanayofanyika nchini Kenya siku ya Jumamosi tarehe 28 March 2015.

Mayunga aliibuka mshindi katika kinyanganyiro cha kusaka Wakali wa vipaji vya mziki kupitia shindano la Airtel Trace Music lililozinduliwa na kampuni ya Airtel Tanzania Mwaka Jana mwezi wa kumi na kushirikiksha washiriki mbalimbali kutoka mikoa mbalimbali nchini ambapo fainali ya kumsaka mshindi ilifanyika mwanzoni mwa mwezi wa februari na kumwezesha Mayunga kuwashinda washindani wengine watano na katika fainali hizo na kuondoka na kitita zawadi ya shilingi million 50.

Akiongea wakati wa kukabithi bendera hiyo, Mkurugenzi wa ukuzaji sanaa na Masoko wa BASATA bi Nsao Shalua alisema” kwanza tunachukua fulsa kuwapongeza Airtel kwa kuanzisha shindano hili na kwa kufata taratibu zote za kuratibu mashindano. Airtel leo wameonyesha mfano kwa kumleta mshindi hapa ofisini, kuaga rasmi na kupatiwa kibali cha kusafiri kutoka baraza la sanaa Tanzania kitu ambacho hakifanywi na makampuni mengi na hata wasaani wengi nchini. Huu ni mfano wa kuigwa na natoa wito kwa watu wote wanaoondoka nchini kwaajili ya kwenda kufanya shughuli za sanaa kuhakikisha wanafata utaratibu kwa kutufahamisha na kupata hati maalumu ya kushiriki shughuli na kuiwakilisha nchi yetu nje ya nchi.

Aidha napenda kumpongeza Mayunga kwa kuibuka kuwa mshindi na kupata nafasi ya kuwakilisha nchi yetu katika mashindano ya Afrika, tunapenda kumwomba atumie fulsa hii vizuri na kwa kufanya hivyo basi tunaamini atafanya vyema. Tunamtakia safari njema na mashindano mema, tunaamini Mayunga atatuwakilisha vyema na kutangaza nchini yetu katika angaza za muziki kwa ujumla.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa Airtel Bi Aneth Muga alisema” Leo tunamuwezesha Mayunga kwenda kushiriki na kuiwakiisha nchi yetu katika mashindano ya Afrika Tunamwezesha kujiwekea umaarufu na kuonyesha kipaji chake kwa wadau wa ndani na nje ya nchi, pamoja na Mayunga tunawawezesha vijana wengi barani Afrika kwa ujumla kuzifikia ndoto zao. Mashindano haya yatafanyika siku ya Jumamosi , jijini Naivasha Kenya ambapo washiriki kutoka nchi 13 barani Afrika watachuana vikali. Mshindi wa Airtel Trace Afrika atapata nafasi ya kwenda nchini marekani na kupata mafunzo kutoka kwa mwanamuziki wa miondoko ya R&B , Akon na kuweza kurekodi nyimbo zake.

Natoa wito kwa watanzania kumpigia kura Mayunga kwa ku tuma SMS, yaani ujumbe mfupi andika neno YUN kwenda 15594, Alhamisi ni siku ya mwisho ya kupiga kura, asiliimia 25 ya ushindi inatoka kwenye kura yako hivyo kura yako ni ya muhimu sana. Aliongeza Aneth.

Akiongea mara baada ya kukabithiwa bendera Malimi Mayunga alisema” namshukuru sana mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kufikia hatua hii, nawaahidi watanzania kuwawakilisha vyema, pamoja na hayo nawaomba sana watanzania waniunge mkono kwa kunipigia kura ili nipate nafasi ya kuweza kuibuka kuwa mshindi.

Hii kwangu ni nafasi ya pekee sana na namshukuru sana Mungu kwa kuniwezesha na Airtel kwa kuwawezesha vijana kama mimi kuonyesha vipaji vyao na kuzifikia ndoto zao kupitia mashindano mengi kama haya Mashindano ya Airtel Trace Music Star yalianzishwa kwa lengo la kuonyesha vipaji vya vijana kimuziki na nakuwapatia fulsa ya kukua kimuziki.


Shirikisho la kanda kanda Nchini England FA sasa linakusudia kuandaa sheria itakayo kupunguza idadi ya wachezaji kutoka nje ya nchi za Umoja wa Ulaya watakaosajiliwa katika ligi za nchi hiyo.
Mwenyekiti wa shirikisho hilo Greg Dyke asema kwamba ligi kuu ya England ipo kwenye hatari ya kutowasaidia wachezaji raia wa Uingereza kama hatua hazitachukuliwa.
Katika mpango pia itaweka sheria ngumu kwa wachazaji wenye vipaji waliokulia nchini humo.
Mikakati hiyo yote ni ya kuimarisha timu ya taifa ya England ambayo imekuwa haifanyi vizuri kwenye mechi za kimataifa.



Timu ya Kiluvya United ya mkoa wa Pwani jana imetawazwa Mabingwa wapya wa Ligi Daraja la Pili (SDL) baada ya kuifunga Mbao FC ya Mwanza kwa mabao 4-2 katika mchezo wa fainali uliofanyika kwenye Uwanja wa kumbukumbu ya Karume jijini Dar es salaam.
Kiluvya United inaunganana timu za Mji Mkuu (CDA) ya Dodoma, Mbao FC ya Mwanza na Mji Njombe ya Njombe kupanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL)msimu ujao, huku timu za Ujenzi Rukwa, Katavi FC na Volcano zikishuka daraja kutoka Ligi Daraja la Pili.

waliotembelea blog