Wednesday, March 25, 2015

Cristiano-Ronaldo
Rais wa ligi kuu ya soka nchini Hispania maarufu kama La Liga amesema kuwa Cristiano Ronaldo naweza akapata adhabu ya ukosefu wa nidhamu kutokana na aina ya ushangiliaji aliouonesha katika mechi ya El Classico dhidi ya Fc. Barcelona na hii ni mara baada ya kusawazisha goli katika mchezo uliochezwa siku ya Jumapili Nou Camp.
Ronaldo alionekana akitoa ishara ya kuwataka mashabiki wa Fc. Barcelona watulie mnamo dakika ya 31 aliposawazisha goli hilo kwa upande wa Real Madrid ndani ya El Classico Camp Nou.
Tebas wakati anaongea na waandishi wa habari alisema “Inatakiwa tuwe makini sana na ishara za ushangiliaji pindi mchezaji anapofunga goli au aina yoyoye ile ya ushaingiliaji wa ishara ambayo inaweza ikachochea vurugu kwa watazamaji”
“Tunaweza kutoa adhabu ya faini au kusimamisha mechi kadhaa, tutaliangalia hili suala”
Mamlaka ya ligi kuu ya Hispania wamekuwa wakiweka jitihada za ziada kuzuia aina ya ushangiliaji yenye ishara za ushawishi tangu tangu kufariki kwa mshambuliaji wa Derpotive La Coruna mwaka jana.
Mnamo mwezi wa 12 mwaka mwaka jana chama cha La Liga kiliripoti kuwa vilabu vitano Real Madrid, Fc. Barcelona, Derportive, Rayo Vallecano na Granada kutokana na aina ya ushangiliaji wa kukera ambapo pia Barcelona waliufanya kwa Cristiano Ronaldo walipomzomea na wakimuita ni mlevi wakati mchezo unaendelea”
Teabs ambaye alikuwa akiongea katika seminar huko Barcelona alisema ligi hiyo ni ligi bora duniani na ilie iendelee kuwa bora ni lazima iwe katika hali ya usalama zaidi hali ambayo itanyamazisha vilio na vurugu katika mpira.
Wakati huohuo kilabu ya Real Madrid imemmpiga marufuku moja kati ya mwanachama wake na kuiomba tume ya nchini humo kufanya uchunguzi kwa mashaiki wengine wawili ambao walionekana wakiwatukana matusi wachezaji kufutia mchezo wa Jumapili dhidi ya Barcelona.
Uongozi wa Real Madrid ulisema mapema jumatatu baada ya kugundua kupitia picha waliweza kumpia marufuku mmoja kati ya wanachama wao kuingia katika uwanja wa Santiago Bernabeu pamoja na kumfuta uanachama wa kilabu hiyo au sehemu yoyote ile itakayohusisha kilabu ya Real Madrid.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog